CCM yamwangukia Bashe!

msivipe umaarufu usiostahili hivi vifisadi vidogo! kuna mambo ya muhimu ya kuzungumzia kuhusu mustakabali wa nchi...simple minds?
 
Katika kile ambacho hadi sasa sijakipatia majibu ni pale nilipo mshuhudia Hussen Bashe muda kati ya saa 10-11 jioni akiwa katika ofisi za IPP na baadae alionekana aki ongea kwa muda mrefu sana na Mhariri wa Nipashe Je si hatari hiyo? mahusiano ya Bashe na IPP yameanza lini?

Kwani kufika Ofisi za IPP ni kosa kisharia?. Au kuongea na mhariri ni dhambi?
 
miongoni mwa maadili ya wandishi w habari ni kutokumhusisha mtu na maovu ya ndugu zake. ukiwa fisadi wewe itakuwa makosa kumzomea mtoto wako, mke wako, hawara wako, baba yako, mama yako na rafiki yako.

hawa watu wenye uhusiano nawe watazomewa tu au kuhusishwa na nawe kama wanashirikiana nawe katika ufisadi huo. ndiyo maana sisi wengine tulilaani sana ilipoandikwa habari magazetini kuwa hakimu ambaye ni mtoto wa makamba afukuzwa kazi kwa ulevi. ilitakiwa kuandika kuwa hakimu fulani wa mahakama fulani kafukuzwa kazi kwa ulevi, fulustopu.

na katika hili la husseni basha kutembelea ipp nasema ni kosa kumfuatilia mtu nyendo zake eti kwa sababu tu ana uhusiano wa damu na fisadi mmoja maarufu nchini anayeshusishwa na kashfa za richmond, dowans na epa (kagoda farms) mtu anayedaiwa kuwa kingmaker katika politics za tanzania.

sisi tumzomee yeye tu huyo fisadi ambaye serikali haitaki kumgusa lakini ndugu zake, watoto wake, wake zake, hawara zake, marafiki zake na jamaa zake tusiwabughudhi kwani ni watz wenzetu wanaotafuta kula kama sisi na wao wana haki za kikatiba kukutana na mtu yeyote, kwenda popote almradi hawavunji sheria.
lovulovu
 
Hao ndio wasiopenda maendeleo ya watu na kwa taarifa yako unadhalilisha mpaka kampuni ya ipp sasa kila anayesoma hii kesho akienda ipp hatokuwa free tena mnaweza hata kumpiga picha muziweke hapa muanzishe mambo yenu na kama hii habari umerushiwa ili uje kuweka hapa unatakiwa ujue hao sio maadui ni watu wanaojuana toka siku nyingi ni wewe tu na umasikini wako unaokusumbua wa fikra mgando
 
Katika kile ambacho hadi sasa sijakipatia majibu ni pale nilipo mshuhudia Hussen Bashe muda kati ya saa 10-11 jioni akiwa katika ofisi za IPP na baadae alionekana aki ongea kwa muda mrefu sana na Mhariri wa Nipashe Je si hatari hiyo? mahusiano ya Bashe na IPP yameanza lini?

Hakuna hatari yoyote ile. Hatari ni siku mafisadi watakapo fanikiwa kumuingiza bungeni! God forbid!! Atamuwakilisha nani? Mpaka sasa Hussein Bashe ni comoner ambaye hana hata hadhi ya kujadiliwa humu!

Cjui Mbongo anamuona tishio kwa misingi gani.
 
Jamani haina maana sana kusema eti watu watoke CCM kwa kuwa wamepingana na maamuzi au na utaratibu wa jinsi mambo yanavyoenda humo. Watu wenye Busara waliwahi kusema kuwa "Endapo yai litapasuka kwa kuanzia ndani, basi kiumbe huwa kimepata uhai, lakini kwa nje matokeo huweza kuwa tofauti, kwamba kiumbe kimepoteza uhai"...yaani yai hilo limevunjwa na nguvu zilizopo nje"

Wengine, kama Nape (I presume) pengine wanapenda kuleta mabadiliko kutokea ndani ya mfumo, wakati wengine kama Zitto wanaamini katika kubadili mambo kutoka nje! Mfumo uliopo unaweza kuwa na matatizo kidogo ambayo wapiganaji wanaamini katika kuyarekebisha na kuufanya uwe bora zaidi!

Naomba kuwasilisha,
Dk. Hamisi Kigwangalla.
 
Jamani haina maana sana kusema eti watu watoke CCM kwa kuwa wamepingana na maamuzi au na utaratibu wa jinsi mambo yanavyoenda humo. Watu wenye Busara waliwahi kusema kuwa "Endapo yai litapasuka kwa kuanzia ndani, basi kiumbe huwa kimepata uhai, lakini kwa nje matokeo huweza kuwa tofauti, kwamba kiumbe kimepoteza uhai"...yaani yai hilo limevunjwa na nguvu zilizopo nje"

Wengine, kama Nape (I presume) pengine wanapenda kuleta mabadiliko kutokea ndani ya mfumo, wakati wengine kama Zitto wanaamini katika kubadili mambo kutoka nje! Mfumo uliopo unaweza kuwa na matatizo kidogo ambayo wapiganaji wanaamini katika kuyarekebisha na kuufanya uwe bora zaidi!

