ZeMarcopolo
Platinum Member
- May 11, 2008
- 14,017
- 7,220
Hivi karibuni umeibuka mtindo wa CHADEMA kufungua matawi nje ya nchi. Tumesikia mgombea Urais mtarajiwa mh. Zitto Kabwe akishirikiana na mbunge wa Tanzania anayeishi Marekani mh. Leticia Nyerere wakifungua tawi Washington DC. Tawi hili la Washington DC baadae tuliona limepewa zawadi ya gari na mwanachama mkereketwa! Leo kumekuwa na taarifa ya aliyevuliwa ubunge wa Arusha Mjini Godbless Lema kuwa Uingereza kwa ajili ya ufunguzi wa matawi saba ya CHADEMA.
Ni dhahiri kuwa CHADEMA wameiga utaratibu huo kutoka CCM. Hata hivyo, tofauti na CCM, katika kufanya hivyo CHADEMA imeanzisha utaratibu huo "kimagumashi".
Kabla CCM haijaanza kufungua matawi nje ya nchi kitu cha kwanza kilikuwa ni kufanya marekebisho ya katiba ili ufunguaji wa matawi hayo ufanyike kwa kufuata katiba ya chama. Ndio maana katika katiba ya CCM sehemu ya tatu, Fungu la kwanza, 22 (1) (i-ii) kuhusu mashina ya chama, inaeleza kuwa kutakuwa na mashina ya ndani ya nchi na nje ya nchi. Katika fungu la pili, 31 (1) (d), imeelezwa kuwa kutakuwa na matawi ya nje ya nchi. Na imeelezwa bayana kuwa matawi hayo yatafunguliwa kwa indhini ya Katibu Mkuu wa chama. Ndani ya katiba ya CCM vikao vyote vya mashina na matawi ya nje ya nchi vimeelezwa kuwa vinafuata utaratubu upi wa uongozi.
Kwa upande wa CHADEMA, Katiba ya chama sura ya saba 7.2.1 inasema tawi litaundwa katika kila eneo la kijiji, mtaa au Shehiya ya kiutawala katika mamlaka za serikali za mitaa. Hata hivyo kinyume na katiba hii, katika mazingira ya "kimagumashi", viongozi wa CHADEMA wameanza kufungua matawi nje ya nchi! Haieleweki nani anatoa idhini ya matawi hayo kufunguliwa! Haieleweki matawi hayo yanamlolongo gani wa kiuongozi (wanareport kwa nani). Haieleweki nafasi ya viongozi wa matawi hayo katika uongozi wa chama! Kila anayeamua ananyanyuka na kwenda kufungua tawi nchi anayotaka, kwenye marafiki zake, kwa sababu zake!
Hata hivyo kwa vile mashabiki wa CHADEMA hawajajenga utaratibu wa kuhoji pale viongozi wao wanapoonekana kufanya "magumashi", mashabiki hao wamekuwa wakifurahia tu ufunguzi huu wa matawi.
Kuna taarifa kwamba kitendo cha Lema kwenda kufungua matawi Uingereza ni kwa ajili ya kumuwahi Zitto asiende pia kuweka kambi yake huko kama alivyofanya Marekani, lakini swali ni je, Zitto na Lema katika huku kuwahiana kwao wanafuata utaratibu upi kikatiba? Haya "magumashi" yao yanakipeleka wapi chama?
Mimi bado najiuliza, hawa watu wako serious na uongozi wa nchi yetu? Mbona maneno yao na matendo yao havifanani hata kidogo?
Ni dhahiri kuwa CHADEMA wameiga utaratibu huo kutoka CCM. Hata hivyo, tofauti na CCM, katika kufanya hivyo CHADEMA imeanzisha utaratibu huo "kimagumashi".
Kabla CCM haijaanza kufungua matawi nje ya nchi kitu cha kwanza kilikuwa ni kufanya marekebisho ya katiba ili ufunguaji wa matawi hayo ufanyike kwa kufuata katiba ya chama. Ndio maana katika katiba ya CCM sehemu ya tatu, Fungu la kwanza, 22 (1) (i-ii) kuhusu mashina ya chama, inaeleza kuwa kutakuwa na mashina ya ndani ya nchi na nje ya nchi. Katika fungu la pili, 31 (1) (d), imeelezwa kuwa kutakuwa na matawi ya nje ya nchi. Na imeelezwa bayana kuwa matawi hayo yatafunguliwa kwa indhini ya Katibu Mkuu wa chama. Ndani ya katiba ya CCM vikao vyote vya mashina na matawi ya nje ya nchi vimeelezwa kuwa vinafuata utaratubu upi wa uongozi.
Kwa upande wa CHADEMA, Katiba ya chama sura ya saba 7.2.1 inasema tawi litaundwa katika kila eneo la kijiji, mtaa au Shehiya ya kiutawala katika mamlaka za serikali za mitaa. Hata hivyo kinyume na katiba hii, katika mazingira ya "kimagumashi", viongozi wa CHADEMA wameanza kufungua matawi nje ya nchi! Haieleweki nani anatoa idhini ya matawi hayo kufunguliwa! Haieleweki matawi hayo yanamlolongo gani wa kiuongozi (wanareport kwa nani). Haieleweki nafasi ya viongozi wa matawi hayo katika uongozi wa chama! Kila anayeamua ananyanyuka na kwenda kufungua tawi nchi anayotaka, kwenye marafiki zake, kwa sababu zake!
Hata hivyo kwa vile mashabiki wa CHADEMA hawajajenga utaratibu wa kuhoji pale viongozi wao wanapoonekana kufanya "magumashi", mashabiki hao wamekuwa wakifurahia tu ufunguzi huu wa matawi.
Kuna taarifa kwamba kitendo cha Lema kwenda kufungua matawi Uingereza ni kwa ajili ya kumuwahi Zitto asiende pia kuweka kambi yake huko kama alivyofanya Marekani, lakini swali ni je, Zitto na Lema katika huku kuwahiana kwao wanafuata utaratibu upi kikatiba? Haya "magumashi" yao yanakipeleka wapi chama?
Mimi bado najiuliza, hawa watu wako serious na uongozi wa nchi yetu? Mbona maneno yao na matendo yao havifanani hata kidogo?