Paul Kijoka
JF-Expert Member
- Oct 25, 2010
- 1,399
- 255
chama cha demokrasia na maendeleo pamoja na baadhi ya vyombo vya habari vinalaumiwa kupotosha taharifa ya waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa mh Benard Membe
Taharifa kamili
WIZARA ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, imesema baadhi ya vyombo vya habari pamoja na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), vilipotosha taarifa ya Wizara hiyo kuhusiana na chama kinachofadhiliwa ili kuleta machafuko nchini.
Imesema Waziri Bernard Membe hakutaja jina la chama wala nchi kinachofadhiliwa na nchi za Jumuiya ya Ulaya ili kuleta machafuko nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, John Haule amesema, Serikali itachukua hatua za kidiplomasia chini ya Mkataba wa Kimataifa wa Vienna kuhusu Mahusiano ya Kidiplomasia wa mwaka 1961, ikiwa itathibitisha nchi na chama hicho.
Haule amesema , Wizara imepokea taarifa za ujumbe wa simu za mkononi unaosambazwa kuwa baadhi ya nchi za Jumuiya ya Ulaya zinatuhumiwa kukifadhili chama cha siasa nchini ili kuleta machafuko na kwamba, raia wa nchi wanachama wa jumuiya hiyo wanakuwa na wasiwasi juu ya usalama wao.
"Tumepokea taarifa hizo na tumezipeleka kwenye vyombo vinavyohusika kwa uchunguzi na ikithibitika, Wizara itatoa taarifa," amesema Haule leo.
Amesema, katika mkutano wa Waziri Membe alioufanya wiki iliyopita na waandishi wa habari, alijibu suala hilo bila kutaja jina la chama wala nchi inayofadhili, lakini Chadema kiliibuka na kumtaka Membe kuzitaja balozi hizo zinazofadhili chama hicho na kiasi cha fedha kinachotolewa
Taarifa hii imetolewa kwa kina nani? Majuha? Kama Membe alitamka kwa kuficha na Sofia Simba akapasua jipu tuseme Membe anajikosha ili agombee urais 2015. Hatudanganyiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiikiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii!