Josh Michael
JF-Expert Member
- Jun 12, 2009
- 2,523
- 77
na Asha Bani
MKURUGENZI wa Mambo ya Nje wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), John Mnyika amesema serikali bado haijawashughulikia mafisadi na kwamba wanaendelea kuitafuna nchi na kuwaacha Watanzania wengi wakiendelea kutaabika.
Mnyika alisema hayo jana alipozungumza na waandishi wa habari kuhusiana na ziara ya Operesheni Sangara inayoanza leo mkoani Tanga.
Alisema Operesheni Sangara inafanyika kwa lengo la kuishitaki serikali kwa wananchi wa mkoa huo kutokana na kushindwa kuwachukulia hatua mafisadi hao pamoja na kuwatumikia wananchi.
Mnyika alisema mkoa huo ulikuwa maarufu kwa ukuaji wa viwanda, lakini sasa vimekufa kutokana na kuwa na usimamizi mbovu.
Ni lazima tuishitaki serikali kwa wananchi kwa kuwa umma ndio waamuzi na ndio ambao wanataabika kwa hali hii iliyopo sasa, ikiwa hata viwanda vyetu vinashindwa kusimamiwa na kufia mikononi mwa serikali inayoongozwa na CCM, alisema Mnyika.
Alisema Kamati Kuu ya chama hicho iliyoketi hivi karibuni ilitafakari hali halisi ya maisha ya Watanzania na kwamba taifa linaendelea kufilisika kutokana na mafisadi kuendelea kutamba.
Mnyika alisema operesheni hiyo itaambatana na kuwashukuru wananchi wa mkoa huo kwa kuichagua CHADEMA katika uchaguzi wa serikali za mitaa, vitongoji na vijiji uliofanyika hivi karibuni.
Naye Mkurugenzi wa Oganaizeshi na Mafunzo Taifa wa chama hicho, Benson Kigaila alisema katika ziara hiyo kutakuwa na vikosi viwili katika kuwafikishia ujumbe wananchi. Alivitaja kuwa ni kikosi cha anga kitakachoongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe na kikosi cha ardhini kitakachoongozwa na Katibu Mkuu, Dk. Willbrod Slaa. Alisema kwa siku itafanyika jumla ya mikutano 34 ambapo kikosi cha anga kitafanya mikutano 18 na kikosi cha ardhi 16.
MKURUGENZI wa Mambo ya Nje wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), John Mnyika amesema serikali bado haijawashughulikia mafisadi na kwamba wanaendelea kuitafuna nchi na kuwaacha Watanzania wengi wakiendelea kutaabika.
Mnyika alisema hayo jana alipozungumza na waandishi wa habari kuhusiana na ziara ya Operesheni Sangara inayoanza leo mkoani Tanga.
Alisema Operesheni Sangara inafanyika kwa lengo la kuishitaki serikali kwa wananchi wa mkoa huo kutokana na kushindwa kuwachukulia hatua mafisadi hao pamoja na kuwatumikia wananchi.
Mnyika alisema mkoa huo ulikuwa maarufu kwa ukuaji wa viwanda, lakini sasa vimekufa kutokana na kuwa na usimamizi mbovu.
Ni lazima tuishitaki serikali kwa wananchi kwa kuwa umma ndio waamuzi na ndio ambao wanataabika kwa hali hii iliyopo sasa, ikiwa hata viwanda vyetu vinashindwa kusimamiwa na kufia mikononi mwa serikali inayoongozwa na CCM, alisema Mnyika.
Alisema Kamati Kuu ya chama hicho iliyoketi hivi karibuni ilitafakari hali halisi ya maisha ya Watanzania na kwamba taifa linaendelea kufilisika kutokana na mafisadi kuendelea kutamba.
Mnyika alisema operesheni hiyo itaambatana na kuwashukuru wananchi wa mkoa huo kwa kuichagua CHADEMA katika uchaguzi wa serikali za mitaa, vitongoji na vijiji uliofanyika hivi karibuni.
Naye Mkurugenzi wa Oganaizeshi na Mafunzo Taifa wa chama hicho, Benson Kigaila alisema katika ziara hiyo kutakuwa na vikosi viwili katika kuwafikishia ujumbe wananchi. Alivitaja kuwa ni kikosi cha anga kitakachoongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe na kikosi cha ardhini kitakachoongozwa na Katibu Mkuu, Dk. Willbrod Slaa. Alisema kwa siku itafanyika jumla ya mikutano 34 ambapo kikosi cha anga kitafanya mikutano 18 na kikosi cha ardhi 16.