Chadema Itatwaa Dola Kama Itaendelea Kama Ilvofanya Arusha na Mwanza (Uwajibikaji, uwajibishaji)

Fredrick Sanga

JF-Expert Member
Jan 27, 2011
3,153
697
Chadema Itatwaa Dola Kama Itaendelea Kama Ilvofanya Arusha na Mwanza (Uwajibikaji, uwajibishaji)
Na: Fredrick Sanga

Baada ya kuangalia mfululizo wa matukio mbali mbali katika nchi hii, kisiasa na kiusalama. Naona ni vyema kutoa neno la hekima kidogo. CCM kwa kweli wamepoteza dira, katika itikadi (Ujamaa na Kujitegemea), hawpo sasa wanafuata itikadi ya ubepari uchwara (Rwaitama; 2012) aina ya wanachama (Wakulima na Wafanya kazi), kwa sasa CCM ni rushwa, ubabe, ubepari, ubwanyenye, ukabaila na ufisadi kwenda kwa mbele. Sawa CCM wanaweza wakashinda umeya Mwanza au ule ubunge Igunga, lakini swali linakuja kwamba, walizingatia kanuni zao, katika katiba yao; mfano rushwa ni adui wa haki au nitasema kweli daima fitina kwangu mwiko. Jibu analijua Nape na Mchemba. Chama cha namna hii hakiishii katika rushwa tu, kinaweza hata kutumia vyombo vya dola kudhoofisha upinzani, hii huwa inawaletea watumishi wa vyombo vya dola mgongano wa kimaslahi na kuharibika kimaadili. Matokeo yake ni hatari sana kwa Taifa, kwani yale ya Rwanda, Burundi na sasa Somalia yanaweza kutukuta.

Hivi karibuni tumeona jinsi Chadema ilivyosimamia kanuani zake na hata ikawagharimu kupoteza Meya na naibu wake huko Mwanza. Kwa kuangalia kwa juu juu, mmoja anaweza kusema kwamba CDM wamepoteza, Nionavyo mimi CDM wameanza kutekeleza kile ambacho watanzania tunakiitaji, yaani kuwajibishana badala ya kulindana. Matatizo mengi tuliyonayo yanatokana na kuweka vyama kwanza halafu umma unafuata baadaye, hili ni janga la Taifa, heri hata chama kikose dola kwa gharama ya maendeleo na maslahi ya Umma wa Tanzania. Na maendeleo hayaji hivi hivi tu bila kuwajibika na inapobidi kuwajibishana. What the use of having a useless Mayor anyway, ni kobomoa chama na kuugharimu umma.

Kwa falsafa ya nguvu ya umma, hatutegemei kabisa katika kipindi hiki cha miaka miwili CDM iendelee kumlinda kiongozi hata mmoja ndani ya CDM, hata kama ni nani, kama si muadilifu na mwenye maslahi kwa umma ang'olewe. Tukianza hivi sasa, hata tunapoenda kuchukua dola 2015, uwajibikaji utakuwepo. Tuanze sasa kwa umakini zaidi kuchunguza au kutathmini utendaji wa viongozi wote wa CDM, wale wa kichama, na wale walioingia katika uongozi wa umma. Kama ikigundulika kwamba wana walakini, basi waondolewe haraka hata ikibidi kupoteza hicho kiti. Kwani bila kufanya hivyo tutaleta dhana ya kubadilishana utawala na kuendelea na udhaifu uleule uliokuwepo kabla ya kubadili chama kinachotawala. Inabainika katika haya mambo ya kuunda serikali za mseto zisizo na dira. Zoezi la uwajibikaji liwe endelevu.

Kuendeleza mfumo wa CCM wa kulindana ndio hasa kutakakoondoa imani ya Umma wa Tanzania kwa CDM. Nashukuru sana kwamba siku tisini (90) za Nape ziliishaisha kitambo nao wanafikiri sisi tumesahau, tunakumbuka kila kitu alichozungumza na tutawahukumu vikali kwa hilo. Sasa hatutaki, nasema hatutaki CDM ilinde viongozi wabovu, dhaifu, wasiowajibika, wala rushwa, mafisadi nakadhalika, wanaojifanya miungu watu. Walichofanya Mwanza na Arusha iwe ni chachu tu, na mwanzo wa kujenga uongozi bora na kuvunja dhana ya bora uongozi = utawala bora.

