siha tanganyika
Member
- Apr 25, 2012
- 10
- 4
HALI ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) imezidi kuchafuka kufuatia vigogo wa serikali kutuhumiwa kuhusiana na kampeni chafu zikiwamo rushwa na fitina, ambapo katika hali isiyokuwa ya kawaida, mmoja wa mawaziri machachari wa serikali ya Jakaya Kikwete amekataliwa asigombee nafasi nzito ya uongozi aliyoomba.
Aliyekwaa kisiki hicho ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Aggrey Mwanri, baada ya Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Siha, mkoani Kilimanjaro kugoma kupitisha jina lake kwenye kinyang'anyiro cha kugombea ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC).
Habari za kuaminika zimesema kuwa uamuzi wa kufuta jina la Mwanri ulifikiwa katika kikao cha halmashauri ya wilaya kilichokaa Agosti 29, 2012, kwenye ofisi ya CCM ya wilaya hiyo.
Mmoja wa viongozi wa CCM wa wilaya aliliambia Tanzania Daima kuwa, katika kikao hicho wajumbe wengi walikataa kabisa kulijadili jina la Mwanri, badala yake wakajadili majina mawili ya waombaji wengine ambao walitajwa kuwa ni Joha Mtawazo na Meejo Laizer.
Imedaiwa kuwa sababu za kuenguliwa kwa naibu waziri huyo ni kuwa kwake na nafasi nyingi za utendaji ndani ya chama na serikali, ikiwa ni pamoja na nafasi yake ya ubunge, na kwamba hawakuwa tayari kurundika vyeo vingi kwa mtu mmoja, wakati kuna vijana wengi wenye uwezo na moyo wa kukitumikia chama.
"Maamuzi ya viongozi wetu ambayo yameungwa mkono na baadhi ya wajumbe ni mazuri kwani kwenye wilaya yetu kuna wanachama wengi tu wenye sifa na wanaweza pia kutuwakilisha vizuri kwenye mkutano wa halmashauri kuu sasa, kwa nini mbunge yeye awe ndo kila kitu," alihoji mwanachama mmoja bila ya kutaka kutajwa jina lake gazetini.
Mwenyekiti wa CCM wilayani humo, Oscra Jeremia bila kukubali wala kukataa kuhusiana na uamuzi wa kufuta jina la Mwanri, alisema kuwa ni jambo la busara sasa kwa viongozi wa chama kufanya maamuzi sahihi katika mgawanyo wa uongozi kisiasa na kuachana na mtindo wa kumuachia mtu mmoja kubeba vyeo vingi wakati kuna wanachama wengine wenye sifa.
"Ni bora kama wapo waliojitokeza na wana sifa wakaachiwa, kwani ukimuachia mtu mmoja kila kitu inaleta balaa zaidi hivyo mbunge inabidi aache busara itumike kwa sababu si vizuri kuchukua kila kitu," alisema.
Hata hivyo, alikiri kuwasiliana na waziri huyo ambaye amedai kuwa baada ya kujua kuwa kuna wagombea wengine waliojitokeza kwenye nafasi hiyo, alikubaliana na uamuzi wa kuondoa jina lake.
"Ni kweli mbunge alikuwa amechukua fomu lakini kanuni zilikataa, hivyo ikabidi aombwe. Sasa kama wapo wenye sifa ni bora wapewe," alisema.
Rushwa, vitisho, ukabila vyatawala
Tuhuma za kukithiri kwa kampeni chafu zimeendelea kuripotiwa sehemu mbalimbali nchini, huku Jumuiya ya Wanawake wa CCM, ikionekana kuelemewa na uchafu mwingi.
Huko Bagamoyo mkoani Pwani, inadaiwa kuwa siasa chafu na utoaji rushwa wa waziwazi unadaiwa kufanywa na wagombea, huku watendaji wa serikali wakidaiwa kuwa vinara wa mchezo huo.
Habari za kuaminika kutoka kwa mmoja wa wagombea katika uchaguzi huo, zinasema kuwa katika uchaguzi wa nafasi ya mwenyekiti uliofanyika Agosti 23, uliompa ushindi Hapsa Kilingo, baadhi ya viongozi wa CCM na serikali akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Subira Mgalu, anayedaiwa kutoa hongo ya fedha na vitenge kwa baadhi ya wajumbe ili ‘mtu' wake ashinde.
Habari pia zinadai kuwa, kampeni zilitawaliwa na siasa chafu zilizobeba udini, ukabila na kuingilia mambo binafsi ya kifamilia ili kuchafuana.
Kiongozi mwingine wa CCM (jina limehifadhiwa) inadaiwa aliwasafirisha wajumbe kwa magari huku akitambua kuwa ni kinyume na sheria za uchaguzi wa CCM toleo la Februari 2010 ibara ya 33 (13).
Hata hivyo, Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Subira Mgalu, aliliambia Tanzania Daima kuwa pamoja na kuwepo kwenye uchaguzi huo, hakuhusika kwenye kampeni zilizokiuka kanuni za uchaguzi na kama kuna mwenye ushahidi wowote juu ya hilo auwasilishe katika sehemu inayohusika.
"Ni kweli nilikuwepo kwenye uchaguzi huo kama mjumbe lakini sikushiriki kwenye kampeni zinazokiuka kanuni za uchaguzi," alisema Mgalu na kuongeza kuwa ikiwa mlalamikaji anao ushahidi, ni vema akaupeleka katika vyombo vinavyohusika ili hatua za kisheria zichukuliwe badala ya kulalamika tu katika vyombo vya habari.
Chenge awania ujumbe wa NEC
Baadhi ya wabunge katika mikoa wa Simiyu na Shinyanga, akiwemo Andrew Chenge, wanadaiwa kujitosa kuwania nafazi za ujumbe wa NEC, huku kukiwa na habari za kuibuka kwa siasa za chuki, fitina na uhasama wa hali ya juu.
Aidha baadhi ya wabunge wanawania nafasi ya uenyekiti ambapo katika Mkoa wa Simiyu nafasi hiyoinawania pia na Mbunge wa Afrika, Luhaga Mpina, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kisesa, wilayani Meatu.
Nafasi hiyo pia inawania na aliyewahi kuwa mbunge wa Afrika Mashariki, George Nangale na Dk. Titus Kamana, Mbunge wa Jimbo la Busega.
Mkoani Shinyanga, vita kubwa imeibuka baina ya mahasimu wawili, mwenyekiti wa sasa Hamisi Mgeja na James Lembeli ambaye ni Mbunge wa Kahama. Wengine ni aliyewahi kuwa mbunge wa Jimbo la Shinyanga Leonard Derefa na Ahmed Salum, Mbunge wa Jimbo la Solwa.
Kuna madai kuwa, makundi ya Mgeja na Lembeli yameanza kampeni nzito na kila moja linatumia kila mbinu kuhakikisha kuwa jina la mmoja wao halirudi.
Kada apinga matokeo ya uchaguzi Songea
Huko Songea Kada wa CC katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea, mkoani Ruvuma, Laula Malekela, amepinga matokeo ya uchaguzi wa Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT) yaliyomwezesha Anna Hinju, kuibuka mshindi katika uchaguzi uliofanyika hivi karibuni.
Malekela anadai hakutendewa haki mara baada ya kuchukua fomu ya kugombea nafasi ya uenyekiti wa UWT Wilaya ya Songea Mjini.
Malekela alisema kuwa uchaguzi huo ulikuwa na mizengwe mingi, ambapo mmoja wa watendaji wakuu wa CCM alionekana akimfanyia kampeni za waziwazi mmoja wa wagombea kinyume cha utaratibu.
Alisema kuwa amewasilisha barua yenye kumb, Na. MGO/SW/002 ya kupinga matokeo ya uchaguzi huo kwa Katibu wa CCM Mkoa wa Ruvuma na kupeleka nakala kwa Katibu Mkuu wa CCM Taifa na Katibu wa UWT Taifa.
Iringa hakukaliki
Huko Iringa taarifa zimesema kuwa baadhi ya wagombea mbalimbali katika chaguzi hizo wanaendesha kampeni chafu za udini na ukabila hali ambayo inaendelea kukigawa chama katika makundi.
Mwenyekiti wa sasa wa chama hicho, Wilaya ya Iringa Mjini, Abeid Kiponza, amesema kuwa hali ya chaguzi katika manispaa si shwari kutokana na kukithiri kwa kampeni chafu za udini na ukabila pamoja na vitendo vya rushwa.
"Ninachosema ni kwamba kuna fununu za baadhi ya wagombea na wanachama ambao wamekuwa wakihusishwa na siasa chafu ambazo kimsingi hazina tija kwa chama.
"Ni kweli kumekuwa na baadhi ya wagombea na hasa vijana wamekuwa wakitumika vibaya kufanya kampeni mapema kabla ya muda wa kufanya hivyo. Kuna baadhi ya wagombea walianza kampeni toka mwaka jana. Wapo watu ambao kwa makusudi wamekuwa wakikiuka taratibu za uchaguzi ndiyo maana tumekuwa tukipata viongozi wabovu, wasio na sifa, jambo hili linakera kwa vile linaleta mvurugano na msuguano usio wa lazima miongoni mwetu na jamii kwa ujumla," Alisema.
Aliyekwaa kisiki hicho ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Aggrey Mwanri, baada ya Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Siha, mkoani Kilimanjaro kugoma kupitisha jina lake kwenye kinyang'anyiro cha kugombea ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC).
Habari za kuaminika zimesema kuwa uamuzi wa kufuta jina la Mwanri ulifikiwa katika kikao cha halmashauri ya wilaya kilichokaa Agosti 29, 2012, kwenye ofisi ya CCM ya wilaya hiyo.
Mmoja wa viongozi wa CCM wa wilaya aliliambia Tanzania Daima kuwa, katika kikao hicho wajumbe wengi walikataa kabisa kulijadili jina la Mwanri, badala yake wakajadili majina mawili ya waombaji wengine ambao walitajwa kuwa ni Joha Mtawazo na Meejo Laizer.
Imedaiwa kuwa sababu za kuenguliwa kwa naibu waziri huyo ni kuwa kwake na nafasi nyingi za utendaji ndani ya chama na serikali, ikiwa ni pamoja na nafasi yake ya ubunge, na kwamba hawakuwa tayari kurundika vyeo vingi kwa mtu mmoja, wakati kuna vijana wengi wenye uwezo na moyo wa kukitumikia chama.
"Maamuzi ya viongozi wetu ambayo yameungwa mkono na baadhi ya wajumbe ni mazuri kwani kwenye wilaya yetu kuna wanachama wengi tu wenye sifa na wanaweza pia kutuwakilisha vizuri kwenye mkutano wa halmashauri kuu sasa, kwa nini mbunge yeye awe ndo kila kitu," alihoji mwanachama mmoja bila ya kutaka kutajwa jina lake gazetini.
Mwenyekiti wa CCM wilayani humo, Oscra Jeremia bila kukubali wala kukataa kuhusiana na uamuzi wa kufuta jina la Mwanri, alisema kuwa ni jambo la busara sasa kwa viongozi wa chama kufanya maamuzi sahihi katika mgawanyo wa uongozi kisiasa na kuachana na mtindo wa kumuachia mtu mmoja kubeba vyeo vingi wakati kuna wanachama wengine wenye sifa.
"Ni bora kama wapo waliojitokeza na wana sifa wakaachiwa, kwani ukimuachia mtu mmoja kila kitu inaleta balaa zaidi hivyo mbunge inabidi aache busara itumike kwa sababu si vizuri kuchukua kila kitu," alisema.
Hata hivyo, alikiri kuwasiliana na waziri huyo ambaye amedai kuwa baada ya kujua kuwa kuna wagombea wengine waliojitokeza kwenye nafasi hiyo, alikubaliana na uamuzi wa kuondoa jina lake.
"Ni kweli mbunge alikuwa amechukua fomu lakini kanuni zilikataa, hivyo ikabidi aombwe. Sasa kama wapo wenye sifa ni bora wapewe," alisema.
Rushwa, vitisho, ukabila vyatawala
Tuhuma za kukithiri kwa kampeni chafu zimeendelea kuripotiwa sehemu mbalimbali nchini, huku Jumuiya ya Wanawake wa CCM, ikionekana kuelemewa na uchafu mwingi.
Huko Bagamoyo mkoani Pwani, inadaiwa kuwa siasa chafu na utoaji rushwa wa waziwazi unadaiwa kufanywa na wagombea, huku watendaji wa serikali wakidaiwa kuwa vinara wa mchezo huo.
Habari za kuaminika kutoka kwa mmoja wa wagombea katika uchaguzi huo, zinasema kuwa katika uchaguzi wa nafasi ya mwenyekiti uliofanyika Agosti 23, uliompa ushindi Hapsa Kilingo, baadhi ya viongozi wa CCM na serikali akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Subira Mgalu, anayedaiwa kutoa hongo ya fedha na vitenge kwa baadhi ya wajumbe ili ‘mtu' wake ashinde.
Habari pia zinadai kuwa, kampeni zilitawaliwa na siasa chafu zilizobeba udini, ukabila na kuingilia mambo binafsi ya kifamilia ili kuchafuana.
Kiongozi mwingine wa CCM (jina limehifadhiwa) inadaiwa aliwasafirisha wajumbe kwa magari huku akitambua kuwa ni kinyume na sheria za uchaguzi wa CCM toleo la Februari 2010 ibara ya 33 (13).
Hata hivyo, Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Subira Mgalu, aliliambia Tanzania Daima kuwa pamoja na kuwepo kwenye uchaguzi huo, hakuhusika kwenye kampeni zilizokiuka kanuni za uchaguzi na kama kuna mwenye ushahidi wowote juu ya hilo auwasilishe katika sehemu inayohusika.
"Ni kweli nilikuwepo kwenye uchaguzi huo kama mjumbe lakini sikushiriki kwenye kampeni zinazokiuka kanuni za uchaguzi," alisema Mgalu na kuongeza kuwa ikiwa mlalamikaji anao ushahidi, ni vema akaupeleka katika vyombo vinavyohusika ili hatua za kisheria zichukuliwe badala ya kulalamika tu katika vyombo vya habari.
Chenge awania ujumbe wa NEC
Baadhi ya wabunge katika mikoa wa Simiyu na Shinyanga, akiwemo Andrew Chenge, wanadaiwa kujitosa kuwania nafazi za ujumbe wa NEC, huku kukiwa na habari za kuibuka kwa siasa za chuki, fitina na uhasama wa hali ya juu.
Aidha baadhi ya wabunge wanawania nafasi ya uenyekiti ambapo katika Mkoa wa Simiyu nafasi hiyoinawania pia na Mbunge wa Afrika, Luhaga Mpina, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kisesa, wilayani Meatu.
Nafasi hiyo pia inawania na aliyewahi kuwa mbunge wa Afrika Mashariki, George Nangale na Dk. Titus Kamana, Mbunge wa Jimbo la Busega.
Mkoani Shinyanga, vita kubwa imeibuka baina ya mahasimu wawili, mwenyekiti wa sasa Hamisi Mgeja na James Lembeli ambaye ni Mbunge wa Kahama. Wengine ni aliyewahi kuwa mbunge wa Jimbo la Shinyanga Leonard Derefa na Ahmed Salum, Mbunge wa Jimbo la Solwa.
Kuna madai kuwa, makundi ya Mgeja na Lembeli yameanza kampeni nzito na kila moja linatumia kila mbinu kuhakikisha kuwa jina la mmoja wao halirudi.
Kada apinga matokeo ya uchaguzi Songea
Huko Songea Kada wa CC katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea, mkoani Ruvuma, Laula Malekela, amepinga matokeo ya uchaguzi wa Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT) yaliyomwezesha Anna Hinju, kuibuka mshindi katika uchaguzi uliofanyika hivi karibuni.
Malekela anadai hakutendewa haki mara baada ya kuchukua fomu ya kugombea nafasi ya uenyekiti wa UWT Wilaya ya Songea Mjini.
Malekela alisema kuwa uchaguzi huo ulikuwa na mizengwe mingi, ambapo mmoja wa watendaji wakuu wa CCM alionekana akimfanyia kampeni za waziwazi mmoja wa wagombea kinyume cha utaratibu.
Alisema kuwa amewasilisha barua yenye kumb, Na. MGO/SW/002 ya kupinga matokeo ya uchaguzi huo kwa Katibu wa CCM Mkoa wa Ruvuma na kupeleka nakala kwa Katibu Mkuu wa CCM Taifa na Katibu wa UWT Taifa.
Iringa hakukaliki
Huko Iringa taarifa zimesema kuwa baadhi ya wagombea mbalimbali katika chaguzi hizo wanaendesha kampeni chafu za udini na ukabila hali ambayo inaendelea kukigawa chama katika makundi.
Mwenyekiti wa sasa wa chama hicho, Wilaya ya Iringa Mjini, Abeid Kiponza, amesema kuwa hali ya chaguzi katika manispaa si shwari kutokana na kukithiri kwa kampeni chafu za udini na ukabila pamoja na vitendo vya rushwa.
"Ninachosema ni kwamba kuna fununu za baadhi ya wagombea na wanachama ambao wamekuwa wakihusishwa na siasa chafu ambazo kimsingi hazina tija kwa chama.
"Ni kweli kumekuwa na baadhi ya wagombea na hasa vijana wamekuwa wakitumika vibaya kufanya kampeni mapema kabla ya muda wa kufanya hivyo. Kuna baadhi ya wagombea walianza kampeni toka mwaka jana. Wapo watu ambao kwa makusudi wamekuwa wakikiuka taratibu za uchaguzi ndiyo maana tumekuwa tukipata viongozi wabovu, wasio na sifa, jambo hili linakera kwa vile linaleta mvurugano na msuguano usio wa lazima miongoni mwetu na jamii kwa ujumla," Alisema.