CCM yamgeuka Lowassa

kilimasera

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
3,068
268
MGOGORO wa kisiasa wa kuhusu uchaguzi wa Meya wa Jiji la Arusha, unaweza kuzaa mpasuko siyo tu kwa wakazi wa Arusha, bali hata kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), baada ya Katibu Mkuu wake, Yusuf Makamba, kutofautiana na mmoja wa makada wake maarufu, Edward Lowassa.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, Makamba akionesha kutofurahishwa na kauli
ya Lowassa ya kutaka mgogoro huo wa umeya wa Arusha umalizwe kwa amani kwa kuzikutanisha pande zinazohusika, alisema taarifa ya Lowassa iliyonukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari jana, imemshitua sana.

Pamoja na kuzungumzia amani, Lowassa pia alisisitiza wahusika kuelimishana ili kuunusuru mji huo wa Arusha na Taifa kwa ujumla, usitumbukie katika ghasia.

Lowassa alivitaka vyama hivyo kukaa meza moja kumaliza vurugu zilizotokana na uchaguzi wa
kumpata meya wa jiji hilo ambapo iliripotiwa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema alisababisha vurugu na kukamatwa na polisi ambapo baadaye aliachiwa.

Jana, baadhi ya magazeti yalimnukuu Lowassa akisema juzi katika mkutano mjini Arumeru kuwa, “leo nimekuta Mji wa Arusha ukiwa umezingirwa na askari Polisi na sehemu zingine kulikuwa na gari la maji ya kuwasha kwa ajili yakulinda usalama wa mji na watu wake.

“Hali hii imetokana na uchaguzi uliomalizika hivi karibuni, nawaomba viongozi wa vyama
vinavyovutana, wakae haraka ili kuondoa hali hii ili Arusha isije kuwa kama Ivory Coast…Arusha ni yetu sote.” Alisema.

Hata hivyo Makamba kutokana na taarifa za vyombo vya habari alisema:“Nimeshitushwa sana na taarifa hiyo, nimeshituka kwa vile namjua vizuri Mheshimiwa Lowassa.

Ni kiongozi makini, hakurupuki, ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa na anazijua sana taratibu za Chama.

Hawezi kukikemea Chama chake kupitia magazetini. “Anapo mahali pa kukikosoa kama kimekosea. Ni katika vikao. Nadhani amenukuliwa vibaya.”

Makamba alisema vurugu zinazoendelea Arusha haziwahusu na wanaopaswa kukemewa kwa kutaka kuigeuza Arusha kuwa Ivory Coast, siyo CCM kwani wao wanaamini uchaguzi uliendeshwa vizuri na mgombea wa chama chao ndiye Meya wa Arusha kwa sasa.

Makamba alisema hoja ya Lowassa kuwataka wakae meza moja na Chadema, haina msingi
ambapo alisisitiza “hatuna ugomvi na Chadema na mgombea wetu ameshinda, upande usioridhika na matokeo unapaswa kuyapinga kwa mujibu wa taratibu zilizopo.”

Alisema uchaguzi huo haukusimamiwa na CCM, bali Mkurugenzi wa Jiji la Arusha hivyo kasoro kama zipo, CCM haipaswi kulaumiwa, akifafanua kuwa “upande ambao hauridhiki na matokeo hayo, unapaswa kuyapinga kwa mujibu wa taratibu zilizopo.”

Lakini akizungumza kwa simu jana jioni kutoka nyumbani kwake Monduli, Lowassa alisema hajayaona magazeti ya jana yalivyoandika, lakini alichokisema juzi ni kwamba vyama husika vikae na kuzungumza namna ya kumaliza tofauti zao kwa sababu vurugu hazina maslahi kwa Arusha na Taifa kwa ujumla.

“Niko Monduli, sijaona magazeti ya leo (jana), lakini nilichokisema juzi ni kwamba vyama husika, vikae na kuzungumza kwa nia ya kumaliza tofauti zao. Sijamkemea mtu, sijasema nani mshindi, nani ameshindwa. Nimetoa ushauri, kwa sababu sitaki amani ivurugwe,” alisema Lowassa.

Alisema katika ushauri wake, hakutaja jina la chama chochote, na anaweza kuwa amenukuliwa
vibaya, lakini la msingi alilosisitiza ni kuwa suala la kuelimishana.

“Pengine hawajui utaratibu, ni suala la kuelimishana. Tusipigane mitaani, tuwaelimishe wenzetu. Nisingependa kuona Arusha inakuwa na vurugu, tunahitaji mji wetu uwe na amani,” alifafanua Mbunge huyo wa Monduli.

Chadema juzi iliandaa maandamano na vijana wa chama hicho kuingia mitaani na kulifanya Jeshi la Polisi kuingilia kati na kuwatawanya kwa maji ya kuwasha.
 
Lowasa anawajua CDM na pepos power ndio maana alishaona kitakachofuata...Makamba yeye annafikiriaa mlungula na kuwatisha wahindi wachangie chama...na yeye...hana fikra kama aliemuweka!!!
 
kwa hili Lowassa was right na tumeona aliyoangaliza...:faint2:
 
Huyu mzee makamba nafikiri anamatatizo ya akili na kimsingi sija wahi kumuelewa.....kauli zake nyingi ni mbofumbofu na ni za kukurupuka. Ni wazi hili swala la arusha ni zito na linahitaji ufumbuzi wa haraka , kama inafikia mpaka watu wanauawa baada ya kupata vibali halali vya kuandamana hili ni suala la kitaifa na sio la chama tena. Pia lazima ajue kuwa we have freedom of expression , Lowasa amezungumza kama yeye na sio kwa niaba ya chama. Kuna watu kibao ambao wamewahi kutoa maoni yao na si kupitia chama lakini Makamba hakutoa tamko kama hili mfano..Mkapa , Sumaye , Warioba etc kwenye suala la Katiba, mbona hakutoa tamko la kuwapinga kama hili......!! huyu ni mnafiki ambaye anastahili shahada ya UNAFIKI ULIOTUKUKA!!!!. Aibu itampata pale serekali itakapo ridhia kurudia uchaguzi..... kama aibu ilivyo mpata kwenye suala la serikali ya mseto zanzibar na suala la Katiba.....!!!
 
Lowasa alisoma alama za nyakati..mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni
 
EL anajua kilichotokea Arusha ndiyo maana anaomba pande zote zikutane!
 
Huyu mzee makamba nafikiri anamatatizo ya akili na kimsingi sija wahi kumuelewa.....kauli zake nyingi ni mbofumbofu na ni za kukurupuka. Ni wazi hili swala la arusha ni zito na linahitaji ufumbuzi wa haraka , kama inafikia mpaka watu wanauawa baada ya kupata vibali halali vya kuandamana hili ni suala la kitaifa na sio la chama tena. Pia lazima ajue kuwa we have freedom of expression , Lowasa amezungumza kama yeye na sio kwa niaba ya chama. Kuna watu kibao ambao wamewahi kutoa maoni yao na si kupitia chama lakini Makamba hakutoa tamko kama hili mfano..Mkapa , Sumaye , Warioba etc kwenye suala la Katiba, mbona hakutoa tamko la kuwapinga kama hili......!! huyu ni mnafiki ambaye anastahili shahada ya UNAFIKI ULIOTUKUKA!!!!. Aibu itampata pale serekali itakapo ridhia kurudia uchaguzi..... kama aibu ilivyo mpata kwenye suala la serikali ya mseto zanzibar na suala la Katiba.....!!!
cha kujiuliza, ni kwanini ccm wanaendelea kumuacha pale wakati yeye ndiye anayekiangusha chama?
 
MGOGORO wa kisiasa wa kuhusu uchaguzi wa Meya wa Jiji la Arusha, unaweza kuzaa mpasuko siyo tu kwa wakazi wa Arusha, bali hata kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), baada ya Katibu Mkuu wake, Yusuf Makamba, kutofautiana na mmoja wa makada wake maarufu, Edward Lowassa.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, Makamba akionesha kutofurahishwa na kauli
ya Lowassa ya kutaka mgogoro huo wa umeya wa Arusha umalizwe kwa amani kwa kuzikutanisha pande zinazohusika, alisema taarifa ya Lowassa iliyonukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari jana, imemshitua sana.

Pamoja na kuzungumzia amani, Lowassa pia alisisitiza wahusika kuelimishana ili kuunusuru mji huo wa Arusha na Taifa kwa ujumla, usitumbukie katika ghasia.

Lowassa alivitaka vyama hivyo kukaa meza moja kumaliza vurugu zilizotokana na uchaguzi wa
kumpata meya wa jiji hilo ambapo iliripotiwa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema alisababisha vurugu na kukamatwa na polisi ambapo baadaye aliachiwa.

Jana, baadhi ya magazeti yalimnukuu Lowassa akisema juzi katika mkutano mjini Arumeru kuwa, “leo nimekuta Mji wa Arusha ukiwa umezingirwa na askari Polisi na sehemu zingine kulikuwa na gari la maji ya kuwasha kwa ajili yakulinda usalama wa mji na watu wake.

“Hali hii imetokana na uchaguzi uliomalizika hivi karibuni, nawaomba viongozi wa vyama
vinavyovutana, wakae haraka ili kuondoa hali hii ili Arusha isije kuwa kama Ivory Coast…Arusha ni yetu sote.” Alisema.

