CHADEMA Haina Itikadi Kama Chama!

John Marwa

JF-Expert Member
May 25, 2011
275
28
Nimepitia kwa Umakini Katiba ya CHADEMA tofauti na matarajio ya Chama chochote cha Siasa lazima kuweka msimamo wake hasa mlengwa wa Kiitikadi!

CHADEMA haijaweka wazi kama ni Chama cha Kijamaa au ni Chama Cha Kibepari! Tofauti na CCM ambao wao Wanasema ni Chama cha Kijamaa japokuwa Ujamaa walisha Uweka kando!

Vyama vingi duniani huonesha mlengo wake hasa kama ni kuamini Ubepari au Ujamaa! Hata marafiki zao wa Ujerumani na Uingereza wamebainisha mlengo wa Vyama vyao!

Wanachama wa
CHADEMA walio wengi hata hapa JF hawajui Itikadi ya Chama Chao(Inasikitisha sana)! Hakuna tofauti kati ya CHADEMA na Timu ya Simba wala Yanga kwani hawana Itikadi!

My Take:
CHADEMA ijipambanua ina itikadi gani Ujamaa au Ubepari! Wanachadema jiulizeni Itikadi ya Chama chenu ni ipi?

3.B. Itikadi ya CHADEMA
3.1.1 CHADEMA ni chama cha itikadi ya MRENGO WA KATI (center party).


3.1.2 CHADEMA ni chama kinachoamini kukuza na kuimarisha uchumi wa nchi kwa kutumia raslimali za nchi yetu bila kuathiri uhuru wa Taifa, na kuhakikisha kuwa umma kwa ujumla unanufaika na raslimali zao.

3.1.3 CHADEMA inaamini katika kujenga na kuimarisha uchumi wa soko huru, utakaoheshimu na kulinda haki na mali za watu, biashara huru na sekta ya watu binafsi bila kupoka mamlaka ya umma katika maeneo nyeti hususani pale penye hitilafu ya soko au penye maeneo nyeti ya kiuchumi. Tunaamini katika soko huru sio soko holela.

3.1.4 CHADEMA inaamini kuhakikisha matumizi bora ya raslimali asilia za nchi ili zichangie kikamilifu katika pato la taifa na hasa kuboresha huduma za kiuchumi zinazotumiwa na wananchi wote.

3.1.5 CHADEMA inaamini katika uzalendo na kuthamini mila na desturi zetu zilizo nzuri.

3.1.6 CHADEMA inaamini katika uhuru chini ya sheria zilizo za haki.

3.1.7 CHADEMA inaamini katika siasa ambazo ziko juu ya vyama zenye kusimamia zaidi maslahi ya Taifa.

3.1.8 CHADEMA inaweka umuhimu wa pekee katika familia kama moja ya taasisi muhimu ya kijamii.

3.1.9 CHADEMA inaamini katika umuhimu wa uhuru wa kuamini katika kujenga maadili ya mwanajamii mmoja mmoja bila kuifanya dini kuwa sehemu ya dola.

3.1.10 CHADEMA inaamini taifa linaundwa na watu, hivyo uhai wake unawategemea watu, na mabadiliko yake yanatokana na watu.

3.1.11 CHADEMA inaamini katika kujenga uwezo wa wazawa katika kumiliki na kuendesha uchumi.

3.1.12 CHADEMA inaamini kumiliki raslimali na mali miongoni mwa wananchi kunawapa uhuru zaidi hivyo tunataka kujenga chama na baadaye taifa lenye kutoa fursa, ambapo kila mtu bila kujali asili na hali yake anaweza kutimiza na kufanikiwa kadiri ya vipaji vyake.

Source:Chama Cha Demokrasia Na Maendeleo – Chadema | Itikadi


Note:


1. Itikadi ya Mrengo wa Kati (Centre) – Huu ni mrengo kati ya Uliberali na Ujamaa wa kidemokrasia. Chadema inatamka hii kama itikadi yake kama chama. Kwa kawaida, Itikadi ya mrengo wa kati (centre) inaamini na kuunga mkono mambo makuu yafuatayo:

· Ongezeko la kodi linaloenda sambamba na ongezeko la vipato vitokanavyo na shughuli za uchumi (progressive taxation); Umiliki binafsi wa mali; Uhuru na haki ya wananchi mbele ya sheria; Uliberali wa kiuchumi na uliberali wa kijamii.
 
Tupe premises mkuu zilizokufanya uende kwenye hiyo conclusion mkuu. Otherwise ts a Crap!
 
Kuna maana gani kuandika uwongo kwenye katiba ya chama kama hao wanamagamba uliowataja?...Umeuona wapi wakitekeleza Ujamaa wanaodai kuufuata?
Kuandika na kutekeleza unaona kipi bora?...Tunawajua nyie kuwa ni mabingwa wa maandishi na kusoma data zisizofanyiwa uchunguzi!
Kuna mkubwa wenu mmoja akianza kusoma miradi ya umeme inayofanyiwa kazi, utajua hakutakuwa na shida nchi hii tena...Lakini njoo kwenye utekelezaji, sihitaji kukupa mifano, maana hapo huenda unatumia jenereta!
 
Nimepitia kwa Umakini Katiba ya Chadema tofauti na matarajio ya Chama chochote cha Siasa lazima kuweka msimamo wake hasa mlengwa wa Kiitikadi! Chadema haijaweka wazi kama ni Chama cha Kijamaa au ni Chama Cha Kibepari! Tofauti na CCM ambao wao Wanasema ni Chama cha Kijamaa japokuwa Ujamaa walisha Uweka kando! Vyama vingi duniani huonesha mlengo wake hasa kama ni kuamini Ubepari au Ujamaa! Hata marafiki zao wa Ujerumani na Uingereza wamebainisha mlengo wa Vyama vyao! Wanachama wa Chadema walio wengi hata hapa JF hawajui Itikadi ya Chama Chao(Inasikitisha sana)! Hakuna tofauti kati ya Chadema na Timu ya Simba wala Yanga kwani hawana Itikadi!
My Take: Chadema ijipambanua ina itikadi gani Ujamaa au Ubepari! Wanachadema jiulizeni Itikadi ya Chama chenu ni ipi?

Gamba likiwa kwenye ubongo huwezi fikiria!
 
Tunaomba Kiongozi wa Chadema atujuze na kutoa maelezo juu ya Itikadi ya Chadema ni jambo la msingi tuielewe Chadema kama chama ambacho kinataka kupata ridhaa ya Watanzania kuongoza Nchi! Wale vijana mnaotukana hapa JF ebu acheni matusi kwa hii hoja! Slaa,Mbowe,Zitto,Mnyika,Regia,Lema,Ndesamburo,Lema wekeni msimamo wa itkadi ya Chadema hapa jamvini
 
Nimepitia kwa Umakini Katiba ya Chadema tofauti na matarajio ya Chama chochote cha Siasa lazima kuweka msimamo wake hasa mlengwa wa Kiitikadi! Chadema haijaweka wazi kama ni Chama cha Kijamaa au ni Chama Cha Kibepari! Tofauti na CCM ambao wao Wanasema ni Chama cha Kijamaa japokuwa Ujamaa walisha Uweka kando! Vyama vingi duniani huonesha mlengo wake hasa kama ni kuamini Ubepari au Ujamaa! Hata marafiki zao wa Ujerumani na Uingereza wamebainisha mlengo wa Vyama vyao! Wanachama wa Chadema walio wengi hata hapa JF hawajui Itikadi ya Chama Chao(Inasikitisha sana)! Hakuna tofauti kati ya Chadema na Timu ya Simba wala Yanga kwani hawana Itikadi!
My Take: Chadema ijipambanua ina itikadi gani Ujamaa au Ubepari! Wanachadema jiulizeni Itikadi ya Chama chenu ni ipi?

