Chadema jaribuni sasa kuwaonyesha wananchi nini cha kufanya kabla ya kuingia madarakani

wa.JPG

hahahahahahahahaha
 
Namimi nakuombea maisha marefu uwe disappointed. Utanikumbuka. Chadema ni chama kwa ajili ya watu aina fulani tu si cha kila mtu, hilo halina siri.
Mkuu CCM ni kwa ajili ya watu maalumu wezi wadhurumati wauwaji na mafisadi wanaofilisi taifa letu ala Tanzani na wameficha fedha zetu huko nje ya nchi Uswiss , SA, CayMans Island offshore Banks!! Labda nikukumbushe kidogo kina Rostam Azizi na KAGODA, list ni ndefu, MEREMETA,DEEP GREEN, Kina IMMA Law FIRM sasa wanatoa majaji nadhani unanielewa!!! Hiyo ndiyo CCM tunayojitahidi kuitoa kwenye madaraka ili tuweze kuwashitaki na kurudisha mabilion yetu!!!Wewe uliyeko huko tunakupa pole maana watanzania woote wameisha funguka macho huwezi kuwadanganya!!!!

 
Mchango wa chadema katika kupambana na upuuzi wa ccm unajulikana.
Akili za tiss nu sawa na akili za mwigulu. Propaganda haisaidii lilote kwenye society ya watu wanaojitambua.

Get a life dude.
Mkuu sijui umefanikiwa kupitia Mjengwa Blog huyo Mwigulu kajimaliza kabisa kaonekana kituko Igunga hadi wananchi wachache waliokuja kwenye mkutano wakaondoka na kuacha kunsikiliza, Mwigulu kwishenei!!! People are tired of CCM and its blaaablaaaa!!!

 
Hawaezi kufanya lolote la maana washukuru hata waliambulia wabunge wachaaachee 2015 hata diwani ndoto
 
Haya basi CUF watapata madaraka ya kuiongoza hii nchi!
Wakuu ebu funguka huyo ni Zomba nduguye Mwigulu kaja hapa kupotezea jamvini kupotezea mada za maana!!! Tafadhari zingatia mada yetu huyo mtoa mada kaomba aelezwe CDM ina mkakati gani wa kuendeleza Watanzania???
Namwambia mtoa mada kuwa CDM haijapewa dola wape dola 2015 uone mipango kabambe tuliyo nayo (hasa ukiangalia kwanye katiba ya chama) na yanatekelezeka bila wasi wasi!!!

 
Tumeona kasi na ukuaji wa chama cha CHADEMA,kiukweli kasi yake ni kubwa na haishikiki.Hujuma nyingi wanafanyiwa ikiwa lengo la kukichafua chama na kukivunja nguvu ambayo imekuwa tishio kwa chama tawala.Kasi hii haiwezi kupuuzwa na kuachwa ipite hivi hivi tu bila kuwa na changamoto ambazo CDM lazima iweze kukabiliana nayo.

Watanzania humu nchini asilimia kubwa wamegubikwa na umasikini uliokithiri,wamekata tamaa ndiyo maana wanaona kimbilio la wakati huu ni CDM.Lakini cha msingi hapa ni kuto kubweteka kwa CDM na kudhani wame concur the world bila kufanyia kazi chanagamoto hizi zinazo wakabili Watanzania maskini.

Tumeona waziri wa serikali ya awamu ya nne ana kiri bila kutafuna maneno kuwa ule mkakati wa kuondoa umasikini hakufikia malengo yake,lakini hajatuambia nini kilichosababisha MKUKUTA 1 kushindwa kufikia malengo yaliyokusudiwa,zaidi ya umaskini kuongezeka japokuwa takwimu za makaratasi zinaonyesha umepungua kwa asilimia 2.6%.

Nchi ina lalamika,watu wake wanalalamika,serikali ina lalamika,wasomi wameshindwa kuonyesha na kutumia taaluma yao ili kuweza kuinusuru nchi na janga hili la kitaifa.

Kwakuwa hata watawala hawajui tatizo la umasikini wetu ni nini kiasi cha Watanzania kupoteza imani na chama tawala na kuamua kuhamishia nguvu za zote na matumaini yao kwa CDM,basi tunaishauri CDM ionyeshe njia kwa vitendo kuliko maneno ya majukwaani kwa kuwakomboa Watanzania kivitendo zaidi kuliko maneno.

Programme ya kwanza ya MKUKUTA haijafikia lengo,je nini plan B ya CDM ili kuweza kufikia malengo ya MKUKUTA.Pili kwa kuwa CDM wamejenga imani kwa wananchi na wananchi kuunga mkono harakati za M4C harakati hizo kwanini zisitumike sasa kwa kutengeneza mazinigra rafiki kwa shughuli za maendeleo ikiwa ni pamoja na kujenga hospitali zenye tija na kuboresha elimu kwa watoto wetu.

