CCM yamwaga Mamilioni kuivaa CHADEMA; Watu wasombwa kwa malori

attachment.php
Duh..yaani mtu unabebwa kwenye fuso kama gunia la viazi!?
 
maskini baba/mama/kaka/dada zangu hawa..!
natamani wangeijua kweli ili kweli iwaweke huru.

Ajabu ni kwamba kuna RC mmoja kapiga malori marufuku kubeba abiria du! na sheria ikoje?

RC apiga marufuku malori kubeba abiria Send to a friend
Saturday, 09 June 2012 08:15
0digg

Salim Mohammed, Tanga
MKUU wa Mkoa wa Tanga, Chiku Gallawa, amepiga marufuku magari ya mizigo kubeba watu kwenda kwenye mikusanyiko ya watu wengi, ikiwamo misibani na harusini lengo likiwa ni kuepusha maafa yanayotokana na ajali.

Agizo hilo limekuja baada ya kukithiri kwa vifo vitokanavyo na ajali za barabarani, ambazo husababishwa na magari ya mizigo kubeba watu kwenda misibani, maharusini na minadani.
Mwaka jana watu 24 walipoteza maisha na wengine 39 kujeruhuiwa na kupata ulemavu wa maisha.
Akizungumza kwenye kikao cha wadau wa usafirishaji na wamiliki wa magari ya mizigo juzi, Gallawa alisema kuanzia sasa ni marufuku magari ya mizigo kubeba watu na kuwapeleka katika mikusanyiko.

Gallawa alisema imekuwa kawaida kwa watu wa Tanga kutumia magari ya mizigo kwenda katika shughuli za jamii na kusahau maafa ambayo yanaweza kutokea, huku wakiacha usafiri wa mabasi.

“Kuanzia sasa ni marufuku kwa magari ya mizigo kubeba watu na kuwapeleka katika sherehe au misibani, tunashuhudia maafa ya mara kwa mara yanayotokana na ubebaji watu kwenye malori, sasa basi!” alisisitiza Gallawa.

Aliwata wakazi wa mijini na vijijini kuacha kutumia usafiri huo, kwani umekuwa ukipoteza roho za watu wengi na watumie mabasi ambayo ndiyo wenye haki za kisheria kubeba abiria.
Kuhusu tabia ya baadhi ya madereva kuweka miti na majani barabarani gari linapoharibika, Gallawa alisema watu hao wamekuwa wakichafua mazingira kwani gari hilo likitengenezwa hawaondoshi uchafu huo.

Alisema tabia hiyo imekuwa kero na wakati mwingine husababisha ajali bila sababu za msingi, hivyo kila kijiji kinatakiwa kuwa na walinzi ambao watanakili namba za magari yanayofanya hivyo.

Source Mwananchi leo.
 
Duh..yaani mtu unabebwa kwenye fuso kama gunia la viazi!?

Kwa ajili ya CCM tutapanda hata punda wacha fuso. CCM wanatuletea ma fuso tupande chadema mnaletewa mitumba ya mafuso mnauziwa mawili kwa million 350, Mchagga anawapatia kweli kweli, halafu ruzuku anachukuwa kila mwezi, posho kibao za bungeni na kuwachangisha mia mia zenu viwanjani. Duh! Na kiwanjani akawaingilia na VX 8 sita kuwaonesha mia mia zenu zinakwenda wapi. Kwi kwi kwi teh teh teh!
 
Kwani hawabebani mi kwamacho yangu siku ya mkutano wa chadema jangwani wanakodi madaladala.sasa kunatofauti gani na CCM wakiamua kuwakodia magari wanachm wao tatizo ni nini kwani na kwani watt wanalazimishwa kupnda kwenye hayo magari si hiyari Yao wenyewe magwanda kinawauma nini watt wakienda jangwani si muwaache Kila Mtu na maamuzi yake
Jamaa yangu mbona unaharaka, ebu fafanua huo usemi wako!Waliwezaje kukodi madaladala kwa macho yako?
 
wadau wa jamii forum natumai mko pouwaaaaa!!!!!!!!!

Ebwana leo niko maeneo ya tabata kinyerezi.huku ndo kwanhiho za maendeleo yanacvhipuka na vigogo wengi wa seririkali mamelangua mahekali ya aridhi ya kutosha tu. any way siyo mada yangu ila ninachotaka kuzungumzia hapa ni namna ninavyo ona dcm zimekodiwa lukuki sijui kwa gharama za chama au common mwananchi zote zimejaa kijani eti zinaelekea jangwani!

Hakika nimeogopa na kushituka mno nimejiuliza maswali mengi nisipate majibu yake na ndo mana imenibidi niulize ccm na kusomba watu mpaka lini???????? nisaidieni katika hili.
 
kWANI haO WANAOBEBWA SI WATU WENYE AKIL ZAO TIMAM? KAMA HAWATAK MALOR YANGEKUA WAZI BILA WATU? WANATAKA KUBEBWA NA NDO MANA WANAPAKIZWA KWENYE MALORI.
 
Vya mwerevu huliwa na mjinga, siku watakuwa kambi ya upinzani ndiyo itakuwa mwisho.
 
jamani nina mishe zangu kariakoo, naomba aliye kwenye mkutano wa nyinyiem aniambie wakati wa kurudi nipate lift walau nitumie kodi yangu!
 
Kwa hiyo unataka watu watoke kinyerezi kwa mguu? Ili iweje? Kama chama chao kina uwezo wa kuwapa usafiri wanachama wake wewe kinakukera nini? Ccm kwa sasa mtaji wao mkubwa ni watu maskini waliokata tamaa na maisha, wasiojua leo watakula nini, watafikaje mjini. Hebu waangalie vizuri hao waliobebwa katika hayo malori wanavyoimba mipasho, kukata viuno n.k, unadhani mtu serious na future ya tz anaweza kufanya hivyo. Waache wabebwe, waimbe, wacheze maana hawajui walitendalo
 
Hata kipindi fulani kuna chama fulani kilikuwa kinafanya hivyo. Ni utaratibu mzuri maana bila hivyo wanachama wengi hawatahudhuria mkutano.
 
Hakika ni maajabu na vichekesho,nimetoka maeneo ya ilala mpaka tabata relini nimekutana na coaster zaidi ya 7 wengi wao ni wanawake,mi nauliza kama hizi pesa hazina kazi si wakawape maskini?
 
Mamluki wamekodiwa kutoka vijijini, na kadi mpya za CDM zimesha kuwa printed ili mamluki wajidai wanazirejesha.

Malipo kwa mamluki hao ni sh. 10'000/=

Mdogo wangu alipewa kazi hiyo na amekataa kupokea hiyo hela
.
Angepokea tu, kwani haibadiri ukweli watanzania wameichoka CCM
 
Back
Top Bottom