CHADEMA dkk 90 za mchezo zimeisha, hakuna ushindi wa mezani subirini 2015

Hawa jamaa hawana jipya, kinachotakiwa sasa ni kufanya usajili wa maana kwa ajili ya mechi ya 2015. Badala yake pesa za rukuku badala ya kuimarisha chama vijijini wao wanalipana posho za maandamano. Kwa taarifa yako posho ya siku ya maandamano ni Tshs 350,000/= , sasa huku si kuwanyonya wananchi na matumizi mabaya ya rasilimali
inakuusu nini wewe si ukamwambie Makamba na shangazi Seifu hamaD
 
huyu mwanzisha thread amesahau kwamba chadema ni chama cha siasa? na maandamano na mikutano inayoendelea sasa ni shughuli za kisiasa na ni jukumu la vyama vya siasa kutoa elimu na habari kwa umma kuhusu hali za kijamii, uchumi na siasa kama wanavyofanya cdm, pia mbali na hayo ni njia mojawapo ya kuongeza wanachama na kutafuta kuungwa mkono na watu wengi zaidi na ndio jukumu lao na ndio kazi ya ruzuku za chama kujipanua na kutoa elimu kama hujui. Sio kwa sababu ccm wamejibweteka tu hapo lumumba ukadhani ni wastaarabu na wao walitakiwa wazunguke coz ndio kazi ya vyama vya siasa. Hata m/kiti wa CCM jk wkt wa uchaguzi aliwambia wananchi wasichague vyama vinavyokuwa active wkt wa uchaguzi tu akirefer wapinzani sasa wamekua active wkt wote kinawauma! Mna nini jamani mko ka popo hamueleweki! Thats why m/kiti wa UWT mh sophia simba kazimia hizi harakati anatamani na CCM na waanze hebu pevuka mawazo acho ushallow minded
 
Jibuni hoja acheni jazba, ndio tatizo la wanachama/wapenzi/viongozi wa CHADEMA, kwenye hoja nyie mnaleta jazba, pevukeni mawazo !

Hiyo ni hoja umeleta??? hata kama ukiitoa nyumbani kwako hata watoto wako watanyamza na kujiondokea kwenda kupumzika kila mtu!
 
inakuusu nini wewe si ukamwambie Makamba na shangazi Seifu hamaD

Tumieni rasilimali mlizopewa na kwa umakini, sio kujibisha matumbo yenu kwa gharama za mlala hoi. Na ndio maana kila siku mnabuni maandamano ili mle posho wakuu, kweli wajinga wali wao
 
Wao walizalisha umeme na uliutumia wewe pia , au kwako hakuna umeme ? acha mawazo mgando na wivu wa kike


Subiri uone wewe Chadema wanazalisha maisha bora kwa kila mtanzania mabayo hata wewe utake usitake utayatumia na watoto wako! Think deep
 
Hiyo ni hoja umeleta??? hata kama ukiitoa nyumbani kwako hata watoto wako watanyamza na kujiondokea kwenda kupumzika kila mtu!

Kwa watu wenye fikra pevu ni hoja, ila kwa watu wenye fikra mgando kama ww si hoja !
 
Subiri uone wewe Chadema wanazalisha maisha bora kwa kila mtanzania mabayo hata wewe utake usitake utayatumia na watoto wako! Think deep

Hawana uwezo huo , kuota mchana . Hata Shibuda aliwaambia kuwa CHADEMA ni kikundi cha wachache wenye maslahi yao binafsi, na yeye ndio mbunge wenu
 
Katika kile ambacho viongozi wa CHADEMA wanahaha kukitafuta hata kwa gharama ya kuhatarisha maisha ya wananchi (mfano mauaji ya arusha) na maandamano mbali mbali ya visingizo kibao (mfano maandamano ya mwanza ) ambapo hakuna hata moja lenye mashiko ya hoja ili mradi tu watimize dhamira yao ya kutaka kushika dola ili hali watanzania tuliisha amua kwa ridhaa yetu kukipa chama na kiongozi anae faa kwenye uchaguzi uliopita wa Oktoba 2010.

