nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
na Salehe Mohamed na Danson Kaijage
CHAMA cha Mapinduzi (CCM) kimesema kina hofu ya kupinduliwa madarakani na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kinachoratibu na kufanya maandamano kwenye maeneo mbalimbali hapa nchini.
Wakati Chama hicho kikihofia maandamano ya Chadema, Mbunge wa Ludewa Deo Filikunjombe (CCM), alisema maandamano ni miongoni mwa njia za kuwafanya watendaji wazembe wa serikali kuwajibika.
Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC) (Uchumi na Fedha Taifa) wa CCM, Mwingulu Nchemba, amevitaka vyombo vya dola kuingilia kati maandamano yanayofanywa na Chadema kwa madai kuwa yanalenga kufanya mapinduzi ya serikali iliyopo madarakani.
Nchemba, alitoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mkoani hapa, ambapo alisema viongozi wa Chadema wana ajenda ya kufanya mageuzi kwa nguvu na kulifanya taifa lisitawalike.
Alisema viongozi wa chama hicho wamekuwa na kauli mbalimbali za uchochezi ikiwa ni pamoja na kutoa ushawishi kwa jeshi la polisi ili wasiweze kukubali amri za viongozi wao jambo ambalo alidai kuwa ni hatari kwa taifa.
"Mimi sikatai maandamano ni haki ya kila mtu lakini ninachosema ni kuwa na meno ya viongozi na ushawishi wa viongozi hao ni ya uchochezi na yanaashiria kupinga uongozi ulio madarakani," alisema Nchemba.
Alisema maandamano ya Chadema yamezidi maandamano ya vyama vingine duniani kwani wanapofanya maandamano wamekuwa na maneno yanalenga kuwahamasisha wananchi kufanya maandamano yanayoweza kuleta mageuzi kama vile, Misri, Libya na nchi nyingine ambazo zina machafuko na wananchi wanavutiwa zaidi na habari hizo.
Wakati CCM, ikihofu kupinduliwa, jana asubuhi katika kipindi cha Tuongee, kinachorushwa na televisheni ya Star Tv, mbunge wa Ludewa Deo Filikunjombe (CCM), alisema hata yeye angeingia mitaani kuhamasisha wananchi wa Ludewa kuandamana kama serikali isingeongeza fedha katika Wizara ya Uchukuzi.
Alisema serikali ina watendaji wazembe ambao wakati mwingine wamekuwa wakikwamisha shughuli za maendeleo hivyo wananchi wanapoamua kufanya maandamano huwaamsha katika usingizi.
"Juzi nilisema kuwa nitawahamasisha wananchi wangu kuandamana kama wanavyofanya Chadema kama shirika la meli lisingepatiwa fedha za kutosha mbazo zitatuwezesha watu wa Ludewa kupata meli mpya au kukarabati zile zilizopo," alisema.
Alibainisha kuwa hakuna sababu ya serikali kuogopa maandamano kama ingekuwa inatimiza wajibu wake wa kutimiza mahitaji ya wananchi lakini imekuwa ikihofia maandamano kwa sababu ya uzembe ulioko serikalini.
Filikunjombe pia alitetea kauli yake kuwa mawaziri na watendaji wazembe wanyongwe ili kujenga taifa lenye uwajibikaji hasa kwa watendaji wanaopewa kusimamia rasilimali za taifa.
"Adhabu ya kunyongwa si mpya hapa nchini, nilichokitaka mimi ni adhabu hiyo itolewe kwa mawaziri na watendaji wazembe na wabadhirifu, hakuna kigeni hapo," alisema.
Wiki mbili zilizopita Mbunge wa Mtera Livingstone Lusinde, (CCM), alisema watendaji wa serikali na chama chake ndiyo wanaopaswa kulaumiwa kwa kusababisha maisha magumu kwa wananchi badala ya kukilaumu Chadema.
Lusinde alisema kama CCM ingeboresha maisha ya wananchi kamwe wasingekubali ushawishi wa Chadema ambayo imekuwa ikifanya maandamano kupinga ugumu wa maisha, kupanda kwa gharama za umeme na mgawo unaoendelea hivi sasa.
