CCM yawatosa Watuhumiwa bila Ushahidi!

Turudi kwenye hadithi ya nyoka kujichuma ngozi yake, hapa inafanana kwa ujumla chama kilikuwa kimechafuka sana kwa uchafu mbali mbali sasa ni wakati muafaka kimeamua kijichuma magamba yake kirudi kuwa kipya. Tuunge mkono, hotuba ya Mwalimu sikumbuki mwaka gani lakini aliitoa enzi za Mwinyi alisema tuhuma tu zinatosha kukufuzisha kazi maana kwanini utuhumiwe? Anasema "Huko Uingereza kuna waziri mmoja alituhumiwa kutembea na malaya wa barabarani, waziri yule akatakiwa ajieleze naye akaona bora aandike barua ya kujiuzulu waziri mkuu alisaini kuidhinisha kujiuzulu kwake" mwisho wa kunukuu. Kwa hiyo na sisi ukizingatia nchi yetu ni changa sana kidemokrasia inabidi tu-rely on this kwa sababu kama wewe ni kiongozi wa serikali na umeapa kuwa muadilifu kwanini utuhumiwe?
 
bubu mfano wako wa nyoka.. umenipa wazo hili...na mnaweza kuninukuu .. "nyoka hubakia kuwa nyoka, hata akijivua magamba".. Hiyo ni methali Original M. M.
 
Hayo ni ya ndani ya Chama ni kwa faida ya wanachama husika ,tunataka na wale ambao ni wateule waliongamiza Taifa kwa maamuzi yao mabaya kupitia mikataba na mengine yanayohusu utendaji wao wa kila siku kikazi ,nao tunaomba Mkuu wa Nchi achukue maamuzi kwa manufaa ya wanachi wote yaani walio na vyama na wasio na vyama.Hapa ndiyo tutaona mapambano yameanza ktk medani ya taifa hadi sasa ni ktk medani ya chama.
 
huyo JK anataka kututia changa la macho tu!
yeye mwenyewe si ndo alosema visubiriwe vyombo vya sheria viamue?? au upinzani hauwezi kuamua lakini yeye anaweza .....
kweli nimeamini tupo kwenye animal farm hapa(kama Mwanakijiji alivyokumbushia) " all animals are equal but some are more equal than others"
 
Hawa watu wamepewa zuio la kugombea nyadhifa walizoomba ndani ya chama.

Muungwana aliongea kule arusha kuwa anapambana na rushwa na ameanzia ndani ya chama. Hii ni kutaka kuwadhihirishia watu kuwa amedhamiria kweli kupambana na rushwa.

Hii ni giriba kwa wananchi, wanajifanya kupambana na rushwa ndani ya chama chao ili kulinda maslahi ya wanamtandao. Mbona kwa hizi kubwa zinazotishia mustakabali wa nchi asi react namna hii. This is non sense. Huu ni usanii wa EL kutaka kulimaliza kundi la wapinzani wake mkoani Arusha. Ni mbinu chafu kabisa za kisiasa kuwahi kutokea katika nchi hii.

Mahali gani ambapo wagombea wa SISIEM hawakutumia rushwa kupata nyadhifa hizo, halafu wanajifanya kuwatoa kafara wachache. But I think siku itafika miti yote itateleza.
 
Hii habari ina mapungufu mengi tu kuna unawezekano mkubwa watu wakawa wanajadili habari isiyokuwepo!
 
Mwanakijiji acha kupotosha watu, mambo ya ndani ya vyama au kwa maana nyingine mambo ya siasa,,, yanafanyiwa maamuzi na masuluhisho tofauti na mambo ya serikali na utendaji wake!, ni kwenye siasa ndio kweny usuluhisho... refer issue CCM na CUF na miafaka yao.


Kwenye siasa tetesi tu yafanya mtu asichaguliwe,,, sina haja ya kukuelezea hili!!!



Kwenye serikali na dola kuna thing has to be proved without doubt!, kama ujumbe ni propaganda zako tumezizoea!!!
 
MWANAKIJIJI,siyo kweli jamaa kwamba wamevuliwa uanachama bali wamewekwa pembeni wasigombee uenyekiti na ujumbe wa NEC katika mkoa wa Arusha mpaka kesi yao iishe kwa maana hiyo mkoa wa Arusha unaanza mchakato upya wa wanaotaka kugombea kuchukuwa fomu ili wawahi kushiriki katika kutano mkuu ambao nadhani utafanyika kati ya tarehee 2,3 au nne mwezi ujao mjini dodoma
 
MWANAKIJIJI,siyo kweli jamaa kwamba wamevuliwa uanachama bali wamewekwa pembeni wasigombee uenyekiti na ujumbe wa NEC katika mkoa wa Arusha mpaka kesi yao iishe kwa maana hiyo mkoa wa Arusha unaanza mchakato upya wa wanaotaka kugombea kuchukuwa fomu ili wawahi kushiriki katika kutano mkuu ambao nadhani utafanyika kati ya tarehee 2,3 au nne mwezi ujao mjini dodoma


Kinachomsumbua Mzee Mwanakijiji ni Ukereketwa/ufurukutwa/ungangari/ungunguri wake... Nadhani tumsamehe tu! lakini wakati tunasoma post zake tujue ni mtu gani anaandika,,, kama ilivyokuwa kwa mgongo x 2
 
Wote mmenaswa mkaanza jadili. wenyewe Kalmati Kuukuu wakaambiwa na wachunguzi wao kuwa Wenye nchi wamebaini kuwa kuna kamchezo kachafu na kakijinga ambacho Kulamaiti walikuwa wakifanye.

Tangazo rasmi litatoka baada ya chaguzi zote kumalizika Novemba!
 
Wakati serikali ya CCM ikidai kuwa watuhumiwa wasichukuliwe hatua yoyote au kuhukumiwa kwa namna yoyote hadi vyombo vya sheria vitimize kazi yake, habari zinazoingia KLH News ni kuwa Kamati Kuu imeamua kuwatosa waliokuwa wa Bunge wa Mkoani Arusha ambao walikuwa wanakabiliwa na TUHUMA ZA RUSHWA. Chama hicho tawala, hakikutaka kusubiri maamuzi ya mahakama au kuacha mchakato wa sheria ufuate mkondo wake na badala yake imeamua kuwa mtoa taarifa, hakimu, polisi, na Mnyongaji!!

Kama taarifa hizi ni za kweli, sasa sisiemu wamefanya nini, na ni kwa nini wanawalaumu wapinzani kwa hatua waliyochukua kwa mafisadi?
Unajua hawa viongozi wa sisiemu mimi nashindwa kabisa kuwaelewa. Wao wanawalaumu wapinzani kwa kujichukulia sheria mikononi kwa kuwaanika hadharani watuhumiwa wa ufisadi, wakati na wao wanafanya hayo hayo. Kwa nini wasiondoe boriti machoni mwao kabla ya kuona vibanzi katika macho ya wapinzani?
Kwa nini wasisubiri mahakama iwasafishe wabunge hawa wa Arusha ndipo wao wawahukumu katika vikao vya chama na kuamua hatima yao katika chama?
huku ni kutowatendea haki hawa wabunge hakika!
 
Uchaguzi CCM Arusha Oktoba 30
NA FURAHA OMARY

UCHAGUZI mkuu wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Arusha, unatarajiwa kufanyika Oktoba 30, mwaka huu.
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Aggrey Mwanri alisema hayo jana.
Alisema hatma ya uchaguzi huo imefikiwa katika vikao vya Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa na Halmashauri Kuu ya Taifa vilivyofanyika katikati ya wiki hii.
Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM katika mkutano uliofanyika Dodoma Septemba 5, mwaka huu ilisitisha kufanyika kwa uchaguzi huo kutokana na baadhi ya wagombea wake kutuhumiwa kwa kosa la rushwa.
Kamati Kuu iliamua kuahirisha uchaguzi huo, ili Chama kipate nafasi ya kutafakari vizuri suala zima la uchaguzi mkoani humo na kuamua ipasavyo. Pia Kamati Kuu ilifikia uamuzi huo ili kutoa nafasi kwa vyombo vya sheria kufanya kazi yake.
Waliotuhumiwa kwa rushwa ni Michael Laizer, mbunge na mgombea wa nafasi ya uenyekiti wa CCM wa mkoa; Elias Molel, mbunge na mgombea wa nafasi ya ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa mkoa wa Arusha na Daniel ole Porokwa, Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Arusha, anayegombea ujumbe wa Mkutano Mkuu wa Mkoa.
“Vikao vya Chama vimetafakari kwa kina hatma ya uchaguzi wa viongozi katika mkoa huo …vimeridhika kwamba mwenendo wa kesi unaonyesha kuwa uamuzi wa shauri hili hautafikiwa hivi karibuni.
“Hali hii itafanya uwakilishi wa Mkoa wa Arusha kukosekana katika Mkutano Mkuu wa Nane wa CCM Taifa utakaofanyika Dodoma Novemba 3 na 4, mwaka huu,” alisema Mwanri.
Kutoka na hilo, alisema halmashauri hiyo imeamua nafasi za uongozi zitangazwe upya na kwamba Laizer na Molel hawatagombea.
“Hatua ya kutangazwa upya kwa nafasi hizo katika mkoa wa Arusha, haimaanishi kuwa Chama kimewahukumu viongozi hao kuwa walitoa rushwa, bali kinaamini katika utawala wa sheria na kwamba mtuhumiwa anabakia ni mtuhumiwa hadi mahakama itakapothibitisha ndipo hatua ziweze kuchukuliwa.

