John Marwa
JF-Expert Member
- May 25, 2011
- 275
- 28
Nimepitia kwa Umakini Katiba ya CHADEMA tofauti na matarajio ya Chama chochote cha Siasa lazima kuweka msimamo wake hasa mlengwa wa Kiitikadi!
CHADEMA haijaweka wazi kama ni Chama cha Kijamaa au ni Chama Cha Kibepari! Tofauti na CCM ambao wao Wanasema ni Chama cha Kijamaa japokuwa Ujamaa walisha Uweka kando!
Vyama vingi duniani huonesha mlengo wake hasa kama ni kuamini Ubepari au Ujamaa! Hata marafiki zao wa Ujerumani na Uingereza wamebainisha mlengo wa Vyama vyao!
Wanachama wa CHADEMA walio wengi hata hapa JF hawajui Itikadi ya Chama Chao(Inasikitisha sana)! Hakuna tofauti kati ya CHADEMA na Timu ya Simba wala Yanga kwani hawana Itikadi!
My Take: CHADEMA ijipambanua ina itikadi gani Ujamaa au Ubepari! Wanachadema jiulizeni Itikadi ya Chama chenu ni ipi?
CHADEMA haijaweka wazi kama ni Chama cha Kijamaa au ni Chama Cha Kibepari! Tofauti na CCM ambao wao Wanasema ni Chama cha Kijamaa japokuwa Ujamaa walisha Uweka kando!
Vyama vingi duniani huonesha mlengo wake hasa kama ni kuamini Ubepari au Ujamaa! Hata marafiki zao wa Ujerumani na Uingereza wamebainisha mlengo wa Vyama vyao!
Wanachama wa CHADEMA walio wengi hata hapa JF hawajui Itikadi ya Chama Chao(Inasikitisha sana)! Hakuna tofauti kati ya CHADEMA na Timu ya Simba wala Yanga kwani hawana Itikadi!
My Take: CHADEMA ijipambanua ina itikadi gani Ujamaa au Ubepari! Wanachadema jiulizeni Itikadi ya Chama chenu ni ipi?
3.B. Itikadi ya CHADEMA
3.1.1 CHADEMA ni chama cha itikadi ya MRENGO WA KATI (center party).
3.1.2 CHADEMA ni chama kinachoamini kukuza na kuimarisha uchumi wa nchi kwa kutumia raslimali za nchi yetu bila kuathiri uhuru wa Taifa, na kuhakikisha kuwa umma kwa ujumla unanufaika na raslimali zao.
3.1.3 CHADEMA inaamini katika kujenga na kuimarisha uchumi wa soko huru, utakaoheshimu na kulinda haki na mali za watu, biashara huru na sekta ya watu binafsi bila kupoka mamlaka ya umma katika maeneo nyeti hususani pale penye hitilafu ya soko au penye maeneo nyeti ya kiuchumi. Tunaamini katika soko huru sio soko holela.
3.1.4 CHADEMA inaamini kuhakikisha matumizi bora ya raslimali asilia za nchi ili zichangie kikamilifu katika pato la taifa na hasa kuboresha huduma za kiuchumi zinazotumiwa na wananchi wote.
3.1.5 CHADEMA inaamini katika uzalendo na kuthamini mila na desturi zetu zilizo nzuri.
3.1.6 CHADEMA inaamini katika uhuru chini ya sheria zilizo za haki.
3.1.7 CHADEMA inaamini katika siasa ambazo ziko juu ya vyama zenye kusimamia zaidi maslahi ya Taifa.
3.1.8 CHADEMA inaweka umuhimu wa pekee katika familia kama moja ya taasisi muhimu ya kijamii.
3.1.9 CHADEMA inaamini katika umuhimu wa uhuru wa kuamini katika kujenga maadili ya mwanajamii mmoja mmoja bila kuifanya dini kuwa sehemu ya dola.
3.1.10 CHADEMA inaamini taifa linaundwa na watu, hivyo uhai wake unawategemea watu, na mabadiliko yake yanatokana na watu.
3.1.11 CHADEMA inaamini katika kujenga uwezo wa wazawa katika kumiliki na kuendesha uchumi.
3.1.12 CHADEMA inaamini kumiliki raslimali na mali miongoni mwa wananchi kunawapa uhuru zaidi hivyo tunataka kujenga chama na baadaye taifa lenye kutoa fursa, ambapo kila mtu bila kujali asili na hali yake anaweza kutimiza na kufanikiwa kadiri ya vipaji vyake.
Source:Chama Cha Demokrasia Na Maendeleo – Chadema | Itikadi
Note:
1. Itikadi ya Mrengo wa Kati (Centre) – Huu ni mrengo kati ya Uliberali na Ujamaa wa kidemokrasia. Chadema inatamka hii kama itikadi yake kama chama. Kwa kawaida, Itikadi ya mrengo wa kati (centre) inaamini na kuunga mkono mambo makuu yafuatayo:
· Ongezeko la kodi linaloenda sambamba na ongezeko la vipato vitokanavyo na shughuli za uchumi (progressive taxation); Umiliki binafsi wa mali; Uhuru na haki ya wananchi mbele ya sheria; Uliberali wa kiuchumi na uliberali wa kijamii.