Kwa sasa kazi ya M4C indelee kwa nguvu zaidi ili kutengeneza muundo mkakati wa kuwabana viongozi dhaifu hata ndani ya CDM. Nimeona katibu mkuu wa CDM amekuwa akilisimamia hili kwa nguvu na umakini mkubwa, akitumia muda wake mwingi, hadi kutia huruma. Unakuta mtu ni mwenyekiti wa wilaya wa CDM lakini hana faili hata moja, hana Taarifa hana mihutasari ya vikao, hata ule wa uchaguzi. Sasa huyu akitolewa katika uongozi, tuwazonge CDM, la hasha, tunataka uwajibikaji. Kuna madiwani wa CDM, ambao hawajui hata wajibu wao, mfano nenda Sinza ukajionee. Sasa tusije tukawa tunafuata nyayo za CCM. Viongozi wengine wa CDM tujiunge na katibu mkuu kukamulisha hili jukumu kabla ya 2014. Mafunzo ya kutosha kwa viongozi yanahitajika, na vichwa ngumu baibai. Hakika mafisadi watakapoinama na kuinuka watakuta CDM imo dolani.

Mwana wa Wasira ameongeza:
(i) Chadema ni Chama cha kizalendo na mkombozi wa dhati wa Mtanzania.
(ii) Chadema kinaleta matumaini mapya kwa Watanzania hasa vijana wasio na kazi na matumaini, Watanzania wenye maisha magumu hata kushindwa kumudu milo miwili kwa siku, akina mama wanaohangaika vijijini bila matibabu ya uhakika, maji, umeme, nyumba bora nk
(iii) CCM imedumaza nchi, nchi imekuwa kama mtu aliyedumaa kwa kukosa protein, haikui tena, Chadema ni damu mpya yenye kuweza kuingiza protein kwenye mishipa ya nchi iweze kufufuka na kukua tena.
(iv) Chadema kina viongozi imara na kwa maneno na matendo yake wanawadhihirishia watanzania kuwa ni waadilifu na wana nia njema ya kuipeleka Tanzania mbele. Alimalizia kwa kuwaasa vijana, akina mama na wazee wajiunge na M4C ili kuijenga Tanzania mpya. Alimalizia kwa kusema, "Kwa msaada wa Mungu, Tanzania Mpya inakuja.


Hakuna kulala mpaka kieleweke
By Fredrick Sanga (Mwanaharakati)Chadema Itatwaa Dola Kama Itaendelea Kama Ilvofanya Arusha na Mwanza (Uwajibikaji, uwajibishaji)
 
Mmm naona kitu hapa. Every good thing has a price to pay so called a sacrifice. There is a truth in what is in this thread, may be what we want is not just a change of a leader but leadership style. I can see CDM shall be willing even to step down the presidency if they train themselves this way. Not what we see now under CCM government, all crooks and good people in one pot. Salt and Sugar, Chittah and goat in a menger, it is comfusing
 
good leadership:200 milioni za kutalii rwanda-madiwani wa chadema moshi!