Hayo yote tisa, kumi ni kuwa sie wananchi hatudanganyiki tena kwa viongozi uchwara wenye uchu wa madaraka, na wenye kuweka maslahi yao binafsi kuliko ya kitaifa. Kwa hiyo hilo wanalo litaka sie wananchi hatuko tayari, wasubiri tena mechi ijayo ya 2015. Hivi sasa mpira umeisha , na washindi wameisha patikana, ushindi wa mezani hakuna kama mlishindwa kuzitumia dkk 90 zenu sawa sawa

Nichangie hayo yaliyoko kwenye red. Sidhani kama umefatilia kwa makini hoja zao kwenye hii mikutano au pengine unaongea kiushabiki au haupo Tanzania kujionea hali kwa uhalisia, kwa kukusaidia hawa jamaa wanafanya maandamano kupinga Mfumuko wa bei, kupanda kwa gharama za maisha, sakata la Dowans ambalo kwa kiasi kikubwa limepelekea tatizo lililopo la umeme na mengineyo (fatilia kwa karibu hoja zo), kwa yote haya Rais amekuwa kimya pasipo kuzungumza lolote kama vile hakuna jambo lolote linalomgusa yeye kama kiongozi wa nchi badala yake kila mtu katika serikali yake anazungumza kile anachokifahamu (rejea baadhi ya mawaziri sakata la Dowans) imefikia wakati mwenyekiti wa kamati ya madini bungeni amekuwa kama msemaji wa serikali juu ya sakata la umeme lililopo na kwa taarifa yako leo ameitisha Public hearing pale Karimjee juu ya sakata hili, je hakuna viongozi husika kufanya hili? Kwa haya yote CDM wamempa Rais siku tisa kuzungumzia juu ya matatizo yanayowakabili hivi sasa vinginevyo wataona ameshindwa kuliongoza taifa hivyo kuitisha maandamano rasmi nchi nzima kumtaka ajiuzulu

kwenye red ya pili, ni kwamba inawezekana wewe binafsi na mimi ndio tuliamua kumchagua Rais kwa ridhaa yetu, lakini usiwasemee watanzania wote maana asilimia ya watu waliopiga kura haifiki hata nusu ya watanzania wote (soma ripoti ya wasimamizi kutoka nje ya nchi iliyotoka hivi karibuni) hivyo si wote waliridhia kumchagua kuwa rais, pia inasemwa kuwa hata mchakato uliotumika kumweka pale haukuwa halali (rejea matukio wakati wa uhesabuji wa kura uliofanywa na Tume ya uchaguzi), kwahiyo unapoongolea suala nyeti kama hili pendelea kutumia umoja badala ya wingi katika kauli zako, si hapa tu hata sehemu zingine.

Katika hiyo red ya tatu, kwa nilivyofuatilia kwa makini toka kuanza kwa maandamano yao sijasikia tamko lao lolote likisema wanataka kuchukua nchi, ama nia yao hiyo ya kutaka kujiuzulu kwa Rais ni kwa manufaa ya Chadema au maslahi yao binafsi bali wanazungumzia maslahi ya taifa kwa ujumla, haibagui dini, rangi wala kabila. Labda kwa kukufahamisha tu ni kuwa wameanza kama Chadema ila mwisho wake utakuwa ni taifa kwa ujumla.
 
Tumieni rasilimali mlizopewa na kwa umakini, sio kujibisha matumbo yenu kwa gharama za mlala hoi. Na ndio maana kila siku mnabuni maandamano ili mle posho wakuu, kweli wajinga wali wao
Nyinyi mmetumia rasilimali zipi mkuu! au unaongea kama brain yako haina ujinius wowote mkuu PUMBAA ZIMEJAA KAMA MAKAMBA!
CDM HAIKUHUSU ACHA WANACHADEMA WATUMIE PESA ZAO KAMA WANAVYOTAKA WENYEWE MKUU MBONA ZAKO NA MAKAMBA HATUJAINGILIA!
 
Nyinyi mmetumia rasilimali zipi mkuu! au unaongea kama brain yako haina ujinius wowote mkuu PUMBAA ZIMEJAA KAMA MAKAMBA!
CDM HAIKUHUSU ACHA WANACHADEMA WATUMIE PESA ZAO KAMA WANAVYOTAKA WENYEWE MKUU MBONA ZAKO NA MAKAMBA HATUJAINGILIA!

Isije kuwa hizo ndio zile na NSSF!
 
huyu mwanzisha thread amesahau kwamba chadema ni chama cha siasa? na maandamano na mikutano inayoendelea sasa ni shughuli za kisiasa na ni jukumu la vyama vya siasa kutoa elimu na habari kwa umma kuhusu hali za kijamii, uchumi na siasa kama wanavyofanya cdm, pia mbali na hayo ni njia mojawapo ya kuongeza wanachama na kutafuta kuungwa mkono na watu wengi zaidi na ndio jukumu lao na ndio kazi ya ruzuku za chama kujipanua na kutoa elimu kama hujui. Sio kwa sababu ccm wamejibweteka tu hapo lumumba ukadhani ni wastaarabu na wao walitakiwa wazunguke coz ndio kazi ya vyama vya siasa. Hata m/kiti wa CCM jk wkt wa uchaguzi aliwambia wananchi wasichague vyama vinavyokuwa active wkt wa uchaguzi tu akirefer wapinzani sasa wamekua active wkt wote kinawauma! Mna nini jamani mko ka popo hamueleweki! Thats why m/kiti wa UWT mh sophia simba kazimia hizi harakati anatamani na CCM na waanze hebu pevuka mawazo acho ushallow minded

