CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Jimbo la Kawe, Mkoa wa Dar es Salaam, kimeanzisha Data Benki, ambayo hutoa ujumbe kwa wananchi ili kuhakikisha uchaguzi mkuu ujao, Chama cha Mapinduzi (CCM), hakishindi.
Katibu wa jimbo hilo, Powell Mfinanga, alisema hayo mwishoni mwa wiki kwenye mkutano ulioandaliwa na viongozi wa CHADEMA, mkoa wa Dar es Salaam, wenye lengo la kukiondoa chama tawala madarakani.
Mfinanga alisema walifikiria kuanzisha mfumo huo, ili kuwawezesha wananchi kupata taarifa mbalimbali, kwa kuwa hivi sasa viongozi wa CCM, wanachukua chao mapema, wakielewa kuwa uchaguzi ujao hawatashinda.
Data Benki ya CHADEMA, inatoa ujumbe kila siku, na kila wiki, kutoa meseji mbalimbali, kutoka CHADEMA, lengo likiwa ni kuwangoa wabunge wanaolala bungeni, alisema.
Naye Katibu wa Vijana CHADEMA, Mkoa wa Dar es Salaam, Renatus Mlashani, aliwataka vijana kubadilika na kuchagua CHADEMA, baada ya Rais Jakaya Kikwete, kukiri kuwa hali ni mbaya nchini.
Alisema hivi sasa CCM imeshakufa, kilichobaki ni kuungana na kuingoa madarakani, kwa kuwa, hivi sasa vijana wanamaliza vyuo lakini hawajui waende wapi kwa sababu hakuna ajira.
Source:Tanzania Daima
Katibu wa jimbo hilo, Powell Mfinanga, alisema hayo mwishoni mwa wiki kwenye mkutano ulioandaliwa na viongozi wa CHADEMA, mkoa wa Dar es Salaam, wenye lengo la kukiondoa chama tawala madarakani.
Mfinanga alisema walifikiria kuanzisha mfumo huo, ili kuwawezesha wananchi kupata taarifa mbalimbali, kwa kuwa hivi sasa viongozi wa CCM, wanachukua chao mapema, wakielewa kuwa uchaguzi ujao hawatashinda.
Data Benki ya CHADEMA, inatoa ujumbe kila siku, na kila wiki, kutoa meseji mbalimbali, kutoka CHADEMA, lengo likiwa ni kuwangoa wabunge wanaolala bungeni, alisema.
Naye Katibu wa Vijana CHADEMA, Mkoa wa Dar es Salaam, Renatus Mlashani, aliwataka vijana kubadilika na kuchagua CHADEMA, baada ya Rais Jakaya Kikwete, kukiri kuwa hali ni mbaya nchini.
Alisema hivi sasa CCM imeshakufa, kilichobaki ni kuungana na kuingoa madarakani, kwa kuwa, hivi sasa vijana wanamaliza vyuo lakini hawajui waende wapi kwa sababu hakuna ajira.
Source:Tanzania Daima