Chadema hongera!

chama

JF-Expert Member
Aug 6, 2010
8,001
2,418
Mafanikio ya chadema katika uchaguzi huu makubwa na yanastahili kupongezwa na kila mtanzania anayeitakia mema nchi hii. Hakuna kificho kuwa Chadema wamedhulumiwa ushindi; hata sisi wanaccm tunayoitakia mema nchi yetu tunaona aibu kutembea vifua wazi kusheherekea ushindi huu. Hii ni sawa na baba kusheherekea arusi ya mtoto shoga aliyepata mume. Hii ni fedheha kubwa kwa kiongozi aneyejinadi kuwa ni mwanademokrasia kila kona ya dunia. Siasa ni ushindani; lakini hatuna ulazima wa kuendesha nchi kama hatuwezi. Watanzania wanachodai ni maendeleo, wale wanaccm mliokimbilia pilau na fulana uchaguzi umekwisha shangwe zenu zimeishia wapi? Kumbukeni Raisi bora ni yule anayewajali wananchi wake kwenye kipindi chote cha utawala na si kwenye uchaguzi tu! CCM inaongozwa na kikundi cha wahuni kwa manufaa ya familia zao na marafiki zao; JK hakubaliki, tumechoshwa na kauli za ccm imeleta amani, hii karne ya 21 acheni kutuongoza kwa siasa za karne ya 20. JAMBO FORUM HONGERA KWA UTANDAWAZI. "WE ARE ALL FIGHTING FOR COMMON CAUSE REGARDLESS OF OUR POLITCAL VIEWS". GODBLESS TANZANIA.
 
mafanikio ya chadema katika uchaguzi huu makubwa na yanastahili kupongezwa na kila mtanzania anayeitakia mema nchi hii. hakuna kificho kuwa chadema wamedhulumiwa ushindi; hata sisi wanaccm tunayoitakia mema nchi yetu tunaona aibu kutembea vifua wazi kusheherekea ushindi huu. hii ni sawa na baba kusheherekea arusi ya mtoto shoga aliyepata mume. hii ni fedheha kubwa kwa kiongozi aneyejinadi kuwa ni mwanademokrasia kila kona ya dunia. Siasa ni ushindani; lakini hatuna ulazima wa kuendesha nchi kama hatuwezi. Watanzania wanachodai ni maendeleo, wale wanaccm mliokimbilia pilau na fulana uchaguzi umekwisha shangwe zenu zimeishia wapi? Kumbukeni raisi bora ni yule anayewajali wananchi wake kwenye kipindi chote cha utawala na si kwenye uchaguzi tu! ccm inaongozwa na kikundi cha wahuni kwa manufaa ya familia zao na marafiki zao; jk hakubaliki, tumechoshwa na kauli za ccm imeleta amani, hii karne ya 21 acheni kutuongoza kwa siasa za karne ya 20. jambo forum hongera kwa utandawazi. "we are all fighting for common cause regardless of our politcal views". Godbless tanzania.

:spider:
 
hata sisi wanaccm tunayoitakia mema nchi yetu tunaona aibu kutembea vifua wazi kusheherekea ushindi huu. [/I]

hapo kwenye RED! unauhakika..?!! chadema imekosa umaarufu mikoa mingi ikiwemo ya pwani,na baadhi ya nyanda za kati , na kule kwenye mizizi wamegawana na chama tawala. sikwambii kuhusu visiwani. !! CCM haiwezi kuangushwa unless wapinzani waungane. ushindi wa chadema niliouna ni wa katika JF POLL!.. hehehehehe! synovate waliwaambia JK atashinda kwa asilimia ngapi, makabisha! ingawa hakupata exactly ziliwalizosema lakini alikaribia!.. nawatakia mafanikio mema , ila mshaurini slaa chonde chonde akubali matokeo.. mileta vurugu waulizeni wapemba walipokiona cha moto mpaka wakawa wakimbizi mombasa.. tunahitaji AMANI NCHI YETU!
 
Sijui ni wangapi walipiga kura kukataa kupunguzwa kwa bei ya BATI na CEMENT, Sijui ni wangapi walipga kura kubariki UFISADI na kuruhusu watanzania kuendelea kubakwa in terms of RASILIMALI zetu, Sijui ni wangapi waliopiga kura kupinga maendeleo ili wao wapate kuendellea kuwa fukara maskini wa mwisho ktk sayari hii... Inauma sana! inauma sana kuona kuwa wananchi wanadhulumiwa haki yao ya kikatiba... Wao walifanyakazi ya ziada kama JK alivyotanabaisha, Sisi wananchi tutafanyakazi ya Ziada kuwang'oa hawa madhulumati. MUNGU IBARIKI TANZANIA
 
Njiwa, ni kweli kuwa vyama viungana CCM itadondoka haraka zaidi, lakini si lazima vyama viungane kuidondosha CCM. Given time CCM itadondoka tu. It is just a matter of time.
 
Njiwa siongelei siasa kama unazi wa yanga na simba; maamuzi ya kisiasa yanagusa maisha yetu na vizazi vyetu, viongozi tulionao ndani ya ccm wanatumia kila njia kuleta mifarakano ndani ya jamii zetu ili washinde, wao walikuwa wakwanza kuhoji udini Tanzania tumeshawahi kuwa na maraisi wakatoliki, je waliatuathiri kitu gani? Dini kuu mbili Tanzania ni uislamu na ukristu kwa vyote vyote raisi atatokana na dini hizo mbili, wanaccm wanaoitakia mema ni wengi sana ndio maana mh. Kikwete kaambulia 61%. Siasa za ubabe zilishapitwa na wakati wala hazina nafasi kwenye dunia hii ya karne ya 21; sijui unanufaika na kitu gani na serikali hii ya mh. Kikwete lakini mtanzania wa kawaida anayekabailiana na ugumu wa maisha hakumpigia kura mh. Kikwete, kama ushindi ni wa halali kulikuwa na haja gani ya kuliweka jeshi kwenye hali ya tahadhari? Lakini mkumbushe JK support ya wanajeshi pekee haimuweki mtawala madarakani. Hakuna mtanzania asiyeijua Chadema, inawezekana hawakuwa na nyenzo za kufika kila mkoa lakini salamu zao. Hao watu mil.12 unaombiwa hawakupiga kura ni watanzania waoitakia mema nchi hii si kwamba hawakupiga bali walimkataa JK . Watanzania wawe wakimbizi mara ngapi? Hali zetu za maisha hazitofautiani na wakimbizi, nenda mbagala ukaone wakimbizi nyumba zao zimeharibiwa na mabomu, nenda kiwalani utaona wakimbizi waliovunjiwa nyumba. CCM ndio tunaochezea amani ya nchi.
 
Back
Top Bottom