Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Unapokuwa umemaliza kupiga kura yako unaishia kwenda nyumbani ukifikiri ya kuwa mshindi atapatikana kutokana na kura zilizomo kwenye sanduku la mahesabu ya kupigia kura. I MUST SAY, IT IS A WRONG ANSWER.
Kwa CCM, kura zinaanza kupigwa baada ya mpiga kura wa mwisho kuainisha matakwa yake na kuishia kwani ushindi huwa unapangwa mezani. Katika chaguzi ndogo kama nne zilizohusisha Bunge lililomaliza kipindi chake hivi NA MCHAKATO WA AWALI WA UCHAGUZI wa hivi karibuni tulijifunza yafuatayo:-
A) CCM kwa kuelewa ukapa wa vyama vya upinzani wapo tayari kuwanunua mawakala wao ili wabariki matokeo ambayo CCM wanayataka. Upo ushahidi wa kutosha wa mawakala kuingia mitini hususani baada ya uchaguzi kufanyika. Mawakala hawa hawapo hata tayari kutoa taarifa au kupeleka fomu za matokeo kwa viongozi wao kwa uhakiki wa ziada!
B) Katika kura za maoni za CCM zilizokwisha hivi punde tu tumejionea wenyewe rafu za waziwazi wagombea wakifanyiwa. Ngazi za juu zipo tayari kumzushia mtu siyo raia ili tu wampitishe mtu wao waliye na uhakika ni mbumbumbu ambaye baadaye atakuwa BW. au Bi. "YES" Bungeni. Kama CCM wapo tayari kufanyiana wao wenyewe unyama na hiyana je VYAMA VYA UPINZANI NA HUSUSANI CHADEMA SI WASUBIRI SHUBIRI TU?
C) Katika kura za ubunge wa chaguzi ndogondogo tumeshuhudia mawakala wa vyama vya upinzani wakikithiri kwa kulalama ya kuwa hawakuwa wamelipwa haki zao na vyama vya upinzani pengine kuchochea ukosefu wa uzalendo kwa vyama vyao pale ambapo CCM wanawadobosha na mapesa wakati wa kuhesabu kura. Kama vyama vya upinzani, havikuwa na bajeti stahili ya kuwatuliza mawakala wao katika chaguzi ndogo je mahitaji ya bajeti ya malipo ya kuwalipa mawakala wote katika uchaguzi mkuu watahimili vishindo?
D) Katika zoezi la kusaili wagombea tumejionea wenyewe jinsi viongozi wa halmashauri ambao ndiyo watendaji serikalini wanavyopewa madaraka na NEC isivyo halali kuwa makamisaa wa uchaguzi na jinsi wanavyozitumia nafasi hizo katika kuwang'oa wapinzani kwenye kinyang'anyiro na hivyo kuwanyima wapiga kura haki yao ya kikatiba ya kupiga kura. Hali hii itachachamaa zaidi kwenye uchaguzi mkuu, kwa sababu NEC kwa makusudi mazima itaendelea kuwatumia vibosile wa halmashauri kama makamisaa!!!!!!!!!
D) CCM imekuwa ikisaidiwa na misamaha haramu ya kodi inayozidi Bilioni 700 kwa mwaka hususani kwenye eneo la madini. Shehemu kubwa ya ulaji huu kazi yake kubwa siyo kusomesha watoto bure. La hasha. Siyo kutoa tiba bure . La hasha... bali ni kuwarubuni mawakala wa upinzani ili washinde chaguzi.
E) CCM imewalipa waalimu tu nyongeza za mishahara kwa kuelewa ndiyo watakaohusika katika kuhesabu kura. Wafanyakazi wengine wa umma wametekelezwa kwa vile mchango wao zaidi ya kupiga kura ambazo CCM wana uhakika watazichakachua watakavyo unabezwa katika kufanikisha azma ya CCM ya ushindi wa Tsunami. Waalimu hawa ndiyo CCM inawategema wawatunzie siri ya uchakachuaji wa matokeo kwa vile kura zinahesabiwa kama njugu na wala siyo kwa kompyuta. Waalimu ambao pamoja na nyongeza ya mshahara kiduchu bado watawakarimu CCM ili wapate fungu la BINGO la ghafla siku ya kuhesabu kura......