Baada ya kamanda Makongoro Wasira kujiunga na M4C siku chache zilizopita, leo tena watoto wengine wa Wasira wamejiunga na M4C na kukitupia virago Chama cha Baba yao CCM. Waliojiunga leo katika Makao makuu ya Chadema na kukabidhiwa kadi na Katibu Mkuu wa Chadema Dr Slaa ni kamanda Ester Wasira na Lilian Wasira. Wakizungumza na waandishi wa habari baada ya kukabidhiwa kadi walikuwa na haya ya kusema:
Ester wasira: (Ni mwanasheria, graduate wa UDSM)(i) Chadema ni Chama cha kizalendo na mkombozi wa dhati wa Mtanzania. (ii) Chadema kinaleta matumaini mapya kwa Watanzania hasa vijana wasio na kazi na matumaini, Watanzania wenye maisha magumu hata kushindwa kumudu milo miwili kwa siku, akina mama wanaohangaika vijijini bila matibabu ya uhakika, maji, umeme, nyumba bora nk(iii) CCM imedumaza nchi, nchi imekuwa kama mtu aliyedumaa kwa kukosa protein, haikui tena, Chadema ni damu mpya yenye kuweza kuingiza protein kwenye mishipa ya nchi iweze kufufuka na kukua tena.(iv) Chadema kina viongozi imara na kwa maneno na matendo yake wanawadhihirishia watanzania kuwa ni waadilifu na wana nia njema ya kuipeleka Tanzania mbele. Alimalizia kwa kuwaasa vijana, akina mama na wazee wajiunge na M4C ili kuijenga Tanzania mpya. Alimalizia kwa kusema, "Kwa msaada wa Mungu, Tanzania Mpya inakuja. Lilian Wasira (Mwanasheria, graduate wa TUDARCO)(i) Alielezea furaha yake kwa kujiunga na Chama makini na chenye kuleta matumaini mapya kwa mtanzania(ii) Aliwaasa vijana, akina mama na wazee wajiandikishe kwa wingi nafasi itakapotokea na 2015 wakamalizie kazi ya ukombozi kwa kuipigia Chadema kura(iii) Amewaasa Watanzania kuacha kulalamikia maovu ya CCM na kuchukua hatua ya kuiweka CCM pembeni na kuleta Chadema kama chama mbadala. Alisema hakuna sababu ya kuwa na mfumo wa vyama vingi kama watanzania hawathubutu kuchagua chama mbadala na badala yake kuendelea kuichagua CCM na kulalamika kila siku kuwa CCM imeshindwa kuongoza nchi(iv) Kwamba CCM imekuwa madarakani kwa zaidi ya miaka 50 hivyo ni wakati sasa wa kuiweka pembeni na kuingiza chama kipya, mawazo mapya na kujenga mfumo mpya wa uongozi. Hakuna kitu CCM imeshindwa kufanya kwa miaka 50 inaweza kufanya kwa miaka 5 au 10 ijayo.(v) Anasema ana imani na sera za chadema kuwa ndizo zitatukomboa. Amewapa moyo viongozi wa Chadema wasitishwe na vitisho na mauaji yanayofanywa na dola na kusema yupo tayari kwa M4C na yupo tayari kulipuliwa kama walivyolipuliwa wanachadema wengine na kuuawa kama itambidi afanye hivyo.(vi) Kwamba Chadema ni Chama kinachosubiri kuingia Ikulu isipokuwa tu watu wajiandikishe, wapige kura na walinde kura.(vii) Nae alimalizia kwa kusema "Kwa msaada wa Mungu Tanzania mpya inakuja."Dr Slaa alitiwa moyo sana na ujasiri ulioonyeshwa na vijana hawa pamoja na maneno ya kizalendo waliyoongea na akawakarisha kwenye uwanja wa mapambano ya M4C.
 

Baada ya kamanda Makongoro Wasira kujiunga na M4C siku chache zilizopita, leo tena watoto wengine wa Wasira wamejiunga na M4C na kukitupia virago Chama cha Baba yao CCM. Waliojiunga leo katika Makao makuu ya Chadema na kukabidhiwa kadi na Katibu Mkuu wa Chadema Dr Slaa ni kamanda Ester Wasira na Lilian Wasira. Wakizungumza na waandishi wa habari baada ya kukabidhiwa kadi walikuwa na haya ya kusema:
Ester wasira: (Ni mwanasheria, graduate wa UDSM)(i) Chadema ni Chama cha kizalendo na mkombozi wa dhati wa Mtanzania. (ii) Chadema kinaleta matumaini mapya kwa Watanzania hasa vijana wasio na kazi na matumaini, Watanzania wenye maisha magumu hata kushindwa kumudu milo miwili kwa siku, akina mama wanaohangaika vijijini bila matibabu ya uhakika, maji, umeme, nyumba bora nk(iii) CCM imedumaza nchi, nchi imekuwa kama mtu aliyedumaa kwa kukosa protein, haikui tena, Chadema ni damu mpya yenye kuweza kuingiza protein kwenye mishipa ya nchi iweze kufufuka na kukua tena.(iv) Chadema kina viongozi imara na kwa maneno na matendo yake wanawadhihirishia watanzania kuwa ni waadilifu na wana nia njema ya kuipeleka Tanzania mbele. Alimalizia kwa kuwaasa vijana, akina mama na wazee wajiunge na M4C ili kuijenga Tanzania mpya. Alimalizia kwa kusema, "Kwa msaada wa Mungu, Tanzania Mpya inakuja. Lilian Wasira (Mwanasheria, graduate wa TUDARCO)(i) Alielezea furaha yake kwa kujiunga na Chama makini na chenye kuleta matumaini mapya kwa mtanzania(ii) Aliwaasa vijana, akina mama na wazee wajiandikishe kwa wingi nafasi itakapotokea na 2015 wakamalizie kazi ya ukombozi kwa kuipigia Chadema kura(iii) Amewaasa Watanzania kuacha kulalamikia maovu ya CCM na kuchukua hatua ya kuiweka CCM pembeni na kuleta Chadema kama chama mbadala. Alisema hakuna sababu ya kuwa na mfumo wa vyama vingi kama watanzania hawathubutu kuchagua chama mbadala na badala yake kuendelea kuichagua CCM na kulalamika kila siku kuwa CCM imeshindwa kuongoza nchi(iv) Kwamba CCM imekuwa madarakani kwa zaidi ya miaka 50 hivyo ni wakati sasa wa kuiweka pembeni na kuingiza chama kipya, mawazo mapya na kujenga mfumo mpya wa uongozi. Hakuna kitu CCM imeshindwa kufanya kwa miaka 50 inaweza kufanya kwa miaka 5 au 10 ijayo.(v) Anasema ana imani na sera za chadema kuwa ndizo zitatukomboa. Amewapa moyo viongozi wa Chadema wasitishwe na vitisho na mauaji yanayofanywa na dola na kusema yupo tayari kwa M4C na yupo tayari kulipuliwa kama walivyolipuliwa wanachadema wengine na kuuawa kama itambidi afanye hivyo.(vi) Kwamba Chadema ni Chama kinachosubiri kuingia Ikulu isipokuwa tu watu wajiandikishe, wapige kura na walinde kura.(vii) Nae alimalizia kwa kusema "Kwa msaada wa Mungu Tanzania mpya inakuja."Dr Slaa alitiwa moyo sana na ujasiri ulioonyeshwa na vijana hawa pamoja na maneno ya kizalendo waliyoongea na akawakarisha kwenye uwanja wa mapambano ya M4C.[/SIZE]
hawa watakuwa wametumwa na baba yao au wanafuata nyao za baba yao
 
