Ta Muganyizi
R I P
- Oct 19, 2010
- 5,361
- 2,734
karibia nihamie nchi jirani humu tz mwishowe nitanunua gun nianze kuondoa fisadi mmoja baada ya mwingine aghhh
karibia nihamie nchi jirani humu tz mwishowe nitanunua gun nianze kuondoa fisadi mmoja baada ya mwingine aghhh
Hapa sijui CCM watasema huyu Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam kapotoka, watu wenye akili waliishatambua hili zamani
Watasema sio kauli ya chamaHapa sijui CCM watasema huyu Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam kapotoka, watu wenye akili waliishatambua hili zamani
Tulimchagulia hao washauri au kajichagulia mwenyewe? kama mbwa akikuuma utamlaumu mbwa au mwenye mbwa? wasilete habari zao za ajabu hapa, wakubali wameshindwa kazi
Watasema sio kauli ya chama
Hapo ndiyo tujue kujadili hoja badala ya watu. Hoja hiyo hiyo ikitolewa na CHADEMA wanaitwa wachochezi, akisema Lowasa, magufuli, au sita hataki kupindua nchi. Akisema Dr. Slaa, Mbowe au Lisu wanadai wananjama. Uchovu ni uchovu tu tena uchovu wakufukili ni mbaya zaidi. CCM wanampaka Mafuta kwa mgongo wa chupa rais, eti kashindwa kuongoza kwa sababu ya ushauri mbaya, kwani alipokuwa anaombakazi ya urais aliomba na washuri wake?. Lakini kama rais anashauriwa vibaya na kwa kipindi chote na hajui kama anashuriliwa vipaya si anapaswa kupimwa bongo yake?Hapa sijui CCM watasema huyu Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam kapotoka, watu wenye akili waliishatambua hili zamani
Wanajf hii nayo imekaa vizuri. inafikia hadi wenyewe wanakiri udhaifu wao
:hand:CCM Dar: JK amekwama
Yataka mitambo ya Dowans kuwashwa haraka
na Betty Kangonga
MWENYEKITI wa Chama cha Mapinduzi, Mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita, amesema Rais Jakaya Kikwete ameshindwa kutatua matatizo mbalimbali yanayoikabili nchi kwa sababu ya kushauriwa vibaya.
Guninita alitoa kauli hiyo jana wakati akitoa ufafanuzi juu ya hatua zinazopaswa kuchukuliwa ili kupunguza tatizo la umeme linaloikabili nchi kwa sasa.
Mambo mengi hayafanyiki kwa kuwa wapo watu wanaoshindwa kumsaidia Rais vizuri, alisema Guninita.
Guninita alikuwa akizungumza jana na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wakati akitoa tamko la Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa iliyokutana Machi sita mwaka huu, kujadili kero mbalimbali zinazowakabili wananchi ikiwemo tatizo la umeme, kupanda kwa bei ya bidhaa, ajira na bomoabomoa.
Alisema kamati hiyo inaunga mkono ushauri na mapendekezo yaliyotolewa na Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini juu ya serikali kutakiwa kuwashwa mitambo ya umeme ya Dowans ili kukabili upungufu wa umeme kauli inayopingana na msimamo wa awali wa viongozi waandamizi wa serikali.
Guninita alisema tatizo la umeme limekuwa kubwa na hasa ukizingatia ndiyo uti wa mgongo wa uchumi hivyo serikali ichukue hatua kuondokana na tatizo hilo.
Kuhusu bomoabomoa, Guninita alisema wamesikitishwa na hatua iliyofanywa na watendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni ya kufanya uvamizi na kuvunja vibanda vya wafanyabiashara ndogo ndogo wa eneo linalojulikana kama, Big brother lililoko Manzese, jijini Dar es Salaam.
Alisema kamati hiyo imeutaka uongozi wa Wilaya ya Kinondoni kuwachukulia hatua watendaji waliotoa agizo hilo ambalo limewatia hasara wafanyabiashara hao na wanapaswa kuwalipa fidia kwa hasara waliyoipata.
Kitendo kilichofanywa si cha kiutu pia kimekiuka makubaliano yaliyokuwepo ya kuondoa mabanda 150 ili kupisha mradi wa mabasi yaendayo kasi na badala yake wamevunja mabanda zaidi ya 350 tofauti na makubaliano, alisema.
Alisema wamemuandikia barua Meya wa Manispaa ya Kinondoni Yusuf Mwenda ya kumtaka kuchunguza kwa haraka uharibifu uliojitokeza pamoja na kuhakikisha wafanyabiashara wote wanalipwa haki zao.
Kuhusu mfumko wa bei ya vyakula, Guninita alisema wameishauri serikali kuhakikisha inaunda tume maalumu itakayowajibika kufuatilia na kusimamia bei ili kuhakikisha wananchi wanapata mahitaji yao kwa bei nafuu.
Kamati imetafakari na kubaini kuwa hakuna sababu ya sukari inayoingizwa nchini na msamaha wa kodi kuuzwa kwa bei ya 1,700 kwa kilo wakati gharama za kuagiza hadi kufika nchini ziko chini, alisema.
Alisema serikali inatakiwa kwa kipindi kifupi kutafuta ufumbuzi wa tatizo la kupanda kwa bei ya vyakula na kuhakikisha bei hizo zinashuka kwa haraka sambamba na kuagiza bidhaa muhimu kama vile sukari, mchele na maharage.
Guninita alisema pamoja na kushuka kwa bei, bado serikali inatakiwa kuwachukulia hatua wafanyabiashara wanaokwenda kinyume na bei zilizopangwa.
Kwa upande wake Mbunge wa Ilala Musa Zungu (CCM), alisema hakuna sababu ya bidhaa na vyakula vinavyopata msamaha wa kodi kuuzwa kwa bei ya juu maana kufanya hivyo ni kutaka kuwaumiza wananchi.
Aidha, juu ya tatizo la ajira nchini, alisema serikali inatakiwa itenge fedha katika bajeti ya mwaka 2011/12 zitakazotoa msukumo katika kuwapatia vijana ajira kama ilivyofanya mwaka 2009 ilipoamua kutenga kiasi cha sh trilioni 1.7 kusaidia kuinua uchumi.
Kwa kuwa tatizo la ajira kwa vijana ni ajenda endelevu ambayo inahitaji utekelezaji usiokoma, hivyo bajeti zetu zote za kila mwaka lazima ziongeze fedha na kasi ya kuwapatia vijana ajira, alisema.
MWENYEKITI wa Chama cha Mapinduzi, Mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita, amesema Rais Jakaya Kikwete ameshindwa kutatua matatizo mbalimbali yanayoikabili nchi kwa sababu ya kushauriwa vibaya.
Guninita alitoa kauli hiyo jana wakati akitoa ufafanuzi juu ya hatua zinazopaswa kuchukuliwa ili kupunguza tatizo la umeme linaloikabili nchi kwa sasa.
Mambo mengi hayafanyiki kwa kuwa wapo watu wanaoshindwa kumsaidia Rais vizuri, alisema Guninita.
Nasikia Rais anajipanga kuhutubia taifa tena ili akemee kauli ya mwenyekiti huyo wa mkoa kuwa anachochea vurugu kwa kusema kuwa ameshindwa kutatua kero kwa wananchi.Hapa sijui CCM watasema huyu Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam kapotoka, watu wenye akili waliishatambua hili zamani