Chadema: Bila kuondoa watu hawa cdm itakuwa kama nccr ya mrema na tlp ya mrema

MBURE JASHA

JF-Expert Member
May 7, 2011
200
46
wanajamvi wote! salaam sana.
CDM ni kimeshaonyesha kuwa ni Chama Mbadala na makini. Ukweli unabaki pale pale. Kinatawala nchi hii kwa mlango wa Nyuma. Vichwa kama Slaa, Mbowe Zitto na wengine muhimu kashakshi zao ndani ya Bunge na Nje ya Bunge na mwenendo wa serikali kwa sasa unaburuzwa na kashkashi za CDM. lakini kuna shida moja naiona kwa CDM ni vyema tuiweke wazi . Siku ya jana nilikuwa naangalia Bunge kuna Mbunge mmoja wa Chadema kuitoka Zanzibar alinichefua kinoma
1. Nilianza kumuona tangu saa 11.00 jioni akifanya mzaha wa kulichekesha Bunge kwa michango yake isiyo na Mashiko, baadae saa mbili akaondoa shilingi na kuunga hoja mkono. Hivi alifundwa huyu ndo akaenda Mjengoni. Lakini kwa sababu najua kuwa Mbunge kabla ya kuingia ukumbini anakuwa na taarifa za kutosha kuhusu shughuli za kikao cha siku hiyo ni vyema CDM mkafanya kikao na wabunge wenu asubuhi kabla ya kuingia ukumbini (morning Pray) ili ku avoid utumbo kama wa Mariam Msabaha.
2. Shibuda nina wasiwasi ametumwa na CCM kuwavuruga. Naamini Mkoa wa shinyanga wote hata watu wakaamshwa saa sita usiku leo watachagua Chama mbadala sio CCM. Mbona kwa Johna Cheyo hawabadiliki mwenye chama ambacho yeye ndio kila kitu. Kama vipi tukienda Igunga kwenye kampeni wakati huo huo tunapiga kampeni kwa Shibuda
 
Aondoke Mbowe na Edwin Mtei(baba mkwe wa freeman Mbowe) ili chama kipate sura ya kitaifa na sio chama cha kifamilia zaidi!
 
Ha ha ha haaaaa hii imetulia sana mkuu !

Mods Tunaomba ipigwe marufuku mwanajamvi kutumia picha halisi ya mwanajamvi mwenzie.

Please take this seriously. Msisubiri mpaka mimi nitumie picha ya maxence Mello kama avater yangu ndio mu react?

Huyu genius brain anatumia picha ya Mwanajamvi mwenzetu Dr. Slaa huku akiandika utumbo mwingi lakini mpo kimya Tu.
 
Aondoke Mbowe na Edwin Mtei(baba mkwe wa freeman Mbowe) ili chama kipate sura ya kitaifa na sio chama cha kifamilia zaidi!

Msipojibiwa mnaota vichwa.
Wakiondoka itakuwaje? nafurahi kwani sasa mnawafahamu mwaka 1992 mlikuwa mnaona wanacheza kibisa. Ila baada ya kuwawewesesha hamsahau majina yao. Mtei atakumbukwa daima katika siasa za Tanzania. kwanza yeye hakuwa mroho wa madaraka aling'atuka mapema kuliko hata Baba wa Taifa. Mbowe ni mwiba mkali sana kwa CCM, najua wengi mnamwota usiku. Mmetuma mamluki ndani ya CDM wanachemsha. kile ni kisiki cha mpingo.

Subiria mzee wa anga anatua Igunga, siku 30, dakika 90. Tunachukua jimbo tunaanza kwa kasi sana.
Yeyote anayemchukia Mbowe alegee, na ashindwe kabisa.
Mbowe ni chadema na chadema ni Mbowe.
 
Safi kweli Chama Cha Demokrasia na Maendeleo....Mbowe mwenyekiti wa maisha

No spinning zone.
Wapi nimesema wa Maisha. Chadema ina demokrasia ya hali ya juu. Uchaguzi ukifika tutachagua Mwenyekiti na kama Mbowe atagombea na Wenzake wakapita poa na kama ataonekana anafaa ataendelea. Ila safari hii tutachuja sana. Screening and vetting vitakuwa vya hali ya juu. Tunahitaji mwenyekiti mwenye ngozi ngumu kama Mbowe. Chama makini kwa watu makini, kwa mambo makini wakati makini na maamuzi makini. Chini ya viongozi shupavu na makini.
 
We Marwa vipi, unajua hata mbuyu ulipokuwa size ya mchicha ulihitaji uangalizi. Hawa ndiyo wazee walioanzisha mawazo na vitendo ambavyo kwa sasa tunaanza kuona dalili za 'intention' yao. Hivi uanzishaji wa kitu kama chama si lazima uanze na mtu au watu wachache ambao sio rahisi kutoka nchi nzima, sasa kuna ubaya gani Mzee Mtei kutokea Moshi/Arusha!!?
Aondoke Mbowe na Edwin Mtei(baba mkwe wa freeman Mbowe) ili chama kipate sura ya kitaifa na sio chama cha kifamilia zaidi!
 
Back
Top Bottom