CHADEMA chama bora mwaka 2008: Tujifunze toka kwao

Eric Ongara

Senior Member
Sep 19, 2006
165
8

Leo ikiwa ni siku ya mwisho wa mwaka sambamba na kumskuru muumba kwa majaliwa yake kwa mwaka ulio ukingoni ni vyema pia tukafanya mapitio ya mwaka mzima ili tuchukue akiba na kubeba yalio mazuri na kufanya jitihada za kuepuka makosa tunavyoelekea mwaka mpya unao karibia. Kwa muktadha huo kwenye anga za siasa napendekeza kwenu liliodhahiri kwamba Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) ndio Chama Bora kwa mwaka 2008.

Tutakubaliana kwamba CHADEMA ni Chama cha siasa kilichojadiliwa sana mwaka huu, kuna waliokikosoa, kitusi,wapo waliokisingizia na wapo walio kiunga Mkono. Waliioyafanya hayo wanatapakaa kwenye maeneo na kada mbalimbali iwe hapa JF, kwenye vyombo vya habari, kauli za wanachi wa kwaida, viongozi wa serekali, vyama vya upizani na hasa kile chama cha mafisadi. Watu wamefanya hivyo kwa miskumo mbalimbali inaweza kuwa kukipenda, kukikubali, kukichukia, kutokubaliana nacho, kukichukia au kukihofia lakini yote haya yanaweza kuwekwa kwenye kapu moja kwamba kazi yake INATAMBULIKA katika jamii ya watanzania.

Ili kujenga msingi mzuri katika kukitambua rasmi kama chama bora kwa mwaka 2008 ni vyema tukafanya mapitio ya jumla kwa muhtasiri mwenendo wa CHADEMA kabla na baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2005.
1.Ndio chama pekee cha upinzani ambacho kimeweza kuwa na awamu tatu za uongozi: Mtei, Makani na Sasa Mbowe na hivyo kuonyesha ukuaji wa demokrasia ndani ya chama

2.Ukuaji wake ni wa kitaasisi zaidi badala ya ukuaji kutokana na umaarufu wa mtu binafsi au mazingira ya kihistoria ya eneo husika tofauti na vyama vingine vya upinzani na hivyo kujenga misingi imara na hivyo kutoyumbishwa pale viongozi wake wanapo hama chama, tumeshuhudia Kaboro(alie kuwa makamu mwenyekiti) na Shaibu Akwilombe(aliekuwa naibu katibu mkuu) wakihama chama pasipo kulete mtikisiko wowote.

3.Ni chama amacho hakikukurupuka kusimamisha mgombea wa uraisi mwaka 95 na 2000, mkazo wake ulikuwa kujenga miundo ya kitaasisi yenye uwezo wa kuhimili mikiki ya kisiasa.

4.Kimejitambulisha zaidi kwa sera kwa kutoa mapendekezo mbalimbali amabayo hata hivyo yamekutana na CCM amacho kinanongozwa na watu wenye uwezo duni na nia mbaya, matokeo yake kushindwa kutumia utajiri wa fikra wa CHADEMA kwa maslahi ya taifa.

5.Leo kinatambuliwa kama chama cha kizazi kipya kilichosheheni wanasiasa mabingwa wa kizazi kipa kama Freema Mbowe, Wilboard Slaa, Zito Zuberi Kabwe, Halima Mdee, Tundu Lissu, John Myika na wengi wanaoendelea kuibuka.


Tuangalie baada ya 2005.
Baada ya uchaguzi mkuu pamoja na Kasumba kuwa vyama vya upinzani ni vyama vya uchaguzi, CHADEMA waliweza kufutulia mbali Kasumba hii kwa kuendelea kufanya uwekezaji mkubwa sana wa kisiasa kwa hatua zifutazo:

•Uamuzi wa aliekuwa mgombea wake wa nafasi ya Uraisi kuamua kwenda kupokea matokeo pale Diamod ulikuwa uwekezaji mzuri sana wa kisiasa kwa kujitofautisha na wagombea wenzake, an kujenga taswira mpya ya mapambazuko ya kisiasa Tanzania.

•Mwaka 2006 alifanya ziara nchi nzima kuwashukuru waliomuunga Mkono wakati wa uchaguzi pamoja na kueleza mikakati ya wanachama hapo badae na kuhakikishia umma kuwa yeye kwa pamoja na chama anachokiongoza watatimiza wajibu wao wa kisiasa katika kukiwajibisha Chama cha Mapinduzi kutekeleza ahadi zake na kuzingatia maslahi ya taifa katika uongozi wao kazi ambayo wameifanya na wanaendelea kuifanya vizuri sana.

