chadema itoke vipi mchakato katiba mpya?

February

Member
Nov 15, 2011
90
21
Juzi rais JK amekula moto na upinzani hususan chadema kwamba wanataka kuyumbisha nchi katika mchakato wa katiba mpya. Kama umesoma katikati ya mistari kitu kilichomtisha sana jk ni hoja ya kuwa na mchakato sambamba wa kupata katiba mpya kwani alianza kujiuliza na kujijibu mwenyewe. Anauliza hao wakienda kwa watu wataenda kama nani na kwa sheria ipi? Watatoa wapi uhalali? Ukiona adui anapinga mkakati wako jua huo mkakati ndio wenyewe. Wengi tuliomsikia kijana kafulila akichambua BBC namna ya kuendesha huo mchakato tulivutika sana. Najua nccr chama bado pengine ndio maana kafulila alikuwa akisisitiza iunganishwe nguvu kwa vyama kama chadema na wanaharakati nje ya siasa. Kwa mtazamo wangu chadema tuchukue wazo hili. Ni agenda ya kudumu. Ndo kampeni ya urais 2015. Ni mpambano wa katiba mpaka kinaeleweka. Naamini slaa akibeba agenda hii kuanzia sasa uchaguzi ujao hakuna namna ya kumzuia ikulu. Lazma cdm ibane hapo. Ikiachia tu jk anateleza.
 
Umesema sawa mkuu, lakini funguka zaidi ueleweke. Kuichukua ajenda kwa ajiri ya uchaguzi 2015 haitoshi. Tunapaswa tujiulize kwa sasa na pengine kushauri nini CDM na NCCR wafanye kuzima njama na ndoto za Kikwete na chama chake. Hatutaki mswaada uliopitishwa utumike
 
Haya magamba hatuyaamini kabisha, yanataka kuiacha nchi kwenye giza ninalo ona. Hawa majamaa yanampango wa kuchakachua katiba na kuandaa mazingira ya kulinda uharifu ulio fanywa na mafisadi.
Hebu jiulize eti kuna usalama wa taifa, kuna TAKUKURU, je kama hizi taasisi zipo iweje watu wanahujumu mali ya umma bila woga, hivi kweli hawa wanalipwa mishahara na marupurupu?
 
Umesema sawa mkuu, lakini funguka zaidi ueleweke. Kuichukua ajenda kwa ajiri ya uchaguzi 2015 haitoshi. Tunapaswa tujiulize kwa sasa na pengine kushauri nini CDM na NCCR wafanye kuzima njama na ndoto za Kikwete na chama chake. Hatutaki mswaada uliopitishwa utumike
Wishful thinking! Muswada utasainiwa na kutumika na nyie mlio mbumbumbu na madikteta wa kutaka kila mnalolipanga ndiyo liwe kaeni mkisubiri mikutano ya jukwaa la katiba wakati wabunge wenu wamekimbia hoja bungeni kwa sababu tu walitaka hiyo ndo waitumie kama ajenda na sasa wamenyang'anywa. Kwani CDM ni nani mpaka wadhani kwamba kila wanalotaka wao ndo lipite!
 
Back
Top Bottom