babukijana
JF-Expert Member
- Jul 21, 2009
- 13,102
- 15,993
MAAMUZI yaliyopitishwa wiki hii na Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika kuwadhibiti wanachama, hususani Wabunge wake ambao wamekuwa msitari wa mbele katika kukipaka matope chama hicho, yanahitaji kupongezwa kwa nguvu zote na wanachama wengine wote walio na nia ya kuhakikisha chama hicho kinaendelea kuiongoza nchi yetu. Wabunge na wanachama hao wamekuwa msitari wa mbele katika kuendeleza makelele ya wapinzani kuhusiana na vitendo vya ufisadi vya watu wachache walio ndani ya chama hicho, bila kujua kwamba chama kina mikakati gani ya kupambana na watu hao ambao wamekwenda kinyume na maadili yake!
Wamesahau kabisa kwamba cha kuandamwa hapa ni watu wenyewe binafsi na si sera au mfumo wa CCM ambao unajulikana kabisa katika kupiga vita uovu wowote ndani ya chama na katika jamii ambayo inaongozwa na serikali yake.
Kwa kifupi, wanachama hao wamekuwa wakinyea kwenye mkeka ambao wanaulalia na ambao wataendelea kuulalia!
Katika mazingira ya sasa ambayo ni ya ushindani wa kisiasa, ni bora wanachama wa CCM wakatambua mfumo uliopo unaotumiwa katika kukosoana miongoni mwa wanachama wake. Na watambue kwamba katika mfumo wa vyama vingi, siasa imekuwa sawa na soko huria. Soko huria kwa maana kwamba vyama vina sera zake na namna ya kuendesha si mapambano yake tu bali na namna ya kujihami.
Hivyo, Wabunge wa CCM na wanachama wengine ambao wamekuwa wakiiyumbisha serikali yao kwa makusudi au bila kujua, wafahamu wamekuwa wakifanya hivyo kwa faida ya vyama vya upinzani na kwa hasara ya CCM!
Tabia ya kusema hadharani kauli zenye kukivunjia hadhi chama chao – badala ya vikao husika vyenye lengo la kukosoana na kuwekana sawa – ni ukiukaji wa kanuni zinazoongoza nidhamu ya chama, hulka ambayo ikiachwa kuendelea, itakiangamiza chama.
Ikumbukwe kwamba CCM ndicho kilichowafikisha mahali walipo watu ambao wanakishambulia kutoka ndani yake. Na pia lazima wafahamu kwamba hakuna chama au kikundi chochote ambacho wanachama wake hawana dhambi au madhambi yoyote!
Pia ni muhimu kufahamu kwamba chama ni kama familia moja ambayo ina kiongozi wake na mfumo maalum wa kutatua matatizo yake.
Ni tabia mbaya ndugu wa familia moja kusaidia kufichua siri au matatizo ya ndani ya familia, hata kama watu wa nje tayari wanayaelewa. Kufanya hivyo, ni kuidhalilisha zaidi familia, na anayefanya hivyo lazima afahamu anajidhalilisha na yeye pia kwani ni lazima atakuwa ameshiriki kwa namna fulani katika kuibuka kwa matatizo ya familia hiyo.
Na dawa ya kumaliza matatizo ya ndani ya familia, ni kwa familia yenyewe kukaa na kuyajadili na kuyapatia mwafaka badala ya kuwasaidia watu wa nje kuyafahamu zaidi, kwani maadui zao wanaweza kuyatumia kuifarakanisha zaidi familia hiyo.
Kwa kweli, kitendo cha kuwaunga mkono wapinzani katika kukipiga vita Chama Cha Mapinduzi ni usaliti wa wazi wa kutoa siri za matatizo ya familia kwa watu wa nje.
Kitu muhimu kwa kila mwanachama wa CCM ni kufahamu kwamba kutoa siri yoyote ya ndani na kuipeleka mitaani ni jambo la madhara makubwa kwani likikosa ufumbuzi kwa kuzidiwa na fedheha matokeo yake ni kufarakanika kwa familia.
