Nimekaa kimya kwa muda bila kuchangia...tangu nilipojiunga enzi ile Forum hii adhim ikiitwa Jambo Forums..tukiwa na magwiji wakiongozwa na E.S, Dr. Who, Kichuguu, Mkandara..n.k. JF imekuwa ni kisima cha elimu.
Nianze kwa kutoa masikitiko yangu...nakumbuka kunamchangiaji mmoja alikuwa akieleza vuguvugu la upinzani katika kipindi cha uchaguzi wa 2010...jinsi CDM na CUF ambapo wangeshiriki kuikaba koo CCM. Sikuwa nikiamini kama CDM ingeweza kuvuta hamasa katika kiwango hiki..na binafsi nilishiriki hata kuandika hivi humu Foramuni.
Kilichotokea baada ya uchaguzi huu ni nguvu ya upinzani kuongezeka kwa kiwango kikubwa..kuanzia kura za uraisi,ubunge na udiwani. Mategemeo yangu yalikuwa nikuona nguvu hii iliyoanza kupatikana ingeimarishwa vizuri ili kuweza kuvuna kura nyingi zaidi.
Kinachotokea sasa ni msiba...muungano ule wa vyama ulisambaratika tena hata kabla ya uchaguzi..huku vyama vikitupiana lawama kuwa mwenzake ni kibaraka. Kuna nadharia nyingi mno ya kiini hasa cha hali hii. Kuna wanaodhani kama kuna mapandikizi ambayo yamewekwa kwa maksudi kuona wapinzani hawaungani. Yaliyojiri baada ya uchaguzi mkuu ambayo yalinishtua, kutaja machache ni haya yafuatayo:-
i) CDM kukataa kuungana na vyama vingine kwenye kambi ya upinzani;
ii) CUF kutoa kiroja cha mwaka, kuunga mkono wagombea wa CCM ili kuidhoifisha CDM (Mpinzani mwenzanke);
iii) Kutoleana maneno ya kashfa hadharani na kuita maridhiano ya CCM na CUF eti ni ndoa ya mkeka;
iv) Kuona kuwa baada ya ndoa hii,CUF imepoteza sifa(legitimacy) ya kuitwa chama cha upinzani;
v) Cha kushtua zaidi, viongozi waandamizi wa CUF kuanza kutembea mikoani kuya rudi maandamano ya CDM na falsafa zake.
Binafsi siamini na wala sintokaa nikiamini kamwe kama CDM peke yao wanaweza kushika dola, vivyo hivyo kwa CUF au chama kingine cha upinzani. Ila naamini kama vyama hivi bado vina viongozi imara,wasomi kuweza kutibu majeraha haya. Nakumbuka Prof. Lipumba aliulizwa siku ile katika mdahalo na ITV kama je kuna uwezekano wa wapinzani kuungana?. Alitaja ugumu wa kikatiba na kutokuaminiana baina ya vyama.
My take (chambilicho cha baadhi ya wachangiaji humu).
Nchi hii inahitaji upinzani imara, viongozi wetu wa kisiasa fahamuni kama kidole kimoja hakivunji chawa. Na natoa wito wa kukaa chini na kuangalia uwezekano wa kurudisha umoja wenu.
Kingwele wa Kingwele.
Kijijini, Kwegole-
Nianze kwa kutoa masikitiko yangu...nakumbuka kunamchangiaji mmoja alikuwa akieleza vuguvugu la upinzani katika kipindi cha uchaguzi wa 2010...jinsi CDM na CUF ambapo wangeshiriki kuikaba koo CCM. Sikuwa nikiamini kama CDM ingeweza kuvuta hamasa katika kiwango hiki..na binafsi nilishiriki hata kuandika hivi humu Foramuni.
Kilichotokea baada ya uchaguzi huu ni nguvu ya upinzani kuongezeka kwa kiwango kikubwa..kuanzia kura za uraisi,ubunge na udiwani. Mategemeo yangu yalikuwa nikuona nguvu hii iliyoanza kupatikana ingeimarishwa vizuri ili kuweza kuvuna kura nyingi zaidi.
Kinachotokea sasa ni msiba...muungano ule wa vyama ulisambaratika tena hata kabla ya uchaguzi..huku vyama vikitupiana lawama kuwa mwenzake ni kibaraka. Kuna nadharia nyingi mno ya kiini hasa cha hali hii. Kuna wanaodhani kama kuna mapandikizi ambayo yamewekwa kwa maksudi kuona wapinzani hawaungani. Yaliyojiri baada ya uchaguzi mkuu ambayo yalinishtua, kutaja machache ni haya yafuatayo:-
i) CDM kukataa kuungana na vyama vingine kwenye kambi ya upinzani;
ii) CUF kutoa kiroja cha mwaka, kuunga mkono wagombea wa CCM ili kuidhoifisha CDM (Mpinzani mwenzanke);
iii) Kutoleana maneno ya kashfa hadharani na kuita maridhiano ya CCM na CUF eti ni ndoa ya mkeka;
iv) Kuona kuwa baada ya ndoa hii,CUF imepoteza sifa(legitimacy) ya kuitwa chama cha upinzani;
v) Cha kushtua zaidi, viongozi waandamizi wa CUF kuanza kutembea mikoani kuya rudi maandamano ya CDM na falsafa zake.
Binafsi siamini na wala sintokaa nikiamini kamwe kama CDM peke yao wanaweza kushika dola, vivyo hivyo kwa CUF au chama kingine cha upinzani. Ila naamini kama vyama hivi bado vina viongozi imara,wasomi kuweza kutibu majeraha haya. Nakumbuka Prof. Lipumba aliulizwa siku ile katika mdahalo na ITV kama je kuna uwezekano wa wapinzani kuungana?. Alitaja ugumu wa kikatiba na kutokuaminiana baina ya vyama.
My take (chambilicho cha baadhi ya wachangiaji humu).
Nchi hii inahitaji upinzani imara, viongozi wetu wa kisiasa fahamuni kama kidole kimoja hakivunji chawa. Na natoa wito wa kukaa chini na kuangalia uwezekano wa kurudisha umoja wenu.
Kingwele wa Kingwele.
Kijijini, Kwegole-