CHADEMA Arusha kwatifuka

wakuu sitawe kutuma picha wala video kwa leo ila nitafanya hivyo kesho kama ngereja ataniruhusu maana leo wakati jaribu ku-upload kwenye youtube ngereja akafanya kazi yake..maandamano yalihusisha pikipiki nne na gari moja la jamaa moja majengo ya juu kwajina ni mbuya huyu ni mtu wa bayo na katibu wakata ya kaloleni
Kwatifuka na pikipiki nne acheni zenu nyie watu wanne ndio mnawaita waandamanaji wengi tena inawezekana mtu wa nne alikuwa kwenye foleni ya kawaida.
 
wakati wakitoka kufunga ofisi zilizoko kwenye jengo la namvua plaza huku wakibandika mabango yenye maneo ya kuutaka uongozi wa chadema mkoa uachie ngazi na lingine likisomeka taizo la Arusha ni Mh lema bila kufafanua..baada ya hapo wafuasi wa upande wanaopinga walianza kumiminika kuona hivyo waasi hao walikimbia huku moja akiacha gari lake na dereva kuna watu walitaka kulichoma moto ndipo dereva alipo liondoa sehemu hiyo
zamani watu (waafrika) walinunuliwa wakatumike physicaly, siku hizi wananunuliwa akili tu! hata hivyo tutafika safari yetu.
 
crashwise
Maandamano ? Au maandamano imepata maana mpya ?
Shangaa na wewe kuna mwingine kasema alikutana na watu wengi baadaye tumeambiwa walikuwa wanne hizi hela za Nape zitatumaliza wengi, infwakti hata ningekuwa mimi ningesema hivo hivo wengi.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Mkuu, kwani wananchi wengi katika jiji la Arusha wapo upande gani upande wa madiwani au upande wa chama?
Ukiongea na watu wengi wanapiga mwafaka huo na wanataka madiwani watimuliwe mfano leo baada ya sekeseke hili niliongea na watu waliofika hapo wakawa wanasema kama tamaa zimeonekana mapema kiasi hiki ni bora kuwafukuza kabiza kuliko kuendelea kufuga maradhi
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Wafuasi wa madiwani wanaounga mkono mwafaka wafunga ofisi ya CHADEMA ARUSHA...picha na video zinakuja
Ninachotaka kujua mimi ni km maandamao hayo yalikuwa na kibali cha polisi.kama la! mbona polisi waiacha waandamane au kwa sababu wanaivuruga chadema.
 
Mimi pia niliona hilo tukio ila nilikuta baadhi ya madereva pkpk wenye bendera za cdm eneo la stand ya mabasi karibu na ofisi ya kurushia matangazo..nilijaribu kudodosa vijana ambao walionekana wenye hasira wakaniambia kuwa wanafunga ofisi ya cdm...wengine walikuwa wakionekana kuwafukuza wengine

Sijui walifika mwafaka gani...jamaa moja kaniambia ''baadhi ya madiwani hawamtaki mbunge na mbunge hawatambui madiwani kwani Pinda amewapa mlungula mrefu sana'' then jamaa mwingine akawa anasema tupeni hela yetu bwana kama kuandamana si tumeshaandama bwana...inaonekana magamba wanatembeza pesa sana hapa arusha...
 
kwani hawa siwalifundishwa kuandamana na viongozi wa makao makuu, sasa leo wanaandamana mnawaziwia mbona hamtendi haki?
 
Mmmmh,haiwezekani waandamanaji wakawa wanne tu,lazima kunashida huko.Crashwise hebu jaribu kuwa mkweli japo inauma.Ephata Nanyaro ebu tueleze kulikoni Ofisi yako kufungwa wakati umetuambia hapa CDM ni IMARA hapo Geneva.
 
Acha zako na wewe kwani UVCCM Arusha hawakuandamana na kutaka kuchoma moto jengo la CCM Mkoa kutaka kumtoa Mary kitanda.
Sijaongelea point yoyote ya maandamano!
CDM ni vigeugeu!
Hawana msimamo!
Kila mtu anajiongelea anachojisikia!
 
Mpaka kieleweke!

Magwanda hii issue ya Arusha haikai sawa mpaka Mbowe akubali kuwa yeye ndiye aliyeingia muafaka na Pinda bila kitafuna maneno wala kuchakachua. Hata Slaa alioujua ukweli akapunguza spidi. Ukweli tu ndio utasaidia magwanda. Nahofia huu moto wa nyasi kurukia nyumba zingine.
 
Enough is enough, CHADEMA wapeni hawa madiwani ULTIMATUM, Ikifika Jummane 9 saa 3 kamili asubuhi kwa saa za Afrika Mashariki (baada ya kufurahia siku ya nane) wawe wamefikisha barua za kujiuzulu. Na kama hawakufanya hivyo by saa 3 na robo asubuhi hiyo hiyo WAFUKUZENI.

Watu wamekinai CCM kwa sababu ya siasa za kununuliwa/usaliti. Watu 3 wamekufa Arusha na wengine wamepata vilema vya maisha kutetea HAKI. Kwanza hata wakijiuzulu hawa madiwani kwa sasa hawafai, wafukuzeni kimoja na wasirudi kabisa.
 
Back
Top Bottom