Changamoto ni nyingi ila support hii ya wananchi isiwafanye mbweteke kiasi cha kusahau matatizo ya Watanzania,kwa ushauri huu wa bure utatuweka Watanzania katika nafasi ambayo tutaamini CDM ndiyo kimbilio letu.Tunajua kweli hamna vyanzo vya mapato lakini mtaji mkubwa wa rasilimali watu mliojivunia katika operation Sangara kwa kuwavua gamba na kuwavalisha gwanda.

Mkakati huu ikiwezekana uitwe okoa uchumi wetu tunza rasilimali zetu.Wananchi wapo tayari kutumia nguvu na rasilimali walizonazo ikiwa tu watashirikishwa katika ujenzi was taifa letu na rasilimali zao.Wakati wa malumbano uimeisha tunataka plan B kuthibitisha mkipewa nchi mnaweza.Anzaeni sasa,tafakarini na chukueni hatua.Nawasilisha
Mkuu kabla ya kutekeleza mipango ya maendeleo lazima kwanza tuondoe corrupt system inayoruhusu wizi rushwa na ufisadi!!! Kufanya maendeleo kwenye hii corrupt system ni kama kutwanga maji kwenye kinu au kubeba maji kwenye kikapu, mifano iko mingi angalia TANESCO!!
Tafadhari soma hii taarifa toka EA Standard

Tiny Rwanda an example to EAC
The East African
10[SUP]th[/SUP] Sept 2012


Rwanda has once more been identified as the most attractive investment destination in East Africa, an achievement that should be a lesson to other members of the East African Community.

The latest survey by the World Economic Forum shows that Rwanda moved up seven places to number 63 out of 144 countries surveyed. It is quite impressive that Rwanda emerged third in Africa behind the much more developed economies of South Africa and Mauritius.

Kenya was a distant number 106 globally, Tanzania number 120, Uganda number 123 and Burundi number 144.Rwanda’s strength lies in its investor-friendly rules and regulations, as well as good security.

It is a warning shot for other countries, especially for Kenya, whose vibrant private sector, advanced infrastructure and unrivalled manpower are weighed down by red tape, corruption and political instability.

The other EAC member states need to borrow a leaf from Rwanda as the region seeks to position itself as a single investment destination.
This article was extracted from the link below
Tiny Rwanda an example to EAC *- Editorial*|theeastafrican.co.ke

 
Mchango wa chadema katika kupambana na upuuzi wa ccm unajulikana.
Akili za tiss nu sawa na akili za mwigulu. Propaganda haisaidii lilote kwenye society ya watu wanaojitambua.

Get a life dude.

Hizi ndio sera za Chadema.
 
Chama huwa kinaandaa ilani wakati wa uchaguzi ambazo inakuwa kama mkataba wanaotakiwa kuutekeleza pindi watakapopewa ridhaa. Nadhan muda bado.

Shughuli za maendeleo hazihitaji ilani mkuu,ilani ni muongozo wa shughuli unazo tarajia kuzifanya,cha msingi hapa nguvu ile ile ya M4C itumike pia kuhamasisha maendeleo na kuwa saidia vijana kupata ajira kwa kujiajiri kutokana na basket fund itayoanzishwa.Ni kimaanisha kiundwe chombo kitakacho tumika kuratibu mikopo na kuanzisha vikundi vya ujasilia mali.
 
Chadema waambieni wananchi CCM wameshindwa kuwafanyia a.b.c sisi Chadema tutawafanyia a.b.c. Siyo kuwaambia wananchi tunataka kuwakomboa utawakomboa kivipi wakati nchi zote duniani zimeishapata uhuru.
 
kuwahamasisha wananchi kuinyima kura haitoshi,kila mpiga kura ameelimika na ana jua machungu ya maisha yaliyosababishwa na sera mbovu za CCM,muhimu ianzishwe opereation nyingine itayoweza kuwakwamua wananchi kwa kuweza kujiletea maendeleo yao kabla ya uchaguzi wa 2015,ikifika 2015 CCM wenyeewe watapisha ikulu.


Mbona kila mikutano ya CDM wanawaambia wananchi Chakufanya mojawapo kubwa ni kuwanyima CCM kura wawape wao. Na baada ya hapo CDM itachukua Uongozi waanze kutekeleza Ilani yao ya Uchaguzi majibu yapo wazi Mkuu kama ni muudhuriaji mzuri wa mikutano yao lakini kama unategemea JF tuu itakuwa ngumu kidogo
 
Chadema waambieni wananchi CCM wameshindwa kuwafanyia a.b.c sisi Chadema tutawafanyia a.b.c. Siyo kuwaambia wananchi tunataka kuwakomboa utawakomboa kivipi wakati nchi zote duniani zimeishapata uhuru.
Watu wamekombolewa vipi wakati nyinyi na CCM yenu mnatuibia fedha na rasilimali zetu mchana kweupe bila woga wala aibu!!Kwa hiyo lazima watu wakombolewe na CDM toka mikono ya mafisadi CCM!!!

 
Back
Top Bottom