Chadema Baada ya Uchaguzi 2015--Great Thinkers Only!

hivi tupambane na watu wa std 7 na failure wa 4m four ,nisawana kukimbizana na kichaa
wewe kweli hamnazo unajua shule ya viongozi wako wa CDM. Hivi Mbowe ana professional gani vile? sio Disco Jocker a.k.a DJ kweli?
 
Ngoja tu nitoe mfano mmoja ungonvi wa ndani ya cham wakati chama bado kichanga.
- tuone mfano kwao vilevile chama bado ni kichanga kuwa na ugonvi kunafanya makundi na yanapelekea milango ya kuvunjika chama.

Mfano mwingine ni kuhusu oil chafu. Wale walio temwa kutoka vyama vingine wanachukuliwa moja kwa moja tu ndani ya chadema. Mfano Shibuda, Marando nk. Baadaye watu hawa wanaterekezwa na kupigwa vijembe ndani ya chama na wanakumbuka kule walikotoka na baadaye wanageuka kuwa spy ndani ya chama. Hii inakifanya chama kuwa na makundi yasiyo ya lazima.

Nadhani hii inatosha kwa sasa.
G


Hahaha...sawa mkuu, ila nina wasiwasi na ushauri wako kama ni sincere, yaani

- Sasa mkuu mbona hutoi ushauri huu MZURI kule kule CCM ambako umesema mambo ni shwari, Kwani tunajua yanayoendelea huko.

Personally sidhani kama ni vibaya mtu kuhama toka chama kimoja kwenda kingine, na nadhani dhana hii ndiyo inayotusumbua watanzania...kudhani kwa kuwa chama ulichojiunga nacho ukikihama ni DHAMBI kubwa, hata kama hicho chama kimepoteza mwelekeo na sababu zilizomvuta mtu huyo huyo hapo mwanzoni.
 
wewe kweli hamnazo unajua shule ya viongozi wako wa CDM. Hivi Mbowe ana professional gani vile? sio Disco Jocker a.k.a DJ kweli?
na huyo ****** mcheza rede na sebene uliza pale udsm alitoka na nini
 
G


Hahaha...sawa mkuu, ila nina wasiwasi na ushauri wako kama ni sincere, yaani

- Sasa mkuu mbona hutoi ushauri huu MZURI kule kule CCM ambako umesema mambo ni shwari, Kwani tunajua yanayoendelea huko.

Personally sidhani kama ni vibaya mtu kuhama toka chama kimoja kwenda kingine, na nadhani dhana hii ndiyo inayotusumbua watanzania...kudhani kwa kuwa chama ulichojiunga nacho ukikihama ni DHAMBI kubwa, hata kama hicho chama kimepoteza mwelekeo na sababu zilizomvuta mtu huyo huyo hapo mwanzoni.

Hii umeisahau Baadaye watu hawa wanaterekezwa na kupigwa vijembe ndani ya chama na wanakumbuka kule walikotoka na baadaye wanageuka kuwa spy ndani ya chama. Hii inakifanya chama kuwa na makundi yasiyo ya lazima.
 
Hii umeisahau Baadaye watu hawa wanaterekezwa na kupigwa vijembe ndani ya chama na wanakumbuka kule walikotoka na baadaye wanageuka kuwa spy ndani ya chama. Hii inakifanya chama kuwa na makundi yasiyo ya lazima.

Isnt that the same thing that happens in CCM, to refresh your memory, the saga abt uchaguzi wa majina DODOMA hivi juzi.
 
Pigeni kelele tu lakini CCM iko juu siku zote hakuna chama kinachoweza kuitoa kwa sasa labda baada ya miaka 30 ijayo.
Mtaimba nyimbo zote eti m4c eti mchaka mchaka mpaka ikulu, eti sikui sangara eti sijui nini.
Hizo ni nyimbo tu viongozi wenu wanajua hawataki kuwadisapoint kwa sasa.



Duh mwenzetu Annael una moyo wa aina yake aisee!!!!!! kweli tumeumbwa tofauti sana na hata tofauti zetu zinatofautiana sana
 
Isnt that the same thing that happens in CCM, to refresh your memory, the saga abt uchaguzi wa majina DODOMA hivi juzi.
Kumbuka Cdm bado chama kichanga ndio kinatambaa, bado hakuja simama mpaka kuja kutembea kitakuwa kimemeguka meguka vipande!
 