Hakuna mwenye kukataa CHADEMA kufanya mikutano , hilo lajulikana ni shughuli za vyama vya siasa, tatizo lenu ni uroho wa madaraka mlio nao. Uchaguzi umeisha, na viongozi wamepatikana, sasa na nyie mnataka kwa wakati huu huu kushika dola , hilo litawezekana wapi ? acheni kuwa narrow minded !
 
Nyinyi mmetumia rasilimali zipi mkuu! au unaongea kama brain yako haina ujinius wowote mkuu PUMBAA ZIMEJAA KAMA MAKAMBA!
CDM HAIKUHUSU ACHA WANACHADEMA WATUMIE PESA ZAO KAMA WANAVYOTAKA WENYEWE MKUU MBONA ZAKO NA MAKAMBA HATUJAINGILIA!

Kwa hiyo na nyie ndio mmeamua kumnyonya mwananchi mlala ho ? kweli kila shetani na zama zake aisee, na hizi ni zama za CDM kuwanyonya na kuwalaghai wananchi
 
Kwa hiyo na nyie ndio mmeamua kumnyonya mwananchi mlala ho ? kweli kila shetani na zama zake aisee, na hizi ni zama za CDM kuwanyonya na kuwalaghai wananchi

Kikwette alivyoondoka Monduli chuo cha Jeshi kwa msukosuko!

Kipindi hicho mkuu wa chuo alikuwa Gideon Sayore, Kikwete alikuwa ni mmoja wakufunzi wa siasa chuoni hapo.
Sasa ilikuwa hivi,
Mzee Sayore alikuwa anafuga ng'ombewengi pamoja kufanya shughuli za kilimo kwawingi wakati huohuo akiwa mkuu wa chuo cha kijeshi Monduli.
Hivyo basi baada ya kuona ng'ombe wanatoa maziwamengi mno na mazao yametapakaa mashambani,. akaamua kuwa awe analiuzia jeshi mazao kama vile maharage na mahindi pamoja na maziwa na nyama kutoka kwenye mifugo yake.......na pesa anachukua yeye mwenye mazo.
Aliendelea kufanya hivyokwa kipindi kirefu tu.. ikiwa ni kama sehemu yake ya maisha....

Sasa bwana ,,kumbe Kikwette (JK) ilikuwa inamuuma sana sana, yaani mno! sasa haieleweki kama ilikuwa kweli ni kwa uzalendo ua wivu tu....akaandika barua kwa raisi kipindi hicho JK Nyerere.
Katika barua hiyo akaandika lawama nyiingi mno na majungu mengi sana dhidi ya Sayore, akimwita bepari, bwenyenye, mnyonyaji n.k huku akisema hafai kuwa mkuu wachuo hicho kwakuwa navunja miiko ya uongozi na mambo mengine meengi (si mnamjua JK anavyojua kupiga fitna!)....basi bwana, akamalizia mwisho kwakujiandika jina lake na sahihi yake huku akijiita mzalendo kamili barua ikapostiwa ikiwa imeadresiwa kwa rais wa nchi wakati huo!......

Mwalimu, aliipata barua ile aliifungua akaisomaaaa kisha akapiga hesabu zake....sijui aliwaza nini mzee yule, akaihifadhi ile barua ikaa sana ofini kwake bila kuchukua uamuzi wowote.
Siku moja alipokuja mkuu wa majeshi wakati huo "General Mtukula" (David Musuguli) ofisini kwa Mwalimu eaisi kipindi hicho, mwalimu akampa ile barua kutoka kwa Kikwete "akisema hayo ni maMbo yenu kayamalizeni hukohuko".

Basi bwana ile barua Mkuu wa majeshi alikaa nayo muda hivi kwenye makabrasha yakee...., sasa siku mija alikuja Mkuu wa chuo cha kijeshi Monduli(Sayore) Dar es salaam kufanya shughuli za kikazi akaenda hadi ofisini kwa Mkuu wa majeshi.