"the head is out of control" serious measures to be taken
 
Nimepitia kwa Umakini Katiba ya Chadema tofauti na matarajio ya Chama chochote cha Siasa lazima kuweka msimamo wake hasa mlengwa wa Kiitikadi! Chadema haijaweka wazi kama ni Chama cha Kijamaa au ni Chama Cha Kibepari! Tofauti na CCM ambao wao Wanasema ni Chama cha Kijamaa japokuwa Ujamaa walisha Uweka kando! Vyama vingi duniani huonesha mlengo wake hasa kama ni kuamini Ubepari au Ujamaa! Hata marafiki zao wa Ujerumani na Uingereza wamebainisha mlengo wa Vyama vyao! Wanachama wa Chadema walio wengi hata hapa JF hawajui Itikadi ya Chama Chao(Inasikitisha sana)! Hakuna tofauti kati ya Chadema na Timu ya Simba wala Yanga kwani hawana Itikadi!My Take: Chadema ijipambanua ina itikadi gani Ujamaa au Ubepari! Wanachadema jiulizeni Itikadi ya Chama chenu ni ipi?
hivi hakuna itikadi nyingine zaidi ya ujamaa na ubepari? ccm itikadi yake ni nini? na je itikadi ya ccm ndo inayoonekana katika mfumowa utawala wa nchi yetu? ujamaa ni nini na ubebari ni nini? hivi hizi si porojo tu za kuwafanya watu wasifikirie mifumo au itikadi zinazowafaa kwa jamiihusika!
 
hivi hakuna itikadi nyingine zaidi ya ujamaa na ubepari? ccm itikadi yake ni nini? na je itikadi ya ccm ndo inayoonekana katika mfumowa utawala wa nchi yetu? ujamaa ni nini na ubebari ni nini? hivi hizi si porojo tu za kuwafanya watu wasifikirie mifumo au itikadi zinazowafaa kwa jamiihusika!
Tunataka majibu zaidi kutoka CDM
 
Nini hasa maana ya Ubepari kama itikadi? maanake nijuavyo mimi Upebari ni mfumo wa kiuchumi unaosisitiza njia zote za production kuwa private owned, ziendeshwe kwa faida na malipo halali kwa wafanyakazi wake. Privatization haiwezi kuwa itikadi hata siku moja kama sii kuturudisha kule kwenye vita baridi.

Marekani UK na nchi kibao leo hii duniani zinafuata mfumo huu wa kiuchumi tukiwamo hata sisi leo hii, hivyo huwa nashindwa kuelewa mtu anaposema Ubepari kama ITIKADI ya chama wakati CCM ndio wanabinafsisha mashirika bila kufikiri kuliko hata Mabepari wenyewe.

Na ndio maana huuliza hivi Democratic ya kina Obama wanapingana na Ubepari!
 
Nimepitia kwa Umakini Katiba ya Chadema tofauti na matarajio ya Chama chochote cha Siasa lazima kuweka msimamo wake hasa mlengwa wa Kiitikadi! Chadema haijaweka wazi kama ni Chama cha Kijamaa au ni Chama Cha Kibepari! Tofauti na CCM ambao wao Wanasema ni Chama cha Kijamaa japokuwa Ujamaa walisha Uweka kando! Vyama vingi duniani huonesha mlengo wake hasa kama ni kuamini Ubepari au Ujamaa! Hata marafiki zao wa Ujerumani na Uingereza wamebainisha mlengo wa Vyama vyao! Wanachama wa Chadema walio wengi hata hapa JF hawajui Itikadi ya Chama Chao(Inasikitisha sana)! Hakuna tofauti kati ya Chadema na Timu ya Simba wala Yanga kwani hawana Itikadi!
My Take: Chadema ijipambanua ina itikadi gani Ujamaa au Ubepari! Wanachadema jiulizeni Itikadi ya Chama chenu ni ipi?

grrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr so unaweza kusema CCM ambao ni chama tawala wana itikadi?
 
Zamani CCM walikiwa 'to the left' sijui sasa practically watasema wako upande gani. CHADEMA ni 'centre -left' Angalia manifesto yao 2010 (chadema manifesto)
 
Mkandara na Mzee wa KIjijini mwacheni kijana kazidiwa baada ya kunywa maji ya bendera yao yamemdhuru kaa E coli .Mpeni pole huyo .
 
