Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 301
Kitendo cha Zitto ambaye ni Naibu katibu mkuu wa Chadema kutuhumiwa kuwa tarehe 3 May 2011 alituma pesa kwa ajili ya kampeni ya mgombea mmoja wa uenyekiti wa Bavicha kwa njia ya M-PESA si cha kupita bila kufanyiwa uchunguzi. Tunajua macho mengi sasa yanakiangalia chama cha Chadema kama chama mbadala, na watu wanakipima endapo kitapewa madaraka ya kuongoza ni mambo yepi kitayapa kipaumbele ikiwa ni pamoja na kuwawajibisha viongozi wake wakuu, kuwajibishwa sina maana ya kufukuzwa uanachama hata kupewa onyo au karipio ni njia mojawapo ya kuwajibika.
Kitendo hicho ambacho kinachoripotiwa na watu mbalimbali ikiwa kitaachwa kipite bila kujadiliwa na kutolewa ufumbuzi na chama kinaweza kuharibu image ya chama kitafanya watu kuwa na walakini na uwezo na umahili wa chama katika kupambana na maozo mbalimbali yawe yamefanywa na viongozi wakuu au wanachama wa kawaida, watu watajiuliza kwa nini chama king'ang'anie kuwachunguza wengine wakati huo kinaacha tuhuma za viongozi wake? Naomba wakati kamati kuu itakapoketi kujadili yaliyojiri kwenye uchaguzi wa Bavicha kama kutakuwa na ajenda ya kuchunguza tuhuma za wagombea ajenda mojawapo iwe ni hii tuhuma inayozidi kusambaa mitaani.
Kitendo hicho ambacho kinachoripotiwa na watu mbalimbali ikiwa kitaachwa kipite bila kujadiliwa na kutolewa ufumbuzi na chama kinaweza kuharibu image ya chama kitafanya watu kuwa na walakini na uwezo na umahili wa chama katika kupambana na maozo mbalimbali yawe yamefanywa na viongozi wakuu au wanachama wa kawaida, watu watajiuliza kwa nini chama king'ang'anie kuwachunguza wengine wakati huo kinaacha tuhuma za viongozi wake? Naomba wakati kamati kuu itakapoketi kujadili yaliyojiri kwenye uchaguzi wa Bavicha kama kutakuwa na ajenda ya kuchunguza tuhuma za wagombea ajenda mojawapo iwe ni hii tuhuma inayozidi kusambaa mitaani.