Wambandwa
JF-Expert Member
- Dec 3, 2006
- 2,249
- 830
Wanabodi..
Mwenendo wa kisiasa, kati ya watani wa jadi CCM na Chedema sasa umeanza kuzua mijadala ndani ya jamii.
Wananchi wanahoji iko wapi kasi na upepo wa mabadiliko ilikuwa nao Chadema mwaka 2010 na mwaka jana ilikoyeyukia.
Huku CCM kilichokuwa kimeanza kudorora sasa kikionekana kupaa zaidi kuliko ilivyotarajiwa na wengi.
Mwamko wa Chadema ulianza kushika kasi mara baada ya Slaa, kuteuliwa kugombea Urais, mwamko huo uliendelea hata baada ya uchaguzi, na hasa baada ya chama hicho kuamua kufanya siasa zake kwa njia ya maandamo mikoa ya Kanda ya Ziwa hadi Nyanda za Juu Kusini.
Wadadisi wa mambo ya kisiasa wameanza kuhoji ni wapi kasi hiyo imeyeyeka ghafla na kukipa nafasi tena CCM kuanza kutamba katika maeneo mbali mbali nchini.
Hali hiyo ya kuanza kudorora kwa Chadema imelezwa pia kukikumba chama cha CUF kupoteza mvuto.
Chadema inatakiwa ibadili sera zake na falsafa mpya za kuendelea kuwashawishi Watanzania.
We naona umelishwa limbwata na ccm, hauhitaji akili nyiingi kuona mabo gani mengi CDM kama chma makini kimefanya. Kumbuka mwaka jana wabunge wa posho wa chama cha magamba walipitisha kwa ushabiki mswada wa kutafuta maoni ya wananchi kuhusu katiba mpya ila CDM waligoma na kutoka nje.
Kwa busara zao ikabidi wamtafute rais na kumweka chini, nasema kumweka chini na kumpa darasa la ni nini katiba tunayotaka. Nafikiri utakuwa unajua ni siku ngapi CDM ilikutana na rais. Mswada uliokuwa tayari umesainiwa na kuwa sheria ilibidi urudishwe bungeni na kufanyiwa marekebisho makubwa kama Chadema walivyotaka - ukiondoa kile kipengele ambacho yule mama mnafiki alishupalia na kikapata support kama kaw ya wabunge wapenda posho wa CCM.
Sasa wewe king'asti wa FF unapayuka nini? Tumia akili kidogo au unataka kuwa kama mdogo wako yule aliyemliza form four pale Feza?