Jambo la kuzingatia ni kwamba kama kweli wanachama wa CCM wanaamini kwamba kuyatoa matatizo ya ndani na kuyapeleka mitaani ndiyo ufumbuzi wa matatizo hayo, ni bora wakajiunga na vyama vya upinzani ambavyo vimeyashikilia bango matatizo binafsi ya baadhi ya wanachama wa CCM.
Na ni vyema wakafanya hivyo mapema!
******************
Wamesahau kabisa kwamba cha kuandamwa hapa ni watu wenyewe binafsi na si sera au mfumo wa CCM ambao unajulikana kabisa katika kupiga vita uovu wowote ndani ya chama na katika jamii ambayo inaongozwa na serikali yake.
Kwa kifupi, wanachama hao wamekuwa wakinyea kwenye mkeka ambao wanaulalia na ambao wataendelea kuulalia!
Katika mazingira ya sasa ambayo ni ya ushindani wa kisiasa, ni bora wanachama wa CCM wakatambua mfumo uliopo unaotumiwa katika kukosoana miongoni mwa wanachama wake. Na watambue kwamba katika mfumo wa vyama vingi, siasa imekuwa sawa na soko huria. Soko huria kwa maana kwamba vyama vina sera zake na namna ya kuendesha si mapambano yake tu bali na namna ya kujihami.
Hivyo, Wabunge wa CCM na wanachama wengine ambao wamekuwa wakiiyumbisha serikali yao kwa makusudi au bila kujua, wafahamu wamekuwa wakifanya hivyo kwa faida ya vyama vya upinzani na kwa hasara ya CCM!
Tabia ya kusema hadharani kauli zenye kukivunjia hadhi chama chao – badala ya vikao husika vyenye lengo la kukosoana na kuwekana sawa – ni ukiukaji wa kanuni zinazoongoza nidhamu ya chama, hulka ambayo ikiachwa kuendelea, itakiangamiza chama.
Ikumbukwe kwamba CCM ndicho kilichowafikisha mahali walipo watu ambao wanakishambulia kutoka ndani yake. Na pia lazima wafahamu kwamba hakuna chama au kikundi chochote ambacho wanachama wake hawana dhambi au madhambi yoyote!
Pia ni muhimu kufahamu kwamba chama ni kama familia moja ambayo ina kiongozi wake na mfumo maalum wa kutatua matatizo yake.
Ni tabia mbaya ndugu wa familia moja kusaidia kufichua siri au matatizo ya ndani ya familia, hata kama watu wa nje tayari wanayaelewa. Kufanya hivyo, ni kuidhalilisha zaidi familia, na anayefanya hivyo lazima afahamu anajidhalilisha na yeye pia kwani ni lazima atakuwa ameshiriki kwa namna fulani katika kuibuka kwa matatizo ya familia hiyo.
Na dawa ya kumaliza matatizo ya ndani ya familia, ni kwa familia yenyewe kukaa na kuyajadili na kuyapatia mwafaka badala ya kuwasaidia watu wa nje kuyafahamu zaidi, kwani maadui zao wanaweza kuyatumia kuifarakanisha zaidi familia hiyo.
Kwa kweli, kitendo cha kuwaunga mkono wapinzani katika kukipiga vita Chama Cha Mapinduzi ni usaliti wa wazi wa kutoa siri za matatizo ya familia kwa watu wa nje.
Kitu muhimu kwa kila mwanachama wa CCM ni kufahamu kwamba kutoa siri yoyote ya ndani na kuipeleka mitaani ni jambo la madhara makubwa kwani likikosa ufumbuzi kwa kuzidiwa na fedheha matokeo yake ni kufarakanika kwa familia.
Jambo la kuzingatia ni kwamba kama kweli wanachama wa CCM wanaamini kwamba kuyatoa matatizo ya ndani na kuyapeleka mitaani ndiyo ufumbuzi wa matatizo hayo, ni bora wakajiunga na vyama vya upinzani ambavyo vimeyashikilia bango matatizo binafsi ya baadhi ya wanachama wa CCM.
Na ni vyema wakafanya hivyo mapema!
******************