CCM yamwangukia Bashe!

Nnauye,
Ningependa nikurudishe nyuma kidogo,kwanza kabisa mimi sijui hizi kaiba za vyama ikiwemo ya ccm/umoja wa vijana.

Sasa nilitaka kujua hili la uchaguzi wa vijana,je kuna kalenda ambayo inaongoza hizi chaguzi au kuna utaratibu gani uliokuwepo ambao unaongoza hizi chaguzi.

Nina uliza hivi kwa sababu wewe binafsi swala la umri lilikuwa ajenda ktk kugombea moja ya nafasi ktk chama.

je kigezo cha umri kiaangaliwa siku ambayo uchaguzi utafanyika au siku ambayo fomu zinatolewa,hii ina maana hata kama uchaguzi utaahirishwa au kusogezwa mbele hauta hathiri umri wa mgombea.


Katibu Tarafa nashukuru kwa swali zuri.

CCM kama vyama vingine vya siasa kwa nchi yetu lazima viwe na katiba, hivyo CCM inatumia Katiba ya CCM ya Mwaka 1977 Toleo la 2007. Sasa ndani ya Katiba ya CCM kuna Jumuiya za Chama, ambazo ni VIJANA, UWT NA WAZAZI,sheria ya nchi hairuhusu Taasisi moja kuwa na Katiba mbili, hivyo hizi Jumuiya zinakuwa na KANUNI ukiacha UWT ambao wanakatiba...lakini kimakosa... jumuiya zingine zinaongozwa na KANUNI bila kuathiri Katiba ya Chama na nchi...

Swala la uchaguzi ni moja ya mambo yanayoelezwa kwenye kanuni za UVCCM. Sasa swala la umri limeanza siku nyingi kujadili umri wa kijana ni upi hasa, mpaka ilipoamuliwa kuwa sifa kubwa ya mwanachama wa UVCCM ni umri nao ni miaka13-35,kama ilivyo sifa ya mwanachama wa UWT ni jinsia yaani MWANAMKE.

Ni mimi nilyeanzisha mchakato huu mwaka 2003 wa kutaka tafsiri sahihi ya uanachama wa mwananchama wa UVCCM, HOJA ILIKUWA KAMA SIFA MOJA WAPO NI UMRI YAANI 13-35 UKIMRUHUSU MWANACHAMA WA MIAKA 32 KWA MFANO ACHAGULIWE KUWA KIONGOZI BAADA YA MIAKA 3 UANACHAMA WAKE UNAKOMA NA HIVYO ANAPOTEZA SIFA YA KUWA KIONGOZI KWANI SI MWANACHAMA.HIVYO LIKATOLEWA PENDEKEZO KUWA KILA ANAYEGOMBEA ASIWE AMEZIDI MIAKA 30 ILI ANAPOMALIZA AWE NDANI YA UMRI WA UANACHAMA WA UVCCM.

Mfano Nchimbi anatuongoza vijana akiwa si mwanachama wetu toka mwaka 2006, ni kinyume na sheria,mtu akienda mahakamani ni mgogoro mkubwa kwa taasisi.

-LILIPOKUJA SWALA LANGU-MIMI NIMEZALIWA TAREHE 07/11/1977,HIVYO MPAKA TAREHE 06/11/2008 MIMI NILIKUWA NA MIAKA 30 NA MIEZI KADHAA, NA KWAKUWA UCHAGUZI NI MCHAKATO/ PROCESS UNAANZA PALE UNAPOCHUKUA FOMU MPAKA SIKU UNAPOPIGIWA KURA NDIO MWISHO WA MCHAKATO. SASA NIMECHUKUA FOMU TAREHE 15/07/2008 NIKIWA NA MIAKA 30 NA MIEZI NA KWAKUWA UTARATIBU HUWA HATUHESABU MIEZI HIVYO KWA MUJIBU WA KANUNI UCHAGUZI UMEANZA MIE NIKIWA BADO NIMO NDANI YA KANUNI..

....na ndo maana baada ya kuona hoja ya umri haiuziki wakaja na hoja kunivua uanachama!! Kusema kweli ni kuigeuza siasa mchezo mchafu wakati haikupaswa kuwa hivyo...na wanajua nguvu waliyotumia kufika hapo walipo fikia.....

Nnauye Jr
 
Nape font size kubwa sana hiyo, inaumiza macho, tumia font 2 au 3 utaeleweka tu.
 
Katibu Tarafa nashukuru kwa swali zuri.

CCM kama vyama vingine vya siasa kwa nchi yetu lazima viwe na katiba, hivyo CCM inatumia Katiba ya CCM ya Mwaka 1977 Toleo la 2007. Sasa ndani ya Katiba ya CCM kuna Jumuiya za Chama, ambazo ni VIJANA, UWT NA WAZAZI,sheria ya nchi hairuhusu Taasisi moja kuwa na Katiba mbili, hivyo hizi Jumuiya zinakuwa na KANUNI ukiacha UWT ambao wanakatiba...lakini kimakosa... jumuiya zingine zinaongozwa na KANUNI bila kuathiri Katiba ya Chama na nchi...

Swala la uchaguzi ni moja ya mambo yanayoelezwa kwenye kanuni za UVCCM. Sasa swala la umri limeanza siku nyingi kujadili umri wa kijana ni upi hasa, mpaka ilipoamuliwa kuwa sifa kubwa ya mwanachama wa UVCCM ni umri nao ni miaka13-35,kama ilivyo sifa ya mwanachama wa UWT ni jinsia yaani MWANAMKE.

Ni mimi nilyeanzisha mchakato huu mwaka 2003 wa kutaka tafsiri sahihi ya uanachama wa mwananchama wa UVCCM, HOJA ILIKUWA KAMA SIFA MOJA WAPO NI UMRI YAANI 13-35 UKIMRUHUSU MWANACHAMA WA MIAKA 32 KWA MFANO ACHAGULIWE KUWA KIONGOZI BAADA YA MIAKA 3 UANACHAMA WAKE UNAKOMA NA HIVYO ANAPOTEZA SIFA YA KUWA KIONGOZI KWANI SI MWANACHAMA.HIVYO LIKATOLEWA PENDEKEZO KUWA KILA ANAYEGOMBEA ASIWE AMEZIDI MIAKA 30 ILI ANAPOMALIZA AWE NDANI YA UMRI WA UANACHAMA WA UVCCM.

Mfano Nchimbi anatuongoza vijana akiwa si mwanachama wetu toka mwaka 2006, ni kinyume na sheria,mtu akienda mahakamani ni mgogoro mkubwa kwa taasisi.

-LILIPOKUJA SWALA LANGU-MIMI NIMEZALIWA TAREHE 07/11/1977,HIVYO MPAKA TAREHE 06/11/2008 MIMI NILIKUWA NA MIAKA 30 NA MIEZI KADHAA, NA KWAKUWA UCHAGUZI NI MCHAKATO/ PROCESS UNAANZA PALE UNAPOCHUKUA FOMU MPAKA SIKU UNAPOPIGIWA KURA NDIO MWISHO WA MCHAKATO. SASA NIMECHUKUA FOMU TAREHE 15/07/2008 NIKIWA NA MIAKA 30 NA MIEZI NA KWAKUWA UTARATIBU HUWA HATUHESABU MIEZI HIVYO KWA MUJIBU WA KANUNI UCHAGUZI UMEANZA MIE NIKIWA BADO NIMO NDANI YA KANUNI..

....na ndo maana baada ya kuona hoja ya umri haiuziki wakaja na hoja kunivua uanachama!! Kusema kweli ni kuigeuza siasa mchezo mchafu wakati haikupaswa kuwa hivyo...na wanajua nguvu waliyotumia kufika hapo walipo fikia.....

Nnauye Jr

Sasa huoni kuwa hapo pana tatizo la kiufundi?

Ni lazima ujiwekee utaratibu si kwa vijana tu bali kwa jumuhia zote.Muwe nna kalenda inayoonyesha tarehe ya uchaguzi ni lini; nikiwa na maana kuanzia siku ya kuchukua fomu, yaani uchaguzi ujao acha huu wa sasa watu wajue kabisa kuwa tarehe fulani ya kila mwaka wa uchaguzi ni siku rasmi ya kuanza mchakato wa uchaguzi. Kwa hiyo watu watakao chukua fomu siku hiyo watakuwa na haki ya kugombea hata kama wamebakisha siku moja kutimiza hiyo miaka 30.

Hapa kijijini kama mtoto inapofika tarehe 31 august kama hajafika miaka mnne basi haruhusiwi kuingia reception hata kama september moja ndio atakuwa na miaka 4.
 
Sasa huoni kuwa hapo pana tatizo la kiufundi,ni lazima ujiwekee utaratibu si kwa vijana tu bali kwa jumuhia zote.Muwe nna kalenda inayoonyesha tarehe ya uchaguzi ni lini nikiwa na maana kuanzia siku ya kuchukua fomu,yaani uchaguzi ujao acha huu wa sasa watu wajue kabisa kuwa tarehe fulani ya kila mwaka wa uchaguzi ni siku rasmi ya kuanza mchakato wa uchaguzi,kwa hiyo watu watakao chukua fomu siku hiyo watakuwa na haki ya kugombea hata kama wamebakisha siku moja kutimiza hiyo miaka 30.
Hapa kijijini kama mtoto inapofika tarehe 31 august kama hajafika miaka mnne basi haruhusiwi kuingia reception hata kama september moja ndio atakuwa na miaka 4.

Nadhani ushauri wako ni mzuri wacha tutashauri ufanyiwe kazi ili kuepuka migogoro isiyokuwa ya lazima.Nashukuru sana kwa ushauri huu, watu hujifunza kutokana na makosa, au matatizo wakati mwingine.....Thanks
 
Kingine nillichozungumza ni swala zima la kufungwa kwa vyuo vikuu nchini....nilisema naamini kinachopigiwa kelele sio SERA YA UCHANGIAJI YENYEWE bali ni UTEKELEZAJI WA SERA, hivyo sioni sababu ya serikali kutumia ubabe kufunga vyuo badala yake wakae chini na wadau kujadili namna bora ya kutekeleza sera hii. Najua kuwa iko katikati ya mwaka wa fedha wa serikali lakini muhimu kukubali kuwa yapo matatizo katika utekelezaji wa sera hii, ili njia bora itafutwe kisha tuwe na utekelezaji bora zaidi mwaka ujao wa fedha. Maghembe aache ubabe si jambo la buisara kila mara kufunga vyuo hivi maana tunaanzisha utamaduni mbovu wa kutojadiliana kumaliza matatizo yetu hili sio jema.....


Nape, umejitambulisha kuwa wewe ni mkuu wa kitengo cha kusimamia utekelezaji wa ilani ya CCM. Je, kwa mtazamo wako, CCM inatekeleza kweli sera na ilani ya uchaguzi inayosema kwamba kutakuwa na mfumo wa uchangiaji elimu ya juu?

Kama mtu anakiwa kununua bidhaa ya shilingi 100. Mtu akakukopesha shilingi 60 ambazo utamlipa, halafu akakwambia utafute shilingi 40 mwenyewe. Je, amekuchangia?

Na kama hiyo bidhaa ya shilingi 100 ulikuwa uize baadae upate faida na kumrudishia fedha zake; yeye akakupa shilingi 60 huku akijua kabisa hutapata shilingi 40 za kumalizia, si mtego tu wa kukufunga kwa kushindwa kununua hiyo bidhaa na kurudisha deni?

Ndio wanafunzi wetu watoto wa masikini ambao wamefutiwa ada ya msingi, wamepunguziwa ya sekondari lakini wanapaswa kugharamia elimu yao yote ya juu: Manake asilimia inayotolewa na serikali wanapaswa kuirudisha kama deni na bado wanatakiwa kulipia wenyewe sehemu iliyobaki.

Wewe unasema serikali ilikukopesha sehemu ya fedha za masomo yako nje, na zingine umesema ulipata mkopo toka CCM. Sasa unadhani vijana wenzako kule vijijini nao wanaweza kupata mkopo toka CCM kama wewe?

Mbona Rais Kikwete pamoja na kusema hakuna mtoto wa masikini atayeshindwa kusoma kutokana na sera ya uchangiaji(Diamond Jubilee, Februari 2007) sasa amegeuaka na kusema wataoshindwa kuchangia watajiju!?(SAUT, Novemba, 2008).

Je, huwa unawashauri warudi kwenye kutekeleza sera na ilani ya chama chetu?

.......ndiyohiyo
 
BTW:

Uchaguzi sio siku unayochukua fomu, uchaguzi ni pale unapoteuliwa. Sasa kama NAPE wewe ndiye uliyeanzisha huo mchakato wa umri, kwani hujua kuwa utarudisha fomu na kujadiliwa ukiwa tayari umeshavuka umri? Kwa nini ukalazimisha?