Baada ya shughuli kwisha na Sayore akiwa anajiandaa kwenda Monduli Mkuu wa majeshi alimwita, akampa ile barua ya Kikwette aliyomwandikia raisi!!....
Sayore akaisoomaaa we akashangaa mno!! na akafurra kwa hasira yule mmasai...., akuliza mwalimu kasemaje? akaambiwa mwalimu kasema yamalizeni wenyewe!!.... akasema naam, na akaondoka na ile barua hadi Monduli...

Alipofika tu yule mmasaai aliitisha kikao cha wakufunzi woote na wakuu wengine pale chuoni, wakati wanajikusanya kwenda kwenye chumba cha mkutano yeye aliamua kwenda kutoa copi ile barua ya Kikwete, kopi nyingi idadi sawa na wajumbe wa mkutano ule....
Balipoingia mkutanoni akawaona wakuu na wakufunzi wote wameketi wakimsubiri wajue alicho waitia,.. akaanza kwa kuwaliza..jamani kama kuna mtu ana matatizo, au anaona kuna jambo haliendi sawa anyooshe mkono na saemekinacho mkereketa......watu wote wakawa kimya huku wengine wakisema hamna mkuu akiwemo Kikwette!!!
Basi bwana, tumalizie mkasa huu wa mkwere...
Sayore akaanza kuwagawia zile nakala(copi) za ile barua ya kikwete kwenda kw a raisi akawagawia wooote inlcuding Kkwete!!! Huku yule mmasasi Sayoreakiwa amefura kwa hasira, macho mekunduuu! akagonga ngumi juu ya meza kwa hasira na kusema someni hiyo baru!! kisha akatoka na kusema anakuja muda si mrefu...

Hapo Kikwete akajua kifo chake kimefika, akikumbuka macho ya yuile mmasai! akatetemeka macho yakamtoka lip! kwa woga!.. na wenzie wakamwanzishia zogo mle ndani.......
Alichokifanya ni kuondoka harakapale kikaoni wenzie wakajua bado yupo chuoni, kumbe safari ya Dar ikawa imeanza...!! jamaa alitembea uchochoroni kwa muda mrefu sana huku akiogo kabisa kuingia barabara ya kuu...
Mashuhuda wanasema yule bwana akaja kupanda lift ya gari za vyama vya ushirika maeneo ya USA RIVER!! hakukumbuka kubeba mzigo wowote!! just imagine kutoka monduli hadi hapo jamaa aliteseka sana... lakini yeye hakujali, cha muhimi ilikuwa kusalimisha maisha yake......

Basi huo ndiyo ukawa mwishi wa JK monduli,........... hukurudi akaja Dar na kupangiwa kazi nyingine na chama...lakini alikuwa anamlaani sana Nyerere eti kwanini alimfanyia vile!! Hicho ndicho chanzo cha JK kumchikia mwalimu na kugoma katakata kumwita baba wa taifa hadileo! yeye humwita mzee nyrere tu au mwalimu baasi...na mara chache akiwa nje ya nchi humwita father of our nation, laikini ni pale napotaka kupigiwa makofi kwa nukuu za Mwalimu....

**Ndugu zangu hiki ni kisa cha ukweli kwa 100%, inawezakana uandishi wangu ukawa na upungufu, lakini niemekipata kutoka watu mbalimbali waliowahi kuwa karibu sana na mkasa huu...​
 
kwa hiyo na nyie ndio mmeamua kumnyonya mwananchi mlala ho ? Kweli kila shetani na zama zake aisee, na hizi ni zama za cdm kuwanyonya na kuwalaghai wananchi
ndo maana yake mkuu kwahiyo we acha tunyonye tuuu!
 
Re: Kikwette alivyoondoka Monduli chuo cha Jeshi kwa msukosuko!

Alipokuwa anaondoka ,alikutana na mwanajeshi mwenzie mfupi kuliko wote wakati huu wakimwita Pimbi wa Monduli Abruhaman Shimbo ,na kwa kuwa walikuwa marafiki kiasi kutokana na uislam wao JK aliamua kumueleza yote yaliyomkuta ndipo hapo shimbo akamuonea huruma sana na kumuandikia kinot mjomba wake aliyekuwa anakaa Tengeru ili amsaidie basi JK alifikia Tengeru kwa mjomba wake Shimbo na hapo akapumzika siku kadhaa yule mzee alimpa nauli na JK akarudi Bagamoyo moja kwa moja kabla hajapangiwa Lindi kwenda kufanya kazi za chama.Ndio maana JK hasemi kitu kwa Shimbo analipa fadhila

Kwa hiyo na nyie ndio mwamalizia za nssf ? kweli wajinga wali wao
 
Back
Top Bottom