CHADEMA: Hatutashiriki Kongamano la Amani la TCD, limefadhiliwa na CCM!

Mkuu hamy yawezekana kesho hakuna msosi ndiyo maana hawaendi jamaa na msosi damudamu.

Lakini pia wao wanahubiri vurugu na mada za kesho zitakuwa zinahusu amani kwa hiyo si zao any way tuendelee kuwapa shule ili vichwa vyao vifunguke .

ImageUploadedByJamiiForums1373296200.804940.jpg

ImageUploadedByJamiiForums1373296279.029004.jpg
 
Nawaunga mkono kabisa; hili ndilo lililopaswa kufanyika kuhusiana na mwaliko wa Ikulu/Ubalozi kwenye dhifa.

a. Mnakaa chini na kuchukua msimamo wa pamoja (ambao naamini ulipaswa kuchukuliwa wiki kadhaa kabla ya Obama kuja)
b. Mnawaambia waandishi wa habari kuwa mmepokea au hamjapokea (haina tofauti) mwaliko
c. Mnaelezea umuhimu na heshima ya Obama kuja Tanzania na mahusiano ya karibu na watu wa Marekani
d. Mnakataa kwa heshima na taadhima zote kwanini hamtoenda kwenye dhifa hiyo
e. Mnatoa sababu kama walivyofanya hapa kwa sababu sababu zilizotolewa hapa ni hizo hizo - la labda na ushahidi zaidi - ambazo zingetolewa.

Sasa kwa vile wamesahihisha kosa lile vizuri sana; natumaini msimamo huu hautakuwa na kigeugeu hadi baadhi ya mambo ambayo mnapigania yanatekelezwa vinginevyo waambieni tukutane 2015.
 
Ukosefu wa ajira za kueleweka ndio umesababisha mkubali kuwa misukule ya lumumba kwa ujira wa buku saba tu per day. Hata hamjionei aibu kwa namna mnavyotumika?
Mwita wewe unajira gani unatumika kama tambala la deki tangu umepelekwa kata ya mianzini kwenda kuitetea chadema ukagongwa na chama kimekufa mianzini ndo basi tena ulidhani bongo ni moshi.

Aibu yako au aibu yenu mtaendelea kusamaratishwa,bado arusha j.pili mtagongwa tena mnajiita chaga development manfesto(chadema) mtaipata tu.
 
BREAKING NEWS

TOKA JIJINI GOMA MAKAO MAKUU YA MKOA WA KIVU YA KSAKAZINI (NORD KIVU)

INASEMEKANA KUANZIA SAA MOJA NA NUSU KWA SAA ZA AFRIKA YA KATI TAYARI VITA IMEANZA.

"Mapambano yameanza 8km na Goma Munusco, fdrl NA fardc wako NA tumpa
kompora kwenye ngome ya m23. M23 inajianda kujibu NA nguvu zisizo za kawaadi.
NA ushindi ni a pa karibuni.

The fighting has asterted at 8 kms of goma. MONUSCO fdlr and fardc are shelling bombs on m23 positions."

HII NI NUKUU YA MMOJA YA WANA JF ALIYEPO GOMA



 
Amani haijadiliwi! Kweli Kigaila?
Inaweza kuwa kweli CCM kupitia TCD imefadhili huu mkutano. Lakini sidhani kama hiyo ni sababu ya kususia.
Chadema inasema ina ushahidi usio na shaka kuhusiana na jinsi serikali ya CCM inavyohusika kueneza chuki na magomvi. Naamini mkutano kama huu ambao CCM wangehudhuria ni fursa ya Chadema kuyasema haya mbele ya CCM huku watu wengi wakisikia na kuchangia.
Njia moja nzuri ya kumjua adui yako ni kumweleza ukweli mbele yake, si kujificha kipembeni na kuanza kumsema ubaya wake.
Naamini Chadema wanapoteza nafasi nzuri sana ya kufanya kile ambacho kingeweza kuonyesha chama hicho kinasimamia nini katika suala hili.
Vema, Chadema imemua kutoshiriki mkutano huu kwa sababu ilizozitoa. je, chenyewe sasa kinadhani nini kifanyike ili kuiridisha nchi katika amani iliyopotea au iliyo katika hatari ya kupotea?
Hicho wanachodhani kinapaswa kufanyika, je, hii haikuwa nafasi ncuwi ya kukisema tena mbele ya wale ambao wanapaswa kutenda ili kutunza amani ya nchi?

