Chadema inabadilisha Nchi na Chama Cha Mapinduzi!!

Kamundu

Platinum Member
Nov 22, 2006
6,605
8,744
Hata kama si mshabiki wa Chadema sisi tulio nje tunaona mabadiliko makubwa ya nchi yetu. Nchi yetu inabadilika kwa uzuri na hata chama tawala cha CCM kinabadilika!!. Hili ni swala muhimu sana kwamba kwa mara ya kwanza kwenye historia Chama tawala kinaogopa watu!. Kwa mara ya kwanza kihistoria Chama cha CCM kinajikosoa chenyewe hadharani bila kujifungia kwenye chumba. Kwa mara ya kwanza naona kuna kaheshima kidogo kwa wananchi kutoka Chama tawala. Hata kama Chadema isiposhinda lakini ikaendelea hivi ni nzuri kwa nchi kwani hata Chama Tawala kubadilika ni vizuri kwa nchi. Ninawapa pongezi Chadema kwa kubadilisha nchi yetu kwa uzuri. CCM itasema kwamba wanabadilika wenyewe lakini si kweli ni kwasababu ya uoga wa kukosa madaraka na kuamshwa kisiasa hili ni jambo zuri sana kwa nchi. Sasa hivi hakuna siri kwenye chochote serikalini tena na sasa tunaona kama maovu ambayo tulikuwa hatuyajui na ndiyo maana tunaona ufisadi lakini ufisadi umefanyika siku nyingi sana. Vilevile Chadema imesaidia kuwaamsha watanzania wafanyakazi wa serikali ambao hawaogopi kuvujisha data kwa vyombo vya habari kwa manufaa ya nchi. Kuna wengi wa kushukuru lakini Chadema ni wa kwanza na vyombo vya habari ni vya pili.
 
Na labda nikseme ktk sifa ambazo pekee naweza kumpa JK ni kutoa Uhuru huu kwani anaweza kabisa kufunga milango kama alivyokuwa Mkapa..Na imewezekana tu kutokana na jadi yake maana mswahili hupenda majungu na drama hivyo kwa kila lisemwalo humpa kicheko na wakati mwingine kuchukia, maadam anakula na kulala siku imepita.. - Ndio maisha ya mwafrika!...
 
Hata kama si mshabiki wa Chadema sisi tulio nje tunaona mabadiliko makubwa ya nchi yetu. Nchi yetu inabadilika kwa uzuri na hata chama tawala cha CCM kinabadilika!!. Hili ni swala muhimu sana kwamba kwa mara ya kwanza kwenye historia Chama tawala kinaogopa watu!. Kwa mara ya kwanza kihistoria Chama cha CCM kinajikosoa chenyewe hadharani bila kujifungia kwenye chumba. Kwa mara ya kwanza naona kuna kaheshima kidogo kwa wananchi kutoka Chama tawala. Hata kama Chadema isiposhinda lakini ikaendelea hivi ni nzuri kwa nchi kwani hata Chama Tawala kubadilika ni vizuri kwa nchi. Ninawapa pongezi Chadema kwa kubadilisha nchi yetu kwa uzuri. CCM itasema kwamba wanabadilika wenyewe lakini si kweli ni kwasababu ya uoga wa kukosa madaraka na kuamshwa kisiasa hili ni jambo zuri sana kwa nchi. Sasa hivi hakuna siri kwenye chochote serikalini tena na sasa tunaona kama maovu ambayo tulikuwa hatuyajui na ndiyo maana tunaona ufisadi lakini ufisadi umefanyika siku nyingi sana. Vilevile Chadema imesaidia kuwaamsha watanzania wafanyakazi wa serikali ambao hawaogopi kuvujisha data kwa vyombo vya habari kwa manufaa ya nchi. Kuna wengi wa kushukuru lakini Chadema ni wa kwanza na vyombo vya habari ni vya pili.

ungetoa data ingependeza..unadai ni uwepo wa CDM ndio maana CCM inajivua gamba..nadhani umepotoka..Kasome Mwongozo wa CCM wa 1982 ambao unaelekeza chama kujikosoa na kujisahihisha..usiwe tu unakurukupia mambo..ebo?
 
I have tried to extract a point from your essay but vainly. All I found is a tenuous statement devoid of any substance.
 
Mkandara,

Heri angelifunga ila nchi ikawa na umeme na kodi ikakusanywa.

Huu uhuru tulionao unatusaidia nini? Wachina sasa ni No. 1 na huko hakuna kufurukuta.

Hata Russia na ubaya wake, wana nafuu sana kwa sasa. Anyway, hayo ni mawazo yangu tu.
 
Mimi nilichofurahishwa na Chadema kuliko vyote ni kusimama from the huge crowd kwamba wao ndiyo upinzani in a way ule utitiri wa vyama sasa unaonekana ni irrelevant hata kwa watu wa kawaida kabisa. Ukiangalia vyama kama TLP na UDP ndiyo vinaishia hivyo maana vinabebwa na majina ya wenyeviti wao ukitoa hao huna chama wala baba yake chama!!!!!!
 
Huyo anayeomba statistics nizi hapa. EPA imeanzishwa na kupigiwa kelele kwanza na Chadema, Ujenzi wa rushwa wa jengo mpya la bank kuu ulianzishwa na kupigiwa kelele na Chadema, Richmond ilianzishwa na kupigiwa kelele na Chadema. Kwanini CCM imeamua kujivua gamba sasa hivi Rostam alikuwepo kwa miaka 15 na kashfa zilezile, IPTL ilikuwepo, Mgao ulikuwepo, Rada ilikuwepo sasa kwanini kujivua gamba sasa hivi ni kwasababu ya nzuvu ya upinzani na kuchoshwa kwa watu. Mimi sijali nani anaongoza nchi lakini nahitaji maendeleo kwa nchi yangu.
Tanzania ndiyo nchi pekee nayoijua ambako umeme wa pre-paid unakatwa!, shule zinazofelisha kila mwaka bado ziko wazi na kulipisha wanafunzi na watu wanaushabikia serikali kwamba inafanya vizuri. Barabara zinajengwa na misaada ya Japan na USA, shule zinajegwa na Norway, German inasaidia maji, Bill Gates anatusaidia Afya wakati tuna kampuni za Gold ambazo hatujui pesa imeenda wapi!!!!. Kama unashabikia kinachoendelea Tanzania ni kwasababu ya ubinafsi lakini iko siku ndugu yako atapata stroke na ndiyo utajua nasema nini!! hata pesa ya ufisadi haitaweza kumkimbiza India!
 
ungetoa data ingependeza..unadai ni uwepo wa CDM ndio maana CCM inajivua gamba..nadhani umepotoka..Kasome Mwongozo wa CCM wa 1982 ambao unaelekeza chama kujikosoa na kujisahihisha..usiwe tu unakurukupia mambo..ebo?

Miaka yote hiyo walikuwa wapi kujikosoa na kujisahihisha na hali wamekuwa wakifanya madudu? muwe munakubali ukweli bwana! Na bado wewe endelea tu utakimbia mwenyewe hapa. Zungumzia maswala ya umeme, mfumuko wa bei, maji nk sio unakuja na utumbo hapa. CCM inakimbizwa mchakamchaka na Chadema na ndio maana haya mabadiliko tunayaona leo. Kama muongozo ulikuwepo kwanini muje muutumie leo wakati toka miaka hiyo yote chama kinabolongo tu? mbona marehemu kolimba aliposema CCM kimepoteza dira hamkujikosoa?
 
Nakubaliana na wewe kabisa,chadema imefanya kazi kubwa sana pongezi zote nawapa kwa moyo mmoja,nashukuru pia kwa kuniamsha mimi binafsi, huyo anayeomba data mwacheni labda si mtanzania,kwa sababu wananchi wengi kwa ujumla tunatambua mchango wa chadema na kama wapo wanaopinga kabisa basi wana mapungufu fulani,
 
Mkandara,

Heri angelifunga ila nchi ikawa na umeme na kodi ikakusanywa.

Huu uhuru tulionao unatusaidia nini? Wachina sasa ni No. 1 na huko hakuna kufurukuta.

Hata Russia na ubaya wake, wana nafuu sana kwa sasa. Anyway, hayo ni mawazo yangu tu.
Mkuu swala sii heri kitu gani maana ukiniuliza mimi nitasema heri asingegombea kabisaaa urais. Tunachozungumzia ni kidogo alichowezesha kati ya kumi aweza moja ingawa nchi imerudi nyuma miaka 10...

Ebu fikiria kama JK singheweza hata kutoa uhuru huu wakati kichwa chake kimelenga Udikteta wa Mkapa sijui tungekuwa wapi leo hii maana matatizo yaliyopo leo hayakuanza jana. Toka Mwinyi hadi Mkapa lugha tunayotumia ni ile ya...WANGE... kwa maana ya mapungufu yao. Kukosekana kwa umeme ni moja ya mapungufu makubwa ya JK na utawala mzima wa CCM.
 
ungetoa data ingependeza..unadai ni uwepo wa CDM ndio maana CCM inajivua gamba..nadhani umepotoka..Kasome Mwongozo wa CCM wa 1982 ambao unaelekeza chama kujikosoa na kujisahihisha..usiwe tu unakurukupia mambo..ebo?

