CHADEMA, huu ni wakati wa kufanya maamuzi magumu...

Status
Not open for further replies.
Naomba kwa muda tuanze kumtambua mchawi wetu ccm kupitia Wassira. Uasi una vyanzo. Vyanzo vyaweza kuwa ni ushawishi, tamaa, utashi wa mtu, hata vitisho. Hili jambo twende nalo kwa akili. Bora imekuwa mapema haya yametokeza na mapema yapatiwe suluhu

Kwenye hil indugu yangu tuiweke CCM pembeni; hili ni la CDM tu. Kwani hawa watu wameshikiwa mapanga na bunduki na CCM kichwani? Au tunafikiri wamekaa kama maroboti ya kisiasa ambao wenye kuyaendesha wako Lumumba? Kuilalamikia CCM kwa yanayoendelea CDM ni sababu tosha ya kwanini CDM inahitaji kufanya kitu. Haiwezekani CCM wapike Lumumba chakula kiive Rufiji!
 
Katika hizi dk. 45 za kipindi cha pili mpira unachezwa kwenye lango la Chadema. Mkakati wa kuishambulia kutoka nje, kupitia kwa kina nape na kina ritz matunda yake hayakuwa mazuri mazuri kwani timu ya washambuliwa ilishirikiana katika kujibu mapigo.

Mpango wa kufanya watu wageuziane silaha wao kwa wao badala ya kulenga adui unafanya wapinzani waibuke washindi bila kupigana. Watoa malumbano haya kwenye umma na supporter wanaodhani huu mkakati unaleta afya kwenye chama wajaribu kuangalia tena kama kweli hii kitu itawafikisha pale wanapodhani au wanapotaka.

Kitu kimoja kutambua ni kwamba kuna watu wa aina kama tatu hivi katika mapambano ya kisiasa.

1. Wafia Chama, hawa katika namna yoyote mapenzi kwa chama ni makubwa kiasi ambacho si rahisi kutokiunga chama katika hali ya namna yoyote. Na hawa wanaweza kuwa siyo wengi sana kiasi cha kufanya chama kupata ushindi kwa kuwategemea hawa.

2. Wasiokipenda chama, hawa hata chama kifanyeje, kiwe na umoja au uzuri wa namna gani hawawezi kukiunga mkono kwa jinsi walivyoamua wenyewe. Hawa pia sio wengi kiasi cha kuogofya, jiitihada za kushawishi watu wa namna hii hazipaswi kuwa kubwa sana kwani ni utapata hasara zaidi kuliko faida.

3. Kundi la kuangalia hali ilivyo(undecided), hawa ndio wengi katika jamii. Hawa wanapaswa kushawishiwa kwa hoja na wajiridhishe katika nafsi zao katika kufanya maamuzi ya nani wamchague mwisho wa siku. Hawa ndo kundi muhimu kabisa katika kuleta ushindi wa chama.

Sasa katika malumbano kati ya viongozi yanayofanyikia katika mahakama ya wazi isiyo na mtu wa kuamua mshindi baina yao yanalipoteza kundi la tatu. Na niwahakikishie hawa wanaodhani kwamba hii inakijenga chama wanakosea sana, kama kuna anayeshangilia zaidi kwa hali hii ni CCM. I can see sasa wameamua kutulia kikosi chao cha mstari wa mbele wanakunywa zao Shampeni wakati mitutu ya wapinzani imegeukiana.
 
Wengine tumekaa kimya kuangalia nani mwenye hekima humo ndani....
Kukaa kimya kuangalia, nako pia ni kusubiri!. Nilifikiri watazamaji ni kina sisi tulio nje, tukiwasubiria mliondani muamue kutenda kwa vitendo na sio kwa maneno!.

Ulipotoa kile kitisho kuhusu Kamati Kuu ya Chadema isipokuja na xyz, then "something would have been done!. Tamko halikutoa ile xyz, nothing was done!. Sasa ndio unakaa kimya kuwasubiria hao wenye hekima wa Chadema?!.