Halafu kwa nini baada ya kuondolewa jina lako ukasema kwamba hukuwa na nia ya kugombea uenyekiti na umefurahia kuchukuliwa wagombea wa nafasi hiyo toka Zanzibar kwa kuwa hiyo ndio ilikuwa ndoto yako?

Sasa una ndoto ngapi? Manake wakati wa kuchukua fomu ulisema ni ndoto yako kuwa mwenyekiti lakini baada ya kuondolewa ukasema ni ndoto yako kuona mwenyekiti anatoka ZNZ. Na ndoto zote hizo uliziiita kuwa ni ndoto zako za siku nyingi

......ndiyohiyo
 
Nape, umejitambulisha kuwa wewe ni mkuu wa kitengo cha kusimamia utekelezaji wa ilani ya CCM. Je, kwa mtazamo wako, CCM inatekeleza kweli sera na ilani ya uchaguzi inayosema kwamba kutakuwa na mfumo wa uchangiaji elimu ya juu?

Kama mtu anakiwa kununua bidhaa ya shilingi 100. Mtu akakukopesha shilingi 60 ambazo utamlipa, halafu akakwambia utafute shilingi 40 mwenyewe. Je, amekuchangia?

Na kama hiyo bidhaa ya shilingi 100 ulikuwa uize baadae upate faida na kumrudishia fedha zake; yeye akakupa shilingi 60 huku akijua kabisa hutapata shilingi 40 za kumalizia, si mtego tu wa kukufunga kwa kushindwa kununua hiyo bidhaa na kurudisha deni?

Ndio wanafunzi wetu watoto wa masikini ambao wamefutiwa ada ya msingi, wamepunguziwa ya sekondari lakini wanapaswa kugharamia elimu yao yote ya juu: Manake asilimia inayotolewa na serikali wanapaswa kuirudisha kama deni na bado wanatakiwa kulipia wenyewe sehemu iliyobaki.

Wewe unasema serikali ilikukopesha sehemu ya fedha za masomo yako nje, na zingine umesema ulipata mkopo toka CCM. Sasa unadhani vijana wenzako kule vijijini nao wanaweza kupata mkopo toka CCM kama wewe?

Mbona Rais Kikwete pamoja na kusema hakuna mtoto wa masikini atayeshindwa kusoma kutokana na sera ya uchangiaji(Diamond Jubilee, Februari 2007) sasa amegeuaka na kusema wataoshindwa kuchangia watajiju!?(SAUT, Novemba, 200.

Je, huwa unawashauri warudi kwenye kutekeleza sera na ilani ya chama chetu?

.......ndiyohiyo
Mkuu mimi ningeshauri tuweke thread tofauti kwa ajili ya kuzungumzia swala la hili la mikopo ya wanafunzi kwa mapana, kwani kama vijana linatuhusu leo na kesho na kwa mstakabali wa taifa letu, so pls fungua thread inayojitegemea tujadili hili,mwisho wa siku tunaweza kuja na kitu kizuri kwa faida ya nchi yetu...
 
BTW:

Uchaguzi sio siku unayochukua fomu, uchaguzi ni pale unapoteuliwa. Sasa kama NAPE wewe ndiye uliyeanzisha huo mchakato wa umri, kwani hujua kuwa utarudisha fomu na kujadiliwa ukiwa tayari umeshavuka umri? Kwa nini ukalazimisha?

Halafu kwa nini baada ya kuondolewa jina lako ukasema kwamba hukuwa na nia ya kugombea uenyekiti na umefurahia kuchukuliwa wagombea wa nafasi hiyo toka Zanzibar kwa kuwa hiyo ndio ilikuwa ndoto yako?

Sasa una ndoto ngapi? Manake wakati wa kuchukua fomu ulisema ni ndoto yako kuwa mwenyekiti lakini baada ya kuondolewa ukasema ni ndoto yako kuona mwenyekiti anatoka ZNZ. Na ndoto zote hizo uliziiita kuwa ni ndoto zako za siku nyingi

......ndiyohiyo

Nashukuru sana kwa kufuatilia uchaguzi huu, nikukumbushe baadhi ya mambo machache. Mwaka 2003/2004 nilipochukua fomu kuomba kugombea uenyekiti UVCCM(T)..nilisema wazi baada ya muda mrefu wa jumuiya hii kuongozwa na vijana kutoka bara si dhambi tukipata mwenyekiti kutoka Zanzibar, lakinikatika mazingira yalivyo ilikuwa na bado ni vigumu sana sana kumshindanisha mgombea kutoka Zanzibar na wagombea toka bara akashinda wa Zanzibar(PIA HAPA SI TU ILIMRADI ANATOKA ZANZIBAR,LAKINI PIA AWE NA UWEZO)..