F) Kutokana na mapungufu ya NEC, CCM imechapisha au kupewa nakala za kutosha na NEC za fomu za kujaza matokeo wayatakayo. Ungefikiria ya kuwa taifa ambalo lisilo la "wahuni" fomu za kujaza matokeo ya uhesabuji wa kura zingekuwa zimetengenezwa kwa gharama kubwa ili kuzuia uchakachuaji lakini CCM na NEC wao kwa kuelewa wanachotaka kukifanya fomu hizo mtu yoyote tu aweza kuzichapisha na hivyo kutanua mianya ya uchakachuaji wa matokeo.
G) Ikumbukwe baadhi ya wagombea wa Chadema wa ngazi za Ubunge na udiwani hawakuchekechwa vizuri. Kama zoezi hili lingekuwa limefanyika kwa umakini pasingekuwepo mgombea amabaye anachukua fomu na kuipeleka CCM ambako anakatiwa dau la TSHS milioni mbili kwa mgombea udiwani na kati ya milioni THS 15 hadi 30 kwa mgombea ubunge ili kuwaachia mawaziri watese bila upinzani na kuashiria kukubalika feki kwa wakubwa hao kwenye majimbo yao. Hali ya dhuluma hii kwa wapiga kura itashamiri zaidi siku ya kupiga kura. Aidha kuwanunua wagombea walioangusha isivyo halali na kinyume na sheria kwa minajili ya kuwazuia kwenda mahakamani au kuwanunua hata wanasheria ambao watawategemea wagombea atjwa katika kuwasaidia mahakamani kwa kuwadai fedha ambazo wanajua hawawezi kuwa nazo. Na mbinu nyingine chafu hata zaidi ya hizo ili mradi kuzima vuguvugu au kuzipooza za kutaka mabadiliko ya mfumo wetu wa uendeshaji wa Nchi hii.
H) Ununuzi wa shahada za wapiga kura ambao CCM inauendesha Nchi nzima waashiria ya kuwa uchaguzi huu fedha ndizo zitamua CCM iendelee madarakani au hapana. Haya yote CCM inayafanya CCM ikielewa NEC iko upande wake. Aidha shahada hizo zitawazuia wapinzani kupiga kura au vilevile CCM itawatumia makada wake kuhakikisha inapiga kura mara mbilimbili. Yote haya ni dhuluma tu kwa Taifa hili.
Kutokana na changamoto hizi mkakati wa Chadema wa kuhakikisha inaibuka kidedea ni huu hapa:-
i) Hakikisha uteuzi wa mawakala unafanyika kwa uangalifu mkubwa ili kukwepa kupandikiziwa makada wa CCM ambao watasababisha kilio na kusaga meno.
ii) Hakikisha bajeti ya kutosha ipo na malipo ya mawakala yanafanywa na makao makuu ya Chadema bila ya kuwaachia wagombea ambao wengi wao ni hohehae kiuchumi.
iii) Kuanza kuchunguza uwezekano wa kisheria wa kuhesabu kura mara ya pili baada ya makamisaa kutangaza matokeo. Uhesabuji wa kura wa mara ya pili utakizima CCM milele. Na hapo tutaanza kuzungumzia utaratibu wa kisheria wa CCM kurudisha mali zote walizopora taifa hili ili zirudishwe kwa wamiliki halali: Wananchi. Baada ya hapo CCM kama ilivyo kwa Kanu hapo Kenya, UNIP kule Zambia na vyama vingine vilivyoleta uhuru kifo chao kitakuwa kimekamilika na taifa la pili la Tanzania litazaliwa.
i) Kuhamasisha raia wote kujitokea saa za jioni kwenye vituo vyao vya kupiga kura ili kuhamasisha mawakala, kushinikiza na kuhakikisha haki itendeke na ionekane ikitendeka.
Taifa la pili kuzaliwa kutaanza na siyo mara baada ya kuchimbwa kwa kaburi la CCM bali baada ya kuhakikisha hata mizimu yake yote ya CCM imefukiwa kilometa nzima ndani ya kaburi lake.
