Chadema imedandia behewa la cuf!

Cufu ni wafu wanaotembea, ndoa yao na ccm inawasumbua. Ushauri wa bure mumeo kama hakutimizii mahitaji daiini taraka. Ya nini kuidandia CDM? Hatuwataki hata mkipaka mkorogo, tunatambua mmeathirika, mnaishi kwa matumaini kwa kumeza ARV'S. Wananchi ndiyo watatoa hukumu, nani anastahili au laa! Funikeni bakuli lenu.
 
HATA APPLE Aligundua komputa lakini haikutumika mpaka pale BILGET alipogundua MICROSOFT. hivyo hakuna jipya, Yote uyaonayo dunia wapo waliogundua bt sisi twatumia. So stil creat then we do. And remember now TZ need ACTION not planning
 
CUF wameingia kwenye ndoa bila kijitambua sasa huyu anasemaje au anamaanisha nini ? Kuwa adui wa CUF ni CHADEMA ili hali vyote ni vyama vya upinzani ? anamaanisha nini ? anamaanisha kuwa CHADEMA wameiga CUF hata bendera ? anyway hapa wanathihirisha uu CCM B, Ni kweli mnapinga kwamba ninyi si CCM B, Lakini maneno yenu na kauli zenu ni ushahidi wa kweli kuwa ninyi ni CCM B

V4C= VIBARAKA 4 CHANGE

umesema kweli si kila kitu CDM imeiga kwa CUF, bali hata CUF imeiga kwa CDM. Mfano CDM ndio ilikuwa ya kwanza kufunga ndoa na CCM Kigoma kabla ya CUF. Hivyo CDM ni mke mkubwa wa CCM
 
hivi mlumbane hadi slogan!!!wangecopy vision for change sawa,lakini yao ni movement for change!!hebu waelezeni watanzania kuwa nyie sio ccm b na sio kutaka umaarufu kwa mambo yasiyo na tija
 
hahahahahahhahha mnatia aibu CDM kwani hamjui kuwa tuliwabeba sana?? kwani hamjui kuwa mliiga hadi rangi za bendera??/ mmesahau kuwa muafaka uliwauma sana kiasi kutuita CCM B??? halafu kweli wewe kilaza umesahau kuwa KIGOMA mlianza nyie NDOA??? then nikukumbushe kitu kaka sera ya serikali ya shirikisho yaani vyama vyote ni ya CUF ccm hawana, cdm hawana wote mnaiga. sasa basi nikuambie kitu CUF ndio wenye sera hiyo. na siyo niye vilaza mnaague vitu ambavyo hamvijui .
Kweli wehu bado wako wengi, wazee wa mashindano, sasa nyie CUF kama nyie wabunifu uzeni basi huo ubunifu wenu tuone mbona mnazidi kufa bila kujua? mmefunga ndoa kaeni na mme wenu awatunze acheni majungu na umbea, ya CDM hayawahusu jadilini ya Mme wenu CCM. Hamna hoja mnaona CDM inavopaa na M4C mnajibaraguza ilikuwa hoja yenu mbona watanzania hawawajui na V4C yenu hiyo wehu hamna lolote.
 
hivi kwaninini cuf wanapoulizwa swali la kwanini wanajibu chadema kwanini?
kwanini wasijibu ccm halafu wanasema wao ni wapinzani
Mkuu jibu ni rahisi CUF siku zote wapinzani wa CDM sio CCM ndio maana kila wasemalo CDM wao wanapinga wanasupport ya Mume wao CCM. Ndoa tamu bwana hujui mume wao anawapa nn ndo mana wakati wote wanawatetea CCM badala ya CDM.
 
Eti Lipumba amefanya utafiti wa rasilimali za Tanzania nchini marekani!!?? eti Chadema wameiga? Yani hata hajui kwamba shughuli ya kuchangia M4C ilianzia arumeru wakati wa uchaguzi mdogo wa arumeru mashariki, shughuli ilifanyika Naura Spring hotel, wakati huo Lipumba hajulikani alipo na cuf ikiwa imeyumba hata ikashindwa kusimamisha mgombea.Baada ya ndipo shughuli ikahamishiwa viwanja vya jangwani kwa ajili ya wakazi wa dar na maeneo jirani.

Usinisemee na mimi mkuu, kama wewe ulikuwa hujui Lipumba yuko wapi basi ni wewe. Mimi najua alikuwa Malaysia anapiga deiwaka hotelini.

