Dumelambegu
JF-Expert Member
- Jan 28, 2011
- 1,052
- 257
Wandugu,<br />
<br />
Nimeguswa na kusikitishwa sana na jinsi habari zinazohusu wabunge wa upinzani hususan wa chadema zinavyochakachuliwa wakati wa taarifa za habari kwenye vituo vya TV mojawapo ikiwa ni ITV. Jana wakati wa taarifa ya habari ya saa mbili usiku walionesha kwenye headlines habari ya wabunge wa chadema waliotolewa nje ya ukumbi wa bunge eti kwa kumi-miss behave. Lakini kwenye taarifa kamili tukio hilo halikuoneshwa kabisa. Ukweli ni kwamba lazima kulikuwa na amri kutoka juu iliyolazimisha taarifa hiyo hiyo isitolewe kwani ni jambo lisiloingia kichwani kwa mtu timamu kuona jambo linaonyeshwa kwenye headlines lakini kwenye habari yenyewe kamili linaondolewa. <br />
<br />
Nachojiuliza ni kwamba kama kweli wabunge walilikosea heshima bunge kiasi cha kufukuzwa nje ya ukumbi, kulikuwa na haja gani ya kuwaficha wananchi tukio hilo!? Kwa nini tukio hilo halikuonyeshwa kwa uwazi ili wananchi waone jinsi wabunge wa upinzani wasivyo na heshima!? Inavyoonekana ni kwamba ccm inatambua kuwa hoja iliyowafanya wabunge watolewe nje ilikuwa na mantiki na ya kizalendo na ingeungwa mkono na watanzania wengi. Kwa wenye akili hatuhitaji maelezo au uchambuzi wa kina kubaini hilo.
Lakini hiyo ni tisa, kumi ni ile hotuba ya Kambi rasmi ya Upinzani iliyosomwa na Mhe. Lema. Hotuba hiyo ni nzito, inasisimua na kuamsha ari ya ukombozi. Ni hotuba iliyosheheni maneno mazito yanayopenya ndani na kuamsha hisia kali kwa wananchi wazalendo wanaoipenda nchi yao. Ni bahati mbaya sana hotuba hiyo itaishia kusomwa kwenye magazeti tu (kama yapo yatakayochapishwa). Hapa ndipo ninapoona umuhimu wa chadema au mwanamapinduzi yeyote kuanzisha kituo cha TV. Ingekuwa hivyo, hotuba hiyo ingerushwa kwa wiki nzima mfululizo. Kuna haja ya viongozi wa chadema kutunza kumbukumbu hizi ili wakati muafaka ukifika matukio kama haya yarejewe na wananchi wapate fursa ya kuona na kusikia. Wadau mnasemaje?
<br />
Nimeguswa na kusikitishwa sana na jinsi habari zinazohusu wabunge wa upinzani hususan wa chadema zinavyochakachuliwa wakati wa taarifa za habari kwenye vituo vya TV mojawapo ikiwa ni ITV. Jana wakati wa taarifa ya habari ya saa mbili usiku walionesha kwenye headlines habari ya wabunge wa chadema waliotolewa nje ya ukumbi wa bunge eti kwa kumi-miss behave. Lakini kwenye taarifa kamili tukio hilo halikuoneshwa kabisa. Ukweli ni kwamba lazima kulikuwa na amri kutoka juu iliyolazimisha taarifa hiyo hiyo isitolewe kwani ni jambo lisiloingia kichwani kwa mtu timamu kuona jambo linaonyeshwa kwenye headlines lakini kwenye habari yenyewe kamili linaondolewa. <br />
<br />
Nachojiuliza ni kwamba kama kweli wabunge walilikosea heshima bunge kiasi cha kufukuzwa nje ya ukumbi, kulikuwa na haja gani ya kuwaficha wananchi tukio hilo!? Kwa nini tukio hilo halikuonyeshwa kwa uwazi ili wananchi waone jinsi wabunge wa upinzani wasivyo na heshima!? Inavyoonekana ni kwamba ccm inatambua kuwa hoja iliyowafanya wabunge watolewe nje ilikuwa na mantiki na ya kizalendo na ingeungwa mkono na watanzania wengi. Kwa wenye akili hatuhitaji maelezo au uchambuzi wa kina kubaini hilo.
Lakini hiyo ni tisa, kumi ni ile hotuba ya Kambi rasmi ya Upinzani iliyosomwa na Mhe. Lema. Hotuba hiyo ni nzito, inasisimua na kuamsha ari ya ukombozi. Ni hotuba iliyosheheni maneno mazito yanayopenya ndani na kuamsha hisia kali kwa wananchi wazalendo wanaoipenda nchi yao. Ni bahati mbaya sana hotuba hiyo itaishia kusomwa kwenye magazeti tu (kama yapo yatakayochapishwa). Hapa ndipo ninapoona umuhimu wa chadema au mwanamapinduzi yeyote kuanzisha kituo cha TV. Ingekuwa hivyo, hotuba hiyo ingerushwa kwa wiki nzima mfululizo. Kuna haja ya viongozi wa chadema kutunza kumbukumbu hizi ili wakati muafaka ukifika matukio kama haya yarejewe na wananchi wapate fursa ya kuona na kusikia. Wadau mnasemaje?