Naomba kuwasilisha,
Dk. Hamisi Kigwangalla.

Mkuu,

Nadhani pamoja na mfumo kuwa na matatizo yake.Suala kubwa hapa ni strategy za wapinzani plus maandalizi hafifu ya wananchi katika elimu ya uraia

So,bado wapinzani hawajaweza kutumia mbinu nzuri katika uhamasishaji au kutumia mashirika yasiyo ya kiserikali katika kutoa elimu ya uraia

And another grave mistake,kutotumia nguvu zao ktk kuelekeza vuguvugu maeneo ya vijijini
 
Thread nyingine zimekaa kaa kama watu wanazitengeneza kujijengea majina JF. anyway JF is a good stepping up/ stepping down political tool.
 
Inasikitisha sana kuona CCM ya JK vyeo vyote sasa ni vya kujuana tu na wala sio uwezo wa mtu.

CCM ya Nyerere ilitafuta viongozi kutokana na uwezo wao hata kama hawakuwa na majina makubwa. Lakini leo hii ukiangalia mtu mzembe kama Rishard Bade ndio anayesukumwa (probably na EL, RA, Kinana) ili kukiongoza chama kikuu TZ.

Hii ni hatari. Tunakoelekea ni kubaya sana kama mabadiliko nchini au angalau ndani ya CCM hayatakuja mapema.
 
Naiheshimu sana forum hii kwani inasaidia kutoa mambo ambyo wakati mwingine hayasemwi na vyombo vingine.Nawashukuru kwa kunikaribisha, napokea kwa heshima kubwa karibu yenu wakubwa, naahidi ushirikiano mkubwa kwa kadri ya uwezo wangu wote.
SASA MAMBO MUHIMU TULIYOONGEA KATIKA KIPINDI CHA MLANGO WA DHARURA NI;

1). Niliunga mkono uteuzi wa wagombea kutoka Zanzibar kugombea Uenyekiti UVCCM. Baadhi ya sababu ni kuwa haya ni maamuzi ya kikao halali cha chama NEC, kwa kuzingatia kuwa hakuna uteuzi ambao usingekuwa na mapungufu, hata huu ninaouunga mkono una mapungufu yake mengi tu, lakini ukilinganisha na uteuzi mwingine kwa MTAZAMO WANGU huu ulikuwa nafuu kuliko mingine. Lakini nilikumbusha kuwa mwaka 2003 niligombea mimi uenyekiti uvccm na kulikuwa na wagombea toka znz ambao hawakurudishwa hivyo sioni sababu ya bara kulalamika leo.
2).Utendaji wa Makamba, nilichosema ni kuwa si dhambi kujadili utendaji wa Makamba kama katibu mkuu wa CCM, tena hata wanachama wa kawaida wana nwajibu wa kujadili hali ya chama chao, KWANI NAAMINI HICHI NI CHAMA CHA WANA CHAMA NA SI VIONGOZI. N a nikaongeza kuwa kikao chenye mamlaka ya kumwajibisha Katibu mkuu wa ccm ni NEC huu ndio utaratibu, hivyo hata baada ya kujadili mwisho lazima malalamiko yaletwe NEC ndo wanaweza kumwajibisha Katibu Mkuu.

3). Nikasema KUGOMBEA URAIS 2010 SI DHAMBI ni huru kwa mwana chama yeyote kwa mujibu wa katiba ya CCM ambayo ndio sheria mama, kwani hata ilani ya uchaguzi inatengenezwa mpya, hivyo sitashangaa kuona watu wanachukua fomu kuomba uteuzi, ndio demokrasia.

4). Nikasema pia si kweli kwamba wanaokosa wanakumbatiwa, inawezekana kwa upande mmoja lakini sio katioka kesi zote, nikatoa mfano wa waliowajibishwa kwa makosa ya Richmond, nikasema hawa walisaliti chama kwani tuliwatuma kutekeleza ilani ya chama wao wakaenda kutekeleza yao.

5.) Nikajibu swala la kufukuzwa uana chama uvccm, nikasema MWENYE AKILI NAJUA NANI MKWELI NANI MWONGO kwani UJENZI MPAKA SASA UNAENDELEA BILA MKATABA, MAPUNGUFU NILIYOYAELEZA NDIYO YALIYOUNDIWA TUME KUREKEBISHWA, SASA MWONGO NA MKWELI IKO WAZI, lakini najua mtu mzima kukiri kosa ni ngumu...maji marefu hapa kwa mzee wangu....

HAKIKA HATUKUMTAJA KABISA HUSSEIN BASHE KATIKA MAZUNGUMZO YOTE, SI MIMI, WALA OMARY KIMBAO AU JERRY SILAA NA HATA MTANGAZAJI KIBONDE, NIMESIKITISHWA NA TAARIFA HIZI KUZIKUTA HUKU, GAZETI LA TANZANIA DAIMA WALICHAPA PIA LAKINI KIMAKOSA, SIKUKANUSHA KULE COZ INGEATHIRI UCHAGUZI KWA UPANDE MMOJA NA HASA MGOMBEA MMOJA.

