Drifter
JF-Expert Member
- Jan 4, 2010
- 4,428
- 4,127
Haya ndio majibu yanayotakiwa kutoka kwa kiongozi Mzanzibar ambaye ni mjumbe wa baraza la Mapinduzi, na sii kuendelea kutukashifu kana kwamba sisi Wabara hatumtegemei Allah ktk matatizo yetu. Kusema kweli serikali lazima iwe makini sana na haya makundi ya hizi jumuiya za madhehebu ya dini yanayojitokeza kuchochea serikali za ubaguzi na hata kuzikosoa imani za dini kwa matakwa ya tafsiri zao wenyewe.
Ingekuwa rahisi kwa serikali kudhibiti ujinga huo kama nayo ingekuwa "innocent" kuhusu kuwepo kwa makundi ya aina hiyo. Bila shaka si vigumu kugundua kwamba "jumuiya" za aina hiyo hazijazuka na kushamiri hivihivi tu; ni mkakati mahsusi wa kisiasa wa baadhi ya watawala ndani ya serikali. SASA, ama waamue kwa dhati kurejesha akili zao walizoziweka pembeni au wabakie kusubiri mavuno tu - na wasijaribu kuyakana hesabu ikitimia!