Chadema imchunguze Naibu Katibu Mkuu wake

Luteni

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
2,274
301
Kitendo cha Zitto ambaye ni Naibu katibu mkuu wa Chadema kutuhumiwa kuwa tarehe 3 May 2011 alituma pesa kwa ajili ya kampeni ya mgombea mmoja wa uenyekiti wa Bavicha kwa njia ya M-PESA si cha kupita bila kufanyiwa uchunguzi. Tunajua macho mengi sasa yanakiangalia chama cha Chadema kama chama mbadala, na watu wanakipima endapo kitapewa madaraka ya kuongoza ni mambo yepi kitayapa kipaumbele ikiwa ni pamoja na kuwawajibisha viongozi wake wakuu, kuwajibishwa sina maana ya kufukuzwa uanachama hata kupewa onyo au karipio ni njia mojawapo ya kuwajibika.

Kitendo hicho ambacho kinachoripotiwa na watu mbalimbali ikiwa kitaachwa kipite bila kujadiliwa na kutolewa ufumbuzi na chama kinaweza kuharibu image ya chama kitafanya watu kuwa na walakini na uwezo na umahili wa chama katika kupambana na maozo mbalimbali yawe yamefanywa na viongozi wakuu au wanachama wa kawaida, watu watajiuliza kwa nini chama king'ang'anie kuwachunguza wengine wakati huo kinaacha tuhuma za viongozi wake? Naomba wakati kamati kuu itakapoketi kujadili yaliyojiri kwenye uchaguzi wa Bavicha kama kutakuwa na ajenda ya kuchunguza tuhuma za wagombea ajenda mojawapo iwe ni hii tuhuma inayozidi kusambaa mitaani.
 
zito ni kaswahili kasikoaminika katu

very true, the problem kanashindwa kujicomouflage over the period....leo hii kanasema TAKUKURU ianze uchunguzi ilihali upande wa pili anasema mwenyekiti mpya aungwe mkono na makundi yote....wapi na wapi??uungwaji gani mkono unaopatikana kwa kupelekana Takukuru?

tunawashukuru wazee wa chadema kwa kuwa na mawani makali ya kutujua sie vijana wenu.....sijutii Mbowe kuendelea kuwa mwenyekiti, nafurahia heche kuwa kamanda wa vijana.....kwa mara nyingine magamba yameshindwa kutuvuruga!!!

nadhani tunamwelewa.na tunazidi kumwelewa sasa.....
 
If the rumours are thrue, then Zitto is not stable in leadership at all!.
.
 
Napata mashaka kuchangia sababu mada inatofautiana na taarifa kwa umma tuliyoipewa baada ya jina la mgombea mmoja wa bavicha kuenguliwa na baada ya uchaguzi wenyewe! Taarifa zilimtuhumu mgombea (sio Zito) huyo kujihusisha na vitendo vya kifisadi ikiwemo kuwatumia wajumbe wa mkutano wa uchaguzi mkuu (Zito sio m1 wao) nauli za kuja mkutanoni. Sasa hizo habari unazosema zimezagaa mtaani ndio unatuletea hapa jamvini tujadili!? Labda kama unamaelezo zaidi au ni chuki/ugomvi binafsi na Zito. Otherwise huu ni upuuzi!
 
very true, the problem kanashindwa kujicomouflage over the period....leo hii kanasema TAKUKURU ianze uchunguzi ilihali upande wa pili anasema mwenyekiti mpya aungwe mkono na makundi yote....wapi na wapi??uungwaji gani mkono unaopatikana kwa kupelekana Takukuru?<br />
<br />
tunawashukuru wazee wa chadema kwa kuwa na mawani makali ya kutujua sie vijana wenu.....sijutii Mbowe kuendelea kuwa mwenyekiti, nafurahia heche kuwa kamanda wa vijana.....kwa mara nyingine magamba yameshindwa kutuvuruga!!!<br />
<br />
nadhani tunamwelewa.na tunazidi kumwelewa sasa.....
hivi takukuru kuchunguza ni tatizo? Kwahiyo mtu akitoa rushwa yanatakiwa yaishe kishkaji kama ya epa? Kuna wale waliotuhumiwa na wao wanahitaji kusafishwa km hawakutoa rushwa au lah. Vinginevyo makovu haya si rahisi kwisha km unavyotuaminisha. Vyombo vya sheria vina nafasi yake katika demokrasia pia, haitoshi mtu kutuhumiwa na yakaisha hivyo.
 
