Chadema hasa mbowe tafadhali jibu hotuba ya rais kikwete ama sivyo tutaamini kila achosema

HISIA KALI

JF-Expert Member
Oct 26, 2010
694
108
Nimesoma na kusikiliza hotuba ya rais kikwete. Pia nimefuatia maoni ya watu mbalimbali kuhusu hiyo hotuba ya rais kikwete.

Kitu kikubwa nilichogua ni kwamba rais kikwete aliandaa hotuba ile kupinga hoja za chadema. Rais ametaja chadema na mwenyekiti wake ndugu freeman mbowe waziwazi ili kuonyesha jinsi gani anapinga hoja zao. Pia rais kikwete ametumia ahadi ya dr slaa wakati wa uchaguzi 2010 kuwa kama angechaguliwa angeanzisha mipango ya katiba mpya ndani ya siku 100. Rais kikwete ametumia hoja hizo kuonyesha kuwa chadema pamoja na viongozi wake wanapotosha wananchi kuhusu mchakato wa katiba mpya unavyeendeshwa na serikali.

Sasa wananchi wameshasikia ya rais. Je rais kuna ukweli gani kwenye hii hotuba ya rais kikwete? Swali hili kwa kiasi fulani linatakiwa lijibiwe na chadema hasa mwenyekiti mbowe ambaye ametajwa wazi wazi kwenye hiyo hotuba.

Ni matumaini yangu na dhani pia ya wananchi wengine wengi kutaka kujua je chadema na mbowe wanasemaje kuhusu zile hoja ambazo rais amezielekeza kwao moja kwa moja?
 
Kwanza tunaomba muwaite vijana wa chadema wakati wa kujibu hizo hoja
 
Unajua hata mimi sijaelewa hoja ya msingi ya kina TUNDU na wenzake iliyowafanya wasusie mswada wa mabadiliko ya sheria. Ingawa sijui sheria lakini angalau JK amenisaidia kunielewesha kuwa wanachokifanya kina TUNDU na wenzake kumbe ni kinyume na katiba.
 
Unajua hata mimi sijaelewa hoja ya msingi ya kina TUNDU na wenzake iliyowafanya wasusie mswada wa mabadiliko ya sheria. Ingawa sijui sheria lakini angalau JK amenisaidia kunielewesha kuwa wanachokifanya kina TUNDU na wenzake kumbe ni kinyume na katiba.

Inabidi waeleze kwa kina ili wananchi waelewe
 
wote mliocomment hapo juu ni masaburi tu,yaani wewe ni nani mpaka utoe hiyo amri ya kujibiwa,kwani aliyaongea huyo anayeitwa 'rahisi' yana hoja gani mpaka ajibiwe,makamanda wana kazi nyingi za kufanya na sio kujibishana na wapuuzi,kamwambie aliyewatuma kuwa....********** sana tu p.......****vu zenu
 
Inabidi waeleze kwa kina ili wananchi waelewe

Msimamo wa CDM uko wazi, na kwa uchache ni kupinga muswada wa sheria ya mabadiliko ya katiba kusomwa mara ya pili bungeni kwa sababu za msingi kuwa, wanachi wengi hawakufafanuliwa kilichomo kwenye muswada.
Unaposema CDM inabidi waleze kwa kina ili wananchi wawaelewe unamaanisha nini? Hivi unadhani watanzania ni wajinga kama ulivyo ww?
Kama unadhani kuna haja ya hicho ulichoita ufafanuzi wa CDM fanya wewe,.
 
Msani,twende polepole wataelewa tu! Na pamoja ya kwamba walio na akili timamu wanaelewa nini chadema inafanya, bt ingekuwa ni vyema chama kikae na kutoa press release sio tu kujibu hotuba ya jana iliyozamiria kupotosha umma bali itoe mustakabali mzima wa nini wananchi tutarajie kutoka kwao badala ya kupindishwa kwa muswada wa katiba.

Ni wale wenye akili finyu tu ndio wanaona hili swala ni la kichama,na sio la kitaifa! Eeh Mungu tuongoze.
 
unaweza tu kumuelimisha mwenzako ambaye hajaelewa bila matusi au kamkashifu civility is very important in politics.
nilichoelewa mimi pamoja na yaliyotajwa hapo ni kuwa CDM wanapinga utaratibu mzima wa namna maoni yalivyokusanywa kwa maana ya mikoa mitatu baada ya kujitahidi angalau wananchi wengi kutoka mikoa mingine pia washirikishwe.
 
Back
Top Bottom