Chadema Itatwaa Dola Kama Itaendelea Kama Ilvofanya Arusha na Mwanza (Uwajibikaji, uwajibishaji)
Na: Fredrick Sanga

Baada ya kuangalia mfululizo wa matukio mbali mbali katika nchi hii, kisiasa na kiusalama. Naona ni vyema kutoa neno la hekima kidogo. CCM kwa kweli wamepoteza dira, katika itikadi (Ujamaa na Kujitegemea), aina ya wanachama (Wakulima na Wafanya kazi), kwa sasa CCM ni rushwa, ubabe na ufisadi kwenda kwa mbele. Sawa CCM wanaweza wakashinda umeya mwanza au ule ubunge Igunga, lakini swali linakuja kwamba, walizingatia kanuni zao, katika katiba yao; mfano rushwa ni adui wa haki au nitasema kweli daima fitina kwangu mwiko. Jibu analijua Nape na Mchemba. Chama cha namna hii hakiishii katika rushwa tu, kinaweza hata kutumia vyombo vya dola kudhoofisha upinzani, hii huwa inawaletea watumishi wa vyombo vya dola mgongano wa kimaslahi na kuharibika kimaadili. Matokeo yake ni hatari sana kwa Taifa, kwani yale ya Rwanda, Burundi na sasa Somalia yanaweza kutukuta.

Hivi karibuni tumeona jinsi Chadema ilivyosimamia kanuani zake na hata ikawagharimu kupoteza Meya na naibu wake huko Mwanza. Kwa kuangalia kwa juu juu, mmoja anaweza kusema kwamba CDM wamepoteza, Nionavyo mimi CDM wameanza kutekeleza kile ambacho watanzania tunakiitaji, yaana kuwajibishana badala ya kulindana. Matatizo mengi tuliyonayo yanatokana na kuweka vyama kwanza halafu umma unafuata baadaye, hili ni janga la Taifa, heri hata chama kikose dola kwa gharama ya maendeleo ya Umma wa Tanzania. Na maendeleo hayaji hivi hivi tu bila kuwajibika na inapobidi kuwajubishana. What the use of having a useless Mayor anyway, ni kobomoa chama na kuugharimu umma.

Kwa falsafa ya nguvu ya umma, hatutegemei kabisa katika kipindi hiki cha miaka miwili CDM iendelee kumlinda kiongozi hata mmoja ndani ya CDM, hata kama ni nani, kama si muadilifu na mwenye maslahi kwa umma. Tukianza hivi sasa, hata tunapoenda kuchukua dola 2015, uwajibikaji utakuwepo. Tuanze sasa kwa umakini zaidi kuchunguza au kutathmini utendaji wa viongozi wote wa CDM, wale wa kichama, na wale walioingia katika uongozi wa umma. Kama ikigundulika kwamba wana walakini, basi waondolewe haraka hata ikibidi kupoteza hicho kiti. Kwani bila kufanya hivyotuleta dhana ya kubadilishana utawala na kuendelea na udhaifu uleule uliokuwepo kabla ya kubadili chama kinachotawala. Inabainika katika haya mambo ya kuunda serikali za mseto zisizo na dira. Zoezi la uwajibikaji liwe endelevu.

Kuendeleza mfumo wa CCM wa kulindana ndio hasa kutakakoondoa imani ya Umma wa Tanzania kwa CDM. Nashukuru sana kwamba siku tisini za Nape ziliishaisha kitambo nao wanafikiri sisi tumesahau, tunakumbuka kila kitu alichozungumza na tutawahukumu vikali kwa hilo. Sasa hatutaki, nasema hatutaki CDM ilinde viongozi wabovu, dhaifu, wasiowajibika, wala rushwa, mafisadi nakadhalika, wanaojifanya miungu watu. Walichofanya Mwanza na Arusha iwe ni chachu tu, na mwanzo wa kujenga uongozi bora na kuvunja dhana ya bora uongozi = utawala bora.

Kwa sasa kazi ya M4C indelee kwa nguvu zaidi ili kutengeneza muundo mkakati wa kuwabana viongozi dhaifu hata ndani ya CDM. Nimeona katibu mkuu wa CDM amekuwa akilisimamia hili kwa nguvu na umakini mkubwa, akitumia muda wake mwingi, hadi kutia huruma. Unakuta mtu ni mwenyekiti wa wilaya wa CDM lakini hana faili hata moja, hana Taarifa hana mihutasari ya vikao, hata ule wa uchaguzi. Sasa huyu akitolewa katika uongozi, tuwazonge CDM, la hasha, tunataka uwajibikaji. Viongozi wengine wa CDM tujiunge na katibu mkuu kukamulisha hili jukumu kabla ya 2014. Hakika watakapoinama na kuinuka watakuta CDM imo dolani.

Hakuna kulala mpaka kieleweke
By Fredrick Sanga (Mwanaharakati)Chadema Itatwaa Dola Kama Itaendelea Kama Ilvofanya Arusha na Mwanza (Uwajibikaji, uwajibishaji)
Nilchofurahi sana ni suala la uwajibikaji na uwajibishaji.
 
Nilchofurahi sana ni suala la uwajibikaji na uwajibishaji.
Dr Lwaitama alitumia neno "CCM wanatumia mfumo wa Ubepari uchwara" hivi hawa jamaa wote unaowaona CCM, si ni wasaliti wa umma. Maana wanatudanganya kwamba waoni wajamaa. Hivi hata hiyo katiba ya tanganyika itarasimiwa na nani. Maana tume inaruka kimanga, kwamba Tanganyika haiwahusu, halafu wanasema ruksa kujadili muungano. Hawa jamaa wamechanganyikiwa? au mimi ndo siwaelewi?
 
Very good critical analysis.

Nikijaribu kulinganisha utendaji wa secretary ya CHADEMA vs CCM naona tofauti kubwa sana.

Kifupi CHADEMA wamejipanga vizuri sana kuongoza wananchi.
 
Very good critical analysis.

Nikijaribu kulinganisha utendaji wa secretary ya CHADEMA vs CCM naona tofauti kubwa sana.

Kifupi CHADEMA wamejipanga vizuri sana kuongoza wananchi.
Hata mimi nimeona. CCM inafuata system uchwara tu.
 
good leadership:200 milioni za kutalii rwanda-madiwani wa chadema moshi!

hio pesa haifiki bei ya benzi moja ya ikulu ambayo inatumika kumpeleka prezidaa air port kwenda msibani ghana
umekomalia hio mbona hutuambii mama tibaijuka na mkuu wa mkoa wa bukoba walienda kutembea uganda kuona ufugaji wa ngombe?
 
Kwa sasa inatakiwa CHADEMA kuwa makini kweli kweli kwani kuna MAMLUIKI kibao wanakimbia CCM na Kuingia CHADEMA ili kukiua kisiweze kushika Dola. Kila anayetoka CCM na kujiunga CHADEMA achunguzwe asije kutuulia Chama Chetu.
 
Kwa kweli ni wazi sasa tunaona tofauti kubwa kati ya CDM na ccm. CDM tukienda hivi, hata kipofu atagundua wazi kipi chama chenye maadili. Na kwa kweli tusidanganyane, Tanzania ya sasa inahitaji chama chenye maadili kitakachoweza kuweka serikali ambayo tutashuhudia kiongozi mwizi akihukumiwa, sio kufikishwa tu mahakamani kimagumashi halafu kesi haiishi na watu wanaendelea kula bata tu kitaa. CDM, huu ni mwelekeo mzuri sana, tunahitaji chama ambacho kiongozi anajiheshimu na anawaheshimu waliompa hiyo dhamana. NA HIYO NDIYO MAANA HASA YA NGUVU YA UMMA. Hatuhitaji chama ambacho kiongozi anageuka na kuwa mungu mtu, akiulizwa na wananchi anavimba na hata kutishia kuwaua utadhani yeye ndio mungu wao. Pipoooooooooozz -- Pawaaaaaaaaaaaa!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom