Chachu na Tamu ya Mapenzi

kilimasera

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
3,068
268
Mwanaume mmoja wa nchini Italia alitumia zaidi ya dola nusu milioni kwaajili ya zawadi na maandalizi ya harusi na mchumba wake lakini siku ya harusi alibaki akilia baada ya kuachwa solemba kanisani huku bi harusi wake akitoroka na mwanaume mwingine.
Mwanaume wa nchini ya Italia ambaye alionja chachu ya mapenzi baada ya kutorokwa na mpenzi wake siku harusi ameenda mahakamani kudai fidia ya dola za Kimarekani 743,000 kwa kuvunjwa moyo na kuchezewa hisia zake na pia kupoteza kiasi kikubwa cha pesa.

Mwanaume huyo mwenye umri wa miaka 32 alitumia pesa nyingi kwaajili ya maandalizi ya harusi na mchumba wake huyo lakini siku ya harusi mchumba wake aliroroka na mwanaume mwingine.

Mwanaume aliyetajwa kwa jina moja la Riccardo, alikodisha jumba la kifahari kwaajili ya harusi yao nje kidogo ya jiji la Rome, alikodisha hoteli kwenye kisiwa kimoja cha Pacific kwaajili ya Honeymoon (fungate) na pia aliifanyia marekebisho makubwa nyumba yake ili kukidhi mahitaji ya mke wake mtarajiwa.

Kwa mujibu wa shirika la habari la Italia, ANSA, siku ya harusi Riccardo na familia yake na ndugu na jamaa walikuwa tayari kanisani wakimsubiri bi harusi awasili lakini badala yake aliwasili kaka wa bi harusi ambaye alimwambia Riccardo kuwa dada yake hatakuja kwenye harusi.

Mchungaji alilazimika kuvunja shughuli zote za harusi baada ya kuambiwa kuwa bi harusi ameteroka na mwanaume mwingine ambaye alikuwa na uhusiano naye wa kimapenzi.

Taarifa zimesema kuwa Riccardo amekodisha wanasheria kwaajili ya kumfungulia kesi aliyekuwa bi harusi wake akimtaka yeye na familia yake walipe gharama zote za harusi alizoingia.
 
Back
Top Bottom