CHADEMA kimezidi kujikaanga na kupoteza mvuto miongoni mwa wananchi tulio makini katika siasa za TZ. Hiki chama kipo mstari wa mbele kupingamana na mamlaka za nchi. Hiki chama kimejingengea umaarufu siku za karibuni kuwa vinara wa VURUGU kila kunapokuwa na mikusanyiko yao.
Hizi ni dalili mbaya kwa chama cha siasa chenye nia ya kushika dola, pia ni ishara tosha ya kutokuwa na uongozi wa kitaasisi ndani ya chama. CHADEMA imedhihirika ni genge la wapiga porojo kupitia majukwaa ya siasa wakiwa ni vinara vya kuchochea misuguano miongoni mwa wananchi wakiwa na lengo la KUHAKIKISHA NCHI haitawaliki!
Hitimisho wananchi tukae chonjo na CHADEMA kwa vile hawana nia nzuri na nchi yetu
Ni wewe pekee ndiye mwenye nia nzuri na nchi yetu (Mafisadi). Endelea kutumia tumbo kufikiri.