Chadema Katavi-soma hii

Hili la ofisi si Mpanda tu hata hapa Dar, maeneo mengi hayana ofisi za CHADEMA, ningeshauri hivi, pamoja na mambo mengine ya wabunge, lakini wahamasishe watu kwenye maeneo yao wafungue matawi, ukweli kinachotakiwa na hamasa kidogo tu watu wako tayari kulipia ofisi kwa gharama zao na kukiendesha chama.

Uendeshaji wa ofisi za matawi ni mgumu. Ofisi za majimbo, wilaya na mikoa inaweza kuendeshwa kwa ruzuku na michango ya wanachama. Ni vigumu mno kumwajiri mtu wa kushinda ofisini asubuhi hadi jioni. Maeneo mengine ofisi hufunguliwa baada ya muda wa kazi na muda wenye matukio muhimu!.
 
Saidi Arfi ataondolewa akitaka asitake. Hii ni chokono imeanza.

Zitto, Safari, wangoje siku yao.

Jinsi haya mauaji ya chadema yanavyoendelea kuna kila sababu za hawa watu kutokukubalika kwani wao hawana imani ya kuuwa.
Suala sio udini kama unavyofikiri,Said Arfi kachaguliwa na wana Mpanda wa dini zote,na anapendwa hakuchakachua matokeo,mimi mwenyewe namkubali sana ni mtu mkarimu na muungwana sana asiye na majigambo ya aina yoyote,ni mtu ambaye nasikia akiwa jimboni anajichanganya hadi kwenye vijiwe vya kahawa na bila kuambiwa huwezi jua kama umekaa na mbunge.Nilichozungumzia cha kwanza ni suala la ofisi ,la pili uwepo wake jimboni na la tatu ambulance,sasa hayo ya dini unayotaka kuleta umeyatoa wapi?.Hamjakoma tu na huo udini wenu mnaoeneza,umewatafuna kwenye sensa lakini bado tu magamba hamjaona madhara ya kuendekeza udini na ukanda.
 
Suala sio udini kama unavyofikiri,Said Arfi kachaguliwa na wana Mpanda wa dini zote,na anapendwa hakuchakachua matokeo,mimi mwenyewe namkubali sana ni mtu mkarimu na muungwana sana asiye na majigambo ya aina yoyote,ni mtu ambaye nasikia akiwa jimboni anajichanganya hadi kwenye vijiwe vya kahawa na bila kuambiwa huwezi jua kama umekaa na mbunge.Nilichozungumzia cha kwanza ni suala la ofisi ,la pili uwepo wake jimboni na la tatu ambulance,sasa hayo ya dini unayotaka kuleta umeyatoa wapi?.Hamjakoma tu na huo udini wenu mnaoeneza,umewatafuna kwenye sensa lakini bado tu magamba hamjaona madhara ya kuendekeza udini na ukanda.

Tumeanza kwa Mungu tutamaliza kwa Mungu!
 
Hata mimi nakubaliana na mtoa hoja, kwanza CDM lazima wajifunze toka magamba japo magamba wanayo mengi maovu lakini mazuri pia yapo kwa hili la ofisi kila kijiji magamba wamejitahidi japo zimejengwa enzi za mwalimu na ni nguvu zetu pia.Lakini kwa cdm wanatakiwa kuiga toka magamba yaani iwe lazima kila kijiji kiwe na tawi na ofisi yake tena ya kisasa kasoro kiyoyozi na pembeni yake liwepo duka au kiosk ili kuifanya ofisi iwe buzzy wanaweza kujenga chumba cha duka halafu wakakodisha kwa mfanya biashara wa pale kijijini ili ofisi iwe live muda wote
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom