CDM kuelekea April 1 jihadharini na...

Rweye

JF-Expert Member
Mar 16, 2011
16,958
7,512
Ikiwa kumebakia siku chache kabla ya kupiga kura huko Arumeru ni vyema ikaeleweka wazi kwamba hakuna maeneo makamanda wa CDM watatakiwa kuwa macho kama muda wa kuhesabu kura,CCM hawana haja ya kupoteza mda kufanya mikutano ila zaidi zaidi wako bizi na jinsi gani kura yao 1 itabadilishwa na kuwa 2 na ile ya CDM ikageuzwa na kusomeka ya CCM

Kibaya zaidi kuna uwezekano makundi ya watu yakarubuniwa wasiende kupiga kura n.k

Kwa uzoefu wa Igunga,CDM wawe makini na wanahabari kwa ujumla wao,mfano siku ya kupiga kura Igunga mambo kadhaa niliyaona na nikagundua ulikuwa ni mkakati ulio rasmi...

a)Matangazo ya upigaji kura (live) yalikatishwa kwenye Tv saa 2:30 asubuhi mpaka saa 8 na kuonesha wazee na akina mama ndo wanaonekana wanapiga kura,kwahiyo ile ya vijana kupiga kura ilizuiliwa kurushwa kimakusudi ili kuuonyesha umma vijana hawakupiga kura kama walivyofanya wazee

b)Umeme ulikatwa saa 4 asubuhi karibu mikoa kibao ili kupunguza usambaaji wa habari kwa kutumia vyombo vya umeme,ulirudishwa majira ya saa 7 mchana

c)Matangazo ya Tv live yalikatishwa tena saa 1:30 jioni kwa sababu za ajabu ajabu ikiwemo eti usiku palikuwepo na mvua na mawasiliano ya moja kwa moja kutoka vituoni kwa wanaoripoti matokeo yakazuiwa baada ya kata moja kujitangazia matokeo ya kura na kutangaza Kafumu kashinda kinyume na sheria kwani kata haitakiwi kutoa matokeo bali yanakusanywa vituoni na kutumwa kwa DED

Kilichofuatia hapa ndugu zangu ilikuwa saa8 usiku ndo ajabu tukaanza kusikia CCM inaelekea kushinda,lakini itoshe tu kusema kwamba CCM wanautegemea sana usiku kuliko mchana katika shughuri hii wakisaidiwa na undumilakuwili wa wanahabari ambao kusema kweli ni wepesi kuliko hata manyoya ya sungura katika kuhongwa

Hebu nawe weka uzoefu hapa ili tuweze kusaidia the way forwad for the victory....
 
Ikiwa kumebakia siku chache kabla ya kupiga kura huko Arumeru ni vyema ikaeleweka wazi kwamba hakuna maeneo makamanda wa CDM watatakiwa kuwa macho kama muda wa kuhesabu kura,CCM hawana haja ya kupoteza mda kufanya mikutano ila zaidi zaidi wako bizi na jinsi gani kura yao 1 itabadilishwa na kuwa 2 na ile ya CDM ikageuzwa na kusomeka ya CCM

Kibaya zaidi kuna uwezekano makundi ya watu yakarubuniwa wasiende kupiga kura n.k

Kwa uzoefu wa Igunga,CDM wawe makini na wanahabari kwa ujumla wao,mfano siku ya kupiga kura Igunga mambo kadhaa niliyaona na nikagundua ulikuwa ni mkakati ulio rasmi...

a)Matangazo ya upigaji kura (live) yalikatishwa kwenye Tv saa 2:30 asubuhi mpaka saa 8 na kuonesha wazee na akina mama ndo wanaonekana wanapiga kura,kwahiyo ile ya vijana kupiga kura ilizuiliwa kurushwa kimakusudi ili kuuonyesha umma vijana hawakupiga kura kama walivyofanya wazee

b)Umeme ulikatwa saa 4 asubuhi karibu mikoa kibao ili kupunguza usambaaji wa habari kwa kutumia vyombo vya umeme,ulirudishwa majira ya saa 7 mchana

c)Matangazo ya Tv live yalikatishwa tena saa 1:30 jioni kwa sababu za ajabu ajabu ikiwemo eti usiku palikuwepo na mvua na mawasiliano ya moja kwa moja kutoka vituoni kwa wanaoripoti matokeo yakazuiwa baada ya kata moja kujitangazia matokeo ya kura na kutangaza Kafumu kashinda kinyume na sheria kwani kata haitakiwi kutoa matokeo bali yanakusanywa vituoni na kutumwa kwa DED

Kilichofuatia hapa ndugu zangu ilikuwa saa8 usiku ndo ajabu tukaanza kusikia CCM inaelekea kushinda,lakini itoshe tu kusema kwamba CCM wanautegemea sana usiku kuliko mchana katika shughuri hii wakisaidiwa na undumilakuwili wa wanahabari ambao kusema kweli ni wepesi kuliko hata manyoya ya sungura katika kuhongwa

Hebu nawe weka uzoefu hapa ili tuweze kusaidia the way forwad for the victory....

Mkuu nashukuru kwa allerts zako. pia ningependa kuwatahadharisha wawe macho zaidi kwani waweza toa
tangazo la hata kusema uchaguzi umeahirishwa na wakayapeleka hayo magazeti kwenye ngome za Chadema.BAADAYE WAKAJATOA UFAFANUZI ETI KUWA NI SKUKUU YA WAJINGA.tuweni makini na siku hiyo kuna watu hawalali wanatafuta kitu cha kufanya siku hiyo
 
Back
Top Bottom