CCM yatoa kadi kwa wanafunzi wa sekondari

Junior. Cux

JF-Expert Member
Feb 3, 2011
5,319
3,767
CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM), Kimeanza staili mpya ya kujijenga kwa wanafunzi wa shule za sekondari huku makamu mwenyekiti wake, pius msekwa akidai kwamba chama cha upinzani cha chadema kimeanzisha mtandao wa wanafunzi wa vyuo vikuu.
msekwa alidai kwamba mtandao wa jamii forums unamilikiwa na vijana wa chadema ambao kila mara wanautumia katika kuchochea vurugu na maandamano yasiyo na msingi.
juzi CCM kilikaribisha idadi kubwa ya wanafunzi kutoka shule ya sekondari ya central iliyopo mita chache kutoka ofisi yake ya makao makuu mjini hapa ambako walikula kiapo cha utii kwa chama hicho na kisha kupewa kadi za uanachama.
katika mkutano huo, CCM kilitangaza kuingiza jumla ya wanachama 670 na katika msururu mrefu uliopita mbele ya msekwa kupokea kadi, alikuwepo mtu mzima mmoja huku idadi yote ikiwa ni ya wanafunzi. Hata hivyo baadhi ya wanafunzi waliohojiwa walieleza kukerwa kwao na hatua hiyo, "sisi tuliambiwa asubuhi kuwa tuje huku CCM kuchukua kadi na tulipomaliza mitihani majira ya saa sita mchana tukakalishwa hadi saa tisa alasiri ndipo tunaletwa" alisema mmoja wa wanafunzi ambaye hakutaka kutaja jina lake...
source: mwananchi j1
 
Sasa yale majigambo jk kuwa wanrudi na utaratibu wa zamani imekuwaje? Lakini nadhaniwanataka kujianda ua uchaguzi ndani ya chama 2012
 
Hiyo ya kutoa kadi kwenye shule za sekondary mbona kawaida sana kwa ccm. We uliza wanafunyi washule za jumuiya ya wazaz ccm kama Vile Sangu high school, Meta sec,Mbalizi sec, Ivumwe kadi zinatolewa hadi kwa watoto wa kidato cha kwanza wanafunzi wakiwa shuleni ni lazima waimbe nyimbo za ccm ucpoimba shule huna au utapewa bakora zakutosha kukudispln
 
Wanamdanganya nani sasa?? Ninachofurahi ni kwamba kwa hali hiyo, inazidi kidhihirisha kuwa CCM ni chama kisichoenda na alama za nyakati bado kimejikita kwenye ukomonisti wa kale kwamba mbinu yao kubwa ni PROPAGANDA tu.....!
 
Haa yaani wale watu 600 wanachama wa chadema aliowataja dwani nape kumbe ni wanafunzi kaaazi kweli kweli na je wanauhakika ni waumini wa kweli au ni magumashi!!!!!!!!!!!!
 
Haa yaani wale watu 600 wanachama wa chadema aliowataja dwani nape kumbe ni wanafunzi kaaazi kweli kweli na je wanauhakika ni waumini wa kweli au ni magumashi!!!!!!!!!!!!

ni wanafunzi alafu asilimia kubwa ni under 18 sa hizo siasa mpka kwa watoto za nini.. wanachukua kadi kwa kulazimishwa lakin chadema ndo chaguo lao na hzo ela zao wanazogawa watazila sana na hakuna mabadiliko.
 
CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM), Kimeanza staili mpya ya kujijenga kwa wanafunzi wa shule za sekondari huku makamu mwenyekiti wake, pius msekwa akidai kwamba chama cha upinzani cha chadema kimeanzisha mtandao wa wanafunzi wa vyuo vikuu.
msekwa alidai kwamba mtandao wa jamii forums unamilikiwa na vijana wa chadema ambao kila mara wanautumia katika kuchochea vurugu na maandamano yasiyo na msingi.
juzi CCM kilikaribisha idadi kubwa ya wanafunzi kutoka shule ya sekondari ya central iliyopo mita chache kutoka ofisi yake ya makao makuu mjini hapa ambako walikula kiapo cha utii kwa chama hicho na kisha kupewa kadi za uanachama.
katika mkutano huo, CCM kilitangaza kuingiza jumla ya wanachama 670 na katika msururu mrefu uliopita mbele ya msekwa kupokea kadi, alikuwepo mtu mzima mmoja huku idadi yote ikiwa ni ya wanafunzi. Hata hivyo baadhi ya wanafunzi waliohojiwa walieleza kukerwa kwao na hatua hiyo, "sisi tuliambiwa asubuhi kuwa tuje huku CCM kuchukua kadi na tulipomaliza mitihani majira ya saa sita mchana tukakalishwa hadi saa tisa alasiri ndipo tunaletwa" alisema mmoja wa wanafunzi ambaye hakutaka kutaja jina lake...
source: mwananchi j1