AMA KWELI '"YOTE YAWEZEKANA BILA YA CCM"
Kwa CCM, kura zinaanza kupigwa baada ya mpiga kura wa mwisho kuainisha matakwa yake na kuishia kwani ushindi huwa unapangwa mezani. Katika chaguzi ndogo kama nne zilizohusisha Bunge lililomaliza kipindi chake hivi NA MCHAKATO WA AWALI WA UCHAGUZI wa hivi karibuni tulijifunza yafuatayo:-
A) CCM kwa kuelewa ukapa wa vyama vya upinzani wapo tayari kuwanunua mawakala wao ili wabariki matokeo ambayo CCM wanayataka. Upo ushahidi wa kutosha wa mawakala kuingia mitini hususani baada ya uchaguzi kufanyika. Mawakala hawa hawapo hata tayari kutoa taarifa au kupeleka fomu za matokeo kwa viongozi wao kwa uhakiki wa ziada!
B) Katika kura za maoni za CCM zilizokwisha hivi punde tu tumejionea wenyewe rafu za waziwazi wagombea wakifanyiwa. Ngazi za juu zipo tayari kumzushia mtu siyo raia ili tu wampitishe mtu wao waliye na uhakika ni mbumbumbu ambaye baadaye atakuwa BW. au Bi. "YES" Bungeni. Kama CCM wapo tayari kufanyiana wao wenyewe unyama na hiyana je VYAMA VYA UPINZANI NA HUSUSANI CHADEMA SI WASUBIRI SHUBIRI TU?
C) Katika kura za ubunge wa chaguzi ndogondogo tumeshuhudia mawakala wa vyama vya upinzani wakikithiri kwa kulalama ya kuwa hawakuwa wamelipwa haki zao na vyama vya upinzani pengine kuchochea ukosefu wa uzalendo kwa vyama vyao pale ambapo CCM wanawadobosha na mapesa wakati wa kuhesabu kura. Kama vyama vya upinzani, havikuwa na bajeti stahili ya kuwatuliza mawakala wao katika chaguzi ndogo je mahitaji ya bajeti ya malipo ya kuwalipa mawakala wote katika uchaguzi mkuu watahimili vishindo?
D) Katika zoezi la kusaili wagombea tumejionea wenyewe jinsi viongozi wa halmashauri ambao ndiyo watendaji serikalini wanavyopewa madaraka na NEC isivyo halali kuwa makamisaa wa uchaguzi na jinsi wanavyozitumia nafasi hizo katika kuwang'oa wapinzani kwenye kinyang'anyiro na hivyo kuwanyima wapiga kura haki yao ya kikatiba ya kupiga kura. Hali hii itachachamaa zaidi kwenye uchaguzi mkuu, kwa sababu NEC kwa makusudi mazima itaendelea kuwatumia vibosile wa halmashauri kama makamisaa!!!!!!!!!
D) CCM imekuwa ikisaidiwa na misamaha haramu ya kodi inayozidi Bilioni 700 kwa mwaka hususani kwenye eneo la madini. Shehemu kubwa ya ulaji huu kazi yake kubwa siyo kusomesha watoto bure. La hasha. Siyo kutoa tiba bure . La hasha... bali ni kuwarubuni mawakala wa upinzani ili washinde chaguzi.
E) CCM imewalipa waalimu tu nyongeza za mishahara kwa kuelewa ndiyo watakaohusika katika kuhesabu kura. Wafanyakazi wengine wa umma wametekelezwa kwa vile mchango wao zaidi ya kupiga kura ambazo CCM wana uhakika watazichakachua watakavyo unabezwa katika kufanikisha azma ya CCM ya ushindi wa Tsunami. Waalimu hawa ndiyo CCM inawategema wawatunzie siri ya uchakachuaji wa matokeo kwa vile kura zinahesabiwa kama njugu na wala siyo kwa kompyuta. Waalimu ambao pamoja na nyongeza ya mshahara kiduchu bado watawakarimu CCM ili wapate fungu la BINGO la ghafla siku ya kuhesabu kura......
F) Kutokana na mapungufu ya NEC, CCM imechapisha au kupewa nakala za kutosha na NEC za fomu za kujaza matokeo wayatakayo. Ungefikiria ya kuwa taifa ambalo lisilo la "wahuni" fomu za kujaza matokeo ya uhesabuji wa kura zingekuwa zimetengenezwa kwa gharama kubwa ili kuzuia uchakachuaji lakini CCM na NEC wao kwa kuelewa wanachotaka kukifanya fomu hizo mtu yoyote tu aweza kuzichapisha na hivyo kutanua mianya ya uchakachuaji wa matokeo.
G) Ikumbukwe baadhi ya wagombea wa Chadema wa ngazi za Ubunge na udiwani hawakuchekechwa vizuri. Kama zoezi hili lingekuwa limefanyika kwa umakini pasingekuwepo mgombea amabaye anachukua fomu na kuipeleka CCM ambako anakatiwa dau la TSHS milioni mbili kwa mgombea udiwani na kati ya milioni THS 15 hadi 30 kwa mgombea ubunge ili kuwaachia mawaziri watese bila upinzani na kuashiria kukubalika feki kwa wakubwa hao kwenye majimbo yao. Hali ya dhuluma hii kwa wapiga kura itashamiri zaidi siku ya kupiga kura. Aidha kuwanunua wagombea walioangusha isivyo halali na kinyume na sheria kwa minajili ya kuwazuia kwenda mahakamani au kuwanunua hata wanasheria ambao watawategemea wagombea atjwa katika kuwasaidia mahakamani kwa kuwadai fedha ambazo wanajua hawawezi kuwa nazo. Na mbinu nyingine chafu hata zaidi ya hizo ili mradi kuzima vuguvugu au kuzipooza za kutaka mabadiliko ya mfumo wetu wa uendeshaji wa Nchi hii.
H) Ununuzi wa shahada za wapiga kura ambao CCM inauendesha Nchi nzima waashiria ya kuwa uchaguzi huu fedha ndizo zitamua CCM iendelee madarakani au hapana. Haya yote CCM inayafanya CCM ikielewa NEC iko upande wake. Aidha shahada hizo zitawazuia wapinzani kupiga kura au vilevile CCM itawatumia makada wake kuhakikisha inapiga kura mara mbilimbili. Yote haya ni dhuluma tu kwa Taifa hili.
Kutokana na changamoto hizi mkakati wa Chadema wa kuhakikisha inaibuka kidedea ni huu hapa:-
i) Hakikisha uteuzi wa mawakala unafanyika kwa uangalifu mkubwa ili kukwepa kupandikiziwa makada wa CCM ambao watasababisha kilio na kusaga meno.
ii) Hakikisha bajeti ya kutosha ipo na malipo ya mawakala yanafanywa na makao makuu ya Chadema bila ya kuwaachia wagombea ambao wengi wao ni hohehae kiuchumi.
iii) Kuanza kuchunguza uwezekano wa kisheria wa kuhesabu kura mara ya pili baada ya makamisaa kutangaza matokeo. Uhesabuji wa kura wa mara ya pili utakizima CCM milele. Na hapo tutaanza kuzungumzia utaratibu wa kisheria wa CCM kurudisha mali zote walizopora taifa hili ili zirudishwe kwa wamiliki halali: Wananchi. Baada ya hapo CCM kama ilivyo kwa Kanu hapo Kenya, UNIP kule Zambia na vyama vingine vilivyoleta uhuru kifo chao kitakuwa kimekamilika na taifa la pili la Tanzania litazaliwa.
i) Kuhamasisha raia wote kujitokea saa za jioni kwenye vituo vyao vya kupiga kura ili kuhamasisha mawakala, kushinikiza na kuhakikisha haki itendeke na ionekane ikitendeka.
Taifa la pili kuzaliwa kutaanza na siyo mara baada ya kuchimbwa kwa kaburi la CCM bali baada ya kuhakikisha hata mizimu yake yote ya CCM imefukiwa kilometa nzima ndani ya kaburi lake.
AMA KWELI '"YOTE YAWEZEKANA BILA YA CCM"