•Uzinduzi wa Tuamini jipya: CHADEMA imewezea kujikarabati na kuundwa upya ili kukomaza miundo yake ya kitaasi katika katika kukabilana na changamoto mbalimbali za kisiasa. Katika uzinduzi wa tumaini jipya walitoa Bendera mpya yenye mvuto zaidi ya ile ya awali na kufanya marekebisho ya katiba katika kukipeleka CHADEMA katika kitovu cha mapambano ya kisiasa. Uzinduzi huu uliandaliwa vipindi maalum na kurushwa katika luninga na hivyo kuweza mfiko wa moja kwa moja.

•Ziara za utetezi wa rasilimali na kupinga ufisadi: Hapa walitumia vizuri sana mtaji wa kisisa baada ya Zito kusimamishwa bungeni kwa kuzunguka nchi zima na hata kuzaa azimio la songea lenye lengo la kutetea rasilimali na kuibukia msisimko wa aina yake katika jamii. Na huu ndio umakini wa chama cha siasa yaani uwezo wa kuona na kufanyia kazi vizuri fursa za kisiasa zinazojitokeza katika kujenga chama.

•Tamo la orodha ya mafisadi 11: Dr. Slaa na Lissu walitumia umakini mkubwa sana katika kuaandaa taamko zito sana liliojitosheleza sana lenye vilelezo vya namna nchi inavyotafunwa. Tamko hili limewaamsha wananchi katika namna ambayo haiwezi kuelezewa na kuendelea kuwa mwiba mkali sana unatishia uhai wa CCM!



Walioyafanya mwaka 2008 na hivyo kustahili kiwa chama Bora.
Hapo juu tumeansiha maelezo hayo ili kujenga msingi kuwa huu ni muendelezo wa misngi imara mabayo CHADEMA imejiwekea. Sasa tuangalie maeneo yaliovutia zaidi kwa mwaka unaoisha:

• Matamko mazito juu ya kuonyesha hali na mwenendo wa nchi kisiasa, kijamii na kiuchumi matamko ambayo mara kwa mara yamefanikiwa kuitingisha serekali na kuwaamsha wananchi na hivyo CHADEMA kutimiza wajibu wake kikamilifu kama chama cha upinzani kinapaswa kusimamia serekali ipasavyo. Bila kusahau kuendelea kuwa maaskari wa mstari wa mbele katika vita dhidi ya ufisadi

•Kujibu mashumbulizi dhidi yake kwa umakini na ufasa mkubwa mathalani hoja ya uchaga na matumizi ya helkopta zilitolewa ufafanuzi wa kina na msingi mzito na hivyo kufifisha hoja laini za washindani wake

•Umakini katika maswala nyeti. Tofauti na vyama vingine vya siasa CHADEMA haikikurupuka kurukia hoja za mahakama ya kadhi na sakata la OIC tofauti na wengine ambao taswira zao zimechuja kutokana na kutoa kauli ambazo zimesigana na maslahi ya makundi mbalimbali katika jamii.

•Kufanikiwa kushinda umeya na hatiame kuwa chama tawala Tarime, hii ji baada ya wilaya ya Tarime kugawanyawa mara mbili, Tarime na Rorya, CHADEMA wamefanikiwa kuongoza halmashauri inazoongoza sambamba na Karatu na Kigoma mjini(katika ubia na CCM).

•Kusimamisha kwa Chacha wangwe na Yaliojitokeza baada ya Kifo chake

Hapa CHADEMA wajipambanua kwa umahiri wake kwa mtazamo huu:
1.Walionyesha uwezo wa kufanya maamuzi magumu kwa kumsimamisha mmoja wa viongozi wake wakuu kutokana na kukiukaa taratibu na misingi ya chama. Kwa tafsiri pana huu ni ujasiri wa uongozi. Tumeona wapinzani wake CCM wakishindwa kufanya hivyo dhidi wa watuhumiwa wa ufisadi lakini CHADEMA walienda hatua moja mbele