Mkuu Mpita Njia ni lini ccm na serikali yake wameanza kuwa wasikivu hadi unadhani kwamba Chadema ikiwasema katika ukumbi mmoja watasikia na kuelewa? Unadhani kwamba ccm na serikali yake hawajui wanachokifanya kwamba ni ufirauni?

Yani ccm inafanya hadaa ya kuitisha mkutano wa kupumbaza watu wakati masuala ya msingi ambayo yalitakiwa kushughukikiwa ili kuleta hiyo amani inayotajwa kupotea yakiachwa pembeni. Kwanini serikali haishughukiki seriously na matukio ya milipuko ya Arusha? (kanisani Olasiti na mkutano wa Soweto)
 
Last edited by a moderator:
Nawaunga mkono kabisa; hili ndilo lililopaswa kufanyika kuhusiana na mwaliko wa Ikulu/Ubalozi kwenye dhifa.

a. Mnakaa chini na kuchukua msimamo wa pamoja (ambao naamini ulipaswa kuchukuliwa wiki kadhaa kabla ya Obama kuja)
b. Mnawaambia waandishi wa habari kuwa mmepokea au hamjapokea (haina tofauti) mwaliko
c. Mnaelezea umuhimu na heshima ya Obama kuja Tanzania na mahusiano ya karibu na watu wa Marekani
d. Mnakataa kwa heshima na taadhima zote kwanini hamtoenda kwenye dhifa hiyo
e. Mnatoa sababu kama walivyofanya hapa kwa sababu sababu zilizotolewa hapa ni hizo hizo - la labda na ushahidi zaidi - ambazo zingetolewa.

Sasa kwa vile wamesahihisha kosa lile vizuri sana; natumaini msimamo huu hautakuwa na kigeugeu hadi baadhi ya mambo ambayo mnapigania yanatekelezwa vinginevyo waambieni tukutane 2015.
Mkuu mwanakijiji kama kunachakula kunawatu wataenda kinyemela.
 
Mpenda amani hata siku moja haweki mashariti ya kujadili amani! Anapenda kujali amani iwe baa, kwenye daladala, kwa mualiko au bila mwaliko. Kwake interest yake ni kupata amani tu kwa manufaa ya wote!
 
Ninyi ni mashahidi wa jinsi Waziri Mkuu Pinda alivyo mstari wa mbele katika kuhubiri kauli za chuki, uhasama, uchochezi, ubabe na ukiukwaji wa haki za binadamu nchini. Siyo mara moja wala mbili, Waziri Mkuu Pinda amesikika, tena ndani ya Bunge, akihamasiha vyombo vya usalama kuvunja sheria kwa kupiga, kuteka na kung'oa meno watu wanaotumia haki zao za kikatiba kushinikiza serikali kuchukua hatua dhidi ya maovu.

Hii imekaa vizuri................ Pinda ni zaidi ya Gaidi. Roho ya Mizengo Pinda ni sawa na sura yake kabisa.
 
Tangu lini Kikwete ana hatimiliki ya Ikulu?

Ana miliki ya Ikulu tangu 2005. Ndiyo maana Mbowe na Slaa hawawezi kufanya dhifa ya kitaifa pale kumkaribisha Obama.At best wataalikwa tu.

Kwa tunaojali etymology, miliki inatoka katika mzizi wa neno Malik, mtawala, ndo hapo unapata na malkia, mke wa mtawala.

Kwa msingi huu Kikwete kama rais huwezi kusema hana miliki ya Ikulu, as a matter of fact kikatiba Tanzania rais ana dhamana ya kumiliki ardhi ya Tanzania nzima, achilia mbali Ikulu tu.
 
Uamuzi sahihi, uamuzi wa busara, uamuzi wenye kuungwa mkono na wapenda amani ya dhati na kweli. Tunakubaliana na msimamo huu wa chadema kwa asilimia mia. Big up makamanda wa kweli.
 
Hii imekaa vizuri................ Pinda ni zaidi ya Gaidi. Roho ya Mizengo Pinda ni sawa na sura yake kabisa.
Vipi sura ya slaa imekaa kama nini hata kwenye aina ya viumbe vya mungu sidhani kama ipo,pinda anakunyima raha ee,pole pinda kaletwa na mungu utafanya nini wewe kidampa tu.
 
Back
Top Bottom