Chadema isitie aibu mrithi wa Regia!

Ndugu kuna watu hawataki hilo,yaani mtu hatakiwi kuhojihoji,vinginevyo anaambiwa katumwa na Nape yaani watu wamekuwa ni misukule ya vyama.

Hawajui kwamba 2015 Chama chenye kura nyingi ndio kitachoshinda na sio chenye kejeli
nyingi.


Mtu anapotoa comment kinyume na chama siku zote mwanachama anapaswa atoe maelezo kwa muhusika bila kuchoka ili mwisho wa siku ahamie kwenye chama chako,
ukijua kwamba kura moja ni dhahabu sasa hapa wanatukana na kukejeli wakitegemea 2015 watajitosheleza wenyewe,wakati ili upinzani ushinde ni lazima wapate ushindi wa Kimbunga.

Kifupi uchanga bado uko mwingi sana saana.

Ndio maana nimeamua ku dedicate time yangu ya kutosha kuwafundisha namna ya kufanya siasa hawa vijana "wanaojituma" humu kwa ajili ya chadema,wataelewa tu hata kwa kuwaburuza ikibidi,chama kimekuwa kikifanya vibaya kwenye chaguzi mbalimbali wakati mwingine kutokana kuwa na makada wa aina hii uliyoizungumza hapo juu,mfano kuna mmoja kaniita mimi mkata majani ya ng'ombe twice!yeye anaona kanikomesha mimi lakini anashindwa kuelewa hesabu rahisi tu kwamba kuna wakata majani ya ng'ombe wangapi kama mimi hapa nchini na je kwa kauli yake hiyo anadhani umaarufu wa chadema kwa wakata majani ya ng'ombe hautaathirika?sasa utaona ni suala la kutokufikiri tu hapa,anadhani kura yake tu na ya watu walio na maisha bora ndio itatosha kuipa ushindi cdm,ccm wanawashindia hapo ndugu zangu hawa lakini bahati mbaya hata wakishindwa huwa hawaji hapa kuambiana ukweli bali wanakuja hapa na visingizio vya kuibiwa kura kutwa wanaibiwa kura wao tu,lakini ukiwaambia mbona mzee wangu ndesamburo pale moshi au zitto kabwe kule kwake haibiwi kura zake,wanakaa kimya!
 
Wengi bado tuna kumbukumbu nzuri ya kilichotokea katika mchakato wa kuwapata wawakilishi wa viti maalum vya kina mama na vijana ndani ya CHADEMA wakati wa uchaguzi mkuu uliopita, ilikua aibu tupu.Waumini wa demokrasia tusingependa kuona chadema inatia tena aibu kwenye mchakato wa kujaza nafasi iliyoachwa wazi na mpiganaji Regia Mtema.

Tunajua yapo majina tayari ya wanaopaswa kuchukua nafasi hiyo kule tume ya uchaguzi kwa mujibu wa taratibu,hivyo basi tunaomba haki itendeke ndani ya chama hasa tukijiamisha ya kwamba chadema kama jina lake lilivyo ni chama cha kidemokrasia zaidi kuliko kisultani.

Nafasi hii itapendeza ikienda kwa mtoto wa mkulima kama alivyokuwa marehemu,sio lazima iende tena kwa watoto ama "wake" wa vigogo ndani ya chadema.Tunasema hivi kwa kuwa kuna dalili za kamchezo hako kuweko sana chadema na tumeshasikia tetesi kuna wake wa wakubwa huko wanaotajwa tajwa kumrithi marehemu na pia upo ushahidi uliozaa manung'uniko ya kuwepo kwa upendeleo wa ndugu na watoto wa vizito "kupewa" nafasi,mfano wapo watu sio wengi wanaolalamika na kudai watoto ama ndugu wa vigogo mfano ndesamburo,zitto n.k.

Walipendelewa kupata nafasi hizo kutokana na majina ya wakubwa hao..hili lisirudiwe kumrithi Regia.
Tatizo ni uelewa mdogo wa "criteria" za uteuzi wa wabunge wa viti maalum kwa baadhi ya wananchi na haswa wapenzi wa chama hiki wanaosikiliza propaganda za magamba. Ukweli ni kwamba zipo kanuni zinazoeleweka katika kufanywa uteuzi wa wabunge wa viti maalum na hata hao mnaosema wamewekwa na vigogo si kweli kabisa kama si uongo na uzushi wa mahasidi wao CCM. Juu ya kiti kilichoachwa na Mpiganaji Regia hilo liko wazi kwani kwa mujibu wa sheria zilizopo majina tayari yapo Tume na chama kitatakiwa tu kutibitisha kama jina la mteule walilo nalo bado ni "valid" yaani yupo, hajafa, hajashtakiwa na kufungwa, ana afya nzuri na bado ana akili timamu na wala hajakoma kuwa mwanachama wa chama husika.
 
Watu wasitake kupotosha , jina linalofuata baada ya wengine ni La subira waziri maarufu kama Koku , ni naibu katibu mkuu wa Bawacha na ni mzliwa wa jimbo la morogoro vijijini ambako makala ni mbunge, hivyo wana morogoro watakuwa hawajapoteza kitu ,ni kijana mwenye watoto wawili na nimchapa kazi kweli kweli maana tangu katibu mkuu wa Bawacha ahamie nccr mageuzi baada ya kunyimwa ubunge amekuwa akiiendesha bawacha kwa mafanikio sana, hata kura tulizopta igunga alichangia kwa kiasi kikubwa sana
 
Mrithi wa Regia atajwa
Na Richard Makore
21st January 2012
Ni Diwani wa kata moja wilayani Karatu
Alishika nafasi ya 26 Viti Maalum Chadema

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema mwanamke aliyeshika nafasi ya 26 katika majina 102 yaliyopelekwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), mwaka 2010 kwa ajili ya kufanyiwa uteuzi wa ubunge wa viti maalum, ndiye atakayemrithi marehemu Regia Mtema, aliyefariki dunia wiki iliyopita.
Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa, alisema hayo alipotakiwa na NIPASHE kutoa ufafanuzi kuhusu nafasi iliyoachwa wazi baada ya kifo cha marehemu Regia.
Habari zilizopatikana kutoka makao makuu ya Chadema, zinaeleza kuwa mwanamke aliyeshika nafasi ya 26 katika majina 102 yaliyopelekwa Nec, mwaka 2010 kwa ajili ya kufanyiwa uteuzi wa ubunge wa viti maalum, ni Cecilia Daniel Pareso.
Cecilia ni Diwani wa Kata ya Qurus, iliyoko katika Halmashauri ya Wilaya ya Karatu, mkoani Arusha.
Habari nyingine zinaeleza kuwa awali, mwanamke aliyekuwa akishika nafasi ya 26 ni aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha), Leticia Mosore, ambaye baadaye alihamia chama cha NCCR-Mageuzi.
Dk. Slaa alisema utaratibu wa kuwapata wabunge wa viti upo wazi kwa mujibu wa sheria na kwamba Chadema hawana mamlaka ya kuongeza wala kupunguza kitu chochote.
Alisema Chadema imeishamuandikia barua Spika wa Bunge, Anne Makinda, kumuarifa rasmi kwamba kuna nafasi iliyo wazi, ambapo naye ataiandikia barua Nec kwa ajili ya kufanya uteuzi rasmi.
Dk. Slaa alisema kuwa kama kutakuwa na mabadiliko ya mtu aliyeshika nafasi hiyo ya 26, ikiwamo mtu huyo kupoteza sifa ya kuwa mbunge kwa kuhama chama ama kuonekana na upungufu mwingine ambao unamnyima sifa, Chadema itaiandikia barua Nec ili achukuliwe mtu mwingine aliyeshika nafasi ya 27.
Alisema kama namba 26 na 27 wote hawatakuwa na sifa, Nec itachukua jina litakalofuata namba 28 ili kufanya uteuzi wa kiti hicho.
"Sisi kwa hili tulishalimaliza mwaka 2010 na tunachoweza kufanya kwa Nec ni kuisaidia itakapotaka maelezo yetu juu ya jina linalotakiwa kufanyiwa uteuzi," alisema Dk. Slaa.
Alisema mwaka 2010 walifanya kazi kubwa na kupata majina 102 ambayo yote yana sifa za kuwa wabunge wa viti maalum na kwamba, Nec ndiyo yenye mamlaka yote ya mwisho na sio Chadema.
Chadema kina wabunge wa viti maalum 25 katika Bunge la 10.



CHANZO: NIPASHE
 
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/89478-leticia-musore-wa-chadema-ahamia-nccr-7.html, Jamani ee,tumieni iyo address apo na mtapata jina la mtu anayefatia kwny orodha baada ya Mh Rebecca Mngodo, kazi ya tume ni kujiridhisha km bado ana sifa za kuwa mbunge au la,ktk hili chadema watahusishwa, na km anazo sifa hawatokuwa na namna yoyote kisheria kumpinga ili tu wamuibue mtu mwingine kutoka mahali patapowafurahisha wasiojua taratibu! Viti maalum havina uchaguzi mdogo, uchaguzi wake hufanyika mara moja ndani ya miaka mi5 kisha walokw kny orodha husubiri kuthibitishwa na tume kuzingatia ukomo kwa namna kila chama kinavostahili, kulijadili hilo sasa in a negative way ni umbumbumbu wa kisiasa, tujitahidi kukua kifikra ndugu zangu
 
Ngugu KAMATI KUU, Bi Subira alikuwa nafasi moja nyuma ya Bi Cecilia Daniel Pareso, so ikiwa Bi Cecilia atathibitika kuwa ana sifa za kuwa mbunge, Bi Subira itabidi aendelee kusubiri majaaliwa ya mwenyezi Mungu!
 
Back
Top Bottom