CHADEMA, anzisheni TV/Radio Station!

Ba Martha

JF-Expert Member
Aug 13, 2010
349
102
Kutokana na msukumo na hali halisi hapa kwetu Tanzania kuonyesha kuwa vyombo vingi vya habari ama kununuliwa na selikali ya CCM au watu wenye maslahi yao binafsi katika kutangaza habari na kutetea upande wao, huku upande wa pili ukikandandamizwa, Ningependa kutoa ombi hasa kwa CHADEMA kumiliki vyombo vyake vya habari hasa televisheni na radio ili wananchi wengi zaidi waweze kupata kile ambacho kinastahili wakipate katika nyanja za kisiasa, kijamii, kiuchumi na kiutamaduni.

Nadhani hilo litakuwa na faida nyingi sana katika kutangaza sera za chama na malengo yake kwa wananchi walio wengi wenye kiu ya mabadiliko katika nchi yetu..

Natoa hoja.
Mungu ibariki Tanzania
Chama cha Democrasia na Maendeleo (CDM) kina kila sababu sasa kuhakikisha kina azisha kituo cha TV, ili kuondoa hujuma tunazo zishuhudia katika TV yetu ya umma TBC dhidi ya kile kinachoonekana dhahiri kuziminya habari za chama hiki na wakati mwingine kutokukipa muda wa kutosha ukilinganisha na CCM.

Wote tunaelewa kuwa chama hiki kimeonesha kukubalika na wengi hasa vijana wengi wao wakiwa mijini,nadhani hapa jitihada za makusudi zinahitajika zifanyike ili elimu ya mabadiliko ifike mpaka vijijini ambako CCM bado imepafanya kama mtaji wa chama.so nafikiri,kama cdm tv itaanzishwa na ikawa na uwezo wa kuchana mawimbi nchi nzima basi moja kwa moja CCM ijiandae kuzikwa rasmi 2015.

Wito wangu kwa viongozi wa CDM kuandaa mkakati kabambe wa kitaifa waje nao kwa wapenzi na wanachama wote wa CDM bila kuwasahau hata wasiokuwa na chama ili kuendesha mchango wa fedha nchi nzima wa kuanzishwa kwa tv CHADEMA. Je, tuko tayari? Lakini nikileta hoja hii kwenu naomba pia nijulishwe je mamlaka ya anga hapa TZ ina kizuizi kisheria juu ya jambo hili kufanyika?
Kwa mujibu wa thread fulani ya siku za nyuma, Dk Slaa ulijitokeza na kusema tarehe 15 tutarajie habari mpya juu ya mabadiliko makumbwa kuhusu vyombo vya habari ikiwemo television.

Naomba utujuze tena mmefanikiwa au laa na kama hamjafanikiwa mchakato unaendelea vizuri?
 
Wanahitaji sana airtime hasa kupitia redio, TV nyingi hazifiki vijijini kwani umeme hakuna radio ingeleta impact zaidi. Airtime ingewasaidia sana sana lakini hawawezi kwa sasa it is too late kununua sidhani kama wana funding wakitaka airtime wanakatiwa basi yaani wamekuwa watoto yatima kwelikweli
 
Too late. Hata kama wakiamua kufanya hivyo, mchakato wake wa kupata go ahead toka TCRA ni mrefu sana probably 6 months minimum (Practically) na hata wakipewa masuala ya ujenzi wa kituo na mambo ya nufundi ni kadhia nyingine.

Isitoshe, sasa hivi ni zama za Digital TV kwa station zote mpya. Kufikisha signals zako kwa watazamaji lazima upitie (Starmedia) ambao ni TBC, au Basic Transmission (ambao ni Star TV + ITV) au upitie Agape Associates.

Kwa hiyo huenda yakawa yale yale ya Kocha wao, wachezaji, wenyewe, marefa wenyewe, don't expect miracle.

Nakutakia Idd njema mkuu!
 
Wanahitaji sana airtime hasa kupitia redio, TV nyingi hazifiki vijijini kwani umeme hakuna radio ingeleta impact zaidi. Airtime ingewasaidia sana sana lakini hawawezi kwa sasa it is too late kununua sidhani kama wana funding wakitaka airtime wanakatiwa basi yaani wamekuwa watoto yatima kwelikweli

Kuna mdau alisema hapa jamvini wakati wa ufunguzi, vituo vyote waliwanyima Airtime. TBC1 walilazimika kwa kuwa UNDP walifund launching ya vyama vyote katika TV. Ila sijui kwa nini vyama vingine vidogo, hawajapewa fursa hiyo.
 
Desperate situations calls for desperate moves. Chadema haiko desperate, acha CCM wachakatuke. Naunga mkono kupata airtime kwenye radio manake wanaoangalia tv (walioko mijini) hawahitaji elimu kama walioko vijijini. Kuna vijiji hapa tz wanajua Nyerere ndo rais hadi leo, mwenge hawajauona for years....If not now, time will tell.
 
Yaani CHADEMA waiombe Serikali ya CCM Kibali cha Kumiliki TV?
 
Mbali na ugumu wa kibali lakini pia kuanzisha Tv station inahitaji capital kubwa sana.
Sijui CHADEMA wana vyanzo vingine vya kujipatia pesa mbali na Ruzuku na ada ya wanachama ambao wengi wao ni wazito kuchangia.
 
Ni wazo zuri na lilishatolewa hapa tokea enzi za uchaguzi...
Nadhani kwa vile viongozi wetu wanapitia hapa wameshaliona hili..
Kinachotakiwa ni wao kulipitia na kuona uwezekanaji wake kisera, then kuna watu ambao walionyesha hata moyo wa kuchangia hii kitu in case ikianza kuoperate!
Ni wazo zuri!
 
Ni kweli wakati umefika kwa chadema kumiliki vyombo vya habari.
 
Ba Martha

Toka lini chadema wametangaza sera na malengo ya chama chao? na hata ikianzishwa sioni kama itakua na jipya zaidi ya kuhamasisha vurugu ambazo hatuzitaki sasa hivi!
 
Last edited by a moderator:
...Kalagabaho, you name answers for yourself so just shut up your f#$%^ing mouth!
 
mbona mnavyo tatizo vinaandika habari zilezile kila siku! vimekosa mvuto!
Nachukia Waafrika wanaoishi kwa propaganda...
Ni vyombo gani registered vya CHADEMA unavyovijua?...kama si spoon-fed information hiyo?
Kuwa mkweli ubaki huru..Ongea ukweli, hutoharibikiwa na kitu.
 
Nachukia Waafrika wanaoishi kwa propaganda...
Ni vyombo gani registered vya CHADEMA unavyovijua?...kama si spoon-fed information hiyo?
Kuwa mkweli ubaki huru..Ongea ukweli, hutoharibikiwa na kitu.

what? you are really black minded moses!
 
Wazo limekuja wakati muafaka, wasitunyanyase na vyombo vyao. Kuna watu ka akina m. Hawaipendi ccm lakini wanawatangaza kwa woga tu.
 
Back
Top Bottom