Kipindi hicho chama kilikuwa kwa maalim, sultani ye alikuwa anasakazake mshiko na HR alikuwa anawapeleka puta kinomanoma. Hivi HR naye kaishia wapi? Jamaa anapenda madaraka yule, eti yeye na wabunge wake 6 alitaka ndio awe kiongozi wa kambi ya upinzani. Kagombania madaraka bungeni weeeeee, kaona haitoshi akataka U-Maalim nusura umtokee puani. Ashukuru makabwela hawanaga ugomvi wa muda mrefu kama walivyo waswahili wote
 
Haya CUF, kila kitu nchi hii mmeanzisha nyie

1. Katiba mpya
2. Vita dhidi ya ufisadi
3. Movement for change
....

CUF bana basi na Vua gamba vaa gwanda pamoja na operation sanagara zote mmeanzisha nyie CUF na Chama cha Mauaji a.k.a CCM.
 
chadema imedandia behewa la cuf!

Kweli sasa unaweza kuamini kuwa si mara zote ujana ni umri, wakati mwingine ni fikra. Huyu naye ni kijana? Anafikiria hivi, sasa umri ukizidi kumwacha atafikiriaje? Kama inalazimu, basi anastahili kujibiwa na kijana wa BAVICHA wilayani au kata, kama si tawi kabisa.

Naona 'kijana' ameanza kutekeleza mkakati wa eti CUF iwe kwenye ligi moja na CHADEMA! Ili eti mapambano haya yaliyoanzishwa yapoteze mwelekeo (focus) kwa CHADEMA na wapenda mabadiliko wengine wabaki kuhangaika na watu wengine wanaotumika kwenye sehemu ya mikakati ya CCM kukabiliana wimbi kubwa la mabadiliko. No room for that league aisee. Tulionao kwenye ligi hii ya super league wanajulikana!

Timu ya daraja la tatu kulazimisha mechi na timu ya Super League, kwa mechi isiyokuwa ya mashindano rasmi, ni jambo la kupuuzwa!


 
chadema imedandia behewa la cuf!

Unahoja nzito, ila usitegemee majibu mazuri. Wafuasi wengi wa CDM humu ndani ni watoto wadogo..walipoanza kupata akili tu ndo wameijua CDM hivyo matusi haya unayoyapata ni kielelezo cha utoto wao. ninachokijua walicho asisi CDM ni uvaaji wa magwanda na kampeni za chopa ambazo hata CCM nao wameziiga.
 
Kzi kweli kweli, sikijua kumbe hata rangi za bendera nazo huwa zinaweza kuleta mvuto hata wananchi wakuunge mkono, hili kwangu nalo jipya! so kumbe hata Africa kusini nao wametuiga sisi Watanzania rangi za bendera yetu so maana wao wameendelea kuliko sisi, jamani, hivi wazo la katiba mpya, hapa wakulaumiwa nilidhani ni ccm, kwenye irani yao ya uchaguzi hili suala halikuwepo, mawaziri wao walikataa kabisa issue ya katiba mpya, mwanasheria mkuu wa serikali naye pia alikataa kuwa na katiba mpya, then Kikwete akasoma upepo akaanzisha mchakato wa hili, hivi hapa wa kulaumia ni CDM kweli? Hapa bwana Ibrahim asipotoshe historia, mwanzoni kabisa mwa mageuzi, enzi hizo sultani alikuwa mshauri wa uchumi wa bwana Mwinyi, akina Mabere Marando (NCCR mageuzi), Abdul Fundikila (UMD), James Mapalala (CUF, mwanzilishi) Mzee Mtei (CDM) walikutana Diamond Jubilee, miongoni mwa mambo waliyazungumza, katiba mya ilikuwepo, hili suala hata Prof Issa Shivji aliliandika sana enzi hizo kwenye magazeti ya Kingereza, narudia, ni enzi hizo, mwaka 1992, Lipumba wakati huo alikuwa mshauri wa uchumi.

Suala la serikali 3, hili nalo, naomba tuweke record vizuri hapa, hii kitu, CUF wasidandie umaarufu, hata CDM sio waasisi wa hiki kitu, nenda kwenye report ya Marehem Jaji Jalali, alipotumwa kukusanya maoni ya mfumo wa vyama vingi, maoni ya Watanzania wengi, pamoja na kile walicho ki sema juu ya chama kimoja au viwili, lakini issue ya muungano iliingia hapo, wengi walitaka mfumo wa serikali 3, Bungeni, i think wengi tunakumbuka ile kitu ilikuwa ikiitwa G 55 ikiongozwa na akina Tumtemeke Sanga (Makete) na wengineo, hawa walikuwa wabunge wa ccm, walitaka serikali ya Tanganyika irudi so, maanake walitaka serikali 3, kama sio mkwara wa Nyerere, leo hii tungekuwa na Zanzibar, Tanganyika na serikali ya muungano, hapa CUF inaingiaje? Mi nafikiri, CUF na CDM wamechukua kile wenye nchi wanataka then wakakiweka kwenye mikakati yao.

Suala la mwisho hapa ni hili, nashangaa sana kwa chama cha CUF kuipinga CDM while indirect unaunga mkono ccm, hivi bado unastahili kuitwa chama cha upinzani? Sasa ndo nimeelewa, ni kwanini Freeman Mbowe alikataa kuunganisha nguvu bungeni na hawa, i now understand why.
 
Sasa nimepata kuamini kwamba CUF ni CCM B, kwani sikutarajia hoja kama hiyo kutolewa na mjumbe wa upinzani.(Lakini kwa nini kusakamana wenyewe kwa wenyewe badala ya kujadili namna ya kuwasaidia wananchi kuondokana na uongozi wa kifisadi wa CCM?)
 
Kwa hiyo mnaanzisha kisha mnafungia kwenye makabati au, CDM awalali katika kuboresha chama na kukileta karibu na wanachi, msilalamike ingieni msituni na ninyi nuonekane, sio kukaa na kulalamika wakati wenzeni wanafight. CDM ni wabunifu na ndio maana hata CCM wanajaribu mbinu zote kukiaribia lakini mpaka sasa wameshindwa kwani wamejipanga vizuri sio mnaongea tu.

Mkuu Ba'mdogo

Mkakati wa sasa wa Chama Cha Mabwepande ni kupitia kitu kinachoitwa V4C, tehe tehe tehe! Yaangalie mambo nyuma ya pazia. Mikakati ya msitu wa pande, ya polisi kutumika kuua, inaonekana haitoshi (si kwamba imeachwa). Wanataka kupoteza focus ya watu makini. Ndiyo maana imefanyika copy and paste. Mpango wote. Wameshtukiwa hata kabla hawajaanza. Wako ligi ya chini.
 
MAJIBU YANGU KWA MALIMA


NIMEZISOMA hoja dhaifu za Naibu Katibu Mkuu JUVICF-Thomas Malima, akijibu makala yangu kuhusu `CUF inapodandia behewa la Chadema.’

Siwezi kujibu kauli za kejeli za kiongozi huyo wa CUF kwa maana sina hakika ya historia yake tangu kuzaliwa, kulelewa, kukua na sasa akikitumikia Chama cha Wananchi (CUF).

Kwa maana unaweza kumjibu mtu ambaye halistahili hilo, hivyo kuzidi kuichanganya jamii.

Pamoja na azma hiyo njema, bila shaka andiko lake linatoa tafsiri halisi ya aina ya viongozi wanasiasa tulio nao (kwa baadhi), uwezo na ‘picha’ wanayoiwasilisha kwenye jamii

Nikiri kwamba si Malima pekee aliyewasilisha hoja yake kwa kejeli na dharau, akishindwa kuukubali ukweli. Wapo wengi ndani ya CUF, akiwemo mjumbe wa mmoja wa Baraza Kuu la Uongozi (jina ninalihifadhi).


Akanipigia simu akiniita mjinga, mshenzi na kwamba maneno hayo anaweza kuyatamka hata kwa mmoja wa viongozi wa ngazi ya juu serikalini.

Kauli mbiu ya Dira ya Mabadiliko ya CUF kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2010 inakuwa msingi wa hoja yao-CUF.

Nikiri wazi kwamba nimefanya kazi na CUF kwa miaka mingi. Nimefanya kazi na viongozi wakuu wa CUF akiwemo Mwenyekiti wao, Profesa Ibrahim Lipumba, Maalim Seif Sharif Hamad na wengine wakiwemo waliowahi kutimuliwa.

So CUF ninaijua kwa kiasi chake na viongozi wake pia. Mmoja wa viongozi wa ngazi ya juu kitaifa katika CUF ni mdogo wangu. Kwa mazingira hayo, sina tatizo na chama hicho.

Kadhalika simo ndani ya Chadema katika orodha ya wanachama wake, chama kilichoshambuliwa na ninachohusishwa nacho. Simo ndani ya chama chochote cha siasa ingawa ninaziishi fikra huru dhidi ya uendeshaji wa vyama
Vya siasa.

V4C

CUF walikuwa na kauli mbiu ya Dira ya Mabadiliko (V4C) na bila shaka bado wanayo.

Waliitamka wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 2010. Kauli mbiu ambao viongozi wake akiwemo Malima wanaendelea kuing’ang’ania.

Hivi kwa akili ya kawaida ya binadamu, Malima anaona ufahari kujigamba kwa kauli mbiu iliyobaki kwenye makaratasi ya CUF kwa takribani miaka 5, pasipo kuiwekea mkakati na shughuli za utekelezaji wake?!

Malima anasema kauli mbiu ya V4C ilikuwepo tangu 2008. Ikifanya nini?

Kauli mbiu ni jambo linaloendana na wakati, likitumika kwa makusudio na malengo ambayo yanapofanikiwa, inaendelezwa lakini yanaposhindwa, inakuwa kifo cha asili (natural death).

Dira ya Mabadiliko ya CUF kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2010 ilikuwa kukivusha chama hicho kutoka kambi ya upinzani na kuwa watawala. Mpango ulioshindwa hivyo kuambulia nafasi ya tatu katika kuwania urais, huku kikikosa jimbo hata ‘la kufutia machozi’ upande wa Tanzania Bara.

Kwa Malima anaona ufahari, akiendelea kuikumbatia kauli mbiu ambayo pamoja na uzuri wake, imeshindwa ki-mkakati na utekelezaji.


Hivi Malima anaweza kutueleza mbali na kuitamka kauli mbiu hiyo jukwaani, maelezo ya utekelezaji wenye lengo la kuifikia V4C yalipatikana wapi?

Na hapo yalipopatikana (kama papo) watekelezaji wake walipaswa kuwa akina nani na shughuli zipi zilianishwa ili utekelezaji huo ufanyike, itoke kuwa kauli mbiu na kuugusa umma unaohitaji mabadiliko?

Kuikumbatia kauli mbiu iliyoshindwa, kisha ikafufuliwa kwa kufuata nyayo za Vuguvugu la Mabadiliko (M4C), wakitumia kila aina ya ubunifu, mbinu na stadi za Chadema ambacho sina shirika nacho kwa namna yoyote, Malima anapata uhalali wa kunikejeli.

Hivi Malima anaweza kumpata, mathalani msichana (kama hajaoa), ashindwe kumhudumia, kisha atokee mume jasiri anayetekeleza jukumu hilo na kufikia hatua ya kumuoa, akamuweka ndani kuwa mzazi mwenzeo, yeye (Malima) abaki kujisifia kwamba “mimi ndo nilikuwa wa kwanza”?

:shut-mouth:

 
SAHIHISHO:

Katika post yangu ya kumjibu Malima, nimeelezea kuwa CUF haikupata hata Mbunge wa kufutia machozi. Hapo nilipitiwa na kusudio lilikuwa kueleza walipata wabunge wawili wa kuchaguliwa waliokifutia machozi chama hicho.

Ninawasilisha.
 
Nichangie kuweka kumbukumbu sawa:

Mtoa hoja amedai kuwa CHADEMA ilianzisha M4C mwaka 2011, na kwamba CUF ilianza Vision for Change mwaka 2008 na hatimaye kuanza kuingiza katika ilani yake 2010. Ukweli ni kuwa CHADEMA katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2005 ilitumia kauli mbiu "Mabadiliko ya Kweli, Uhuru wa Kweli" (Real Change, Real Freedom) na wakati huo kuna maneno tulikuwa tukiyarudiarudia sana kwenye kampeni, mabadiliko ya kweli hayawezi kuletwa na mafisadi walewale, wa chama kile kile, chenye uoza ule ule wakiendeleza yale yale kwa ari, nguvu na kasi mpya. Ilani yetu ya wakati huo iliyokuwa na vipaumbele vichache tulikuwa tukiinadi kuwa ni dira ya mabadiliko ya taifa letu. Mara baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2005, nilibahatika kuwa mwezeshaji wa tathmini ya chama baada ya uchaguzi na maandalizi ya Mpango Mkakati wa Chama 2006-2010 ambayo msingi wake mkuu ulikuwa ni kufanya mabadiliko ndani ya chama kama msingi wa kushinda uchaguzi na kuleta mabadiliko makubwa katika taifa.