Nimepitia kwa Umakini Katiba ya Chadema tofauti na matarajio ya Chama chochote cha Siasa lazima kuweka msimamo wake hasa mlengwa wa Kiitikadi! Chadema haijaweka wazi kama ni Chama cha Kijamaa au ni Chama Cha Kibepari! Tofauti na CCM ambao wao Wanasema ni Chama cha Kijamaa japokuwa Ujamaa walisha Uweka kando! Vyama vingi duniani huonesha mlengo wake hasa kama ni kuamini Ubepari au Ujamaa! Hata marafiki zao wa Ujerumani na Uingereza wamebainisha mlengo wa Vyama vyao! Wanachama wa Chadema walio wengi hata hapa JF hawajui Itikadi ya Chama Chao(Inasikitisha sana)! Hakuna tofauti kati ya Chadema na Timu ya Simba wala Yanga kwani hawana Itikadi!
My Take: Chadema ijipambanua ina itikadi gani Ujamaa au Ubepari! Wanachadema jiulizeni Itikadi ya Chama chenu ni ipi?

 
Tunakubali,CCM itikadi yao ilikuwa ujamaa.Yako wapi hayo mafanikio ya ujamaa?Matokeo yake wamefilisi mashirika ya umma.Sasa ni mabepari wanawanyonya wananchi.wakijilimbikizia mali ya umma wao wenyewe.Tunafikiri na wewe nimmowapa wa hawo wanyonyaji wa CCM ndio maana unaleta hoja isiyokuwa maana kwa wa Tanzania.Wacha ulimbwikene wewe mfisadi.Lete za kuwatetea wananchi.
 
Nimepitia kwa Umakini Katiba ya Chadema tofauti na matarajio ya Chama chochote cha Siasa lazima kuweka msimamo wake hasa mlengwa wa Kiitikadi! Chadema haijaweka wazi kama ni Chama cha Kijamaa au ni Chama Cha Kibepari! Tofauti na CCM ambao wao Wanasema ni Chama cha Kijamaa japokuwa Ujamaa walisha Uweka kando! Vyama vingi duniani huonesha mlengo wake hasa kama ni kuamini Ubepari au Ujamaa! Hata marafiki zao wa Ujerumani na Uingereza wamebainisha mlengo wa Vyama vyao! Wanachama wa Chadema walio wengi hata hapa JF hawajui Itikadi ya Chama Chao(Inasikitisha sana)! Hakuna tofauti kati ya Chadema na Timu ya Simba wala Yanga kwani hawana Itikadi!
My Take: Chadema ijipambanua ina itikadi gani Ujamaa au Ubepari! Wanachadema jiulizeni Itikadi ya Chama chenu ni ipi?

Hata panya na mende pale kabatini waliisoma wakaelewa hata hawakuitafuna katiba ya chama kuwa Chadema ni mrengo wa kati usiofungamana na east/west. You Slave in the new era!
 
soma website ya chadema vyote utavikuta itikadi mrengo na mengine mengi tu, usiwe mvivu wa kutafuta knowledge soma mwenyewe tu ukishindwa ndo uombe msaada na si lazima kiongozi wa chama akujibu vitu viko wazi na unaweza kuvipata usipende kutafuniwa kila kitu utazoea vibaya
 
Zamani CCM walikiwa 'to the left' sijui sasa practically watasema wako upande gani. CHADEMA ni 'centre -left' Angalia manifesto yao 2010 (chadema manifesto)

Safi sana mkuu. Kama mtu ameuliza swali ajibiwe kama ulivyofanya. Hilo ndilo tendo la kiungwana kwa waungwana: Hoja dhidi ya hoja badala ya matusi. Kumbe CHADEMA ina itikadi lakini inaonekana wengine hawaijui ndio maana badala ya kujibu hoja wanaanza kutukana.
 
Back
Top Bottom