Wala hajakurupuka. CCM walisha yazika yoye hayo, (kama walivyozika Azimio la arusha, ujamaa etc) uwepo wa chadema ndio umewazindua kama wewe unavyozinduka kukumbuka mwongozo wa Nyerere ( ambaye alikuwa mwadilifu bila mfano wake ). Yote wanayo lakini wameyazika.
 
ungetoa data ingependeza..unadai ni uwepo wa CDM ndio maana CCM inajivua gamba..nadhani umepotoka..Kasome Mwongozo wa CCM wa 1982 ambao unaelekeza chama kujikosoa na kujisahihisha..usiwe tu unakurukupia mambo..ebo?
mkuu kuwepo kwa mwongozo ccm wangianza kujikosoa tangia cdm hawajanza kuwakosoa kwani ufisadi ccm wameanza tangia kuanzishwa kwa cdm. Mwongozo kitu gani mbona sheria zinawekwa na hawahawa viongozi wetu na kutozifuta ndio wao wakwanza, CHENYE MWANZO HAKIKOSI KUWA NA MWISHO NA HUU NDO MWISHO WA CCM aka MAGAMBA
 
Kwa mara ya kwanza kihistoria Chama cha CCM kinajikosoa chenyewe hadharani bila kujifungia kwenye chumba. Kwa mara ya kwanza naona kuna kaheshima kidogo kwa wananchi kutoka Chama tawala. Hata kama Chadema isiposhinda lakini ikaendelea hivi ni nzuri kwa nchi kwani hata Chama Tawala kubadilika ni vizuri kwa nchi
.

Nami ninatambua Mchango mkubwa wa CDM na hivyo kukubaliana na sehemu kubwa ya mchango wako lakini hapo kwenye RED ndio tunapingana. Na ninaomba tukubaliane kutokukubaliana. Kimsingi CDM imejengwa na viongozi makini ambao hata wasipokuwepo Bungeni bado mchango wao unaweza kuonekana uraiani, lakini ni vizuri kutambua kuwa usimamizi mzuri wa seikali ungekuwepo kama CDM wangekuwa na seat nyingi Bungeni. Hivyo nibora kuwahimiza wananchi kutambua mchango mkubwa wa vyama vya upinzani haswa CDM ili wavipe kura nyingi na vizidi kutuwakilisha. Angalia ni hoja ngapi zilizozimwa bungeni kwa sababu ya wingi wa wabunge wa CCM
 
Bora mwili ukiwa na magamba unaangalau tumaini utachukua hata vipande vya chupa na visu uyatoe,magamba yakiwa kwenye ubongo utayatoa kweli aaaaah,hivi leo 2011 eti mtu anahitaji data nakuleta mwongozo wa 1982!!so!umekusaidia nini mlipokuwa mnaiba benki kuu hako ka mwongozo kenu hakakuwepo, unajua unaweza ukawa mzima unatembea unaenda kazini unaenda michezoni kumbe haupo na sisi ulisha jifia siku nyingi umebaki picha tu.
 
HAKUNA MAREFU YASIYOKUWA NA MWISHO WANANCHI WOTE WANAKARIBIA KUJUA HILO KABLA YA Mwaka 2015 tuungane kwa pamoja kuufikia mwisho huu.Tuache ushabiki wa kijinga bali nchi kwanza CDM wanafanya kazi kiukweli hakuna hata haja ya kumsifia JK bali huwezi kuziba midomo ya watu wenye hasira kama wakati huu nenda kokote Tz wananchi wanaihukumu CCM.
 
ungetoa data ingependeza..unadai ni uwepo wa CDM ndio maana CCM inajivua gamba..nadhani umepotoka..Kasome Mwongozo wa CCM wa 1982 ambao unaelekeza chama kujikosoa na kujisahihisha..usiwe tu unakurukupia mambo..ebo?
Kweli wewe ni pumbatupu wa ukweli!!
 
Na labda nikseme ktk sifa ambazo pekee naweza kumpa JK ni kutoa Uhuru huu kwani anaweza kabisa kufunga milango kama alivyokuwa Mkapa..Na imewezekana tu kutokana na jadi yake maana mswahili hupenda majungu na drama hivyo kwa kila lisemwalo humpa kicheko na wakati mwingine kuchukia, maadam anakula na kulala siku imepita.. - Ndio maisha ya mwafrika!...
kwa akili yako unadhan JK katoa huu unaouita uhuru? Muda umemlazimisha, hakuna utawala unaoweza kunyamazisha watu kwa jinsi technolojia ilivyokua
 
Hakika wewe ni "pumba tupu"
ungetoa data ingependeza..unadai ni uwepo wa CDM ndio maana CCM inajivua gamba..nadhani umepotoka..Kasome Mwongozo wa CCM wa 1982 ambao unaelekeza chama kujikosoa na kujisahihisha..usiwe tu unakurukupia mambo..ebo?
 
ungetoa data ingependeza..unadai ni uwepo wa CDM ndio maana CCM inajivua gamba..nadhani umepotoka..Kasome Mwongozo wa CCM wa 1982 ambao unaelekeza chama kujikosoa na kujisahihisha..usiwe tu unakurukupia mambo..ebo?
Wewe acha upuuzi! Mwongozo upi umewahi kutekelezwa! danganya wahisani hizo! ili wapate misaada waibe na kushibisha matumbo yao sasa wamejulikana wanajitetea.
 
Back
Top Bottom