Hivyo basi nikaahidi kuwa nagombea nikishinda tuta "recrut" kijana kutoka Zanzibar na kuwashawishi wapiga kura wakikubali tupate M/kiti kutoka Zanzibar 2008!!Niliisema hii mwaka 2003/2004,kumbukumbu zipo!

Sikushinda uchaguzi ule,alishinda "Dr" Nchimbi..ilipofika mwaka 2008 kwakuwa nilijua ilihitaji utashi mkubwa wa kisiasa na kushawishi ili kumpata mkiti kutoka Zanzibar ndoto yangu ikawa ni jaribu tena kuingia ili niitimize ndoto yangu mwaka 2013, lakini ikatokea vikao vikaamua wagombea watoke Zanzibar!!Tazama mtiririko huo KUONA KWANINI NILISEMA NAFURAHI KWAMAAMUZI HAYA KWANI NDOTO ZANGU ZIMETIMIA


Angalizo..

Si kwamba sikuwa namipango mingine mingi tu juu ya vijana mara zote nilipogombea,bali hili lilikuwa moja ya mipango hiyo ya muda mrefu.
SWALALA UCHAGUZI...nilichokisema ni kuwa uchaguzi ni MCHAKATO NA SI KWELI KWAMBA NI SIKU UNATEULIWA/UTEUZI SI SAHIHI.

Uchaguzi unaanza pale mtu anapochukua fomu mpaka anapopigiwa kura na kutangazwa mshindi ndo uchaguzi unakuwa umekwisha
.
 
Nape big up!

Kwa lolote lililotokea be happy you are a man! wakati mwingine hawa watu ni kuwaingilia hukohuko, siyo lazima kwenda vyama vingine.

Hongera pia kuonekana kwenye jamvi, hili limewashinda wengi sana, kwa mfano mtu kama Nchimbi akitokea humu kwa Identity yake tunayomjua siku hiyohiyo Mkapa ataenda Jela!!

Hana ujanja huo wala hataweza, hivyo basi kukuweka wewe remotely far better than him!

waberoya
 
Nnauye Jr
kuna mahali mwanzoni mwa hii thread ulisema unataka kuerekebisha mambo kabla hayajafika mbali...nikasema yameshafika mbali tayari. Wewe mwenyewe shahidi ulitegemea kujieleza namna hii? Hapa ni JF hakuna hoja ndogo. Karibu kijana umeonesha ushirikiano mzuri
 
Mkuu mimi ningeshauri tuweke thread tofauti kwa ajili ya kuzungumzia swala la hili la mikopo ya wanafunzi kwa mapana, kwani kama vijana linatuhusu leo na kesho na kwa mstakabali wa taifa letu, so pls fungua thread inayojitegemea tujadili hili,mwisho wa siku tunaweza kuja na kitu kizuri kwa faida ya nchi yetu...

Sasa umeanza kukwepa hoja. Wewe mwenyewe ndio umeanzisha hoja ya mikopo ya elimu ya juu hapo juu. Hivyo, naomba unijibu hiyo hoja yangu tafadhali. Tukifungulia thread nyingine itakuwa mjadala mpana zaidi. Mimi nimetaka jibu lako kutokana na hoja uliyotoa na wasifu wako uliolezea kuwa wewe ni Mkuu wa Kitengo cha kusimamia utekelezaji wa Ilani ya CCM

....ndiyohiyo
 
Nashukuru sana kwa kufuatilia uchaguzi huu, nikukumbushe baadhi ya mambo machache. Mwaka 2003/2004 nilipochukua fomu kuomba kugombea uenyekiti UVCCM(T)..nilisema wazi baada ya muda mrefu wa jumuiya hii kuongozwa na vijana kutoka bara si dhambi tukipata mwenyekiti kutoka Zanzibar, lakinikatika mazingira yalivyo ilikuwa na bado ni vigumu sana sana kumshindanisha mgombea kutoka Zanzibar na wagombea toka bara akashinda wa Zanzibar(PIA HAPA SI TU ILIMRADI ANATOKA ZANZIBAR,LAKINI PIA AWE NA UWEZO)..

Hivyo basi nikaahidi kuwa nagombea nikishinda tuta "recrut" kijana kutoka Zanzibar na kuwashawishi wapiga kura wakikubali tupate M/kiti kutoka Zanzibar 2008!!Niliisema hii mwaka 2003/2004,kumbukumbu zipo!

Sikushinda uchaguzi ule,alishinda "Dr" Nchimbi..ilipofika mwaka 2008 kwakuwa nilijua ilihitaji utashi mkubwa wa kisiasa na kushawishi ili kumpata mkiti kutoka Zanzibar ndoto yangu ikawa ni jaribu tena kuingia ili niitimize ndoto yangu mwaka 2013, lakini ikatokea vikao vikaamua wagombea watoke Zanzibar!!Tazama mtiririko huo KUONA KWANINI NILISEMA NAFURAHI KWAMAAMUZI HAYA KWANI NDOTO ZANGU ZIMETIMIA


Angalizo..

Si kwamba sikuwa namipango mingine mingi tu juu ya vijana mara zote nilipogombea,bali hili lilikuwa moja ya mipango hiyo ya muda mrefu.
SWALALA UCHAGUZI...nilichokisema ni kuwa uchaguzi ni MCHAKATO NA SI KWELI KWAMBA NI SIKU UNATEULIWA/UTEUZI SI SAHIHI.

Uchaguzi unaanza pale mtu anapochukua fomu mpaka anapopigiwa kura na kutangazwa mshindi ndo uchaguzi unakuwa umekwisha
.


Hebu kuwa mkweli Nape nasema kutoka moyoni. Nakubaliana nawe kuwa wakati ukichukua fomu umri wako ulikuwa ukikuruhusu kuchukua fomu. Lakini je, wakati kikao cha kuchuja majina kinafanyika, je umri wako ulikuwa unakuruhusu kugombea?

Kama umri ulikuwa umeshazidi, unadhani ingekuwa ni halali jina lako lipitishwe kugombea? Manake waliokuwa wanachuja majina hawakuwa wakiangalia, huyu wakati anachukua fomu alikuwa na umri gani. Wanaangalia huyu kwenye fomu yake amezaliwa tarehe ngapi mwezi wa ngapi na je siku ya kupigiwa kura kutokana na tarehe hiyo ya kuzaliwa, ana umri unaokidhi vigezo?

Ifike mahali Nape ukiri kwamba ulikuwa umezidi umri, useme tu kwamba uligombea ili kuibua huo mjadala wa kuwashughulikia kina Nchimbi. Hivi kama wewe ungekuwa ndio uko kwenye kikao cha mchujo, likaletwa jina la mgombea mwenye utata wa umri kama lilivyokuwa lako; ungelipitisha? Kwa sababu zipi?

......ndiyohiyo
 
Nape Jr: Sipendi kuchangia sana kwenye hoja hizi mnazolumbana hapa, maana nyingi zinahusu chama chenu, lakini nilitaka kusema kwamba you are incredibly convincing in your argument na inaonekana kumbe hata huko kwenye UVCCM kuna watu wanafikiri!!!

Maana wakati mwingine huwa tukisoma mawazo ya viongozi wenu tunasikitika sana, lakini kupitia thread hii umenitia moyo. Wakati mwingine watu mnaowaweka mbele kuwasemea wanawaaibisha na kuonekana kama vile katika UVCCM wote hamnazo!! Nakumbuka niliangalia mdahalo mmoja kati ya kiongozi wenu wa UVCCM (naomba nisimtaje jina) na Mnyika wa BAVICHA, ilikuwa aibu-ni kama vile Mnyika alikuwa anapambana na mtoto aliyetoka kufanya mtihani wa darasa la nne!

Great man, you certainly have a great future in Tanzanian politics. My only worry is that you may be in a place where you're slowly but surely eroding your potential instead of realising it-good if you realised this sooner than later-I may be wrong though! Read my article: CCM ya Nape ni nadharia...http://www.chadema.net/makala/mkumbo/kitila_18.html
 
Nape Jr: Sipendi kuchangia sana kwenye hoja hizi mnazolumbana hapa, maana nyingi zinahusu chama chenu, lakini nilitaka kusema kwamba you are incredibly convincing in your argument na inaonekana kumbe hata huko kwenye UVCCM kuna watu wanafikiri!!!