Namwomba ndugu yangu asituharibie heshima ya forum hii, naamini nimeeleza kwa kifupi yaliyotokea.
Nnauye Jr

OgwaluMapesa tumepata upande wa pili wa habari, tunaomba uthibitishe, habari yako umeipata wapi? Kuna kupingana sana kati ya post yako na habari ya jr. Ni vizuri kujua hali ilivyo maana uzushi JF si mzuri na sijui kama Mods wanaweza kufanya kitu kuzuia hali hii.
 
Inasikitisha sana kuona CCM ya JK vyeo vyote sasa ni vya kujuana tu na wala sio uwezo wa mtu.

CCM ya Nyerere ilitafuta viongozi kutokana na uwezo wao hata kama hawakuwa na majina makubwa. Lakini leo hii ukiangalia mtu mzembe kama Rishard Bade ndio anayesukumwa (probably na EL, RA, Kinana) ili kukiongoza chama kikuu TZ.

Hii ni hatari. Tunakoelekea ni kubaya sana kama mabadiliko nchini au angalau ndani ya CCM hayatakuja mapema.

Mkuu umeona jr amekanusha hapo chini, subira yavuta heri siku nyingine
 
Nape Jr: Sipendi kuchangia sana kwenye hoja hizi mnazolumbana hapa, maana nyingi zinahusu chama chenu, lakini nilitaka kusema kwamba you are incredibly convincing in your argument na inaonekana kumbe hata huko kwenye UVCCM kuna watu wanafikiri!!!

Maana wakati mwingine huwa tukisoma mawazo ya viongozi wenu tunasikitika sana, lakini kupitia thread hii umenitia moyo. Wakati mwingine watu mnaowaweka mbele kuwasemea wanawaaibisha na kuonekana kama vile katika UVCCM wote hamnazo!! Nakumbuka niliangalia mdahalo mmoja kati ya kiongozi wenu wa UVCCM (naomba nisimtaje jina) na Mnyika wa BAVICHA, ilikuwa aibu-ni kama vile Mnyika alikuwa anapambana na mtoto aliyetoka kufanya mtihani wa darasa la nne!

Great man, you certainly have a great future in Tanzanian politics. My only worry is that you may be in a place where you're slowly but surely eroding your potential instead of realising it-good if you realised this sooner than later-I may be wrong though! Read my article: CCM ya Nape ni nadharia...http://www.chadema.net/makala/mkumbo/kitila_18.html

Hivi Nape Nauye Jr alirudi tena kweli?
 
Kwa nini Nape asijiunge na chama kipya cha CCJ? Chama hicho kinasema kinahitaji watu waadilifu - wakweli katika dhamira na kauli zao kama Nape!
 
Asalaam alykum waungwana!

Husen au Hussein kama wengine wanavyopenda kumuita ni kijana anayejua kucheza karata zake japo si msafi na hafai kuwa Mbunge wa Nzega. Kiukweli hajatumwa na mtu japo wapo walio nyuma yake.

Bado nakusanya data zake na Muda si mrefu nitazitoa hewani. Ninawatafuta waliosoma nae wanipe vitu.
 
ZYANSIKU,
Sina shida Bashe katumwa na nani, japo naamini katumwa na dhamira yake mwenyewe kwanza. ILA WEWE ndo umetumwa na BASHE na Magazeti ya pale SInza Kijiweni. Usitake kutudanganya ku imply kuwa wewe ni mkazi wa Nzega mwongo mkubwa, wewe umeenda huko kwa kazi maalumu ya kuratibu kampeni za Bashe.

Kabla Bashe hajaanza harakati za ubunge ulikuwa hujafika Nzega sasa leo unajifanya ni mkazi wa huko? acha uongo huo- Next time nitakulipua au hujui mimi nina immunity hapa hata nikikutaja jina sitafungiwa kabisa- jiaangalie mwanawani................ (umeniudhi sana)
 
Nsoga,

Mimi nina shida sana ya kuuweka ukweli hewani. Na hujanielewa kabisa Bwana Ntambaswala. Sasa naanza kumbomoa kama ifuatavyo: -
1. Bashe ni raia wa Somalia na hajawahi kuwa raia wa Tanzania japo amesomeshwa na Tanzania kwa nia ya kurudi na kuungana na "alshabau". Hata baba yake ameukana uraia juzi tu. (namaanisha siku chanche zilizopita)
2. Kwa sababu hii hafai kuwa mgombea wa hata nyumba kumi kwani si Raia ngwanawane!!
3. Juzi alikuwa anahangaikia kuukana uraia wa Somalia lakini haitawezekana hata kama Rostam akimpa vijisenti.

Upo Hapo?

Nina usongo nae sana kesho nitakupa ukweli mwingine usioujua!!!!!!!!

Nadhani sasa tuko pamoja kwenye jahazi moja!
 
Back
Top Bottom