Chadema imefanikiwa kutoa somo la uraia nchini

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,890
6,896
167043_116610821744803_100001876575512_129089_3593898_n.jpg


Kwa mtazamo wa haraka na ninavyoona kada mbalimbali zinavyoamka kudai haki zao za msingi na jinsi serikali haikujipanga kufanya mambo kwa utaratibu unaweza kuaminika na kukubalika ni dhahiri elimu ya uraia ya Chadema imewafungua akili wengi. Serikali ijue sasa wananchi wameanza kuelewa nini serikali inatakiwa iwafanyie na haki zao za msingi haziwezi kuwekea rahani maisha yao kwa ajili ya wachache wanaonufaika na matunda ya mti tunaomwagilia wote.
 
Kaka umeweka kisu kwenye mfupa. U have hit the nail on the head. Tehe tehe tehe. Kitu kingine cha muhimu kabisa ambacho kinapaswa kuendelea kueleweka kwa watu, Watanzania ni juu ya dhana na msingi wa amani na utulivu vinavyoimbwa na watawala kwenye majukwaa, maneno bila vitendo. Sasa wananchi wanaanza kuelewa na wanapaswa kuendelea kuelewa kuwa msingi wa amani na utulivu ni utendekaji wa haki na matumaini waliyonayo wananchi kwa uongoz/viongozi.

Vinginevyo, tutakuwa tunaelekea kubaya. Walioko madarakani ambao wamejigeuza kuwa watawala badala ya kulongola njia, kama ilivyo mantiki ya uongozi, wanapaswa kujua kuwa umma sasa umeamuka, wanataka kuona uwajibikaji wa serikali na viongozi wake katika kutengeneza fursa za Watanzania kutoa jasho lao na kujienedeleza. Umma umetekeleza wajibu sasa unadai haki. Unataka wajibu na haki viende sambamba na ionekane hivyo. Aluta continua mkuu.

Ni class struggle ya wazi kabisa. Kupigania haki na wajibu. Panapokuwa na uminywaji wa haki, ukiamua kuwa neutral, umechagua kuwa upande wa mvunja haki na mkandamizaji.
 
Bado haijafanikiwa hasa katika eneo la madhara ya uhuru wa kutoa taarifa kwa umma kama hauna uhakika nazo. Jf tumekuwa wakati mwingine tunatengeneza taarifa za uongo na kuzirusha humu kwa lengo la kuijeruhi CCM au Chadema lakini kumbe tunaijeruhi nchi yetu. Bado hatuna utaifa.
 
Nchi ni kubwa kazi hii sio ya muda mfupi hata kama chadema ina lengo hilo. Chadema haijafanikiwa.
 
Bado haijafanikiwa hasa katika eneo la madhara ya uhuru wa kutoa taarifa kwa umma kama hauna uhakika nazo. Jf tumekuwa wakati mwingine tunatengeneza taarifa za uongo na kuzirusha humu kwa lengo la kuijeruhi CCM au Chadema lakini kumbe tunaijeruhi nchi yetu. Bado hatuna utaifa.

Katika uwanja wa mapambano madhara ya wasiohusika na mapambano hayawezi kuepukika. Watakaofaidi matunda watajua historia ya waliotengeneza njia ya kufikia walipo.
 
Kabisa Mkuu. Hata hivyo, pamoja na CHADEMA kufanya mengi, bado Mkutano wa Septemba 15, 2007, Mwembeyanga, Dar es Salaam utabaki katika historia ya vizazi na vizazi kama mwanzo mpya wa taifa letu. Mkutano huo uliokuja na hitimisho lililoitwa "Orodha ya Aibu - List of Shame" neno kuu likiwa UFISADI kwa kuthubutu kuwataja mafisadi HADHARANI hakika siku hii itabaki katika historia.

Kama mnakumbuka akina Makamba (former CCM Secretary General) na wenzake wakaibuka wakijidai eti neno UFISADI halikuwa katika KAMUSI YAO (ya CCM) lakini leo hadi Mwenyekiti wao anaimba na kucheza ngoma ya UFISADI; labda wamesharekibisha hiyo kamusi waliyoikana mwanzoni!

Kwa wale ambao hatukuwepo wakati wa Uhuru wa kwanza wa Mwl. Nyerere (Desemba 9, 1961) angalau Septemba 15, tuliweza kushuhudia Uhuru wa Pili wa kimawazo, kifikra, uthubutu, na mwanzo mpya chini ya Dr. Wilbroad Slaa, Katibu Mkuu wa Chadema na makamanda wenzake.
 
Kabisa Mkuu. Hata hivyo, pamoja na CHADEMA kufanya mengi, bado Mkutano wa Septemba 15, 2007, Mwembeyanga, Dar es Salaam utabaki katika historia ya vizazi na vizazi kama mwanzo mpya wa taifa letu. Mkutano huo uliokuja na hitimisho lililoitwa "Orodha ya Aibu - List of Shame" neno kuu likiwa UFISADI kwa kuthubutu kuwataja mafisadi HADHARANI hakika siku hii itabaki katika historia.

Kama mnakumbuka akina Makamba (former CCM Secretary General) na wenzake wakaibuka wakijidai eti neno UFISADI halikuwa katika KAMUSI YAO (ya CCM) lakini leo hadi Mwenyekiti wao anaimba na kucheza ngoma ya UFISADI; labda wamesharekibisha hiyo kamusi waliyoikana mwanzoni!