Kufuatia kupitisha Mpango Mkakati huo tarehe 13 Agosti 2006 tulifanya mkutano mkuu wa chama na kuzindua TUMAINI JIPYA, siku hiyo tulizindua katiba mpya ya chama, bendera mpya ya chama, mabaraza ya chama na mpango mkakati wa chama. Hatua hiyo ilitanguliwa na mchakato wa kukusanya maoni toka kwa wanachama na ngazi za chini za chama na nilibahatika kuwa katibu wa kamati iliyofanya marekebisho hayo ambayo kwa upande wa masuala ya falsafa na itikadi ilikuwa chini ya Profesa Baregu. Kupitia kazi hizo nilizozifanya wakati huo nikiwa pia Mkurugenzi wa Taifa wa Vijana nilipata wasaa wa kuifahamu kwa kina historia ya chama na pia kufanya rejea ya historia ya mageuzi nchini.

Mkakati wa M4C haukuanza mwaka 2011 kama ambavyo CUF inajaribu kupotosha, mwaka 2006 mara baada ya kupitisha mkakati huo wa chama tulianza shughuli mbalimbali za utekelezaji wa mkakati huo, kati ya shughuli hizo wakati huo nikiwa Mkurugenzi wa Vijana wa CHADEMA tulianzisha Y4C (Youth for Change) ikiwa ni kundi la vijana wenye dira na dhima ya kuona mabadiliko katika taifa, tulifanya matukio kadhaa mwaka 2006, 2007 kipindi ambacho CUF haikuwa imezindua Vision for Change. Mwaka 2007, mara baada ya kutoa orodha ya mafisadi (List of Shame) Septemba 15 MwembeYanga tulikaa kutafakari tutaendelezaje vuguvugu la mabadiliko nchini, ni wakati huo likaja wazo la kuwa na Movement for Change (M4C), miezi michache baadaye chama kilifungua akaunti katika benki mbalimbali kwa ajili ya harambee ya kukusanya michango ya umma kwa ajili ya mabadiliko; Akaunti hizo ziliitwa M4C. Mwaka 2008 tukaingia katika uchaguzi wa marudio katika Jimbo la Tarime ya kushinda, baada ya ushindi huo M4C iliendelea kama mkakati wa kukusanya rasilimali za umma kwa ajili ya mabadiliko hata hivyo kwa vuguvugu lililokuwepo wakati huo baada ya ushindi tukaamua kuzindua Operesheni 'Sangara'. Miezi michache baadaye CUF nayo ikazindua Operesheni Zinduka CCM ikaanza Operesheni Nyavu. Mwaka 2009 CUF ilifanya kongamano Diamond Jubilee kuhusu Dira ya Mabadiliko, na ni ukweli katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 ilani yake iliita dira ya mabadiliko (Vision for Change) hata hivyo katika uzinduzi huo CUF haikutumia kifupi V4C.

Miezi michache baada ya CHADEMA kuzindua M4C kwa upande wa Arusha, ndipo CUF akatangaza tena Vision for Change safari hii ikitumia pia kifupi cha V4C. Wakati huo CHADEMA ilianza pia shughuli ya "Vua Gamba, Vaa Gwanda", CCM nayo ikaja ".....Vaa Uzalendo". Ni wazi kwamba M4C ni tofauti na V4C, ni wazi pia kwamba M4C ilitangulia V4C; kama ambavyo Operesheni Sangara ilitangulia Operesheni Zinduka. Baada ya uchaguzi wa 2010, watanzania wanaweza kupima vizuri zaidi matokeo ya Operesheni Sangara ukilinganisha na Zinduka, na baada ya uchaguzi wa 2015 watanzania watapima M4C vs V4C vs "Vaa Uzalendo ya CCM". Na kwa kweli, CHADEMA inachotazama zaidi ni kufanya mabadiliko kwa kuiondoa CCM madarakani na kuweka uongozi bora, sera sahihi, mikakati makini na oganizesheni thabiti kwa maendeleo endelevu ya Tanzania. Nikipata wasaa mwingine nitajibu upotoshaji uliojitokeza kuhusu bendera ya CHADEMA, people's power na madai ya katiba mpya kwa kuwa nimepata bahati katika kipindi cha kati ya 2004-2010 kushiriki kwa karibu kwenye michakato muhimu ndani ya CHADEMA na ya kamati za ushirikiano iliyohusisha CUF na vyama vingine. Yote kwa yote, suala la msingi si nani ameanzisha nini, muhimu ni nini kinafanyika kuwezesha mabadiliko ya kweli nchini kwa maslahi ya umma.

JJ
 
Mbona hiyo V4C haionekani Zanzibar mliko madarakani, AMA ninyi ni kuanza utekelezaji zero?
 
Back
Top Bottom