2.Ukomavu wa kichama: wapo waliodhani kuwa sakata la wangwe kusimamiswa lingweza kusimbaratisha chama na hata kufikia hatua ya kufananisha na mgogoro wa NCCR mageuzi amabo ulikisambaratisha kabisa mnamo miaka ya tisini. Wanachosahau NCCR ilikuwa na ukuaji wa puto tafauti na CHADEMA iliyokuwa imekuwa kitaasisi. Ukuaji wa ghafla wa NCCR ulitokana watu maarufu kujiunga kwa wingi mda ule lakini hakukuwa na miundo thabiti ya kitaasisi kulelea na kukudumisha ukuaji ule, ndio maana ulipoibuka mgogoro ambao ni jambo la kawaida kwa taasisi yoyote ya kibinadamu hakukuwa na miundo au mfumo unaukubalika katika pande zote kutatua mgogoro ule iihali CHADEMA tayari imekuwa sana kitaasisi na hivyo kutoyumbishwa na migogoro. Kwa hulka za kibinadamu migogoro ipo, suala ni mifumo ya kuitatua na namna ya kuitatua. CCM wana migogoro mingi tu, ya NAPE, wabunge wa CCM na ngumi za UWT na wengine kufikia kutoa nguo za ndani lakini zipo jitihada mbaya za kuonyesha kuwa kuna migogoro upinzani pekee. Kwa namana walivyo kabili hili CHADEMA wanapaswa kupewa heko. Tunaweza kusema sasa zipo dalili njema kuwa kuna chama kingine imara kinachokuwa na kusukwa kila uchao pamoja na kukabiliana na mazingira magumu.

3.Hawakukurupuka kujibu kasfha zilizobuniwa na wapinzani wake hasa CCM, vyombo vya habari na badale viongozi wa CUF,NCCR na TLP, zilifanyika jitihada nyingi sana kupandikiza mbegu mbaya na chuki dhidi ya CHADEMA wakijenga hoja ya kukihusisha CHADEMA na viongozi wake wakuu kuwa wanahusika na kifo cha Wangwe!

Ilikuwa ni kama vile dunia nzima dhidi ya CHADEMA. Viongozi wa CHADEMA walikuwa watulivu na wakomavu sana, walitulia wakafanya maamuzi sahihi yakiwemo kuwasilisha malalamiko yao katika mamlaka sahihi na hatimae kuvuka katika kipindi kigumu.Kuweza kuvuka katika mtego uke mbaya, tuko tayari kumpenedekeza Freeman Mbowe kama kiongozi bora wa mwaka kwa namna alivyoongoza chama chake katika kipindi hiki kigumu.

•Ushindi wa Tarime: CCM inafanya jitihadi kujaribu kujenga hoja kuwa ule ni ushindi wa kawaida kwa kuwa CHADEMA imeshinda na kutetea jimbo lake lakini ukweli ni kuwa ushindi ule ni mkubwa na una maana kubwa katika mapambano ya kidemokrasia nchini Tanzania.

Ieleweke kuwa huwa na vigumu kuishinda CCM katika uchaguzi mdogo na pia rekodi zinaonyesha kuwa ni mara ya pili kihistoria baada ya Mrema Temeke. Lakini uzito wa Tarime umekuja wakati ambapo kulikuwa na jitihada nzito zimefanyika kukichafua na kukiweka katika mazingira magumu sambamba na CCM kuungana na vyama vyingine vya upinzani kukishambulia lakini wapi nguvu ya umma ikajidhihirisha, wakachukua jimbo dhidi ya CCM na "muungano" wa vyama vingine vya upinzani hasa DP na NNCR mageuzi. Taathira ya Tarime imekuwa kubwa mno katika medani za sisa Tanzania.

• Ubunifu: Operesheni sangara ni kielele cha ubunifu wa viongozi wa CHADEMA na ubingwa wao katika kutumia fursa za kisiasa zinazojitokeza. Kama ilivyokuwa kwenye ziara za utetezi wa rasilimali hapa waliamua kudumisha hamasa na kutumia fursa ya kufanya uwekezaji wa kisiasa kwa kubuni Operesheni sangara wakati ambapo vuguvugu la ushindi wa Tarime linatokota. Jina lenyewe lina mvuto wa aine yake. Wameweza kufanya ziara za unenezi zilizo amasha, sisimua na kulitikisa taifa kwa namna yake.

• Mikutano wa vyuo: CHADEMA imeendelea kuwa makini kwa kufanya mikutano mingi na wanavyuo mbalimbali mathalani, Arusha, Iringa, Mwanza, Dar es salaam na Morogoro,hii inazidi kuijengea hadhina kubwa ya vijana wa kileo wenye uwezo mzuri wa kitaalamu na hivyo kuimarisha “benki” yake ya rasilimali watu.



