CHADEMA & CCM tunahitaji majibu: Tanzania inahitaji Mtawala au Kiongozi?

Profesa

JF-Expert Member
Oct 28, 2010
905
624
Kwa hali ilivyo sasa na haya tunayojifunza katika siasa za leo, natamani kuona mtu atakaenichambulia hizi dhana mbili na kutuambia kuhusiana na Raisi tunaemtaka kwa sasa.

Nataka kuona dhana ya Utawala Bora na Uongozi Bora, tofauti yake ni nini? Misingi ya kila moja wapo ni nini? Na je ni lipi kati ya hayo tunayahitaji? Je Ifikapo 2015 na vigezo hivi vitakuwa na umuhimu wowote katika kuamua nani au chama cha kukipigia kura ?Je, Bila vigezo hivi, tukibadili chama, kutakuwa na jipya?

Chama peke yake kinaweza kubadili hali ya bmambo, bila vigezo hivyo hapo juu? Kama ndiyo, ni vitu gani vinaweza kuleta ushawishi wa mageuzi bila kutegemea vigezo hivyo ninavyoviulizia hapo juu?
 
kwanini umeelemea vyama viwili vya siasa na sio vyama vingine vya siasa je wao hawana majibu ya maswali yako? na je hata wakikikujibu majibu yao utayachukulia kama ni ya CDM au CCM maana inaonesha unawauliza CCM na CDM wakati kuna vyama vingi tu hapa Bongo..
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom