Gosbertgoodluck
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 2,855
- 401
WanaJF na hususan viongozi wa CHADEMA,
Ninaandika thread hii nikiwa serious kabisa. Nimetazama mikutano mingi ya CHADEMA na ya CCM na kubaini tofauti kubwa ya mahudhurio ya wanawake. Ni jambo lisilopingika kwamba watu wanaojaa sana kwenye mikutano ya CCM ni wanawake. Kinyume chake, watu wanaojaa sana kwenye mikutano ya CHADEMA ni wanaume, wazee na vijana. Mfano mzuri ni mkutano uliofanyika Mabibo. Ukiangalia kwa makini utabaini kuwa ninachoongea kina ukweli ndani yake.
Ndugu zangu viongozi wa CHADEMA, tusibeze umuhimu wa wanawake katika ukombozi wa taifa letu kutoka kwenye makucha ya chama kinachowahifadhi na kuwapalilia mafisadi. Lazima iwekwe mikakati ya sayansi jamii ya namna ya kubadili fikra potofu walizopandikiza CCM kwenye vichwa vya mama zetu kiasi cha kuamini kuwa bila CCM amani ya nchi hii itatoweka. Akina mama wengi (na siwalaumu kwa hilo) ni wahanga wa vurugu zinazotokea maeneo mengi Duniani. Wengi wao ni waoga. Wanaona bora waendelee kuteseka na hali ya mbaya ya maisha lakini siyo kwa vurugu za kubakwa, kupigwa risasi na kuishi kama wakimbizi ugenini, n.k. Wenzenu wa CCM wameiona hiyo 'potential' na wamebuni 'injili ya vitisho' na wanaihubiri barabara kila wanapopata fursa hiyo adhimu.
Ushauri wangu kwa viongozi, wanachama na wapenzi wa CHADEMA, waanze mara moja kupanga mikakati ya kubadili fikra ya kundi hili kubwa la wapiga kura. Tusibeze hata mara moja umuhimu wa kundi hilo katika ukombozi wa nchi yetu. Kazi kubwa imefanyika ya kumobile watu lakini bado kuna kazi nyingine ya kumobilize akina mama.
Hilo likifanyika, CCM itachinjiliwa mbali na kuzikwa maana hata mbinu zao za kuchakachua matokeo hazitafua dafu, itayeyuka kama barafu juani.
Ninaandika thread hii nikiwa serious kabisa. Nimetazama mikutano mingi ya CHADEMA na ya CCM na kubaini tofauti kubwa ya mahudhurio ya wanawake. Ni jambo lisilopingika kwamba watu wanaojaa sana kwenye mikutano ya CCM ni wanawake. Kinyume chake, watu wanaojaa sana kwenye mikutano ya CHADEMA ni wanaume, wazee na vijana. Mfano mzuri ni mkutano uliofanyika Mabibo. Ukiangalia kwa makini utabaini kuwa ninachoongea kina ukweli ndani yake.
Ndugu zangu viongozi wa CHADEMA, tusibeze umuhimu wa wanawake katika ukombozi wa taifa letu kutoka kwenye makucha ya chama kinachowahifadhi na kuwapalilia mafisadi. Lazima iwekwe mikakati ya sayansi jamii ya namna ya kubadili fikra potofu walizopandikiza CCM kwenye vichwa vya mama zetu kiasi cha kuamini kuwa bila CCM amani ya nchi hii itatoweka. Akina mama wengi (na siwalaumu kwa hilo) ni wahanga wa vurugu zinazotokea maeneo mengi Duniani. Wengi wao ni waoga. Wanaona bora waendelee kuteseka na hali ya mbaya ya maisha lakini siyo kwa vurugu za kubakwa, kupigwa risasi na kuishi kama wakimbizi ugenini, n.k. Wenzenu wa CCM wameiona hiyo 'potential' na wamebuni 'injili ya vitisho' na wanaihubiri barabara kila wanapopata fursa hiyo adhimu.
Ushauri wangu kwa viongozi, wanachama na wapenzi wa CHADEMA, waanze mara moja kupanga mikakati ya kubadili fikra ya kundi hili kubwa la wapiga kura. Tusibeze hata mara moja umuhimu wa kundi hilo katika ukombozi wa nchi yetu. Kazi kubwa imefanyika ya kumobile watu lakini bado kuna kazi nyingine ya kumobilize akina mama.
Hilo likifanyika, CCM itachinjiliwa mbali na kuzikwa maana hata mbinu zao za kuchakachua matokeo hazitafua dafu, itayeyuka kama barafu juani.