Ukae ukijua kwamba ni aibu kubwa sana kusema "CCM INAJIPANGA". CCM Imekuwa madarakani kwa kipindi cha miaka hamsini, inategemewa kuwa tayari kwa uchaguzi hata kesho. Huo ukweli tu kwamba CCM inalazima kujipanga kama mnavyosema wenyewe ni ushahidi kwamba CCM iko kwenye wakati mbaya sana katika historia ya uwapo wake.

Mkae mkijua kwamba, hizo kelele zenu za kujipanga sio ishara za kuitishia CHADEMA, bali mnajivua nguo, mnachokifanya ni sawa sawa na mzee wa miaka 60 kumuambia kijana wa miaka 30 kwamba amejiandaa kumkabili kwenye mjadala wa kutatua tatizo la kifamilia.

Good example kamanda.......... CCM ni mzee wa miaka 51 sasa na CHADEMA ni kijana wa miaka 20 tu. Sasa mzee anajipanga kupambana na mtoto/mjukuu na hii ninashangaa hata kikwete huwa anasema hivi hivi hawa kazi yao kwisha. SI AJABU WANGELIANZISHA LEO PALE KILOMBERO(Arusha) KWENYE UVAMIZI WA WAMACHINGA KAZI YAO INGEKUWA IMEISHA au angalau safari ingekuwa inazidi kusonga maana huku tumewachoka mno na wao wanajua kabisa
 
ccm ikishinda 2015 nitakuwa disappointed sana na wananchi,.cdm ikishinda itabidi iende extra mile kuibadilisha hii nchi maana imeharibiwa vya kutosha

hakuna chama cha upinzani kilichojipambanua kuwa ni cha kitaifa hadi sasa.vyote vina elements za ubaguzi.
 
Iwapo Chadema itashindwa uchaguzi Mkuu 2015 maisha yataendela kama kawaida,hakuna kiongozi au Mwanachama yeyote wa Chama atakaye chukua hatua za kujiondoa uhai, Chadema tumeshakubalika na kuaminika kwamba tunaweza kusogeza nchi yetu hapa ilipo na kuipeleka mbele,nilifanya research yangu binafsi hapa Arusha,niliongea na watu 47 kwa week moja na kutaka kujua uwezo wao wa kuelewa nini maana ya Serikali na uongozi wake,niligundua watanzania wengi sasa hivi wanaelewa maana ya Serikali na wajibu wa serikali kwa wananchi wake,swali la mwisho nililowauliza utachagua chama gani iwapo uchaguzi mkuu utaitishwa leo,watu 45 kati ya 47 walisema watachagua chadema,2 walisema hawajui,hakuna hata mmoja aliyesema atachagua ccm.

Hii inaonyesha wazi ni jinsi gani Chadema ilivyofanya kazi kubwa ya kuwaelimisha watanzania kujua haki zao na uwajibikaji wa serikali yao kwa ujumla Kama mwanachama wa kawaida wa Chadema nimeona nitoe maoni yangu hapa JF kwa kuwa viongozi wa Chama na wapenda mabadiliko wenzangu mpo hapa
Nisingependa kusubiri 2015 kuona matokeo yakitangazwa na tume ya uchaguzi ambayo ipo chini ya ccm na kuitangazia ushindi ccm,nini kifanyike ili kwa vyovyote vile uchaguzi 2015 tuwe na uhakika 100% tutaondoka na ushindi wa kishindo?

Chadema ilikuja na kelele za ufisadi na wizi wa raslmali za taifa letu,kelele hizo zilifanya kazi kubwa ya kuwaamsha watanzania waliokuwa wamelala usingizi mzito na kuwafanya kuwa na hasira kali dhidi ya serikali ya ccm, tunakoelekea hizi kelele zitakosa ile nguvu yake ya asili na kubakia kama kelele za kawaida kwa sababu watanzania ni watu wa kusahau haraka na pia kwa jinsi maisha ya mtanzania yalivyo itakuwa ngumu sana kukumbuka yote haya,nini cha kufanya ili hizi kelele zibaki na nguvu yake mpaka november 2015?

Kuna haja ya Chadema kusogea another level???

yes ipo haja sasa kwa sababu tayari Chadema imeshakubalika nchi nzima,na kelele zote za ufisadi na wizi zimesikika kwa wenye nchi yao,
je kuna haja ya kuendelea kupiga kelele za ufisadi tena??jibu ni noo!
nasema hivyo kwa sababu ngoma ikilia sana mwisho hupasuka,Chama kwenda another level ni kuchukua hatua na kusonga mbele kuangalia jinsi ya kushawishi wapiga kura wakichague. Chadema inatakiwa kupunguza kelele za ufisadi kwa sababu moja tu!CCM inajipanga upya,nani anajua labda watakuja na safu mpya isiyoshutumiwa??

kama ikiwa hivyo kelele za chadema zitaenda wapi??we need to go another level now! Chadema ikianza sasa hivi kupigia kelele kazi na mabadiliko watakayofanya kwa watanzania,na kuwafundisha watanzania kuhudhuria mikutano yao na kalamu na daftari ili waandike watakachofanya watakapoingia madarakani itakuwa ni another level!

watanzania wakianza kusikiliza na kuandika nini kitafanywa na serikali na sio kunyanyua vidole viwili juu itakuwa ni hatua kubwa kuelekea ukombozi, wingi wa watu kwenye mikutano sio wingi wa kura,kunyanyua vidole viwili juu kama tulivyozoea sio wingi wa kura, Chadema hakuna njia mmbadala zaidi ya kuanza kueleza sera zako na kuzipigia kelele za nguvu hadi watanzania wasikie na kuelimika kwani hiyo ndiyo nguvu pekee ya kushinda hii vita ingekuwa ni rahisi kuondoa CCM madarakani ingeondoka 2010,lakini bado ipo na wanajua walitakiwa watoke wakalazimisha,ni nani anajua kama hawatalazimisha 2015??

Kila la kheri Chadema




Hapo kwenye blue kumbuka CDM hakipigi vita ufisadi kwa ajili ya kutafuta umaarufu bali kulinda na kutetea maslahi ya Taifa. Unaposema CDM kisiendelee kupigia kelele vitendo vya ufisadi una maana ama kama taifa UFISADI siyo tatizo tena na haupo kabisa nchini au unalenga kukifanya chama kiwe sehemu ya kulinda uozo ulioko Serikalini na ndani ya CCM.

Hata hivyo, nakubaliana na wewe katika suala moja kwamba CDM kinahitaji kwenda hatua moja mbele. Kwanza kijikite zaidi katika kukosoa sera mbovu za CCM na kuwaelimisha wananchi jinsi Sera hizo zinavyosababisha Ufukara wao.

Sera zinazopaswa kukosolewa na CDM kuonesha mapungufu yake ziwe zenye kugusa maisha ya kila siku ya Mtanzania na rasilimali zake. Mfano Sera ya uwezekezaji, Madini, Elimu, Mikopo kwa wanafunzi wa Elimu ya juu,Afya, Ardhi, Makazi, Kilimo nk. nk.
Hili lazima liende sambamba na CDM kuonesha sera mbadala zenye mguso mkuu kwa wananchi. Ili kutekeleza hili ipasavyo CDM kinahitaji kuanzisha Idara ya Mipango, Sera na Uratibu ambayo majukumu yake yanaweza kuwa pamoja na mengine haya yafuatayo:

1. Kufanya stadi za sera na mipango yote ya Serikali ili kubaini mapungufu yaliyomo na kuja
na mapendekezo mbadala.

2. Kufanya utafiti wa maeneo mbalimbali ya kisekta ambayo yanapaswa kuwekewa mipango na Sera lakini Serikali ya CCM haijaweza kufanya hivyo. nk. nk.

Idara hii lazima ipewe nguvu za Utendaji na iwezeshwe ipasavo ili muda wote ije na mipango, tafiti na Sera mbadala ambazo zitaonesa kwa vitendo utayari wa CDM kuchukua madaraka mwaka 2015 na kuwaondoa Watanzania kwenye lindi la ufukara.

Jambo la pili ambalo nadhani CDM wanaweza kulifanya ni kuwaaminisha Watanzania kwamba maisha bila CCM yanawezekana na yatakuwa bora zaidi na zaidi. Ukiacha njia ya kuonesha sera na mipango mbadala hili linaweza kufanyika pia kwa CDM kushiriki kwa vitendo katika shughuli mbalimbali za maendeleo. Kwa maana ya kuhamasisha nguvu ya umma katika kushiriki miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo mwisho wa siku itasimama kama miradi iliyosukumwa na kusimamiwa kwa mafanikio makubwa na CDM yenyewe. Mfano; kupitia Sera ya Tokomeza Nyumba za Matembe, CDM wanaweza kuchagua vijiji vitano vya mfano kutoka mikoa tofauti tofauti, kisha katika kila Kijiji wakamjengea Mzee mmoja maarufu nyumba bora ya kisasa ambayo itakuwa ni mfano katika utekelezaji wa sera yake hiyo ya kuboresha makazi ya Watanzania. Hili linaweza kufanyika kwa njia mbalimbali katika maeneo mbalimbali.Naimani litaiweka CDM juu sana na bahati nzuri haliwezi kuwa na gharama kubwa ukilinganisha na impact itakayotengenezwa.
 
CDM haiwezi kushinda

Haiwezi kushinda katika kundi la wapiga kura wanazi wa CCM kama wewe, lakini katika kundi la wapiga kura wengine ambao ni wengi CDM itashinda!! CDM itashinda!!. Wewe mwenyewe unajua hilo!
 
Kiukweli tunahitaji mabadiliko ya kweli hapa petu tz. Mi binafsi siamini kama ccm inaweza kufanya jambo lolote la maana nchi hii. Anayeamini hilo anaweza kuwa na matatizo makubwa sana.
 
Kumbe mnajua CCM inajipanga na mnajua 2015 hamuwezi kupata uraisi. Vizuri sana vijana.

CCM mnajipanga hatukatai, ila hamtakuwa na jipya. Kuna msemo wa kiswahili unasema, "msitu mpya nyani wale wale". Kwa yeyote mwenye akili hawezi kutegemea jipya hata mjipange vipi! Mfano mzuri ni kwamba wote wenye kupigania maslahi ya watanzania hamtaki wawe nanyi. Tazama majina yaliyoondolewa kwenye kinyang'anyiro cha nafasi mbali mbali za NEC-CCM, kama Zambi, Mpina, Fulikunjombe etc, wamepigwa chini!! Hapa mtakuwa mnajipanga kwa lipi?? Pamoja na kwamba wewe ni shabiki wa CCM, ila bado hufanyi tathmini ya kina kuhusu mwenendo wa chama chako. Endeleen kujipanga kwa kuwachagua watakaolinda maslahi ya mafisadi huku mkiamini Watanzania wa leo ni mambumbu!! "Chumvi ikiharibika itawekwa nini hadi ikolee"??
Zomba kaweka mada yake kuhusu ukweli wa udhalimu wa serikali ya CCM, nashukuru ameanza kuelimika. Wewe pia hautakuwa mbali na kuelimika. Mpango wetu ni watanzania waelimike, na mda si mrefu Mungu saidia, nawe utaelimika!!!
Kila la kheri Mkuu, kumbuka Tanzania tunayoipigania sio kwa ajili ya uchaguzi ujao bali ni kwa ajili ya watoto, wajukuu na vitukuu vyetu(next generation)!!!
 
Chadema waaebdelee kwa nafasi hii hii walipo, "challengers" kuifanya serikali kuwa Makini na kuichallenge serikali kuweZa fikia tija katika kiwango kizuri
As chadema kutoa challenge ina impact yake (honestly) kwa serikali kufanya Mbinu zote kuwa effective na efficiency katika kuwatumikia watanzania tuliowengi Kupata nafuu.
Chadema haitakiwi kwenda next level kwa sababu Huko next level sio kwamba wakiwa ndo wenyewe ishu haziwezi enda tena kwa sababu challenger hawatakuwepo kwa hiyo watakuwa wapigaji tu.
Kwa faida ya sisi wananchi Wabaki kuwa challengers tu ili faida itufikie watanzania wote kwa ujumla.
Lakini Kama tunataka faida ya chadema na sio ya watanzania wote Wa move to the next level.
Ambalo swala Hilo la to the next level we won't give them that opportunity at all.
 
Research yako utakuwa umeifanyia maeneo ya Matejoo kwa wanywa piwa. Pitia Tengeru uone.
 
CCM wanajipanga sasa kuiba kura, kumbuka uchanguzi mwaka jana mtoto wa jk Miraji alienda india kusomea jinsi ya kuiba kura kwa kuingilia mtandao wa nec hasa matokeo ya rais na ofisi zao zilikuwa pale upanga, njia nyingine , ccm wanajua idadi ya wanachama wao na mahali walipo hivyo wao huhakikisha inawazuia wananchi wengi wasipige kura kumbuka mwaka 2010 walipo hakikisha vyuo vinafugwa ili wanafuzi wasijitokeze kupiga kura baada ya kujiridhisha jamii kubwa ya wanavyou wapo CDM, pia kumbuka vituo vya kupigia kura vingine viliwekwa mbali na wapiga kura wa eneo analoishi hali iliyiopelekea wengi kukata tamaa kwenda kupiga kura ambapo ccm wanjua kuwa mtaji wa wanachama wao ni watiifu na wanaweza kwenda kupiga kura popote.
 
Back
Top Bottom