Hata hivyo Makamba kutokana na taarifa za vyombo vya habari alisema:“Nimeshitushwa sana na taarifa hiyo, nimeshituka kwa vile namjua vizuri Mheshimiwa Lowassa.

Ni kiongozi makini, hakurupuki, ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa na anazijua sana taratibu za Chama.

Hawezi kukikemea Chama chake kupitia magazetini. “Anapo mahali pa kukikosoa kama kimekosea. Ni katika vikao. Nadhani amenukuliwa vibaya.”

Makamba alisema vurugu zinazoendelea Arusha haziwahusu na wanaopaswa kukemewa kwa kutaka kuigeuza Arusha kuwa Ivory Coast, siyo CCM kwani wao wanaamini uchaguzi uliendeshwa vizuri na mgombea wa chama chao ndiye Meya wa Arusha kwa sasa.

Makamba alisema hoja ya Lowassa kuwataka wakae meza moja na Chadema, haina msingi
ambapo alisisitiza “hatuna ugomvi na Chadema na mgombea wetu ameshinda, upande usioridhika na matokeo unapaswa kuyapinga kwa mujibu wa taratibu zilizopo.”

Alisema uchaguzi huo haukusimamiwa na CCM, bali Mkurugenzi wa Jiji la Arusha hivyo kasoro kama zipo, CCM haipaswi kulaumiwa, akifafanua kuwa “upande ambao hauridhiki na matokeo hayo, unapaswa kuyapinga kwa mujibu wa taratibu zilizopo.”

Lakini akizungumza kwa simu jana jioni kutoka nyumbani kwake Monduli, Lowassa alisema hajayaona magazeti ya jana yalivyoandika, lakini alichokisema juzi ni kwamba vyama husika vikae na kuzungumza namna ya kumaliza tofauti zao kwa sababu vurugu hazina maslahi kwa Arusha na Taifa kwa ujumla.

“Niko Monduli, sijaona magazeti ya leo (jana), lakini nilichokisema juzi ni kwamba vyama husika, vikae na kuzungumza kwa nia ya kumaliza tofauti zao. Sijamkemea mtu, sijasema nani mshindi, nani ameshindwa. Nimetoa ushauri, kwa sababu sitaki amani ivurugwe,” alisema Lowassa.

Alisema katika ushauri wake, hakutaja jina la chama chochote, na anaweza kuwa amenukuliwa
vibaya, lakini la msingi alilosisitiza ni kuwa suala la kuelimishana.

“Pengine hawajui utaratibu, ni suala la kuelimishana. Tusipigane mitaani, tuwaelimishe wenzetu. Nisingependa kuona Arusha inakuwa na vurugu, tunahitaji mji wetu uwe na amani,” alifafanua Mbunge huyo wa Monduli.

Chadema juzi iliandaa maandamano na vijana wa chama hicho kuingia mitaani na kulifanya Jeshi la Polisi kuingilia kati na kuwatawanya kwa maji ya kuwasha.

Baniyani Mbaya lakini kiyatu chake ni dawa Heko Lowassa sasa amekubali uliyoyasema wiki hivi nyuma endelea kuwa na msimamo wako asikunyime usingizi kitaka taka makamba na kukuzonga .
 
No he is not a hero. Lowassa anaelewa kwamba uki-provoke watu wa Arusha fujo itakua kubwa, na watu watakimbilia kuteketeza vitega uchumi vyake vilivyoko Arusha. Ni hilo tu! Tunaweza kusema anajua kuisoma jamii yake vizuri lakini he is still fisadi papa.
 
cha kujiuliza, ni kwanini ccm wanaendelea kumuacha pale wakati yeye ndiye anayekiangusha chama?

mimi huwa najiuliza siku zote ivi bado kuna watu wanaosikilizwa na chama kwenye CCM zaidi ya kikwete na Makamba. Pamoja na kwamba most of them ni mafisadi lakini busara ndogo ndogo nazo hamna kabisa? Nilifikiri wale wazee waliokuwapo kipindi cha Nyerere na Mwinyi bado watakua na busara fulani yakukishauri chama kuepusha mambo kama ya Arusha. Where is Malecela, Msuya, Msekwa, Kingunge, Mwinyi, Kimiti, Bomani, Warioba, Kahama etc etc etc. Sitaki kuamini na wao wanamuogopa Rostam.
 
sijamuelewa vizuri makamba alivyosema uchaguzi wa meya ulisimamiwa na mkurugenzi na wala si CCM,nakaka kujuzwa mkurugenzi anachaguliwa au anateuliwa kama RC na DC? Kama anateuliwa bila shaka serikali ya ccm si ndio imemuweka madarakani?logically ni mmoja wao tu,kwa hili hawawezi kunidanganya.
 
Back
Top Bottom