Kutokana na msukumo na hali halisi hapa kwetu Tanzania kuonyesha kuwa vyombo vingi vya habari ama kununuliwa na selikali ya CCM au watu wenye maslahi yao binafsi katika kutangaza habari na kutetea upande wao, huku upande wa pili ukikandandamizwa, Ningependa kutoa ombi hasa kwa CHADEMA kumiliki vyombo vyake vya habari hasa televisheni na radio ili wananchi wengi zaidi waweze kupata kile ambacho kinastahili wakipate katika nyanja za kisiasa, kijamii, kiuchumi na kiutamaduni.
Nadhani hilo litakuwa na faida nyingi sana katika kutangaza sera za chama na malengo yake kwa wananchi walio wengi wenye kiu ya mabadiliko katika nchi yetu..
Natoa hoja.
Mungu ibariki Tanzania
hoja imeungwa mkono kwa mikono miwili. natumaini wametupata