Ch10,ITV,Star tv na TBC1,jirekebisheni uchambuzi wenu wa magazeti unakera

Feb 27, 2016
109
138
Wana Jf,
Naamini habari hii mtaikuta asubuhi mkiamka.

Kwakweli uchambuzi wa magazeti wa Ch.10 ,ITV ,Star tv na TBC1 unakera. Hivi ni kwa nini wasitenge muda maalumu kama wenzao Clous tv kama wanashindwa kutendea haki walaji wa habari muda wa uchambuzi? hawa jamaa wa Clouds ni mfano wa kuigwa nchini.

Utakuta eti mtangazaji anatumia dk3 ameshachambua magazeti yote.
Amechambua nini sasa.Kama hao TBC1,Chn.10 na ITV ni afadhali hata star tv kidogo wanasoma taarifa muhimu japo sio sana wanatumia muda mfupi halafu wanakimbilia kwenda kuchambua mada zisizo na mashiko. Kuhoji kwenyewe poor,poorer,poorest. huko startv kabaki Doto Emmanuel Bulendu na kipindi chake cha jumosi. Kidogo na mkongwe mzee wetu Angalieni Mpendu.

Huko Chn.10.Wengine wanaacha kuwaeleza wananchi taarifa muhimu wanapoteza muda kwa kukimbilia kutoa ufafanuzi wa vibonzo vinavyomchekesha yeye mwenyewe mtangazaji na kukidhi interest zake. magazeti ya kingereza wakati mwingine yanatafsiriwa "kiswanglish" na kupotosha kabisa lengo la watoa habari.ni afadhali asome hivyo hivyo kingereza kama hawezi kutafsiri.ama wawe wanatuliza kichwa waache haraka na kujikuta wanasema uongo au wanatoa tafsiri kinyume. bure kabisa...

Huko TBC1 haya "tuungane na Fulani atupe kidogo uchambuzi wa magazeti" mezani pana UHURU,MAJIRA,HABARI LEO.na THE DAILY NEWS basi Akiona habari ya ku-criticize gvt anairuka haraka. Magazeti maalumu ya habari za michezo kama DIMBA,CHAMPION hayageuzi upande wa pili.Anasoma upande mmoja tu na anasoma habari za ndani tu.Yanga na Simba basi. dk2 eti kamaliza.

Anakimbilia kumrudishia mwenzie na mwenzie kazi yake kubwa ni kushangaa idadi ya masterz alizosoma mgeni mualikwa ama kushangaa jambo Fulani juu ya mgeni mualikwa.
Jins ya kuhoji very poor.Anampa leading questions mgeni. hamna kitu kabisa sijui hawa watangazaji wametoka wapi.Vijana wamemaliza Bachelor za journalism na wame major broadicasting wanahangaika mtaani kufanya kazi za utapeli.Hivi hawa wafanyakazi wa TBC hawana target? mtu akishindwa ku-meet target apishe damu mpya? au ndiyo business as usual? Dr Rioba fanya mabadiliko Mkuu,pesa za watanzania zinateketea bure.

ITV wanasoma heading tu."WABUNGE WATATU WAPANDISHWA KIZIMBANI...ukitaka kujua majina yao ni wakinanani, na kwa nini,kalitafute gazeti Fulani, tunajua kituo hiki ni kizuri na ni superbrand no.1 Tanzania lakini kwa uchambuzi wa magazeti,ni very poor. Basi kama hamna haja ya kusoma japo one paragraph, hata one line ili kumu-alert mlaji wa habari kufanya maamuzi kamili ya kwenda kununua gazeti husika. Mkishindwa kabisa basi msisome magazeti wekeni kwenye screen Mkuze halafu walaji wa habari watasoma wenyewe.

Kwa tabia hii very soon I can see clouds tv is going to shine,na kale ka ubunifu kao ka mwewe...nadhani Mh.Rais kavutiwa na mengi hawa jamaa ni wabunifu sana,wanachambua soka mpaka unashindwa kupokea simu kusubiri wa malize. Hata radio yao wakichambua soka kwa wale wapenda soka,kama unadrive ni vema upaki maana wanakuhabarisha mpaka adrenalin zinashtuka.

JAMANI CH.10,ITV,STAR TV,NA TBC 1 JIREKEBISHENI UCHAMBUZI WA MAGAZETI ASUBUHI MNAKERA,IGENI MFANO WA CLOUDS TV.

tuchangie ili kuleta mabadiliko kwa media zetu.

"KUKOSOLEWA NI VEMA KULIKO KUSIFIWA MAANA UKIKOSOLEWA UTAREKEBISHA MAPUNGUFU YAKO NA KUONGEZA UBUNIFU.UKISIFIWA HUTAONA MAPUNGUFU YAKO HIVYO UTABAKI HAPOHAPO ULIPO"
 
Wakikusomea magazeti yote habari kamili nna atakae enda kununua gazeti sasa maana we hapo utakuwa umeokoa 1000 yko.
 
Labda hao wengine watayafanyia kazi maoni yako lakini sio TBC ccm ambao wanajua kuwa mpende msipende mtalipa kodi za kuindesha hiyo Tv
 
JPJM kawaambia kiutu uzima/kikubwa, kuwa Clouds ndio bora ktk uchambuzi wa Magazeti, Radio na Channel zote tisa lakini kumi na mdebwedo ni hao TBC waliojitoa akili,
 
Mheshimiwa Rais mwenyewe anasema anapenda sana uchambuzi wa magazeti wa Clouds Tv,acha waendelee na mambo yao watakuwa wanajiangalia wenyewe studio.
 
Mimi hapo nawalaumu ITV kwa sababu ndiyo tv ninayoiangaliaga, hizo tv zingine wafanye wanavyotaka kwanza huwa hawasikilizi ushauri
 
Wenyewe wanaita udondozi wa magazeti. Na kweli ni udondozi tu
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom