Safari_ni_Safari
JF-Expert Member
- Oct 5, 2007
- 23,268
- 17,097
MWENYEKITI wa Kampeni wa mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana, amesema chama hicho na mgombea wake havihusiki na taarifa za kuongezewa nguvu za ulinzi usioonekana kama inavyoelezwa na Mnajimu Sheikh Yahya Hussein.
Kinana alisema jana kwamba, Rais Kikwete ni muumini mzuri wa dini ya Kiislamu aliyelelewa katika misingi ya dini, anaamini afya njema au maradhi, vyote huletwa na Mwenyezi Mungu na vivyo hivyo katika suala la ulinzi wa afya ya mwanadamu.
Alisema Sheikh Yahya ni Mnajimu, anao uhuru wa kusema vitu anavyoviona, lakini Rais
Kikwete wala CCM visihusishwe na mambo hayo.
Alisema mbali na ulinzi wa Mungu, Rais Kikwete ana kikosi madhubuti cha walinzi waliofundwa vyema kuhakikisha usalama wa Rais.
Kauli ya Kinana imefuatia taarifa za baadhi ya vyombo vya habari kuwanukuu wanasiasa
na kiongozi mmoja wa dini wakimtaka Rais Kikwete atoe tamko kuhusu madai ya Sheikh
Yahya ya kumpatia ulinzi usioonekana.
Sheikh Yahya alikaririwa akisema atatoa ulinzi usioonekana kwa macho ili kumkinga Rais Kikwete, ili mtu yeyote asijaribu kumfanyia mchezo wowote katika kipindi hiki cha kuelekea katika uchaguzi mkuu mwezi kesho.
Hata hivyo, jana Sheikh Yahya alitoa ufafanuzi wake juu ya taarifa aliyoitoa awali akisema
ilitafsiriwa vibaya na baadhi ya watu na kusisitiza kila mtu ana jini wake na kusema jini wa
mgombea wa Chadema, Dk. Slaa anaitwa Subiyani.
Mimi sikuzungumzia nguvu za giza na wala sifanyi uchawi au ushirikina nilikuwa
nazungumzia majini ambao ni viumbe kama sisi isipokuwa wao wameumbwa kwa moto na
sisi tumeumbwa kwa udongo na wametajwa katika vitabu vyote vitakatifu vya Waislamu na Wakristu na Mwenyezi Mungu amesema tushirikiane nao, alisema.
Akifafanua zaidi, alisema hata Mfalme Solomon alikuwa na Jeshi la Majini na aliwatumia
katika ujenzi na vita.
Kwa hiyo nawataka viongozi wa kidini na kisiasa wasihusishe mambo haya na uchawi haya ni mambo ya kawaida na yanafanyika ulimwenguni kote hata hao viongozi wa kidini nao
wanawatumia majini katika kazi zao, alisema.
HABARI LEO
Jumla Maoni (7)
Maoni SHEIKH ASIJARIBU KUMSAFISHA KIKWETE WALA KINANA ASITUDANGANYE. HUU WOTE NI USHIRIKINA NA VITABU VYA KIKRISTO INAWAKATAA MAJINI HATUNA USHIRIKIANO NAO. CCM INAUHUSIANO NA WANAJIMU KWAKUA SHEIKH ALISHASEMA ATAKAEMPINGA KIKWETE ATAKUFA, NA BADO CCM HAMKUKANUSHA USEMI HUO BALI TAARIFA ILITOKA IKULU KUSEMA MANENO YA SHEIKH YAHESHIMIWE.
SASA HIVI MMEONA KUA WATANZANIA TUMEWATILIA SHAKA KUBWA NDO MNAANZA KUTUTAJIA MAJINI. MBONA MNAMSEMA SLAA PEKE YAKE KUMPAKAZIA SUBIYANI NA WENGINEO HAMUWATAJII. SI KIINGINE NI KWAKUA MNAMUONA NI TISHIO.
SHEIKH YAHAYA NA KIKWETE NI DAMUDAMU. Hatudanganyiki
Maoni Mungu wa mbinguni atusamehe na asamehe nchi yetu Tanzania mapepo na majini ni walimuasi mungu sisi kama wanadamu Tulioubwa kwa mfano mungu wa mbinguni tukaishi maisha yanayo fanana nae tunakuwa na uwadui na mapepo na majini.na shetani ndipo mungu akatupa malaika ili atulinde malaika awakumuasi mungu kwaiyo razima ujue kuna maraika wa mungu na mapepo majini wa shetani
Maoni Wapinzani wa Mh, J K, muache woga, km mmeisha jipanga kushindana mkubali kwa moyo mweupe, tukitegemea ushindani wa sera, nasi wananchi tutachuja PUMBA NA MCHELE wenyewe, Huu woga mnaoanza kuuonyesha, mwishowe mtagongwa na kuta mkiogopa kivuli chake. Km kawekewa majini ili yamlinde asidhulike, sasa anayelifuatilia alitaka yamlinde yeye?? au mmeambiwa baada ya hapo yatapiga kura siku ya uchaguzi?? Kwa kuwa uhuru upo, basi nalo lipeleke km Pingamizi, Hakuna mtanzania mwenye umri wa kupiga kura, atakayeburutwa siku hiyo ya 31 Octoba,kila mtu kwa maamuzi yake atamchagua anayeona anafaa.TUACHE TABIA YA KUTUKANANA KUSIKOJENGA,SISI WOTE NI WATZ,
Maoni Ccm wakubali tu kuwa wamamtumia sheik ipasavyo kwanwote tunajua siasa nauchawi nikurwa nadoto.
Maoni I am sorry, sheik yahya aende zake na majini yake asimhusishe Dr slaa na ulinzi wa majini hapa. Dr slaa analindwa na malaika na kama sheik yahya amepeleka huyo jini anayemwita subiyani kwa Dr slaa ili akamdhuru basi ajue hana mafanikio. Na hataweza kumzuia Slaa asiingie Ikulu. Huyu jamaa alisema atampa majini ya ulinzi kikwete, leo anamwingiza Dr Slaa ili iwe nini? Utukome Sheik yahya na majini yako.
Maoni Huyo sheikh Yahaya asitake kumdhalilisha Rais Kikwete kuwa anatumia nguvu ya giza,Yeye anashida zake asijipendekeze kwa kumdhalilisha Rais ni aibu
Maoni Huyu mzee yahaya huwa ana tabia ya kutafuta mamlaka kwenye jamii kwa nguvu. Wale watu wa makamo mnakumbuka jinsi alivyokuwa anatafuta mamlaka kupitia dini bila ridhaa ya waamini hapo miaka ya nyuma na kusababisha mifarakano kila wakatu kwa kuingilia taasisi halali za kiislamu. Baada ya kudhibitiwa sasa amehamia uganga kwa kujidai mnajimu huku anawatia watu hofu na kuwazidishia imani ya kishirikina. Sasa anajidai anamwekea kinga rais, yeye ni taasisi yoyote kisheria hadi atangaze kitu kama hicho? Angesema anamuombea kwa mungu usalama tungeelewa, lakini eti yeye atamuwekea ulinzi wa majini, hii ni kitu gani? Huyu mzee inafaa adhibitiwe maana hana tofauti na wale waganga wa kule mwanzana shinyanga wanaosababisha maauwaji ya watu kwa imani za kishirikina
Kinana alisema jana kwamba, Rais Kikwete ni muumini mzuri wa dini ya Kiislamu aliyelelewa katika misingi ya dini, anaamini afya njema au maradhi, vyote huletwa na Mwenyezi Mungu na vivyo hivyo katika suala la ulinzi wa afya ya mwanadamu.
Alisema Sheikh Yahya ni Mnajimu, anao uhuru wa kusema vitu anavyoviona, lakini Rais
Kikwete wala CCM visihusishwe na mambo hayo.
Alisema mbali na ulinzi wa Mungu, Rais Kikwete ana kikosi madhubuti cha walinzi waliofundwa vyema kuhakikisha usalama wa Rais.
Kauli ya Kinana imefuatia taarifa za baadhi ya vyombo vya habari kuwanukuu wanasiasa
na kiongozi mmoja wa dini wakimtaka Rais Kikwete atoe tamko kuhusu madai ya Sheikh
Yahya ya kumpatia ulinzi usioonekana.
Sheikh Yahya alikaririwa akisema atatoa ulinzi usioonekana kwa macho ili kumkinga Rais Kikwete, ili mtu yeyote asijaribu kumfanyia mchezo wowote katika kipindi hiki cha kuelekea katika uchaguzi mkuu mwezi kesho.
Hata hivyo, jana Sheikh Yahya alitoa ufafanuzi wake juu ya taarifa aliyoitoa awali akisema
ilitafsiriwa vibaya na baadhi ya watu na kusisitiza kila mtu ana jini wake na kusema jini wa
mgombea wa Chadema, Dk. Slaa anaitwa Subiyani.
Mimi sikuzungumzia nguvu za giza na wala sifanyi uchawi au ushirikina nilikuwa
nazungumzia majini ambao ni viumbe kama sisi isipokuwa wao wameumbwa kwa moto na
sisi tumeumbwa kwa udongo na wametajwa katika vitabu vyote vitakatifu vya Waislamu na Wakristu na Mwenyezi Mungu amesema tushirikiane nao, alisema.
Akifafanua zaidi, alisema hata Mfalme Solomon alikuwa na Jeshi la Majini na aliwatumia
katika ujenzi na vita.
Kwa hiyo nawataka viongozi wa kidini na kisiasa wasihusishe mambo haya na uchawi haya ni mambo ya kawaida na yanafanyika ulimwenguni kote hata hao viongozi wa kidini nao
wanawatumia majini katika kazi zao, alisema.
HABARI LEO
Jumla Maoni (7)
Maoni SHEIKH ASIJARIBU KUMSAFISHA KIKWETE WALA KINANA ASITUDANGANYE. HUU WOTE NI USHIRIKINA NA VITABU VYA KIKRISTO INAWAKATAA MAJINI HATUNA USHIRIKIANO NAO. CCM INAUHUSIANO NA WANAJIMU KWAKUA SHEIKH ALISHASEMA ATAKAEMPINGA KIKWETE ATAKUFA, NA BADO CCM HAMKUKANUSHA USEMI HUO BALI TAARIFA ILITOKA IKULU KUSEMA MANENO YA SHEIKH YAHESHIMIWE.
SASA HIVI MMEONA KUA WATANZANIA TUMEWATILIA SHAKA KUBWA NDO MNAANZA KUTUTAJIA MAJINI. MBONA MNAMSEMA SLAA PEKE YAKE KUMPAKAZIA SUBIYANI NA WENGINEO HAMUWATAJII. SI KIINGINE NI KWAKUA MNAMUONA NI TISHIO.
SHEIKH YAHAYA NA KIKWETE NI DAMUDAMU. Hatudanganyiki
Maoni Mungu wa mbinguni atusamehe na asamehe nchi yetu Tanzania mapepo na majini ni walimuasi mungu sisi kama wanadamu Tulioubwa kwa mfano mungu wa mbinguni tukaishi maisha yanayo fanana nae tunakuwa na uwadui na mapepo na majini.na shetani ndipo mungu akatupa malaika ili atulinde malaika awakumuasi mungu kwaiyo razima ujue kuna maraika wa mungu na mapepo majini wa shetani
Maoni Wapinzani wa Mh, J K, muache woga, km mmeisha jipanga kushindana mkubali kwa moyo mweupe, tukitegemea ushindani wa sera, nasi wananchi tutachuja PUMBA NA MCHELE wenyewe, Huu woga mnaoanza kuuonyesha, mwishowe mtagongwa na kuta mkiogopa kivuli chake. Km kawekewa majini ili yamlinde asidhulike, sasa anayelifuatilia alitaka yamlinde yeye?? au mmeambiwa baada ya hapo yatapiga kura siku ya uchaguzi?? Kwa kuwa uhuru upo, basi nalo lipeleke km Pingamizi, Hakuna mtanzania mwenye umri wa kupiga kura, atakayeburutwa siku hiyo ya 31 Octoba,kila mtu kwa maamuzi yake atamchagua anayeona anafaa.TUACHE TABIA YA KUTUKANANA KUSIKOJENGA,SISI WOTE NI WATZ,
Maoni Ccm wakubali tu kuwa wamamtumia sheik ipasavyo kwanwote tunajua siasa nauchawi nikurwa nadoto.
Maoni I am sorry, sheik yahya aende zake na majini yake asimhusishe Dr slaa na ulinzi wa majini hapa. Dr slaa analindwa na malaika na kama sheik yahya amepeleka huyo jini anayemwita subiyani kwa Dr slaa ili akamdhuru basi ajue hana mafanikio. Na hataweza kumzuia Slaa asiingie Ikulu. Huyu jamaa alisema atampa majini ya ulinzi kikwete, leo anamwingiza Dr Slaa ili iwe nini? Utukome Sheik yahya na majini yako.
Maoni Huyo sheikh Yahaya asitake kumdhalilisha Rais Kikwete kuwa anatumia nguvu ya giza,Yeye anashida zake asijipendekeze kwa kumdhalilisha Rais ni aibu
Maoni Huyu mzee yahaya huwa ana tabia ya kutafuta mamlaka kwenye jamii kwa nguvu. Wale watu wa makamo mnakumbuka jinsi alivyokuwa anatafuta mamlaka kupitia dini bila ridhaa ya waamini hapo miaka ya nyuma na kusababisha mifarakano kila wakatu kwa kuingilia taasisi halali za kiislamu. Baada ya kudhibitiwa sasa amehamia uganga kwa kujidai mnajimu huku anawatia watu hofu na kuwazidishia imani ya kishirikina. Sasa anajidai anamwekea kinga rais, yeye ni taasisi yoyote kisheria hadi atangaze kitu kama hicho? Angesema anamuombea kwa mungu usalama tungeelewa, lakini eti yeye atamuwekea ulinzi wa majini, hii ni kitu gani? Huyu mzee inafaa adhibitiwe maana hana tofauti na wale waganga wa kule mwanzana shinyanga wanaosababisha maauwaji ya watu kwa imani za kishirikina