“Tunasisitiza kwamba viongozi hao bado ni watuhumiwa, siyo wakosaji ndio maana wanaendelea na nyadhifa zao za ubunge,” alisema Mwanri.
Mwanri alitoa ratiba ya uchaguzi huo, ambapo leo hadi Jumatatu ijayo ni siku za kuchukua na kurejesha fomu.
Jumatano ijayo Kamati ya Siasa ya Mkoa itajadili na kutoa mapendekezo kwa Kamati Kuu, wakati Oktoba 20, Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa itaratibu mapendekezo ya mkoa.
Kwa mujibu wa ratiba hiyo, Oktoba 25, Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa itafanya uteuzi wa mwisho kwa niaba ya Halmashauri Kuu ya Taifa na Oktoba 30, Mkutano Mkuu wa uchaguzi wa Mkoa utafanyika.
Katika hatua nyingine, CCM inakusudia kuifikisha mahakamani Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), endapo itaendelea na msimamo wake wa kutoitendea haki katika uchaguzi wa diwani wa kata ya Namkutwe, wilayani Chunya.
Mwanri alisema hatua hiyo inatokana na tume kumkataa mgombea wa CCM, Bosco Nyembe katika uchaguzi wa diwani wa kata ya Namkutwe, wilayani Chunya.
Katika uchaguzi huo NEC ilimtangaza kuwa mshindi mgombea wa TLP, Rula Stephano, ambaye awali alikataliwa na msimamizi wa uchaguzi huo kutokana na kukosa sifa.
Habari za uhakika zilizopatikana jana mjini Dar es Salaam zilieleza kuwa Stephano, licha ya kuenguliwa kutokana na kukutwa na kasoro kadhaa, ikiwemo ya fomu zake kutokamilika, aliruhusiwa kugombea na Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya hiyo.

Huo ndio ukweli hayo mengine ni porojo za vijiweni tu...

Kwa wale wanaosubiri kujaza nafasi za ubunge za majimbo hayo mawili mtaendelea kusubiri sana....
 
Kuteleza sio kuanguka, and we learn from mistakes. hakuna haja ya kumuita mwanakijiji mzushi kwani hata yeye hutegemea different sources ili kutuhabarisha. M/kijiji usikatishwe tamaa, songa mbele. Count this as a challenge for your work.
 
Kuteleza sio kuanguka, and we learn from mistakes. hakuna haja ya kumuita mwanakijiji mzushi kwani hata yeye hutegemea different sources ili kutuhabarisha. M/kijiji usikatishwe tamaa, songa mbele. Count this as a challenge for your work.

ntamwita maana na yeye kazidi kuwa biase, mtu kama yeye alitegemewa awe makini kabla ya kuleta news, sasa ikiwa anakuwa hivi ni rahisi kumjua yuko vipi.

yeye kukurupuka na kuleta udaku huu ni hatari kwa taifa, na hatari kwa yeye mwenyewe.

changamoto nnayoitoa mkjj awe makini zaidi na aache umame mame wa machuchu mane
 
ntamwita maana na yeye kazidi kuwa biase, mtu kama yeye alitegemewa awe makini kabla ya kuleta news, sasa ikiwa anakuwa hivi ni rahisi kumjua yuko vipi.

yeye kukurupuka na kuleta udaku huu ni hatari kwa taifa, na hatari kwa yeye mwenyewe.

changamoto nnayoitoa mkjj awe makini zaidi na aache umame mame wa machuchu mane

mwanamme una mambo wewe! Hivi ni lini Mwanakjj alifanya jambo likakuridhisha? Ungejua ile taarifa alivyoileakisha mzee wetu humu iliharibu mambo vibaya sana. Kosa la mwanakijiji ni kuweka hadharani maamuzi ya kikao kabla hayajatamkwa hadharani. Ndio maana Mwanri alipotokea kesho yake alisema maneno haya:

"Tunasisitiza kwamba viongozi hao bado ni watuhumiwa, siyo wakosaji ndio maana wanaendelea na nyadhifa zao za ubunge,"

Hivi kwanini unafikiri walisema "wanasisitiza" kwani nani aliyesema wametoswa? kabla ya kuandikwa hapa JF. Sisi tuliobahatika kuwa maeneo ya kikao cha Kamati Kuu, uamuzi wa kwanza jioni ile ulikuwa ni kuwavua uanachama, habari hiyo ikavuja, na kama mwanakijiji asingeiweka hapa bila ya shaka ingetangazwa kesho yake na Mwanri. Kwa wakijiji kuiweka hapa, amewasaidia CCM na kuumbuka.

Mwanakijiji aendeleza kazi kaka, influence yako ni kubwa kuliko hawa wanavyodhani.

Asante!!
 
Uamuzi wa kumvua mwanachama uanachama wake ni ni pendekezo la Shina pamoja na Tawi kitu ambacho sidhani kama kitafanyika kwa Elissa na mwenziwe.
Tukubaliane na Mwanri kuwa chama kiendelee na shughuli zake na hao jamaa kama wataachiwa huru sheria na kanuni zinazoiongoza CCM wazitumie ktk kudai haki yao ktk chama chao
 
Back
Top Bottom