Kwa ujumala wamechangamsha sana siasa za TZ mwaka 2008 na kudumu katika ramani ya siasa mwaka mzima.Tunawapongeza sana viongozi wa CHADEMA ni matumaini yetu mtaendelea kuimarisha chama chenu na kujenga demokarsia Tanzania mwaka 2009.Hasa tukikumbuka kutakuwa na uchaguzi wa serekali za mitaa. Hakika: Hakuna kulala mpala kieleweke.
 
Last edited by a moderator:
Kibunango uwe unachukua muda kidogo na kusema mawazo yako kwa undani badala ya kuwa una crash tuuuuuuuuuuuuu na husemi la maana .
Yaani mtu mmoja anatoka huko alikotoka na kuja kusema Chadema chama bora,na vigezo vyake vya ajabu ajabu! Ni lazima nitamwona kuwa yupo ndotoni tu!
 
Kulingana na maelezo yenye ukweli ndani yake pamoja na sababu zilizoorodheshwa na mtoa mada nashawishika kuunga mkono hoja.. Ukweli ni kuwa CHADEMA ndicho chama pekee cha upinzani kinachokwenda na wakati na kinachokubali na kuhimili changamoto za kisiasa pamoja na kijamii.
Kwa ujumla hawa jamaa ni VICHWA.
 
Yaani mtu mmoja anatoka huko alikotoka na kuja kusema Chadema chama bora,na vigezo vyake vya ajabu ajabu! Ni lazima nitamwona kuwa yupo ndotoni tu!

Vigezo vya ajabu ajabu?Vilivyo bora ni vipi ili itusaidie kutoafikiana na Eric?Ni muhimu kutambua Chadema (and other opposition parties) ilizaliwa lini as compared to CCM which has been around for ages.And it seems as if the older CCM grows,the more self-destruct it becomes.

Hoja hupanguliwa kwa hoja.Frankly speaking,Chadema wamefanya kazi nzuri 2008 hasa katika kufichua ufisadi.Mazuri husahaulika mabaya kuliko mema lakini kwa wenye uchungu na nchi yetu tunakumbuka namna chama hicho kilivyoshikia bango ishu ya EPA,RIchmond,Buzwagi,etc na matunda yanaanza kuonekana japo kwa kasi isiyoridhisha sana.However,uzembe wao huko Mbeya vijijini umeniacha nikiwa very disappointed.Call it finishing a year with a wrong note.But that would not in itself tarnish rekodi nzuri waliyoiweka mwaka jana.
 
Mimi si mwananchama wa CHADEMA lakini ukivitathmini vyama vyote vya siasa Tanzania kwa mwaka uliokwisha wa 2008 basi CHADEMA imeweza kugusa nyoyo za Watanzania walio wengi katika vita dhidi ya mafisadi wa EPA, mikataba ya uchimbaji wa madini, uuzwaji wa kiholela wa nyumba za serikali, kasheshe ya Richmond/Dowans, kasheshe ya Kiwira n.k.

Pamoja na juhudi za CCM kutaka kuonyesha kwamba CHADEMA ni chama cha Wachaga, kushinda kwao katika uchaguzi uliokuwa na ushindani wa hali ya juu Tarime, kufuatia kifo cha Mbunge Wangwe inaelekea juhudi za CCM za kuonyesha kwamba CHADEMA ni chama cha kikabila zimepiga chini. Mbeya vijijini pia kulikuwa na kila dalili za kunyakua kiti hicho, I hope rufaa yenu itakubaliwa ili mshiriki katika uchaguzi huo na kupata ushindi mwingine.

Hongereni sana CHADEMA msikate tamaa katika kuikomboa Tanzania mikononi mwa mafisadi, kuhakikisha rasilimali za Tanzania zinawanufaisha Watanzania pia na Tanzania hakuna yeyote yule anayepaswa kuwa juu ya sheria za nchi. Kama kafanya madudu ya kuifisadi nchi yetu basi ni lazima afikishwe kwa pilato akajibu tuhuma dhidi yake.
 


•Umakini katika maswala nyeti. Tofauti na vyama vingine vya siasa CHADEMA haikikurupuka kurukia hoja za mahakama ya kadhi na sakata la OIC tofauti na wengine ambao taswira zao zimechuja kutokana na kutoa kauli ambazo zimesigana na maslahi ya makundi mbalimbali katika jamii.

.
"If you are neutral in situations of injustice, you have chosen the side of the oppressor. If an elephant has its foot on the tail of a mouse and you say that you are neutral, the mouse will not appreciate your neutrality".... Desmond Tutu
kwa mtaji huu Chadema walishajichagulia Upande wa Oppressor...!!!
 