Kwa wale ambao hatukuwepo wakati wa Uhuru wa kwanza wa Mwl. Nyerere (Desemba 9, 1961) angalau Septemba 15, tuliweza kushuhudia Uhuru wa Pili wa kimawazo, kifikra, uthubutu, na mwanzo mpya chini ya Dr. Wilbroad Slaa, Katibu Mkuu wa Chadema na makamanda wenzake.

Kama maandamano yao yanakubalika kwa nini wamesitisha? Si wameona hayaleti manufaa kwao bali ni kujazana na kesi mahakamani?
 
Kabisa Mkuu. Hata hivyo, pamoja na CHADEMA kufanya mengi, bado Mkutano wa Septemba 15, 2007, Mwembeyanga, Dar es Salaam utabaki katika historia ya vizazi na vizazi kama mwanzo mpya wa taifa letu. Mkutano huo uliokuja na hitimisho lililoitwa "Orodha ya Aibu - List of Shame" neno kuu likiwa UFISADI kwa kuthubutu kuwataja mafisadi HADHARANI hakika siku hii itabaki katika historia.

Kama mnakumbuka akina Makamba (former CCM Secretary General) na wenzake wakaibuka wakijidai eti neno UFISADI halikuwa katika KAMUSI YAO (ya CCM) lakini leo hadi Mwenyekiti wao anaimba na kucheza ngoma ya UFISADI; labda wamesharekibisha hiyo kamusi waliyoikana mwanzoni!

Kwa wale ambao hatukuwepo wakati wa Uhuru wa kwanza wa Mwl. Nyerere (Desemba 9, 1961) angalau Septemba 15, tuliweza kushuhudia Uhuru wa Pili wa kimawazo, kifikra, uthubutu, na mwanzo mpya chini ya Dr. Wilbroad Slaa, Katibu Mkuu wa Chadema na makamanda wenzake.

Naridhia hoja hii na hoja yako kwa kuwa hapo awali kabla Chedema kuwa Chama kikuu cha upinzanii haikutokea hali ya derikali kunyoshewa kidole na wananchi, lakini sasa hivi naona mambo yameanza kuiwia vigumu serikali kuendesha mambo kiulaini kama ilivyozoea.
 
Nchi ni kubwa kazi hii sio ya muda mfupi hata kama chadema ina lengo hilo. Chadema haijafanikiwa.
dalili za ukimwi tunaambiwa kutoka vidonda midomoni, kuhara, na homa za mara kwa mara na dalili ya mvua wanasema mawingu ,dalili za chadema kufanikiwa wananji kugomea malipo ya dowans, migomo ya wanafunzi migomo ya madaktari wananji kuwatimua wabunge wao hasa wa magamba majimboni wanapopeleka hoja mbalimbali; mkuu haitajiki mizukulu jilala kukufahamisha kuwa hawa jamaa wamefanikiwa sana tena sana tu na baaaaaaado kudadadadeki mtatafuta pa kutokea
 
dalili za ukimwi tunaambiwa kutoka vidonda midomoni, kuhara, na homa za mara kwa mara na dalili ya mvua wanasema mawingu ,dalili za chadema kufanikiwa wananji kugomea malipo ya dowans, migomo ya wanafunzi migomo ya madaktari wananji kuwatimua wabunge wao hasa wa magamba majimboni wanapopeleka hoja mbalimbali; mkuu haitajiki mizukulu jilala kukufahamisha kuwa hawa jamaa wamefanikiwa sana tena sana tu na baaaaaaado kudadadadeki mtatafuta pa kutokea

Haswaaa, maana wanavyozidi kukorogana hata mfano wa historia ya nchi yetu haijapata kutokea. Hali hiyo ndiyo iliyonifikirisha kuona kama elimu ya uraia itolewayo na Chadema imeanza kuwaingia watu. Walithubutu kutamka siku za nyuma kwamba Chadema wanafanya nchi isitawalike, hii ni kutokana na kuzoea kuwaendesha watanzania kama gari bovu.
 
Haswaaa, maana wanavyozidi kukorogana hata mfano wa historia ya nchi yetu haijapata kutokea. Hali hiyo ndiyo iliyonifikirisha kuona kama elimu ya uraia itolewayo na Chadema imeanza kuwaingia watu. Walithubutu kutamka siku za nyuma kwamba Chadema wanafanya nchi isitawalike, hii ni kutokana na kuzoea kuwaendesha watanzania kama gari bovu.
unajua candid scope mambo yanavyotokea hivi sasa licha ya chadema kutoa elimu ya uraia pia mitendo michafu inayofululiza inayofanywa na hii migamba inaaccerelate hii motion na main problem this people already reach the point of non return they can not, shall not and will not change and by any means we have to chase them out 2015 na hii wakishinda kwa matendo yote waliyofanya tutawawatoa kwa ngumi
 
Kama maandamano yao yanakubalika kwa nini wamesitisha? Si wameona hayaleti manufaa kwao bali ni kujazana na kesi mahakamani?

Hawajasitisha mkuu. Yako kwenye pause tu. Kikao cha bunge kitakapomalizika yataanza tena: Mwanza, Mbeya, na this time Darisalama.
 
Back
Top Bottom