We do not have Crisis but we have difficulties and we will solve them within our familiy -Sepp Blatteer .Je Chadema now ndiyo wazee wameona waende mwendo huo kwa manufaa ya Chama ?
 
The issue hapa ni zito anaonekana ana kiu ya kugeuza cdm chama kama tlp na nccr....na dovutwa na sau,..n..k

mbinu hii ccm wameitumia for a decade na wamefanikiwa sana kudominate domestic politics....they can not imagine kwa nini haiwork cdm

aliyekuwa anataka kuplant watu ni yeye mwenyewe...ashindwe na alegee....

Sasa anataka tumpe nape pumzi.....au kwa namna nyingine ni kumpa tabu heche......hatufanyi hivyo ng'o....

Imekula kwao wanamagamba! Walipolala sie ndio tumeamkia...aka wamekumbuka shuka kumekucha!!!

Hiyo imebumba!
 
hivi takukuru kuchunguza ni tatizo? Kwahiyo mtu akitoa rushwa yanatakiwa yaishe kishkaji kama ya epa? Kuna wale waliotuhumiwa na wao wanahitaji kusafishwa km hawakutoa rushwa au lah. Vinginevyo makovu haya si rahisi kwisha km unavyotuaminisha. Vyombo vya sheria vina nafasi yake katika demokrasia pia, haitoshi mtu kutuhumiwa na yakaisha hivyo.

Ikidhibitika walitoa rushwa ndo makovu yataisha au yataongezeka? Mida mingine busara itumike kuamua mambo ya Chama. Kuhusu vyombo vya sheria, yeyote anayeona ameonewa akate rufaa mahakamani kwa kudai kuwa walisigiziwa kwamba alitoa rushwa. Chombo cha sheria siyo TAKUKURU tu.
 
hahaha...naona mnacheza nage sasa!
nadhani njia rahisi ni Chadema kuunda tume ya Ethics, ichunguze haya madai yote! Watakaopatikana na hatia wapigwe ban!
 
Pongezi kwa wazee wa chama kwa maana tumeziona busara zao na ni kupitia kwao CDM imefanikiwa kuovercome mitego mingi sana internally na xternally

CCM wanakesha wanacheza drafti lakini uadirifu wa wazee chini ya M/kiti unastahiri HEKO!
 
Kitendo cha Zitto ambaye ni Naibu katibu mkuu wa Chadema kutuhumiwa kuwa tarehe 3 May 2011 alituma pesa kwa ajili ya kampeni ya mgombea mmoja wa uenyekiti wa Bavicha kwa njia ya M-PESA si cha kupita bila kufanyiwa uchunguzi. Tunajua macho mengi sasa yanakiangalia chama cha Chadema kama chama mbadala, na watu wanakipima endapo kitapewa madaraka ya kuongoza ni mambo yepi kitayapa kipaumbele ikiwa ni pamoja na kuwawajibisha viongozi wake wakuu, kuwajibishwa sina maana ya kufukuzwa uanachama hata kupewa onyo au karipio ni njia mojawapo ya kuwajibika.

Kitendo hicho ambacho kinachoripotiwa na watu mbalimbali ikiwa kitaachwa kipite bila kujadiliwa na kutolewa ufumbuzi na chama kinaweza kuharibu image ya chama kitafanya watu kuwa na walakini na uwezo na umahili wa chama katika kupambana na maozo mbalimbali yawe yamefanywa na viongozi wakuu au wanachama wa kawaida, watu watajiuliza kwa nini chama king'ang'anie kuwachunguza wengine wakati huo kinaacha tuhuma za viongozi wake? Naomba wakati kamati kuu itakapoketi kujadili yaliyojiri kwenye uchaguzi wa Bavicha kama kutakuwa na ajenda ya kuchunguza tuhuma za wagombea ajenda mojawapo iwe ni hii tuhuma inayozidi kusambaa mitaani.
Luteni, Zitto kama Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, angetumia nafasi yake kumpendelea mgombea fulani, hapo ingekuwa kosa, lakini kuna Zitto ambaye ni human being, anaruhusiwa kuwa na marafiki wowotw anaowasupport na sio kosa kutoa fedha mfukoni mwake na kumtumia yoyote.

namuunga mkono Zitto sio kwa blind faith bali kwa vission ya over and above partisan politics. Zitto ni rafiki na Jussa, January nadhani hata Nape. Chama chake kilipomtimua Kafulila na kumuita sisimizi, Zito came on open na kusema atamsupport kokote atakakokwenda, wengine wanaliona hili kama usaliti, sisi tusio na blind faith, au more broad minded tunaliona hili kama politics za over and above party lines.

Tembelea blog yake au fb yake (G8 add its support for transparency « Zitto na Demokrasia) uone jinsi alivyo mkombozi wa taifa kwa kuwa pressure group ya transparency kwenye mikataba ya madini.
 
Haina maana uchaguzi umepita, wamkanye tu asirudie
Uchaguzi umepita sawa lakini nasikia yeye anapeleka barua kwa Katibu mkuu kutaka Chadema iwaite Takukuru huoni hiyo ni kwamba anataka kuendeleza makundi wakati yeye mwenyewe alisema hatajihusisha na uchaguzi anachotaka nini zaidi. Ndio maana nikasema katika kutumia busara wazee wa Chadema wachunguze pia tuhuma zake za kutuma pesa na kusababisha mgombea kuenguliwa.
 
Luteni, Zitto kama Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, angetumia nafasi yake kumpendelea mgombea fulani, hapo ingekuwa kosa, lakini kuna Zitto ambaye ni human being, anaruhusiwa kuwa na marafiki wowotw anaowasupport na sio kosa kutoa fedha mfukoni mwake na kumtumia yoyote.

namuunga mkono Zitto sio kwa blind faith bali kwa vission ya over and above partisan politics. Zitto ni rafiki na Jussa, January nadhani hata Nape. Chama chake kilipomtimua Kafulila na kumuita sisimizi, Zito came on open na kusema atamsupport kokote atakakokwenda, wengine wanaliona hili kama usaliti, sisi tusio na blind faith, au more broad minded tunaliona hili kama politics za over and above party lines.

Tembelea blog yake muone jinsi alivyo mkombozi wa taifa kwa kuwa pressure group ya transparency kwenye mikataba ya madini.
Pasco kama kila kiongozi Slaa, Mbowe, Mtei na wengine wangetoa pesa kwa wanaowa support uchaguzi ungefanyika salama? kumbuka yeye alituambia hatajihusisha na mambo ya uchaguzi akasema ndio maana hajahudhuria kikao chochote cha uchaguzi kwa nini sasa baada ya uchaguzi, badala ya kuwapongeza na kuwashauri walioshindwa washirikiane na m/kiti aliyeshinda yeye anawashauri waende mahakamani WHY? kama si kutaka kuleta makundi kama ya CCM ni nini, na kumbuka historia ya Zitto ilivyochafuka kwenye uchaguzi wa Bavicha uliopita na huu pia ni yeye tu anatajwa kwa nini asitajwe Mnyika something is wrong somewhere hata kama unasema yuko above partisan politics lakini lazima ajiangalie awe level moja na wenzake.
 
Ni muhim kufahamu kama kweli mh Zitto alituma pesa kwa mgombea mojawapo kwa ajili ya uchaguzi
Inawezekana pia ni namna tu ya kumchafua,lakini ktk swala la kuthibitisha kama alituma fedha kwa sab ya uchaguzi nadhani si jambo gumu kuthibitisha
 
Tembelea blog yake au fb yake (G8 add its support for transparency « Zitto na Demokrasia) uone jinsi alivyo mkombozi wa taifa kwa kuwa pressure group ya transparency kwenye mikataba ya madini.
Hata Rostam huwa anachangia maendeleo tena anatoa misaada hadi makanisani lakini kwangu ni adui namba moja wa taifa.
Let me tell you and I have been saying that Zitto is a failed timed bomb in Chadema wazee wameshashtukia, viongozi wenzake wameshastuka hawamwamini ndiyo maana wakaamua kusimamia uchaguzi wenyewe, Pasco kama wewe ni kiongozi halafu kila sekta inakutenga utajisikiaje kwanza wabunge wenzake hawana imani naye pili wazee hawana imani naye sasa yeye amebaki kuwa kiongozi wa vyombo vya habari ajiulize.
 
Kitendo cha Zitto ambaye ni Naibu katibu mkuu wa Chadema kutuhumiwa kuwa tarehe 3 May 2011 alituma pesa kwa ajili ya kampeni ya mgombea mmoja wa uenyekiti wa Bavicha kwa njia ya M-PESA si cha kupita bila kufanyiwa uchunguzi.


Hizi tuhuma zilitolewa wapi na nani?
 
Back
Top Bottom