Katika mabandiko yote ya Chadema ya mwaka 2008... Bandiko hili linashika mkia...
 
Kila mtu ana haki ya kutoa maoni yake. Aliyesema CHADEMA ni chama bora 2008 ana haki ya kufanya hivyo. Anayetaka kutofautiana naye ana haki ya kufanya hivyo vile vile, ila aache ad hominem attacks. (These are body blows. Yaani kumshambulia mtu badala ya kushambulia hoja yake).

Mimi si mwanachama wa chama chochote Tanzania (or anywhere else for that matter). Lakini ningeambiwa leo ni lazima nijiunge na chama kimoja, basi ingekuwa CHADEMA.

Vita vya ufisadi viliongozwa na viongozi wa CHADEMA, hasa Dr. Slaa na Zitto. Vile vile, Dr Slaa alionyesha uwezo mkubwa wa kupambana na mahasimu wake walipotaka kumwondoa Ubunge kwa kupitia mahakama. He is a great leader. CHADEMA has this particularly attractive leader as one of its many assets.

Kwani kuna chama gani kinaweza kikaonekana kilikuwa Bora zaidi ya CHADEMA kwa kipindi hicho cha 2008?
 
- JF bwana kila tunapojaribu kuwa kwenye line na ishus za taifa, then yanakuja maneno ya Chadema kuwa bora, huku wamesahau kuwa sheria ndogo tu inayosema mgombea ubunge anatakiwa kuapishwa kwa hakimu, mgombea wao anaenda kujiapisha mwenyewe, so much kwa chama bora!

- Vyama vyote vya siasa nchini vimefanya kazi nzuri kwa taifa, sasa ni kuendeleza mshikamano wa kusimamia hoja nzito kitaifa bila kujali vyama na kukubaliana kutokubaliana kwenye hoja zingine, lakini ya ubora kwa chama kilichoshindwa kupata hata kura 15% nationwide kwenye uchaguzi wa rais, pamoja na kuburuza helikopta kila kona ya taifa letu, ni matusi makubwa sana kwenye wengine tusiokuwa wanachama wa Chadema hapa JF, it is about time sasa wakaondoa ukabila kwanza huko Chadema ili waweze kua current na sheria za taifa kwa vyama vya siasa nchini, hatupendi hii mijadala ya yanga na simba lakini mnatulzimisha wenyewe, tunakubali kuwa mko wengi sana humu JF, lakini it does not mean anything kihoja, maana ni uzito wa hoja na sio nani maarufu kati ya yanga na simba, au CCM na Chadema,

- Nia na madhumuni ya chama chochote cha siasa duniani ni kushinda uchaguzi mkuu wa taifa until then kujiita bora na maarufu ni kujidanganya na kuwadanganya wananchi bure, fanyeniu kazi ya wananchi ndio mtalipwa kwenye uchaguzi lakini sio kujipigia debe bila matokeo, kwenye hili ninaomba kukubali kutokubaliana, ila pole pole tusiburuzane kama magari mabovu!

Thanxs!
 
Field Marshall Es,
Mkuu bado hujanipa Ubora wa chama CCM, hayo ya ushindi wa Uchaguzi yamepita miaka mitatu au umesahau hoja inasema mwaka 2008..
CCM kama chama kusema kweli hakikufanya kitu zaidi ya watu binafsi kusimama nje ya matakwa ya chama..
Binafsi nampongeza Kikwete kafanya mengi mazuri ambayo sikutegemea kabisa ikiwa ni pamoja na kurudisha haki ya waandishi, kupigana na Ufisadi akiungwa mkono na kina Mwakyembe, Mama Kilango, Sitta na baadhi ya wabunge na wastaafu ambao wameweza kusimama nje ya chama kwa maslahi ya Taifa... Pamoja na yote haya,Chadema kama chama wamejitahidi sana kuonyesha Ubora wa chama mwaka huu..
Hizo habari za mbunge wa Mbeya vijijini kujaza form jambo la kawaida kuliko ile ya mama meghji waziri mzima wa Fedha kuingizwa mkenge na Balali akapitisha malipo bila hata supporting document, kuna ujuha gani zaidi ya huo..Kisha basi huko vijijini hakimu wenyewe wangapi basi!.. unaweza kuta hakimu ni mmoja au wawili wakiondoka basi kila kiitu kimelala..