CHAMA cha Mapinduzi (CCM) kimesema kina hofu ya kupinduliwa madarakani na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kinachoratibu na kufanya maandamano kwenye maeneo mbalimbali hapa nchini.
Wakati Chama hicho kikihofia maandamano ya Chadema, Mbunge wa Ludewa Deo Filikunjombe (CCM), alisema maandamano ni miongoni mwa njia za kuwafanya watendaji wazembe wa serikali kuwajibika.
Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC) (Uchumi na Fedha Taifa) wa CCM, Mwingulu Nchemba, amevitaka vyombo vya dola kuingilia kati maandamano yanayofanywa na Chadema kwa madai kuwa yanalenga kufanya mapinduzi ya serikali iliyopo madarakani.
Nchemba, alitoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mkoani hapa, ambapo alisema viongozi wa Chadema wana ajenda ya kufanya mageuzi kwa nguvu na kulifanya taifa lisitawalike.
Alisema viongozi wa chama hicho wamekuwa na kauli mbalimbali za uchochezi ikiwa ni pamoja na kutoa ushawishi kwa jeshi la polisi ili wasiweze kukubali amri za viongozi wao jambo ambalo alidai kuwa ni hatari kwa taifa.
"Mimi sikatai maandamano ni haki ya kila mtu lakini ninachosema ni kuwa na meno ya viongozi na ushawishi wa viongozi hao ni ya uchochezi na yanaashiria kupinga uongozi ulio madarakani," alisema Nchemba.
Alisema maandamano ya Chadema yamezidi maandamano ya vyama vingine duniani kwani wanapofanya maandamano wamekuwa na maneno yanalenga kuwahamasisha wananchi kufanya maandamano yanayoweza kuleta mageuzi kama vile, Misri, Libya na nchi nyingine ambazo zina machafuko na wananchi wanavutiwa zaidi na habari hizo.
Wakati CCM, ikihofu kupinduliwa, jana asubuhi katika kipindi cha Tuongee, kinachorushwa na televisheni ya Star Tv, mbunge wa Ludewa Deo Filikunjombe (CCM), alisema hata yeye angeingia mitaani kuhamasisha wananchi wa Ludewa kuandamana kama serikali isingeongeza fedha katika Wizara ya Uchukuzi.
Alisema serikali ina watendaji wazembe ambao wakati mwingine wamekuwa wakikwamisha shughuli za maendeleo hivyo wananchi wanapoamua kufanya maandamano huwaamsha katika usingizi.
"Juzi nilisema kuwa nitawahamasisha wananchi wangu kuandamana kama wanavyofanya Chadema kama shirika la meli lisingepatiwa fedha za kutosha mbazo zitatuwezesha watu wa Ludewa kupata meli mpya au kukarabati zile zilizopo," alisema.
Alibainisha kuwa hakuna sababu ya serikali kuogopa maandamano kama ingekuwa inatimiza wajibu wake wa kutimiza mahitaji ya wananchi lakini imekuwa ikihofia maandamano kwa sababu ya uzembe ulioko serikalini.
Filikunjombe pia alitetea kauli yake kuwa mawaziri na watendaji wazembe wanyongwe ili kujenga taifa lenye uwajibikaji hasa kwa watendaji wanaopewa kusimamia rasilimali za taifa.
"Adhabu ya kunyongwa si mpya hapa nchini, nilichokitaka mimi ni adhabu hiyo itolewe kwa mawaziri na watendaji wazembe na wabadhirifu, hakuna kigeni hapo," alisema.
Wiki mbili zilizopita Mbunge wa Mtera Livingstone Lusinde, (CCM), alisema watendaji wa serikali na chama chake ndiyo wanaopaswa kulaumiwa kwa kusababisha maisha magumu kwa wananchi badala ya kukilaumu Chadema.
Lusinde alisema kama CCM ingeboresha maisha ya wananchi kamwe wasingekubali ushawishi wa Chadema ambayo imekuwa ikifanya maandamano kupinga ugumu wa maisha, kupanda kwa gharama za umeme na mgawo unaoendelea hivi sasa.