CDM : Twendeni kimkanda mkanda Arumeru

GeniusBrain

JF-Expert Member
Nov 3, 2010
4,315
306
CHADEMA leo hii wanategemea kuzindua kampeni zao za uchaguzi wa Jimbo la Arumeru katika uwanja wa shule ya Msingi Liganga ambapo viongozi wakuu na wabunge wao wote wanategemea kuhudhuria. Wakati hayo yakitegemewa kutokea leo, hali bado ni tete ndani ya chama kuhusu mustakabali wa kampeni hizo. Kwani chama hakina rasilimali za fedha na vifaa kuendeshea kampeni hizo kwa sasa kwa ajili yakukidhi matumizi ya timu ya kampeni, Helikopta, magari nk,. Na mkakati pekee ambao wanaoutegemea ni kupitisha bakuli kwa wananchi. Kwa maana hii basi , ni wazi kabisa CDM kuendesha kampeni hizi kimkanda mkanda na wadadisi wa mambo wanaliona hili litakuwa ni tatizo kubwa tofauti na wenzao wa CCM ambao wanaonyesha wazi wako vizuri kifedha, watu na kimkakati.
 
silaha yetu kubwa tunayojivunia ni UZALENDO na MSHIKAMANO ambavyo hivi ni zaidi ya pesa. watu wako tayari kujitolea bila Posho hii ni tunu kubwa ambayo chadema inabidi iitunze sana kwa maana CCM wenzetu wameipoteza kwa maana wanachama wao hawaulizi tena swala la pesa bali ni kiasi gani mtatulipa kwanza ?? . kama ambavyo wengi mlisikia umoja wa vijana wakilalamikia posho ya shs.5000 kuwa ni ndogo. matumizi ya pesa ni sumu mbaya sana ktk uongozi kama mnavyoona imeshaanza kuitafuna CCM.

binafsi nitasafiri kwenda Arusha na kujitolea usafiri wangu kutumwa kokote chama kitapoona unaitajika.
 
silaha yetu kubwa tunayojivunia ni UZALENDO na MSHIKAMANO ambavyo hivi ni zaidi ya pesa. watu wako tayari kujitolea bila Posho hii ni tunu kubwa ambayo chadema inabidi iitunze sana kwa maana CCM wenzetu wameipoteza kwa maana wanachama wao hawaulizi tena swala la pesa bali ni kiasi gani mtatulipa kwanza ?? . kama ambavyo wengi mlisikia umoja wa vijana wakilalamikia posho ya shs.5000 kuwa ni ndogo. matumizi ya pesa ni sumu mbaya sana ktk uongozi kama mnavyoona imeshaanza kuitafuna CCM.

binafsi nitasafiri kwenda Arusha na kujitolea usafiri wangu kutumwa kokote chama kitapoona unaitajika.

Hii ni dhana yakizamani sana. Bila pesa helikopta itaruka kwa kuweka maji ? bila pesa matangazo yatafanyikaje? bila pesa mgombea atatembeaje kwa wapiga kura? bila pesa timu yakampeni itakula nn ?. Kampeni za sasa ni pesa kwa vyovyote utakavyo

 
Mbona ume tone down leo ,jana siulikuja na matusi kuonyesha kampeni meneja hajua afanyalo au umekuja kusesembua ili ujue kama wana pesa au hawana , hakuna mjinga hapa weye,embu toa suluhisho basi
 
CHADEMA leo hii wanategemea kuzindua kampeni zao za uchaguzi wa Jimbo la Arumeru katika uwanja wa shule ya Msingi Liganga ambapo viongozi wakuu na wabunge wao wote wanategemea kuhudhuria. Wakati hayo yakitegemewa kutokea leo, hali bado ni tete ndani ya chama kuhusu mustakabali wa kampeni hizo. Kwani chama hakina rasilimali za fedha na vifaa kuendeshea kampeni hizo kwa sasa kwa ajili yakukidhi matumizi ya timu ya kampeni, Helikopta, magari nk,. Na mkakati pekee ambao wanaoutegemea ni kupitisha bakuli kwa wananchi. Kwa maana hii basi , ni wazi kabisa CDM kuendesha kampeni hizi kimkanda mkanda na wadadisi wa mambo wanaliona hili litakuwa ni tatizo kubwa tofauti na wenzao wa CCM ambao wanaonyesha wazi wako vizuri kifedha, watu na kimkakati.

Kizabi zabina haachi umbea. Haya tuambie na ninyi wenzetu nchi haina hela mnatembezea bakuli kwa ROST TAMU AU EL?
 
money is not everything!! Think Twice My Dear!! Wapo watu wako Tayari kuwezesha ili Demokrasia iweze Kufanya Kazi Yake!!
 
Back
Top Bottom