Mkuu, nadhani hoja hapa ni chama sio watu binafsi na tukianza kuweka list za watu walioboronga sidhani kama ukumbi huu utatosha..
 
Mkuu bado hujanipa Ubora wa chama CCM, hayo ya ushindi wa Uchaguzi yamepita miaka mitatu au umesahau hoja inasema mwaka 2008..
CCM kama chama kusema kweli hakikufanya kitu zaidi ya watu binafsi kusimama nje ya matakwa ya chama..

- Ni kama vile ambavyo sijaona sababu ya huu ubora wa Chadema unaosemwa hapa, ubora wa chama cha siasa ni kwenye kura za uchaguzi mkuu kwanza, mara ya mwisho uchaguzi wa taifa ulipofanyika CCM ilishinda kwa miaka mitano, sasa tupo kwenye wa tatu na CCM imekuwa ikishinda for the last 47 years, huo ndio ubora wa chama cha siasa.

- Kama kuna ubora wa the last three years, tutauona kwenye uchaguzi wa 2010, kwenye uchaguzi uliopita ni CUF ndio walioshika namba mbili sio Chadema, CCM ndio chama tawala kilichochaguliwa na wananchi wengi wa Tanzania for the last 47 years, we can talk kuhusu viongozxi wachache ndani ya chama chochote cha siasa bongo, lakini as far as CCM so far hao viongozi wachache hawajaathiri mtizamo mzima wa chama,

- Ukweli ni kwamba mijadala ya namna hii ndani ya hii forum ni very low, lakini hatuna njia ila kujibu tu, ingawa ni very low kwa taifa!
 
Wananchi ndio wataamua chama kipi ni bora kupitia kwenye sanduku la kura.
 
Kuna credits wanastahili tuwape kwa kazi nzuri ktk maeneo fulani .Lkn je hili linakifanya kuwa chama bora 2008?
Kwa haraka haraka mapungufu niliyoyaona na kwangu ni makubwa:
1.Uongozi wa juu hawakubali kukosolewa na viongozi wenzao eg Marehemu Chacha vs Viongozi wenzake.
2.Kuna ukiukwaji wa protocol ktk usemaji wa chama kuna wakati kila kiongozi anasema kwa niaba ya chama na kupelekea mgongano kauli.
3.Uchaguzi wa wabunge wa kuteuliwa ushirikishe wanachama wote na hizo nafasi watu wasigombee kwa kupigiwa kura ndani ya chama ktk vikao vya juu na si kama sasa kwa uteuzi unavyofanywa na kikundi cha watu,Hili sina hakika katiba yao inasema nini na kama ndiyo katiba inavyosema basi nitaomba wanachadema mfanyie marekebisho katiba ili kutoa wigo wa demokrasia zaidi ktk kuwapata wabunge wa kuteuliwa ili kusitokee manung'uniko ya ubinafsi na upendeleo ktk uchaguzi kama ilivyowahi tokea awali.
4.washirikisheni wanachama kupitia vikao halali ktk maamuzi yanayohusu mikopo ,mapato na matumizi yake kama vile utumiaji wa helicopter wkt wa chaguzi ili kuepuka kuwabebesha mzigo wanachama wa kulipa deni bila ya kuwashirikisha ktk mchakato mzima wa kukopa na matumizi hapo awali na kuja kuwashirikisha ktk kulipa deni tu.
5.Inapotokea kiongozi wa juu anakikopesha chama wanachama washirikishwe na wakubali kukopeshwa na wanapokubali kiongozi aliyekopesha asiwe muamuzi mkuu wa utumiaji wa kile alichokikopesha ili kuwe na uhakiki na kuepusha wanachama kulipa kile ambacho wameambiwa kimekopeshwa chama na kutumiwa bila ya uhakiki wa hali juu na mkopeshaji huyo huyo ambaye bado ni kiongozi hapa kuna conflict of interest hasa inapotokea mkopeshaji ndiyo huyo huyo mtumiaji au mwenye mamlaka ya kuidhinisha utumiaji.
6.Kwani uongozi wa juu unaamua wao pekee yao kutoungana na vyama vingine upinzani kama walivyokubaliana awali ,kwanini wasirikishwe wanachama wote ktk ishu kama hii ili kuweka ushirikishwaji wa wananchama ktk maamuzi makubwa kama haya.
 
Nawapa Chadema kuwa ni kituko cha kufunga mwaka!. Ikiwa hata kujaza fomu za ubunge mgogoro then mnatuambia chama bora!

Kweli ukipenda pengo huita mwanya!
 
Back
Top Bottom