Maana wakati mwingine huwa tukisoma mawazo ya viongozi wenu tunasikitika sana, lakini kupitia thread hii umenitia moyo. Wakati mwingine watu mnaowaweka mbele kuwasemea wanawaaibisha na kuonekana kama vile katika UVCCM wote hamnazo!! Nakumbuka niliangalia mdahalo mmoja kati ya kiongozi wenu wa UVCCM (naomba nisimtaje jina) na Mnyika wa BAVICHA, ilikuwa aibu-ni kama vile Mnyika alikuwa anapambana na mtoto aliyetoka kufanya mtihani wa darasa la nne!


Great man, you certainly have a great future in Tanzanian politics. My only worry is that you may be in a place where you're slowly but surely eroding your potential instead of realising it-good if you realised this sooner than later-I may be wrong though! Read my article: CCM ya Nape ni nadharia
CCM ya Nape ni nadharia, ya Nchimbi ndiyo iliyopo
Mkuu Kitila,

Heshima mbele kama kawaida yako, alyways sharp mind na on to the point, maneno mazito sana haya.
 
Nape jr: Sipendi kuchangia sana kwenye hoja hizi mnazulumbana hapa, maana nyingi zinahusu chama chenu, lakini nilitaka kusema kwamba you are incredibly convincing in your argument na inaonekana kumbe hata huko kwenye UVCCM kuna watu wanafikiri!!! Maana wakati mwingine huwa tukisoma mawazo ya viongozi wenu tunasikitika sana, lakini kupitia thread hii umenitia moyo. Wakati mwingine watu mnaowaweka mbele kuwasemea wanawaaibisha na kuonekana kama vile katika UVCCM wote hamnazo!! Nakumbuka niliangalia mdahalo mmoja kati ya kiongozi wenu wa UVCCM (naomba nisimtaje jina) na Mnyika wa BAVICHA, ilikuwa aibu-ni kama vile Mnyika alikuwa anapambana na mtoto aliyetoka kufanya mtihani wa darasa la nne!

Great man, you certainly have a great future in Tanzanian politics. My only worry is that you may be in a place where you're slowly but surely eroding your potential instead of realising it-good if you realised this sooner than later-I may be wrong though! Read my article: CCM ya Nape ni nadharia...CCM ya Nape ni nadharia, ya Nchimbi ndiyo iliyopo

Nami nasubiri kwa hamu ajibu hizo hoja ndio nimuunge mkono. Walau huyu anaweza kutuongoza vizuri UVCCM kuliko Dr Nchimbi na swahiba wake Benno Mallisa

.....ndiyohiyo
 
Nape umeongea ya kutosha kwenye hii thread, kuna wenye masikio na macho tumekusikia tayari huna sababu ya kuongeza anything!

Mungu akubariki na kukuzidishia nguvu, uweze kulitumikia taifa letu wka uadilifu mkubwa kama ulivyo sasa.
 
kwa vyovyote vile na kwa akili ya kawaida, Beno na Zainab ni wajumbe wa NEC tayari kupitia UVCCM nafasi wanayogombea inawapa pia nafasi ya kuwa wajumbe wa NEC. BASHE si MNEC kwa nini vijana wasitumie nafasi hiyo kumchagua Bashe ili kuongeza wigo wa Uwakilishi wa vijana katika NEC! swala si kujaza vyeo tu kwa mtu mmoja au kikundi kimoja cha watu, nawashauri vijana wa CCM wakifika DODOMA wamchague Bashe pamoja na kuwa na uwezo wa kuongoza !
 
Jumapili iliopita Husen bashe alifanya mkutano mkubwa NZega katika uwanja wa Park, mkutano huo kwa akili ya kawaida tu haiwezekani ukawa umeandaliwa na bashe mwenyewe je ni nani yupo nyuma ya bashe maana mkutano ulikuwa mkubwa muno
 
Jumapili iliopita Husen bashe alifanya mkutano mkubwa NZega katika uwanja wa Park, mkutano huo kwa akili ya kawaida tu haiwezekani ukawa umeandaliwa na bashe mwenyewe je ni nani yupo nyuma ya bashe maana mkutano ulikuwa mkubwa muno

kwani wewe kakutuma nani hapa JF? NDIO KWANZA UNA POST MOJA UMEANZA NA MAJUNGU.

BY THE WAY HAKUNA MTU ANAITWA HUSEN BALI KUNA HUSSEIN.MWAMBIE BOSI WAKO AKUFUNDISHE KUANDIKA KWANZA.
 
Back
Top Bottom