Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
- Thread starter
- #21
Je tunaweza kuamini kuwa Chadema ilivyo sasa inaweza kuongoza Taifa la watu karibu milioni 40, kuunda serikali na kuisimamia serikali hiyo kwa uaminifu kushinda CCM? Ni kitu gani kinawafanya watu waamini kuwa Chadema ikiingia madarakani basi matatizo kadhaa ya ufisadi yatakomeshwa na kutakuwa na nidhamu mpya ya matumizi ya fedha na raslimali za taifa letu?
NI jambo moja kuangalia suala kwa mwanga wa kisoma (intellectual perspective) na jambo jingine kabisa kulisimamia na kufuatilia jambo kiutawala. Mtu anayeweza kuona matatizo ya sekta ya madini kisomi ukimpa nafasi ya kutawala atalazimika kuangalia maslahi zaidi ya yale anayoyaona kisomi. Nyerere alitoa mfano mzuri sana kuhusu kutaifishwa kwa mashamba ya Mkonge. Alisema kuwa kiakili aliona umuhimu wake lakini ilipokuja utekelezaji kulikuwa na kuboronga kwa hali ya juu.
Sasa ni kitu gani kinawafanya watu waamini kuwa ati Chadema ikiingia madarakani sasa hivi basi matatizo kadha wa kadha ya kiutawala na utendaji yataondolewa na Tanzania itaanza safari ya kuelekea matumaini? Je tumejifunza lolote kutoka Kenya, Zambia, Malawi ambapo vyama vya upinzani viliingia na kushika madaraka.
Je ni kitu gani kitaizuia Chadema ikiwa madarakani kuanza kutengeneza mfumo wa kutumia serikali kunufaisha Chama kama CCM wanavyofanya? Tunategemea wema au ahadi za watu?
NI jambo moja kuangalia suala kwa mwanga wa kisoma (intellectual perspective) na jambo jingine kabisa kulisimamia na kufuatilia jambo kiutawala. Mtu anayeweza kuona matatizo ya sekta ya madini kisomi ukimpa nafasi ya kutawala atalazimika kuangalia maslahi zaidi ya yale anayoyaona kisomi. Nyerere alitoa mfano mzuri sana kuhusu kutaifishwa kwa mashamba ya Mkonge. Alisema kuwa kiakili aliona umuhimu wake lakini ilipokuja utekelezaji kulikuwa na kuboronga kwa hali ya juu.
Sasa ni kitu gani kinawafanya watu waamini kuwa ati Chadema ikiingia madarakani sasa hivi basi matatizo kadha wa kadha ya kiutawala na utendaji yataondolewa na Tanzania itaanza safari ya kuelekea matumaini? Je tumejifunza lolote kutoka Kenya, Zambia, Malawi ambapo vyama vya upinzani viliingia na kushika madaraka.
Je ni kitu gani kitaizuia Chadema ikiwa madarakani kuanza kutengeneza mfumo wa kutumia serikali kunufaisha Chama kama CCM wanavyofanya? Tunategemea wema au ahadi za watu?