Mbaha
JF-Expert Member
- Nov 26, 2010
- 697
- 73
Msema kweli mpenzi wa Mungu ,sasa inabidi niwambie ukweli ambao nimeupata kutoka kwa kigogo mmoja wa CCM ambae anaushawishi mkubwa kabisa ndani ya Chama ,chama ambacho kinafuata itikadi na mwenendo wa baba wa Taifa hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ,mzalendo alieiwezesha Tanzania kufika hapa ilipofikia na kuweza kujulikana ulimwengu mzima.
Habari zinasema kuwa kama kufa basi Chadema itakufa na kusahaulika kabisa na pengine kujulikana kwakwe itakuwa Chama kilichokuja juu kama uyoga na kufa kama uyoga.
WaTanzania walio wengi wameanza kuona ubabe,ubeberu,ubepari unyanyasaji unaofanywa na chama hiki cha ajabu chenye kauli zinazobadilika kama rangi ya kinyonga.Chadema kama inavyojulikana kuwa ni chama cha kkijadi au chenye itikadi ya ukabila na udini mbele ,kimekuwa kikianguka kila siku ingawa kinapoanguka huzusha jipya na kupata wafuasi na baadae wafuasi hukikimbia kutokana na umangimeza ulio ndani ya chama hicho.
Uchaguzi wa 2015 ndio utakaoimaliza na kuisambaratisha Chadema ,CCM ambao hadi hapa tulipo wameshaanza kujenga mazingira ya ushindi na kujinyakulia ushindi mnono wa uchaguzi wa 2015 ,mgombea wa Chadema Safari ambae hakubaliki na jamii huenda akapambana na Salim Ahmed wa CCM.
Time will tell.... That's what I understand and believe....