Wale wote wana miaka 18 na zaidi , ni haki yao and its nice move kwa kuwaangalia wanafunzi hao
 
Wale wote wana miaka 18 na zaidi , ni haki yao and its nice move kwa kuwaangalia wanafunzi hao

kwanza namashaka na jina lako, halikufai ata kidogo... Wanafunzi wanakosa walimu na nyenzo za kufundishiwa afu stil unawabebesha mzigo wa siasa tena kwenye chama cha mafisadi kama hicho 2takua 2najenga taifa gan.? Alafu usidhani kipindi hiki ndo kama enzi zenu mlivyokua mnasoma watu mnamaliza mkiwa mshaoa sa hivi vijana miaka 17 kamalza form 4
 
acha wajifariji wanawapa wanafunzi wa sekondari wasiojua lolote tena kwa lazima,wakikua wote wanarudi upinzani.Wote wale walivyoonekana gazetini ni U-18,hakika ccm kwishina
 
Propaganda ni sehemu muhimu ya siasa, haikwepeki. Chadema wanahitaji kufanyia kazi jambo hili kwa sababu, kwanza, ni kinyume cha sheria kushirikisha watoto wadogo kwanye siasa, lakini pia, ni mtaji wa kisiasa kwa Chadema. Viongozi wa Chadema Dodoma wakusanye ushahidi madhubuti (ni rahisi kuupata kwakuwa, nina uhakika, wanafunzi hao hawakupokea kadi kwa utashi wao, hivo ni wazi watatoa ushirikiano). Kisha kwa kutumia ushahidi huo wawasilishe malalamiko kwa msajili wa vyama vya siasa. Lakini kwakuwa msajili wa vyama vya siasa hafanyi kazi kwa usawa, hivyo hatachukua hatua yoyote ya maana dhidi ya CCM, Chadema waitishe mkutano na wanahabari na kuuambia umma juu ya upuuzi huu.

CCM wameshazoea kufanya vitendo hivi. Nakumbuka wakati wa uchaguzi wa nafasi za wagombea ubunge ndani ya CCM huko Manyara/Arusha??, mgombea mmoja ambaye alikuwa ni kigogo (waziri) ndani ya serikali, aliwapa kadi bandia wanafunzi wa sekondari na wakampigia kura na akashinda. Hata hivyo, kwa nguvu za haki, mgombea huyo alipigwa chini na mgombea wa Chadema katika uchaguzi mkuu.

Mimi nilipomaliza kidato cha sita, nilifundisha katika shule moja ya Jumuiya ya Umoja wa Wazazi ya CCM. Kama ilivo ada, nililazimishwa kuwa mwanachama wa jumuiya hiyo (wakati mimi sikuwa mzazi) kwa kupewa kadi (sikumbuki hiyo kadi iko wapi sasa). HIvyo, madhambi haya yanaendelea ndani ya CCM na ndio maana chama hiki hakiwezi kupata uhai tena, zaidi ya huu uliopo kuendelea kuporomoka.

Hatua za dhati zinahitajika kukinusuru chama hiki. Mambo yanayofanywa sasa, eti kuwapa mafisadi siku 90, ni masihara makubwa. Tangu lini wahalifu wakapewa muda? Kama kweli CCM wana nia ya dhati kujisafisha, wanapaswa kuwavua uanachama wanachama wake wote ambao wanawafahamu kuwa wanakiondolea haiba chama chao.

CAG aefichua ubadhilifu mkubwa serikali kuu na za mitaa. Hakuna kinachofanyika. Nilitarajia, leo hii, huko mawizarani na kwenye halmashauri kuwe hakukaliki kwa wahalifu hawa kufukuzwa kazi na kufikishwa mahakamani. Lkn kwa serikali ya CCM hilo haliwezi kufanyika.
 
Naikumbuka kauli hii ya JK alipokuja Udom kuzindua chuo:-Siasa haitakiwi mashuleni na vyuoni sa kutokana na kauli iyo leo P. Msekwa anagawa kadi kwa wanafunzi wa sekondari kwa upande wangu ccm imepoteza mwelekeo.
 
Back
Top Bottom