Unapoona nyumba ya jirani inafuka moshi kwa tishio la kulipuka moto, utasubiri mpaka moto ulipuke, ndipo usaidie kwa kuita fire, au hatua ya kwanza ni ku stretch a helping hand, and bila kusubiri, if there is anything you can do, you just have to do it1, na sio kusubiri if "they can't reign, ndipo "will help you!?.

Haya na tuendelee kusubiria hiyo help itolewe only when they can't reign!, which means by now, they still reign!. Inamaana hiki kinachoendelea ni rasharasha tuu, tusubirie mvua, ndipo tukatafute mwamvuli!.

Pasco.
 
Naomba kwa muda tuanze kumtambua mchawi wetu ccm kupitia Wassira. Uasi una vyanzo. Vyanzo vyaweza kuwa ni ushawishi, tamaa, utashi wa mtu, hata vitisho. Hili jambo twende nalo kwa akili. Bora imekuwa mapema haya yametokeza na mapema yapatiwe suluhu
Unaendeleo kutafuta mchawi wakati "kikulacho"!.
 
Ule umakini wa wana CDM naona kama unamomonyoka taratibu, na juhudi zetu za kuipigania chadema huku mtaani inakuwa ni sawa na bure!!
 
Hizo ndizo faida za mtandao. Mtandao umeijenga CHADEMA na mtandao huo huo ndio unaimaliza CHADEMA! Mkuu wacha watu wamwage nyongo. Nadhani taarifa zingine itabidi polisi wazifanyie kazi hasa linapokuja suala la vijana kutishina kuuana kwa njia mbalimbali. Watu wanalegeza nati za matairi ili mtu afe. Kuna kilio kiliwahi kutoka kwamba kiongozi mmoja wa CDM alilegezewa nati akapata ajali akafariki sasa na hizi zingine zinasema gari la Zitto lililegezwa nati! Wacha wasemane na kutajana yaishe.
wewe kimbunga mbona hutumii akili hata kidogo? Waambie hao policcm kwanza wawashugulikie bashe na kigwangala kwa kutoleana pistol hadharani, wote walioshikwa wakitoa rushwa wakati wa uchaguzi wenu! Malumbano ndani ya chama ni dalili ya kukua kwa demokrasia na uhuru wa kutoa mawazo ndani ya chama, upande wenu nani anasubutu kufungua mdomo?
 
Mimi naona chadema kama uongozi wamefanya vyema katika huu mgogoro wa hutu tu vijana so far. Kimsingi hakuna jinsi ambavyo wangeweza kuziepuka hizi fujo. Chadema si chama kutoka paradiso, kinaongozwa na wanadamu, walio wengi wao ni vijana, wengine wamemaliza juzi shule na chadema ndio kazi yao ya kwanza.

Ukiangalia vizuri uongozi wa juu wa chama ni kama vile wanajua sana kinachoendelea kuliko hata sisi tunavyojua, ila wameacha magugu na ngano vyote viote kwa pamoja halafu mvunaji si ana akili timamu? Si atapembua ngano na mbegu mwitu? Na mimi hiyo naona ni busara sana kwa sababu chama kimekua vya kutosha, wajumbe ni wengi sana, kufahamu nani tope nani lulu ni ngumu sana kwao kuzingatia hali halisi pamoja na njaa, ulafi na kukosa hekima kwa baadhi ya vijana (na hata wazee) wa kitanzania.

Sanasana kama kuna la kujifuza kama taifa kwa ujumla katika mtifutifu huu wa vijana wa chadema, ni kwamba vijana si watu wa kuwekea dhamana. Na itakuwa makosa kuruhusu kwenye katiba vijana chini ya miaka 40 kugombea urais. Hawaaminiki.
 
Wanafiki ni wengi sana Chadema.Mtu Ana kadi mbili za chama wewe unafikiri nini kinachoendelea
 
wewe kimbunga mbona hutumii akili hata kidogo? Waambie hao policcm kwanza wawashugulikie bashe na kigwangala kwa kutoleana pistol hadharani, wote walioshikwa wakitoa rushwa wakati wa uchaguzi wenu! Malumbano ndani ya chama ni dalili ya kukua kwa demokrasia na uhuru wa kutoa mawazo ndani ya chama, upande wenu nani anasubutu kufungua mdomo?

Hivi uhuru wa kutoa mawazo ndio uko hivi CDM?.
 
nasikia sikia sana habari za kuchinjana. Kuuana nk. Nasikia habari hizi kwa watu wale wale wa kikundi kile kile. Moja, natoka Kigoma. Nimeaga kwetu. Nitakufa kwa amri ya Mungu. Siogopi kufa. Iwapo kifo changu kitatokana na mkono wa mtu, sidhani kama kwa mtu huyo kama hata panya atabaki nyumbani kwao. Underline this.
 
Je, tuamini kuwa vijana hawawezi kupewa uongozi? Kwa mtaji huu wa malumbano jinsi hii nachelea kusema yawezekana kabisa vijana wanaolilia uongozi busara zao za kuongoza ni finyu.
 
Guys:

Kama CCM wakaamua leo kulipuana Mitandaoni kama Mnavyofanya nyie wana CDM, It will be completely Dead.
Siamini kama ni haki kwa nyie viongozi vijana na tegemeo kwa Chadema kuanza kulimbana na kulipuana mitandaoni tena mtandao maarufu kama Huu.

Sidhani kama hii ni busara hata kidogo. Tunaomba hayo mambo yenu ya ndani malizieni kwenye vikao. Kuna wengine tulishaona ukombozi ukija kupitia CDM. ila kwa haya yanayojitokeza sasa naomba nikiri kukosa Imani na CDM. na kwa mwendo huu niseme tu hiki Chama hakifai kupewa Dola.

Nguvu zote, Gharama zote zilizotumiaka kwenye M4C zimekua Bure? hivi mnajua kuna watu wamepoteza maisha kwaajili ya kuitetea Chadema? ni raia wangapi wamepigwa risasi kwenye mikutano ya CDM?

Leo hii kula kitu kimekua bure? hivi haya malumbano mnayaleta huku jamvini kwa faidi ya nani? Kwahiyo tumeshajua yote hayo, mnataka tuchukue hatua gani?

Kumbukeni sisi hatuna la kufanya zaidi ya kufanya maamuzi ya Binafsi kuhusu CDM. Hivi nikisema haya malumbano yameshusha umaarufu wa CDM nitakua nimekosea?

Ishi!!!!!!!!!, si mlisema CDM ni chama makini???? Wapi bwana.........' Chama gani makini kinakuwaga na viongozi na wabunge wa kuteuliwa wanaotoka mkoa mmoja? CHADEMA hamna lolote!!!! Ni ukabila, na ubinafsi. Chama kinachotaka kuigawa nchi kwa mfumo wa majimbo???? Sera za wapi hizo??? Chama hakina hata ofisi mikoani....' leo kituletee maendeleo? Kinataka huruma ya wananchi kwa kufanya maandamano yasiyokuwa na tija..... yaliyobatizwa jina la M4C!!! Jina lenyewe ni kama la kigaidi maana linafanana na waasi wa Congo DRC.... Leo mmejionea wenyewe chadema hakifaiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii.
 
Wameshapoteza mwaka mzima; na wanaingia 2013 na haya madudu; kweli kabisa; if they don't do something tutawasaidia kuchemsha chungu kizima maana moto wana uwasha wa nini kama hawataki kupika? Wanataka kuota tu halafu waondoke au wanataka uunguze nyumba? Wengine tumekaa kimya kuangalia nani mwenye hekima humo ndani....
Mzee Mwanakijiji

Tuwe wavumilivu, kauli za Zitto na Ben zilielezea utayari wao wa kuyafikisha haya kwenye vyombo vya chama, nadhani hapo ndio tutaanza kuwapima vyema.
 
Siku zote wagombanao ndio wapatanao.Ni vyema ugomvi wa mume na mke mkausemea ndani ili majirani wasijue mmekwaruzana.Nitamlaumu zaidi Zitto Kabwe sababu yeye ni kiongozi wa Taifa kwa sasa.Kama Mbunge hakutakiwa kujibizana kwenye mtandao.Ajifunze kwa makosa.Binadamu haachwi kusema wakiacha kukusema basi umeshakuwa maiti.Poleni mliogombana ila msivunje chama bali ugomvi huu uwe wa kukiimarisha chama zaidi.
 
....hakuna dhambi mbaya kama unafiki...ndio maana ktk taasisi za kiusalama, unafiki unatafsiriwa kama uasi, ambao adhabu yake ni moja tuuu...hapa tunachokiona kikiibuliwa ktk skandali nzima ni unafiki wa vijana wengi ktk cdm...basi..kama kulikuwa kuna mawasiliano ya kujadili masuala ya chama, ambayo yalikuwa ni ya nje ya taratibu na kanuni za cdm baina ya kina saa nane, na wenziwe kama tunavyosoma sasa, basi huo ulikuwa ni unafiki na hujuma kwa chama....mimi siku zote nilikuwa naamaini afadhali ya kuwa na aina ya watu kama "mzee wa ujira mwia"..hawajifichi, kuliko "snake in the monkey shadow"...hofu yangu, hawa wapuuzi wanaojidhalilisha leo, wasijekuwa ni vivuli vya huuma nzima, nyuma yao kuna "mabwege" wakubwa, si tayari jina la kitila linatokea ktk upuuzi huu...?
 
Tatizo kubwa sana pia wachambuzi maarufu wa siasa za Tanzania akiwemo MM Mwanakijiji ambao mchango kwenye mabadiliko ni mkubwa wanataka wasionekane wabaya kila upande hakuna anayesema tatizo moja kwa moja!

Hakuna aliyeonya wazi kwa kusema fulani wewe ni tatizo kama tunavyomsema wazi Mh Rais Kikwete wote tuna hit around the bush kwa kuzungumzia tatizo tukidhani mifumo peke yake itatusaidia bila kukosoana kwa uwazi.

Tunawasema viongozi wanaogopana lakini hata wachambuzi wakubwa tu hawana jeuri ya kusema Dr Slaa umekosea hapa,Zitto umekosea hapa,Mkumbo,Mbowe n.k inafikia kipindi wote wanadhani anayesemwa ni adui yake!

Mwl Nyerere aliwahi kumsema Mh Mwinyi akiwa madarakani na wengine wengi kwa kutaja makosa yao.Hebu twende hatua moja mbele tuseme wazi pamoja na kuimarisha mifumo lakini kiongozi fulani hana maadili ya kuongoza alafu tunazunguka zunguka tu haisaidii.

Tuache porojo za kujaza pages hapa tuseme tatizo wazi,wengine tayari tupo biased hamtatuelewa.
 
...kila mapinduzi hutengeneza mashujaa na wasaliti wake...ukisha lijua hili haya yanayotokea sasa Chadema hayawezi kukupa-shida,ni kiasi cha kuchambua pumba ni zipi na mchele ni upi tu...
 
Mzee Mwanakijiji

Tuwe wavumilivu, kauli za Zitto na Ben zilielezea utayari wao wa kuyafikisha haya kwenye vyombo vya chama, nadhani hapo ndio tutaanza kuwapima vyema.


Tofauti na hawa vijana wengine toka BAVICHA, Zitto yuko kwenye safu ya juu ya uongozi wa CHADEMA, sijui kwanini hakuona busara kupeleka haya mashauri kwenye vikao vya chama? The minute alivyojibu madai ya Mamuya, kila kitu kilibadilika. Mambo ya kitoto kabisa!
 
Good MTAZAMO ili uponyaji wa kweli upatikane,kwa hali ilipokuwa imefikia ni
kweli lazima kila kitu kiwe wazi.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom